Mchango wa Dr. Slaa Bungeni June 16, 2010

wakati mwingine kunaitajika ili iwepo heshima serikalini
Big up TBC
Kwa maslah ya watanzania
 
Mnakumbuka last time ktk BUNGE alikuwa anapiga nyundo kisha TBC wakazima mitambo?

Mnyika akiingia bungeni tutakuwa na nyongeza ya wawakilishi makini

Serikali na Watanzania itambue kuwa hawa wanaowaita wapinzani si wapinzani wa maendeleo bali ni fikra mbadala kwa kuendeleza gurudumu la maendeleo na ustawi wa nchi yetu mbele.

Ninawaunga mkono wapinzani makini yes.

ushawahi kuona mbinguni ukiwa dunian
ur welcome...msubiri dodoma
 
Dr. Slaa angekuwa ananunulika wangemnunua siku nyingi tena kwa gharama yoyote maana anawasumbua vichwa. Lakini waelewe mbinu zozote za kumzimisha ndizo zinafanya azidi kupanda juu kisiasa zaidi, sasa hivi hata watanzania vijinini wanamuanini kupita kiasi.
 
labda ilikata maramoja na kurudi wakati anaanza, kwani mimi nimeisikiliza sehemu kubwa ya hotuba hiyo kwenye TBC mpaka anamaliza mida ya mchana hivi.

ilikuwa nzuri sana na alionyesha kipengele kwa kipengele namna serikali isivyokuwa makini kwenye maeneo mbalimbali. Thanks Invisible kwa kutupa doc nzima
 
labda ilikata maramoja na kurudi wakati anaanza, kwani mimi nimeisikiliza sehemu kubwa ya hotuba hiyo kwenye TBC mpaka anamaliza mida ya mchana hivi.

ilikuwa nzuri sana na alionyesha kipengele kwa kipengele namna serikali isivyokuwa makini kwenye maeneo mbalimbali. Thanks Invincible kwa kutupa doc nzima
Basi inawezekana waliokata matangazo sio TBC bali king'amuzi, kama unauhakika uliisikia hotuba ya Dr. Slaa mwanzo-mwisho, then ni kingamuzi changu, naiomba msamaha TBC , na kwa niaba ya wale wote walioilaumu.
 
Basi inawezekana waliokata matangazo sio TBC bali king'amuzi, kama unauhakika uliisikia hotuba ya Dr. Slaa mwanzo-mwisho, then ni kingamuzi changu, naiomba msamaha TBC , na kwa niaba ya wale wote walioilaumu.

sikuanza mwanzo, kuna sehemu nilikuwa napita nikaona hiyo hotuba ya Mh Slaa ikabidi nikae niisikilize mpaka mwisho.
ilikuwa ni connections za kawaida na si king'amuzi
 
Nduguzanguni msiwe wepesi kunyooshea kidole kila kitu. Hii haileti picha nzuri na ni dalili ya kukosa umakini, uzulumishi na fault finding.
 
Wakuu,

Jamani mmeweza kuupitia mchango wa Dr. Slaa vizuri?...

Nimewahi kuwaambia kwama Mkapa alivurunda kabisa ktk Ukusanyaji wa kodi na Ukimsoma Dr.Dlaa toka kifungu cha 39 mtachoka wenyewe... Yaani Serikali inakusanya kodi zake toka Wafanyabishara wasiozidi 570,000 (wenye TIN) na kati ya hawa asilimia 75 wanatoka Dar es Salaam kisha kodi ya Wafanyakazi wa serikali na sekta binafsi wasiozidi 1,000,000.

Duh! yaani nchi nzima wananchi walipa kodi hawafiki millioni 2 na hawa ndo wanabeba mzigo woote - I knew something was very wrong!

Je, hii kweli inaonyesha ufanisi ktk muundo wa kukusanya kodi? Nambieni mnaosifia pengine kuna kitu sikuwahi kukiona...
 
Wakuu,

Jamani mmeweza kuupitia mchango wa Dr. Slaa vizuri?...

Nimewahi kuwaambia kwama Mkapa alivurunda kabisa ktk Ukusanyaji wa kodi na Ukimsoma Dr.Dlaa toka kifungu cha 39 mtachoka wenyewe... Yaani Serikali inakusanya kodi zake toka Wafanyabishara wasiozidi 570,000 (wenye TIN) na kati ya hawa asilimia 75 wanatoka Dar es Salaam kisha kodi ya Wafanyakazi wa serikali na sekta binafsi wasiozidi 1,000,000.

