Mchechu wa NHC aundiwa zengwe

Mchechu wa NHC aundiwa zengwe

kweli kabisa nhc itarudi kule kule kipindi kile ofisi zao ziko kama gesti.....za uswahilini.kingine nchi hii mtu akitaka pigania kufufua makampuni ya serikali basi atapigwa vita balaa....

Ndo maana watu wakipewa kuongoza haya mashirika huwa wanapiga tu hela kiroho mbaya maana wanajua serikali ya haya MaCCM haina shukrani,, ukifanya vizuri utasifiwa, ukiharibu huku unawahonga hao WAZEE WA CCM kwenye hizo bodi ndio unaonekana uko poa kwa vile MaCCM Ni mabinafsi ya kutupwa.
 
Mtu wa hali ya chini Tanzania hata mlo wa siku Ni kitendawili, Hana assets zozote anamiliki then unataka anufaike na shirika la nyumba. Kwa akili yako ndogo inawezekana unataka shirika lijenge nyumba na kuwapa bure hao watu Wako wa chini, no way hiyo itatokea mahali popote duniani.

Hapa naona kuna zengwe yule Mama wa Kihaya anataka kuweka Mhaya mwenzie baada ya kuona mafanikio. Hata UN aliwavuta Nshomile kibao, but NKM ameweka standards juu Sana lazima watachemka Tu. Kwanza namshangaa kwa CV yake Mchechu kuendelea kufanya kazi chini ya hawa LOOSERS wa CCM

huyo mama prof wake sjui kaupatia pale mwananyamala kwenye yale madanguro...huyo mama anajifanya smart wakati she is a big looser wizara kaishindwa...safi sana mchechu amefanya changes kubwa sana na tunajua there is more to come...
 
Ndo maana watu wakipewa kuongoza haya mashirika huwa wanapiga tu hela kiroho mbaya maana wanajua serikali ya haya MaCCM haina shukrani,, ukifanya vizuri utasifiwa, ukiharibu huku unawahonga hao WAZEE WA CCM kwenye hizo bodi ndio unaonekana uko poa kwa vile MaCCM Ni mabinafsi ya kutupwa.

serikali hii ya magamba washalaaniwa mara milion kumi...kingine lazima hawa wadosi watakuwa wanatembeza mkwanja kumngoa huyu mchapakazi na mfanya mabadiliko mchechu.....maana anawabana vilivyo
 
Now you are talking. This means huyu jamaa anafanya vitu kwa manufaa ya uma,maana hakuna maana kujenga majumbani halafu yanauzwa kwa bei ambayo wananunua mafisadi tu.

Lakini ishu inabaki kuwa Mchechu kachukua hatua gani baada ya serikali kukataa? Je kaweza kutumia huo uzoefu wake na CV yake kupata the other way around to make sure watu wa kipato cha chini wananufaika na hizo nyumba

Wewe Mbulumundu, ili nyumba za bei nafuu unazotaka na mambulumundu wenzio zipatikane lazima serikali iweke ruzuku ya fedha. Kokote kule unakoona serikali duniani zimesaidia kupatikana nyumba za bei nafuu na kwa kuweka hela sio kwa njia ya mkato. Hilo shirika la nyumba linanunua cement, kokoto, mchanga na vifaa vyote vya ujenzi unakonunua wewe, sasa hizo nyumba za bei nafuu zitapatikanaje hapo? Au unataka shirika lijenge NYUMBA ZA TEMBE AU NYASI kama alizokuwa anakaa Babu yako kijijini?

