Mchango wa Dini katika ustawi wa maisha ya Binadamu

Mchango wa Dini katika ustawi wa maisha ya Binadamu

Naam, naam.

Nimejitahidi sana kusoma dini.Binafsi nyumbani kwa mzee wangu alipotokea ni kanisani. Kwa kuwa baba yake alikuwa mchungaji.
Kwa hivyo, yeye alikuwa si tu anaenda kanisani, bali aliishi kanisani.

Nimejitahidi kusoma Ukristo, Uislamu, Uyahudi, Uhindu, Ubuddha, na dini nyingine nyingi.

Dini kwa upande mmoja, ni kitu kizuri sana. Inarudisha watu kwenye mstari wa kuishi kwa upendo, kukataza mabaya, kuhimiza mema na kumtofautisha mtu na hayawani.

Upande huu wa dini naupenda sana.

Ila, pia, dini ina upande mwingine, mbaya. Wa kubaguana, kuona watu wa dini yako ndio wenye ukweli na wengine wapotofu, kuhalalisha mambo mabaya kwa kigezo cha dini, vita vya kidini, dini kutumika kama siasa, dini kutumika ku manipulate watu kwa uongo, dini kupinga maendeleo ya elimu na kudumaza fikra za watu kwa ujinga, na mambo kem kem kama hayo.

Kiukweli, dini ni nyenzo, kama moto.

Moto si mzuri wala mbaya. Moto upo tu.

Jinsi gani unautumia moto ndiyo inaweza kuwa nzuri au mbaya.

Unaweza kuutumi moto kupika chakula watu wakala wakashiba. Hapo moto umetumika vizuri.

Moto huo huo, unaweza kuutumia, ukaunguza nyumba, ukaua watu. Hapo moto umeutumia vibaya.

Vivyo hivyo kwenye dini.

Unaweza kutumia dini ukawaunganisha watu, ukapunguza uhalifu katika jamii. Hapo umeitumia dini vizuri.

Unaweza pia kutumia dini kuwagawanya watu, ukaanzisha vita ya kidini, watu wakauana kwa mamilioni. Hapo umeitumia dini vibaya.

Dini kama dini haina maana. Si mbaya wala nzuri. Maana ya dini unaipa wewe muumini.

Moto kama moto si mbaya au mzuri. Ubaya au uzuri wa moto unakuja kulingana na mtumiaji anavyoutumia.
Mkuu napenda sana unavyo tudadavulia mada ngumu Kama hizi
 
Tunaongelea dini hatuongelei watu wa Dini. Kwani Dini gani katika hizi dini zinazo amini uwepo wa Mola muumba zinafundisha unafiki, uzinzi, uongo,kupiga dili, uchawi ?
Uko sawa ila kuna hili la Ubaguzi dhidi ya imani nyingine. Ukisoma baadhi ya mistari ya vitabu hivyo vya dini utayaona hayo.

Na jambo hilo la ubaguzi wa dini moja kujikweza dhidi ya nyinginezo limechochea chuki na hata mauaji.
 
Uko sawa ila kuna hili la Ubaguzi dhidi ya imani nyingine. Ukisoma baadhi ya mistari ya vitabu hivyo vya dini utayaona hayo.

Na jambo hilo la ubaguzi wa dini moja kujikweza dhidi ya nyinginezo limechochea chuki na hata mauaji.
Sasa iweje Mola ni mmoja halafu Dini ziwe nyingi ? Ujue hapo lazima Dini moja ni sahihi na hizo nyingine na fikra za watu kama vile Ubudha, Uhindu, Upagani (Naturalism) , na mfano wao.
 
Sali Sana brother, nina uhaukika uhuni na maisha niliyoyaishi,hata nusu hutafika,ila ni Mwenyezi Mungu anayejua,sali sana nasema tena sali sana...safari ya Kristo kuikomboa dunia sio historia,na ni mwendelezo, nashukuru Kristo alitufikia,ingawa waliotuletea habari njema walikuwepo wazuri na wabaya pia(agents of colinialism).Ila tunashukuru ,Sali sana na ukamuegemee Kristo Mfalme wa wafalme.
Unasali ili upate nini?,maana kuna wengine wanasali wapate toyota tako la nyani 😁😁,wengine wapate hela
 
Bila shaka ni kiarabu sivyo?
Nakupa maana nyingine ni hii :

Nanukuu : "Maana ya dini kwa mtazamo wa fani ya Elimu ya jamii: “dini ni idadi maalumu ya itikadi, matendo, alama pamoja vitengo vya kidini ambavyo vimejengwa na wanajamii ndani ya jamii mbali mbali”. Imenukuliwa kutoka kwa Talcott Parsons."
 
