Mchakato Katiba Mpya: 44% wanasema maoni yao hayakuwekwa kwenye Katiba iliyopendekezwa

Hiyo siyo sahihi! Kumpunguzia rais madaraka kunamfanya rais afanye kazi kwa weledi na uaminifu zaidi. Sababu akifanya kinyume, wawakilishi wa wananchi na wananchi wenyewe waliomchagua ndiyo watamwajibisha. Hata kwa katiba mpya ataendelea kufanya vizuri kama rais ilimradi atafanya kazi yake kwa misingi ya sheria na katiba. Siyo kukurupuka tu hatutaki mambo hayo.
Ni hatari kumpunguzia Rais Madaraka. Ni hatari sana hasa kwa nchi zetu hizi.. Ni hatari kweli kweli.. Natamani ungenielewa!
 
katiba.jpg
RIPOTI YA TWAWEZA: Pale walipoulizwa nani anapaswa kuongoza mchakato wa mabadiliko ya katiba, mwananchi
mmoja kati ya watano (20%) anasema kuwa wananchi walipaswa kuongoza mchakato huo.

Mwananchi mmoja kati ya kumi (11%) anasema hivyo ndivyo ilivyokuwa. Vilevile, nusu ya wananchi (49%) wanasema Rais ndiye aliyepaswa kuongoza mchakato huo, wakati wananchi
wanne kati ya kumi (39%) wanasema Rais ndiye aliyeongoza mchakato huo.

Inashangaza kuona kuwa 26% ya wananchi hawafahamu aliyeongoza mchakato mzima wa kupata katiba mpya.
 
Kwan katiba mpya pale kwa chama rafiki(Jubilee) inawasaidia nn Wakenya hii iliyopo inatufaa kwa kizazi hiki makengeza!!!!!!#
 
Hivi Rais Magufuli amehusikaje kukwamisha mchakato wa Katiba?
Rais ndiyo mkuu wa serikali ya muungano wa jamhuri ya Tanzania sawa? Na serikali yake ndiyo inayotoa mikakati na vipaumbele vyote miaka yake 5 ikiwa madarakani. Hivyo yeye kama rais amewapa mawaziri wake majukumu na vipaumbele vya wizara zao..

1) Ulisikia bajeti ya wizara ya sheria na katiba ya mwaka huu na ujao wa fedha? Kifupi, hakuna mpango wala mkakati wa wizara hiyo ya kuendeleza mchakato wa katiba hiyo. Pro. Kabudi wala hakujibu swali alivyoulizwa kwa nini serikali haijetenga fedha za mchakato huo.

2) Kama rais angetaka kumalizia juhudi za rais mstaafu za mchakato wa katiba basi angefanya hivyo. Lakini hataki na ndiyo maana aliwaambia waandishi wa habari yeye hakuizungumzia katiba katika kampeni yake. Baada ya kuulizwa na swali na Paschal Mayala za mwendelezo wa katiba.

3) Swala la katiba ni swala la jukumu lake kuhakikisha linafanyika si swala la kuchagua sababu liko kwenye ilani ya CCM si ndiyo? Na CCM si wanasema mambo yaliyoko kwenye ilani yao ya uchaguzi yatekelezwe au?
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!

Hebu fafanua tunapigia kura ipi?

1. Ya ccm ambayo mzee sita nawezie walijitengeneze

Au

2. Ya wananchi kama ambavyo Mzee warioba avokusanya michango na mawazo yetu
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!

Sisi sio watoto wa kuandaliwa katiba na wanasiasa. Ww kwasababu uko vizuri kwani uko serekalini ndio ungojee uandaliwe taratibu za kazi.
 
Ni hatari kumpunguzia Rais Madaraka. Ni hatari sana hasa kwa nchi zetu hizi.. Ni hatari kweli kweli.. Natamani ungenielewa!
Siyo hatari ni vizuri kwa faida ya wananchi. Sasa mfano rais wa sasa anatumia baadhi madaraka kufanya mambo mazuri ambavyo ni sawa OK? Sasa ukimpata rais mwingine mfano fisadi na umeshampa madaraka mengi kama hayo utamfanya nini? Na mfano mdogo ni hata Magufuli mwenyewe kaanza kupinda katiba yenyewe sasa huo siyo utawala bora. Rais ni wa watanzania wote umeapa kutetea katiba ya jamhuri wa muungano sawa? Sasa mfano: Rais unawahukumu baadhi wa watanzania kwa kosa la kughushi vyeti na unamwacha mwingine eti kwa sababu ni mfanyakazi mzuri hata kama kaghushi vyeti! Kwani hata wale waliofukuzwa si walikuwa wafanyakazi wazuri pia.. It doesn't make any sense that is hypocrisy and very unfairly.
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!

kasome tena mchakato wakatiba ulivyo!

hiyo iliyopendekezwa ikikataliwa, bunge linaitishw atena then wanakwenda kukubaliana, then kura tena, ikkataliwa basi tunarudi ya zamani.
 