Dr Slaa aliwaambia mumchague awashushie bei ya cement hadi shs 5,000 kwa mfuko mkamkataa na kuchagua mcheza ngoma, sasa isomeni namba
 
Acheni ushabiki wa kijinga! Jiulizeni kwanza maswali ya msingi ? Board hiyo kazi yake ni nini? ni kweli Mchechu amefanya kazi kubwa NHC hatukatai lakini tujiulize mchango wa Shirika hilo kwa maendeleo ya Taifa ni nini! Au ni kuboresha tu mishahara ya watumishi wa Shirika hilo? NHC sasa hivi wanatoza kubwa kodi kubwa za pango kuliko private sector! Mfano katika jengo lao jipya wanalomalizia hapa Musoma kodi ya "fremu" ni kati ya laki tatu hadi laki nne !kwa mzunguko wa biashara gani!? tatizo hapa nchini tumekuwa na ushabiki wa kijinga kwa kila kitu ! na hii ni kutokana ma-graduate wengi wa vyuo vikuu vya kata wasio na kazi mtaani ! Nehemia lazima mwisho wa siku lazima ajue vision ya shirika ni kusaidia Watanzania na si kuwanyonya Watanzania! Amefanya vizuri ku-improve image ya shirika lakini kama ataki kubadilika kuhusu rates anazotoza basi ama aombe tumbinafsishie shirika hili ama Board imfukuze tu aende akafanyie ujasiriamali wake kwingine! CCM kuweni macho na Mchechu mkimchekea na sifa za kijinga mtazikosa kura za wafanyabiashara wengi walioko NHC 2015!

Kwa hiyo kwa akili yako ndogo unaona bora wakati shirika linajifia, majengo yamegeuka gofu watu wanatumia kama gesti bubu na kutupa condoms kuliko sasa lina nyumba nzuri, kali, linapamba miji yenu? Kwanza hapo Musoma bila Mathayo Manyinyi msingekuwa na nyumba nzuri kupendezesha mji wenu, sasa unataka hata business offices mzipate kwa bei kama vijumba vyenu vya tembe kule Mukendo?
 
Huyu Nehemia alikuwa ni school mate wangu pale Milambo secondary school tabora ingawa mie nilikuwa O-level yeye alikuwa A-level na alikuwa akichukua EGM, walikuwa darasa moja na mkuu wa mkoa wa arusha kwa sasa Magesa Mlongo na wote wakichukua combination 1, alikuwa ni mcheshi sana kwa kila mtu, alikuwa hana majivuno, ingawa sikumbuki MIlambo secondary kupewa Uongozi, lakini ni mtu 1 poa sana
 
akisha complete mission yake nhc.....awekwe shirika la ndege atc.... alifufue maana limekufaaaa.kuna vigogo hawataki kuliona shirika hilo lina simama tena

Akiondoka NHC atawekwa mwizi mwingine aanze kuliua shirika, akifika ATCL atalifufua akipelekwa kwingine huku nyuma atakuja mwizi mwingine ataliua tena.

Yan ni cycle, bora abaki hapo hapo
 
Tangu lini huyo Jamaa akawa Kijana? Mtu anaonekana keshavuka miaka 40 na bado unamuita Kijana? Argrghhhhhhhhh

Definition ya kijana kwa watanzania inaishia miaka 45 kwa hiyo bado ni kijana. Inategemea na namna unavyomchukulia. Ila kwangu mimi Mchechu ni Kijana mchapa kazi ambaye hata wewe sidhani kama unaweza kumfikia "let alone achieving his credentials with experience". Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
 
Wewe Mbulumundu, ili nyumba za bei nafuu unazotaka na mambulumundu wenzio zipatikane lazima serikali iweke ruzuku ya fedha. Kokote kule unakoona serikali duniani zimesaidia kupatikana nyumba za bei nafuu na kwa kuweka hela sio kwa njia ya mkato. Hilo shirika la nyumba linanunua cement, kokoto, mchanga na vifaa vyote vya ujenzi unakonunua wewe, sasa hizo nyumba za bei nafuu zitapatikanaje hapo? Au unataka shirika lijenge NYUMBA ZA TEMBE AU NYASI kama alizokuwa anakaa Babu yako kijijini?

