TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 6,551
- 20,259
Naam, naam.
Nimejitahidi sana kusoma dini.Binafsi nyumbani kwa mzee wangu alipotokea ni kanisani. Kwa kuwa baba yake alikuwa mchungaji.
Kwa hivyo, yeye alikuwa si tu anaenda kanisani, bali aliishi kanisani...
Nakubaliana na uliyoyasema, na kwa mtazamo wangu, ili dini itumike vizuri ni lazima wale wanaoitumia wawe na upeo fulani wa uelewa, na kiwango fulani cha maendeleo.
Mimi hua nafananisha dini na filosofia zingine kama vile "demokrasia". Kwa watu wenye upeo mdogo, dini lazima itazusha mikingamo na vurugu kubwa sana, kama jinsi ambavyo demokrasia inazusha vurugu!
Ukishakua na watu wenye upeo mdogo wa kufikiri na kiwango cha chini cha maendeleo, uwezekano wa dini kutumika vizuri ni mdogo sana. Badala yake utaibuka uadui kati ya dini moja na nyingine, watu watatengana, undugu utavunjika, vita zitatokea nk. Na pia watatokea wajanja wachache wataoitumia hii nafasi kujinufaisha kwa namna moja ama nyingine.