Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Psychologically utawachanganya sana hawa wanawake. Ninakuonea huruma na wewe mwenyewe. Kitu kikubwa kumbuka hakuna shida isiyo na mwisho, haya unayoyapata wewe sio wa kwanza, ni vizuri umekuwa muwazi kuomba ushauri. Ufikirie na damu yako itakavyolelewa nchi ambayo hawapendi weusi. Kama walivyoshauri wengine, mwambie wife utafika siku moja/mbili mbele, ukitoka airport tafuta hoteli. Baada ya siku mbili unaingia nyumbani kwa wife unamueleza yaliyotokea. Nyinyi wote watatu mpange future upya.
 
Tafuta jamii forum y huko korea afu uombe huu ushauri kisha ulete mrejesho wako hp jf ya bongo.me naweza kukushauri vzr ila nataka ujifunze na uwe pia mfano kw wengine wasijekuharibikiwa.
Wabongo mmezoea utapeli na usanii ht shm zisizostahili tunapenda kucheza na feelings za wengine.bora toka mwanzo ungemwambia ht mkorea kwamba ulikuwa unaishi na mke wa kaka yako ambae ni marehemu kidogo ungeweza kucheza kipindi cha pili
 
Kama suala la kuchagua mimi nashauri uchague kubaki na Mke kuliko huyo mkorea.

Sacrifice mahusiano ya huyo mkorea.

Kwa jinsi ninavyo wajua wazungu. Ukiamua kumuacha Mkeo ili uendelee kuishi na huyo Mkorea, hakika nakwambia ipo siku atakumbuka kwa na atakuambia anahitaji kurudi kwao na mtoto, tena kwa lengo la kuishi huko moja kwa moja.

(Wanasema mfuga nyani awe tayari siku nyani atakapo kumbuka pori na kuamua kurudi)

Hapo ndipo utakapo anza kumkumbuka mkeo na kujutia kwa nini ulimuweka pembeni na kumpa nafasi mkorea.
amekwambia mkorea siyo mzungu wewe wa wapi wewe
 
Nahofu nikimwambia nikiwa bado ndani ya ardhi ya naweza pata matatizo. Huyu binti aliwaahi kusimama kidete kumpinga mama yake na ndugu zake wengine. Alikuwa yuko radhi tuache kuache kusoma Korea twende tukasomee South Afrika ili tuishi kwa ama mimi na yeye bila bughudha za ndugu zake.
kweli asiyesikia la mkuu ,sasa binti atawakumbuka wazazi wake
 
Sikiliza wewe kakate tiketi yako kwa pesa yako siku nyingine na ndege nyingine halafu mtoroke ila akikisha unamwandikia mail yenye ukweli wote kisha ama hapo ulipo nenda kapige shopping kwa ajili ya familia kisha unasepa kimya kimya. Hqkijua ukweli hawezi kukutafuta tena maana roho itamwingia nyongo na kama akikutafuta au akija Bongo ujue huyo kaja kukuua
Nimelipenda hili wazo, nitalizingatia. Ila itabidi niache baadhi ya vitu vyangu ili asishitukie mapema.
 
Pole sana, pia ufikirie mtoto wako huyo mkorea ni damu yako hiyo, unaiacha vipi? Pia umwambie ukweli mkeo kuwa unatarajia mtoto na mkorea umpe story nzima. Hakuna kitu nakithamini kama damu yangu. Ukimkimbia huyo mkorea baadae utakuja kuwaza kuhusu mtoto wako, na unaweza kujutia maamuzi yako. Ulishindwa kusema ukweli mwanzo, useme wote sasa Lubebenamawe
Kweli kaka damu yangu ni muhimu sana, ila cha muhimu ni kutafuta suluhisho wa tatizo hili lilipo kwanza.
 
Hivi hawa wakorea si ndio kina JUMONG? na kina IRIS? Mkuu hilo unalo. Cha kufanya muandae rafiki yako wa Tz akuandalie nyumba mbali na kwako. Mwambie wife umeahirisha safari utamwambia ukiwa tayari, acha kuwasiliana na wife kwa muda. Njoo Tz ukifika jipange maisha mapya na mkorea. Baada ya Muda mpange sasa ili ajue A-Z.
Wazo zuri mbadala litalizingatia.
 
Njoo nae TZ ila mfikie hotel, then mkifika muambie ukweli tu na kwamba mtaishi wote ila mkeo wa ndoa hutamuambia. Itabidi umtafutie nyumba ili awe mke mdogo. Lete mbegu ya ki-korea Tz kaka. U never know ya mbeleni mana unaweza ukamuacha na akagoma kutoa mimba na itansumbua sana hiyo kitu. Wewe njoo nae ni bora ajulie ukweli akiwa huku tu.
Hili wazo nimelikubali hapa ningekuwa mm ningetumia njia hii
 
Kweli kaka damu yangu ni muhimu sana, ila cha muhimu ni kutafuta suluhisho wa tatizo hili lilipo kwanza.

Obama alizaliwa katika mazingira kama haya, unaweza kutuletea future Tanzania President kaka. Sijajua kipato chako ukirudi nyumbani kama utaweza kupanga nyumba ya mkorea lakini ninavyomsoma huyu binti akijua situation hawezi kukaa, ataamua kurudi kwao.
 
Nimelipenda hili wazo, nitalizingatia. Ila itabidi niache baadhi ya vitu vyangu ili asishitukie mapema.
ushauri mbaya sana huo sawasawa na kupiga ramli tu.umemdanganya binti wa watu ,umemchonganisha na wazazi wake na hela zake umekula .sasa hivi umemaliza shida zako unamwachia tumbo unamtoroka .laana hiyo itawaangukia watoto wako lazima watapatwa na mabaya na mimi naomba iwe hivyo.
 
Psychologically utawachanganya sana hawa wanawake. Ninakuonea huruma na wewe mwenyewe. Kitu kikubwa kumbuka hakuna shida isiyo na mwisho, haya unayoyapata wewe sio wa kwanza, ni vizuri umekuwa muwazi kuomba ushauri. Ufikirie na damu yako itakavyolelewa nchi ambayo hawapendi weusi. Kama walivyoshauri wengine, mwambie wife utafika siku mojo/mbili mbele, ukitoka airport tafuta hoteli. Baada ya siku mbili unaingia nyumbani kwa wife unamueleza yaliyotokea. Nyinyi wote watatu mpange future upya.
Noted.
 
Back
Top Bottom