Dr Slaa aliwaambia mumchague awashushie bei ya cement hadi shs 5,000 kwa mfuko mkamkataa na kuchagua mcheza ngoma, sasa isomeni namba

Nashukuru kwa kunitusi mkuu japo haikuwa na sababu maana hapa nia ni kujenga kwahiyo unapokuwa na hoja tofauti ndio dhumuni linatimia maana tukiwa na mitazamo sawa haina maana

Nafikiri hujasoma comment zangu za nyuma mkuu,na hata hiyo ambayo ume quote hujasoma ukanielewa ndio maana umeishia kunitusi,ila mimi sito kutusi maana ndio uungwana na great thinker hatukani.Mimi sijakataa hoja yako,kwenye comment yangu kwa juu huko nimekubaliana na Kabembe kuhusu changamoto ambayo Mchechu anaipata kuhusu kutozwa kodi na serikali kukataa kupunguza kodi.Lakini mtu kama Mchechu kwa CV yake niategemea awe na mbinu mbadala,mimi sio mtaalamu wa real estate lakini huwa naamini kila changamoto ina suluhisho kwahiyo ukikumbana na kikwazo kimoja lazima utafute njia mbadala.

Ni hayo tu,matusi si uungwana mkuu.You don't benefit anything kwa kumtukana mtu na pia jitahidi uwe unasoma comments zote kabla hujaamua Kumtusi mtu.uwe na siku njema
 
Last edited by a moderator:
Nchi hii
kasi ya utendaji kazi ya mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa (nhc), nehemia msechu imesababisha aundiwe zengwe kwa lengo la kutaka ang'olewe nafasi hiyo.

Jambo leo, limeelezwa kuwa, tayari msechu amepewa masharti mazito na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika hilo, yakiwamo ya kumtaka apunguze wakurugenzi wake katika idara mbalimbali.nchi hii ukiwa mwadilifu sana huwezi kudumu maana unazuia riziki za vigogo.

Wakati hayo yakiendelea, imeelezwa kuwa msechu alipewa likizo wakati akitafakari masharti aliyopewa na bodi hiyo, inatokana na kumaliza muda wake, kabla ya kuingia naye makubaliano mengine ya kulitumikia shirika hilo, kazi ambayo ameifanya kwa uadilifu na uamifu wa hali ya juu.

Msechu ambaye alilikuta shirika hilo katika hali mahututi na kutumia nafasi yake kupanga safu ambayo imerudisha heshima ya nhc kwa kuendelea na miradi ya ujenzi wa nyumba za kisasa na bei nafuu kwa ajili ya watanzania, ameonekana kutofurahisha wale ambao hawapendi shirika hilo lifanye kazi yake kwa maslahi ya taifa.

Vyanzo vya kuaminika vimeliambia jambo leo kwa nyakati tofauti kuwa, msechu kwa sasa amemaliza mkataba wake wa kulitumikia shirika hilo na
kinachosubiriwa ni serikali kupitia waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, profesa anna tibaijuka kumuidhinisha tena ili aweze kuendelea.
Hata hivyo, wakati anasubiri kuidhinishwa tena, mizengwe imeendelea kufanywa na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika hilo.

"kwa sasa kinachoonekana ni kama vile kumuundia zengwe msechu ili asiendelee katika nafasi hiyo ambayo ameifanya kwa uamunifu mkubwa. Kuna baadhi ya wajumbe wa bodi wanaotaka asirudi na ndiyo wanaochelewesha kumuidhinisha.
"wameamua kumpa masharti mazito katika kipindi hiki wakitaka atafakari, na moja ya masharti hayo ni kwamba, apunguze idadi ya wakurugenzi wake kwenye
idara, huku pia wakitaka apunguze mishahara ya watumishi wake.

"yote hiyo ni kutaka kumvunja nguvu ili mikakati yao itimie. Sababu za msingi za kutoa masharti hayo hazipo, bali kinachoonekana utendaji wake wa kazi kwa kiwango cha kutukuka ndiyo unaosababisha wasiopenda mafanikio ya rais jakaya kikwete, wamchukie na kumtengenezea mazingira ya kumweka kwenye wakati mgumu," kilisema moja ya chanzo cha taarifa hizo (jina tunalo).