Duh! yaani nchi nzima wananchi walipa kodi hawafiki millioni 2 na hawa ndo wanabeba mzigo woote - I knew something was very wrong!

Je, hii kweli inaonyesha ufanisi ktk muundo wa kukusanya kodi? Nambieni mnaosifia pengine kuna kitu sikuwahi kukiona...

Mie pia nimeiona nikapigwa na bumbuwazi
 
ancient philosophers and religious figures of past have pondered about this question: why do bad things happen to good people? Now we probably have a clue.... CCM could be one of the reasons!
 
Asante kwa kuweka hotuba ya Mheshimiwa Slaa hapa. Nimeisoma yote na ikanikumbusha kitabu cha Bw Maliti 'Honest to my Country'. Dr Slaa ni mwaminifu kwa nchi yake. Ana uchungu, anajua na anasema na haogopi!
 
Hii hotuba ya Dr Slaa ni nyundo kama Serikali ingekuwa sikivu naamini wangeyafanyika kazi yaliyoongelewa humu..Halafu mimi huwa naishangaa hili Bunge letu mara nyingi hoja za wapinzani huwa hazifanyiwi kazi.Kwanini sasa kuna kambi ya Upinzani Bungeni?na Role yao no nini hasa kama Bunge halijali uwepo wao?hivi kazi yao ni kuwasikiliza tu?
 
1st post updated, tumepata nakala toka kwa Dr. Slaa

Mkuu Asante sana.
Ukiisoma hii dossier utaelewa kwa nini TBC kumekuwa na "pattern" au technical problem!!
Hivi tutaanza lini kuwa serious na usimamizi mzuri wa public funds? Data za Dr; zimeonyesha wazi jinsi bajeti ilivyokuwa kichekesho kwa macho ya wenye kuona, maana mwanachi wa kawaida hawezi ona haya yote!!

Serikali bado domo zito over meremeta, kagoda, Tangold etc. Mweh...
 
Katika mengi nimeshtushwa pia na serikali kununua samani kila mwaka.!!!!!! Nadhani itakuwa ni manunuzi hewa
 
Katika mengi nimeshtushwa pia na serikali kununua samani kila mwaka.!!!!!! Nadhani itakuwa ni manunuzi hewa

Ni jambo la kawaida katika taasisi za serikali! Zile za mwaka jana zinaweza zikatolewa zikawekwa nje zikanyweshewa mvua miaka nenda rudi au kwenye ghala. Furnishing a director's house can cost up to Tshs 25m and you can imagine the rest. Dr Slaa ameweza kusemea hili, lakini mimi na wewe ingawaje tunayaoona hatukuweza kufungua mdomo. Kumbe na mimi ni BURE kabisa kwa nchi yangu, na wewe pia; sasa TUSIJISAHAU TENA.
 
Nimeisoma yote ni nzuri isiyo mfano.

Anatoa tafsiri hii kuhusu kilimo:
Anasema mwaka 2009/2010 Wizara ya Kilimo ilitengewa Jumla ya Tshs 92,694,254,000 na mwaka 2010/2011 imetengewa Tshs 103,952,371,000.


Lakini mwaka 2009/2010 Dola ya Marekani ilikuwa inabadilishwa kwa $1= Tshs 1200, leo $ 1 ni sawa na Tshs 1,450 Hivyo uwezo na nguvu ya manunuzi ya Shillingi imeshuka kwa zaidi ya Tshs 250 hivyo kwa fedha hizo kazi unazofanya inaweza kufanana na zile za mwaka jana au hata chini ya hapo.

Kwa tafsiri rahisi budget ya kilimo imeongezeka kwa 11.2% lakini thamani ya pesa imeshuka kwa 12%. kwa maana hiyo budget ya kilimo kwanza ya mwaka huu purchasing power yake ni ndogo kuliko ya mwaka jana.
 
Nimeisoma yote ni nzuri isiyo mfano.

Anatoa tafsiri hii kuhusu kilimo:
Anasema mwaka 2009/2010 Wizara ya Kilimo ilitengewa Jumla ya Tshs 92,694,254,000 na mwaka 2010/2011 imetengewa Tshs 103,952,371,000.


