Jifunze kunukuu hoja kwa ukamilifu, nitakuuliza baada ya kukupa unachostahiki, vioi hoja yako sikuidhoofisha ?
Ad Hominem inahusu hoja nzima mwanzo mpaka mwisho. Nakuonyesha sasa ya kuwa wewe umejenga "Strawman Argument". Nilipo muuliza muulizwaji swali la "Je unaamini nini juu ya chanzo cha ulimwengu". Aidha kwa kutokujua kwako (Hili nina hakika zaidi) ukajenga hoja mfu juu ya kile nilicho uliza,kisha ukauliza "Kwanini nimemsetia niliye muuliza swali katika mlengo wa kiimani" (Au kama ulivyo andika). Hii ni hoja mfu ambayo kiuhalisia hailengi nilicho muuliza niliye muuliza, badala yake ukaunda swali ambalo kiuhalisia halipo ili kudhoofisha ni"icho kiandika. Mfano wa swali lako mfu (Strawman Argument) ni kama walimu wawili hawa :
Mwalimu A : Inabidi tuwawekee wanafunzi wetu ratiba nzuri na kuwafundisha kwa bidii ili wapate kufaulu vizuri masomo yao.
Kisha mwalimu B anajengs hoja mfu kwa mwalimu A ili adhoofishe hoja yake.
Kisha...
Mwalimu B : Hatuwezi kuruhusu A zipatikane kizembe zembe sisi.
Huu sasa ndiyo mfano wa "Strawman Argument" ambao unaukuta katika swali lako, yaani nauliza swali kulia unaleta hoja mfu kulazimisha ya kuwa nimekusudia kushoto.
kwanza sio kweli kwamba ad hominen inahusu hoja nzima mwanzo mpaka mwisho kama wewe unavyopotosha. Ad hominiem haigusi hoja bali ni shambulio binafsi (persnal attack) au ("Poisoning the Well") kumshambulia mpinzani aliyeleta hoja badala ya kujikita kuijadili hoja yenyewe.
Strawman inajihusisha katika disproving against opponent arguments kwa kuzidisha (misrepresented) maneno au kutia chumvi, yatakayo mpa urahisi mpinzani kurahisisha hoja za upande unaopinga kwa kum critique. Hizi ni hoja ambazo zinakua na conclusion inayo finalize kua opponent hayuko sahihi
Mara nyingi ni watu ambao wanakuwekea maneno mdomoni ambayo wewe hukuyasema wala kuyaandika kisha kupitia hayo hayo maneno waliyoweka wanaanza kutengeneza njama kukuonesha hoja yako ni potofu
Mfano ni huu, kumiliki silaha kwa ajili ya kujilinda ni jambo zuri
We unakuja kusema, aah sio kweli nina ushahidi katika hilo silaha zinatumiwa na majambazi kuua watu kila siku matukio ya kihalifu yanafanyika na watu wanaomiliki silaha hivyo umiliki wa silaha ni jambo la hatari na sio zuri
Sasa wewe umeuliza swali kua unaamini nini juu ya uwepo wa mbingu? Mimi nikaona swali lako umelilengesha kwenye majibu unayoyataka wewe umetengeneza hoja kwa kutumia assumption kwamba jibu lake ni lazima liwe katika imani pekee when actually seems there are several
Swali langu la mimi kukutaka wewe ufafanue kwanini ulitumia imani kama ndio nguzo ya kupewa jibu halipo kwenye strawman argument wala logical fallacy yeyote ile kwasababu kwanza swali langu linakutaka uinyambue hoja yako ieleweke vizuri.
Pili strawaman ina deal kwenye kupandikiza maneno ya uongo ambayo na kuhitimisha kua kilichodaiwa na opponent ni uongo.
Mimi sijakuzushia maneno ya uongo ambayo hujayaandika hapo, bali nimeuliza swali, sijahitimisha kwamba wewe ni muongo kwa ku twist maneno ambayo nimeyapachika ili kunipa urahisi wa ku-shut down hoja yako. Sasa hapo utasemaje swali langu linalokutaka ufafanue ulichokiuliza ni strawman argument?