Imeelezwa kuwa, kutokana na mambo yanayoendelea dhidi ya msechu, ndiyo maana hata rais kikwete alipokuwa kwenye ziara yake mkoani tanga, hakwenda zaidi ya kutuma mwakilishi wake.pia, msechu ameshindwa kwenda kwenye maeneombalimbali ya miradi ya nhc inayoendelea sasa, na hiyoyote ilitokana na ukweli kwamba, hajafahamu hatma yake ndani ya shirika hilo.

Wakati hayo yakiendelea, utendaji kazi wa msechu umekuwa gumzo katika maeneo mbalimbali nchini na hiyo yote ni kutokana na kazi nzuri ambayo ameifanya ya kulitumikia taifa na kurudisha hadhi yake ambayo ilipotea. Rais kikwete mara kadhaa amekuwa akizungumzia mafanikio ya shirika hilo ambayo yameletwa na msechu kwa kushirikiana na wakuu wake wa idara na watumishi wengine.

Hotuba za msechu ambazo amekuwa akizitoa katika maeneo mbalimbali wakati wa uzinduzi wa miradi ya ujenzi, amekuwa akiweka wazi ushirikiano uliopo kati
yake na watumishi wengine, ni sawa na timu ya real madrid au barcelona ambazo zinapokuwa uwanjani zinafanya kazi moja tu, ya kuhakikisha zinafanikiwa
kushinda.

Pamoja na hayo, imefahamika kuwa baadhi ya viongozi na wabunge ambao wamekuwa wakitumia shirika hilo kuweka ndugu, marafiki na jamaa zao wapo kwenye
mkakati wa kuhakikisha msechu anaondolewa nhc. "baadhi ya viongozi na wabunge wamesimama kidete kuhakikisha msechu harudi na hiyo inatokana na ukweli
kwamba, hawakubaliani na misimamo ya mkurugenzi huyo ya kuhakikisha haki inatendeka katika kupata nyumba za shirika hilo," kilisema chanzo kingine.

Alipotafutwa profesa tibaijuka ili kuzungumzia hatma ya msechu, simu yake ya mkononi haikuweza kupatikana. Hivyo juhudi za kumtafuta zinaendelea ili
aweze kutoa ufafanuzi wa taarifa hizo. Pia, mchecu naye alipotafutwa kuzungumzia taarifa za vyanzo hivyo, simu yake ya mkononi iliita bila
kupokelewa.

Chanzo: Jamboleo
 
Definition ya kijana kwa watanzania inaishia miaka 45 kwa hiyo bado ni kijana. Inategemea na namna unavyomchukulia. Ila kwangu mimi Mchechu ni Kijana mchapa kazi ambaye hata wewe sidhani kama unaweza kumfikia "let alone achieving his credentials with experience". Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
Acha UONGO!

Ukomo wa ya kijana Tanzania ni Miaka 35, na hilo utaliona kila Mahali hata kwenye kuomba kazikama wanatafuta kijana watakwambia mwisho Miaka 35 juu ya Hapo SIYO kijana tena!
 
Huyu Mchechu amekaa safi sana kwa maendeleo ya taifa ila kama kuna rafiki yake Rizmoko anahitaji nafas hiyo nabidi tumsahau, au pengine ni wale wajajanja waliokuwa wanauza nyumba hz kimya au kuingia mikataba mibovu ya kujenga pamoja, kama ile ya BMTL na NHC au Kuuzwa kama walivyouza Saramanser Hotel kwa Manji.

Huenda kuna mkono wa wahnd wa Upanga waliojichukulia majumba kwa muda mrefu wakajifanya yao, hawa kwa rushwa ni hatare, utakuta "'Wabodeeee !Bhana Bhana toa hii chechu taka chechua sisi tuingie uswazi bakati nyumba zilikuwa za mababu zetu bhana skia" hapo wana Body ndio bwana BHANJI kan
 
KASI ya utendaji kazi ya Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Msechu imesababisha aundiwe zengwe kwa lengo la kutaka ang’olewe nafasi hiyo.

Jambo Leo, limeelezwa kuwa, tayari Msechu amepewa masharti mazito na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo, yakiwamo ya kumtaka apunguze wakurugenzi wake katika idara mbalimbali.