Lakini mwaka 2009/2010 Dola ya Marekani ilikuwa inabadilishwa kwa $1= Tshs 1200, leo $ 1 ni sawa na Tshs 1,450 Hivyo uwezo na nguvu ya manunuzi ya Shillingi imeshuka kwa zaidi ya Tshs 250 hivyo kwa fedha hizo kazi unazofanya inaweza kufanana na zile za mwaka jana au hata chini ya hapo.

Kwa tafsiri rahisi budget ya kilimo imeongezeka kwa 11.2% lakini thamani ya pesa imeshuka kwa 12%. kwa maana hiyo budget ya kilimo kwanza ya mwaka huu purchasing power yake ni ndogo kuliko ya mwaka jana.

Point yake ni nzuri sana ingawa mfano huo wa viwango vya kubadilishia fedha ulioutoa hapo juu una kasoro. Kwa kifupi katika kipindi cha miaka miwili (2007 mpaka Nov 2009) uwezo wa manunuzi wa shilingi mia moja ulipungua hadi kufikia shilingi 87 ( takwimu hizi na grafu yake nilishaweka hapa wiki kadhaa zilizopita kipindi kile cha sakata la TUCTA na hizi ni takwimu ni za kutoka NBS).

Hoja za waheshimiwa kama Zitto na Slaa zinaonyesha ukomavu wa hali ya juu katika haya maswala ila tatizo ni hao wavivu wa CCM wanaojaza nafasi huko Bungeni. Bajeti hii ni busu la mauti.
 
Point yake ni nzuri sana ingawa mfano huo wa viwango vya kubadilishia fedha ulioutoa hapo juu una kasoro. Kwa kifupi katika kipindi cha miaka miwili (2007 mpaka Nov 2009) uwezo wa manunuzi wa shilingi mia moja ulipungua hadi kufikia shilingi 87 ( takwimu hizi na grafu yake nilishaweka hapa wiki kadhaa zilizopita kipindi kile cha sakata la TUCTA na hizi ni takwimu ni za kutoka NBS).

Hoja za waheshimiwa kama Zitto na Slaa zinaonyesha ukomavu wa hali ya juu katika haya maswala ila tatizo ni hao wavivu wa CCM wanaojaza nafasi huko Bungeni. Bajeti hii ni busu la mauti.

Mkuu kutoka Tsh 100 kwenda Tsh 87 ni punguzo la asilimia 13 na data zake zinaonyesha ni asilimia 12.1 statistically si mbali sana.
 
Abdulhalim,

Thanks.

Waziri Mkuu alizungumza kwa zaidi ya saa 1 na Waziri wa Nchi naye akazungumza kwa takriban Saa 1. Mimi nilipewa Dk 30 kujibu hotuba ambaye kimsingi tumekuja kuiona ukumbini.

Hivyo kwa kuwa nilikuwa ninajua kuwa nina dakika 30, baada ya Kitabu cha Waziri Mkuu kugawiwa ndani ya Ukumbi, nikapaswa kufanyia review ile ya kwangu ili kujibu baadhi ya hoja ambazo hatukuwa tunazifahamu kabla. Hiyo ndiyo iliyofanya Summary yangu pia nisiweze kumaliza.

Watu wengi hawajui kuwa Hotuba zote za Kambi ya Upinzani zinaandikwa bila kujua Waziri atakuja kuzungumza nini, hivyo tunafanya Research sana, na hasa kwa kutumia indicators mbalimbali na Past Speeches ndio tunaandaa hotuba zetu.

Tunapopata vitabu vya Serikali kama nafasi inaturuhusu ndio tunachomeka yale muhimu ambayo hatukuwa nayo awali. La msingi ni kuwa siyo fair, Waziri Mkuu na Waziri wa Nchi kuzungumza kwa saa mbili, na anayetoa upande wa pili wa shilingi kuwa na nusu saa tu. Haya ni baadhi ya mabadiliko ya msingi ambayo yanahitajika iwapo tuko serious na tunatambua umuhimu wa kusikia upande wa pili. Vinginevyo utapata upande wa pili 'seriously watered down kwa sababu ya technicality ya muda.

Nawashukuru wana JF kwa interest na kwa kufuatilia kwa kina kiasi hicho.
 
Back
Top Bottom