Kijana mbona una ruka ruka sana. Kwani Dini kwa Kiswahili ni nini mzee ?

Siyo Kiarabu.

Pili, unapo sema Kiarabu una maanisha ya kuwa Kiarabu kinakosea au Kiarabu siyo Lugha au nini ? Nieleweshe hapo maana naona umeanza kuogopa mapema sana.
Nigeuzie hii kwa kiswahili, najua we ni expert kwenye kiarabu Huwezi shindwa



الإيمان بعبادة قوة خارقة مسيطرة ، خاصة إله شخصي أو آلهة.
al'iiman bieibadat quat khariqat musaytirat , khasat 'iilah shakhsiun 'aw alihat.
 
Nakupa maana nyingine ni hii :

Nanukuu : "Maana ya dini kwa mtazamo wa fani ya Elimu ya jamii: “dini ni idadi maalumu ya itikadi, matendo, alama pamoja vitengo vya kidini ambavyo vimejengwa na wanajamii ndani ya jamii mbali mbali”. Imenukuliwa kutoka kwa Talcott Parsons."
Elimu ya jamii ni nini?
 
Nigeuzie hii kwa kiswahili, najua we ni expert kwenye kiarabu Huwezi shindwa



الإيمان بعبادة قوة خارقة مسيطرة ، خاصة إله شخصي أو آلهة.
al'iiman bieibadat quat khariqat musaytirat , khasat 'iilah shakhsiun 'aw alihat.
Sijui maana yake.
 
Sasa iweje Mola ni mmoja halafu Dini ziwe nyingi ? Ujue hapo lazima Dini moja ni sahihi na hizo nyingine na fikra za watu kama vile Ubudha, Uhindu, Upagani (Naturalism) , na mfano wao.
Hilo la Usahihi wa dini moja ni tafasiri yako moyoni na imani yako. Kila mmoja ataona dini yake ni sahihi.

Jamii zetu ni tofauti, historia, tamaduni na mazingira. Dini ni 'social construct' tokea enzi hapajawahi kuwa na dini moja na sidhani kama itatokea iwe hivyo.
 
Dini imepeleka huduma kama hospitali na mashule, umeme, barabara, usafiri hasa huko vijijini ndanindani.

Kuna vijiji nilienda miaka fulan walikua hawana usafir kabisa ukitaka kusafir unamngoja padre aje jumapili kusalisha hlf unaomba lifti akuache tauni.
Nakurudi?
 
Sijui maana yake.
Icheki na hii kutoka kwenye kamusi kuu ya kiswahili
IMG_20201006_230552_914.JPG
 
Tunaongelea dini hatuongelei watu wa Dini. Kwani Dini gani katika hizi dini zinazo amini uwepo wa Mola muumba zinafundisha unafiki, uzinzi, uongo,kupiga dili, uchawi ?

Unawezaje kutenganisha dini na watu wa dini? Kuna dini isiyo na watu?
 
Nakuongezea na maana nyingine hii toka "Wikipedia".

Nanukuu :

Dini (kutoka Kiarabu اﻟدﻴن, tamka: ad-din) inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji.
Sasa hii ndio maana halisi ya dini na sio ile yakihuni kutoka uarabuni uliyoiweka awali
 
Swadakta..

Na wachina wanawapiga jamii ya waislam wa Uyghur huko kwao

Waislam na wakristo ndio vinara wa vita za kidini duniani, na hili halijaanza leo. Ndio maana nimesema vita karibu zote za kidini lazima utakuta ni ama mkristo na muislamu, au mojawapo kati ya dini hizo mbili vs dini nyingine.
 
Hilo la Usahihi wa dini moja ni tafasiri yako moyoni na imani yako. Kila mmoja ataona dini yake ni sahihi.

Jamii zetu ni tofauti, historia, tamaduni na mazingira. Dini ni 'social construct' tokea enzi hapajawahi kuwa na dini moja na sidhani kama itatokea iwe hivyo.
Kwa akili ya kawaida tu, zinaweza vipi dini nyingi zote zikawa sahihi ?
 
Back
Top Bottom