Wakati hayo yakiendelea, imeelezwa kuwa Msechu alipewa likizo wakati akitafakari masharti aliyopewa na bodi hiyo, inatokana na kumaliza muda wake, kabla ya kuingia naye makubaliano mengine ya kulitumikia shirika hilo, kazi ambayo ameifanya kwa uadilifu na uamifu wa hali ya juu.

Msechu ambaye alilikuta shirika hilo katika hali mahututi na kutumia nafasi yake kupanga safu ambayo imerudisha heshima ya NHC kwa kuendelea na miradi ya ujenzi wa nyumba za kisasa na bei nafuu kwa ajili ya Watanzania, ameonekana kutofurahisha wale ambao hawapendi shirika hilo lifanye kazi yake kwa maslahi ya taifa.

Vyanzo vya kuaminika vimeliambia Jambo Leo kwa nyakati tofauti kuwa, Msechu kwa sasa amemaliza mkataba wake wa kulitumikia shirika hilo na
kinachosubiriwa ni Serikali kupitia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kumuidhinisha tena ili aweze kuendelea.
Hata hivyo, wakati anasubiri kuidhinishwa tena, mizengwe imeendelea kufanywa na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo.

“Kwa sasa kinachoonekana ni kama vile kumuundia zengwe Msechu ili asiendelee katika nafasi hiyo ambayo ameifanya kwa uamunifu mkubwa. Kuna baadhi ya wajumbe wa bodi wanaotaka asirudi na ndiyo wanaochelewesha kumuidhinisha.
“Wameamua kumpa masharti mazito katika kipindi hiki wakitaka atafakari, na moja ya masharti hayo ni kwamba, apunguze idadi ya wakurugenzi wake kwenye
idara, huku pia wakitaka apunguze mishahara ya watumishi wake.

“Yote hiyo ni kutaka kumvunja nguvu ili mikakati yao itimie. Sababu za msingi za kutoa masharti hayo hazipo, bali kinachoonekana utendaji wake wa kazi kwa kiwango cha kutukuka ndiyo unaosababisha wasiopenda mafanikio ya Rais Jakaya Kikwete, wamchukie na kumtengenezea mazingira ya kumweka kwenye wakati mgumu,” kilisema moja ya chanzo cha taarifa hizo (jina tunalo).

Imeelezwa kuwa, kutokana na mambo yanayoendelea dhidi ya Msechu, ndiyo maana hata Rais Kikwete alipokuwa kwenye ziara yake mkoani Tanga, hakwenda zaidi ya kutuma mwakilishi wake.Pia, Msechu ameshindwa kwenda kwenye maeneombalimbali ya miradi ya NHC inayoendelea sasa, na hiyoyote ilitokana na ukweli kwamba, hajafahamu hatma yake ndani ya shirika hilo.

Wakati hayo yakiendelea, utendaji kazi wa Msechu umekuwa gumzo katika maeneo mbalimbali nchini na hiyo yote ni kutokana na kazi nzuri ambayo ameifanya ya kulitumikia taifa na kurudisha hadhi yake ambayo ilipotea. Rais Kikwete mara kadhaa amekuwa akizungumzia mafanikio ya shirika hilo ambayo yameletwa na Msechu kwa kushirikiana na wakuu wake wa idara na watumishi wengine.

Hotuba za Msechu ambazo amekuwa akizitoa katika maeneo mbalimbali wakati wa uzinduzi wa miradi ya ujenzi, amekuwa akiweka wazi ushirikiano uliopo kati
yake na watumishi wengine, ni sawa na timu ya Real Madrid au Barcelona ambazo zinapokuwa uwanjani zinafanya kazi moja tu, ya kuhakikisha zinafanikiwa
kushinda.

Pamoja na hayo, imefahamika kuwa baadhi ya viongozi na wabunge ambao wamekuwa wakitumia shirika hilo kuweka ndugu, marafiki na jamaa zao wapo kwenye
mkakati wa kuhakikisha Msechu anaondolewa NHC. “Baadhi ya viongozi na wabunge wamesimama kidete kuhakikisha Msechu harudi na hiyo inatokana na ukweli
kwamba, hawakubaliani na misimamo ya mkurugenzi huyo ya kuhakikisha haki inatendeka katika kupata nyumba za shirika hilo,” kilisema chanzo kingine.

Alipotafutwa Profesa Tibaijuka ili kuzungumzia hatma ya Msechu, simu yake ya mkononi haikuweza kupatikana. Hivyo juhudi za kumtafuta zinaendelea ili
aweze kutoa ufafanuzi wa taarifa hizo. Pia, Mchecu naye alipotafutwa kuzungumzia taarifa za vyanzo hivyo, simu yake ya mkononi iliita bila
kupokelewa.

Chanzo: JamboLeo

Daaa watu wana zengwe daa haya someni link hiyo iliyotoka leo http://www.nhctz.com/kit/Press_release2.pdf
 
Hilo zengwe lazima wahindi wanahusika hawamtaki jamaa hapo Nhc
 
Kuwa na miradi mingi ya ujenzi ni kweli ipo ila kuna maswali mawili
user-online.png
mhalisi unatakiwa kuongeza kwenye hoja yako (1) Is there Value for Money for ongoing projects in other words can you buy a two bed rooms at TZS 100 million? and (2) How is NHC performance as far as operating cash flows is concerned?
user-online.png
mhalisi
 
Kuna story nilisikia kama two weeks ago kwamba kuna ubadhirifu jamaa kafanya kupitia Wakurugenzi wa idara na Mameneja wake Mikoani na kuna ushahidi kibao umeshapelekwa vyombo vya juu, ikiwemo wizara ya ardhi. Ni vitu ambavyo vilinishtua coz binafsi Mchechu is my Role Model.....kaipaisha sana NHC.

Anyway, huenda ni majungu tu!
 
Toka Msechu akate jina langu kwenye final 3 list ya interview ya Ukurugenzi pale NHC sina hamu naye kabisa.huyu hafai kabisa na kweli bodi imefanya jambo la maana sana ..mpaka mke wa Ridhiwani eti ni mkurugenzi wa sheria NHC !!!!! mxxxxxxx aende zake na asirudi kabisa ..Kwanza si kawa mwenyekiti wa bodi kule serengeti breweries anataka nin tena na liupara lake lile?
 
watu wanaropoka tu wala hawajui operation modal ya nhc, hili shirika sasa hivi linaendeshwa kibiashara linadaiwa mikopo ya bank (mortgage finance) kama bishara nyingine zozote zile. Sasa nyie mkitaka liendeshwe kama lile la zamani you are wrong.

baelezee
 
Mimi rafiki yangu naona kama kichwa chako ni kidogo sana sana, eti mwisho wa siku anatakiwa kujuwa vision ya shirika ni kuwasaidia watanzania na si kuwanyonya. Kwahiyo huko nyuma shirika limeshawahi kuwasaidia watanzania? wewe una mjomba wako hata mmoja alikuwa anaweza kupata nyumba ya NHC???

Unaongelea kodi ya fremu kupanda mpaka laki tatu mpaka nne, utakubaliana na mimi kwamba huko nyuma hata kodi ingekuwa shs milioni mbili usingeweza kupata??? Unataka kuniambia kwamba zamani ili upate nyumba ya NHC lazima utoe kilemba????? Kwa hapa Arusha maeneo ya Goliondoi kilemba si chini ya milioni 40 kitu ambacho Nehemia ameondoa.

Acha mambo ya kijinga bwana kama hujui historia ya shirika kaa pembeni kwenye hii mada. Big up Nehemia and the team

Bwn Msoma anayo point
hivi wangapi wanaishi au wanajua kodi ya sasa ya nyumba za NHC, hilo siyo shirika binafsi hivyo kuna vitu ambavyo lazima viwe considered.
NHC chini ya mchecu inachaji gharama ya kuchonga barabara, kuweka nguzo, mabomba ya maji n.k vyote vinawekwa kwenye bei ya nyumba au kodi hiyo bado mnaona sawa?

Ajibu hizo zilizo semwa hoja, au waziweke wazi tuzijue

SP
 
Back
Top Bottom