Rasimu ya katiba hii ni bora kuliko katiba ya sasa. Tatizo Rais Magufuli haitaki sababu anajua itambana na yeye pia kwenye majukumu yake na yeye hataki. Yuko hiari mabilioni ya pesa za walipa kodi zipotee kuliko kupatatika na kwa katiba hii. Sasa yeye kama mzalendo na uchungu wa rasilimali za watanzania. Kwa nini hana uchungu wa mabilioni ya haya yaliyotumika kwa mchakato wa katiba mpya?? Tena ni ya kwao CCM wenyewe?

Si kwlei rasimu ni mbovu tu. ni bora wasilete hiyo mpya, tupate sababu ya kudai mpya kuanzia kwa warioba, kuliko kuletewa mpya mbovu.
 
Hivi hawa twaweza wanapataje hiyo sample ya wanaoshiriki tafiti zao? Na ni wangapi wanahojiwa? Mbona wengine hatujawahi kushirikishwa hata mara moja? Usikute twaweza ni kampuni tanzu ya chama fulani na wanafanyia utafiti humo chamani
 
Dar es Salaam. Two out of three Tanzanians think that it is important for the country to get a new constitution, according to the views contained a new research brief by Twaweza issued October 19.


The brief, titled: Unfinished Business: Tanzanians’ views on the stalled constitutional review process, is based on data from Sauti za wananchi a nationally representative high-frequency mobile phone survey.

The findings are based on data collected from 1,745 respondents across Mainland Tanzania in June-July 2017.

Findings show that just over half of citizens (56 per cent) think that the final draft Constitution should be voted in a public referendum.

However, the survey further show that half of citizens (48 percent) believe that process to write a new major law will not happen within the next three years.

Eight out of ten want ministerial appointments to be confirmed by Parliament (79 per cent), and six out of ten want to be able to remove MPs between elections (64 per cent).

Read. Pressure mounts on State to revive Katiba review process
The Executive Director of Twaweza, Mr Aidan Eyakuze, said citizens want a new constitution.

“Many want to start with a new Commission and a clean sheet of paper. But others are willing to go forward with the draft from the last commission,” he said adding:

“They also support the accountability orientation of the original draft constitution and they are clear that they want a new, more inclusive process to move forward with.”

“It is telling that direct mention of UKAWA causes citizens to judge the boycott more harshly than they do when asked about boycotts in general. When it comes to their politics, citizens' passion often overwhelms their objectivity,’’ he added.

According to the survey, citizens are more divided on some accountability measures including stopping foreign bank accounts for leaders and civil servants (54 per cent in support), term limits for MPs (52 per cent in support), and having transparency and accountability as part of the core set of national values (48 per cent support).


Alongside strong views on content, nine out of ten citizens (91%) agree that both the process of creating the constitution and the content itself are important. While 2 out of 10 citizens (18%) remember being part of the constitutional review process, 4 out of 10 (44%) feel that the process was about collecting views that were not necessarily then reflected in the constitution and 2 out of 10 (23%) feel that the process was just about sharing information not collecting citizens’ views.
 
Binafsi naona mchakato wa katiba ulianza kupotezwa na jaji warioba mwenyewe kwa kuto heshimu maoni ya wengine. Mchakato ulikuwa na vipengele muhimu kadhaa, baadhi ni ukusanyaji wa maoni ya wananchi, kuyachambua, na lililokuwa la mwisho, ambalo ni muhimu kabla ya kupiga kura, ni bunge la katiba. Hapa ndipo babu alipotuyumbisha. Kazi kubwa ya bunge la katiba ilikuwa kuijadili rasimu ya katiba na SI KUIPITISHA. Sasa mzee Warioba na ukawa walitaka ipitishwe, jambo ambalo lilikuwa halileti maana ya kuwa na bunge la katiba. Ninavyojua mimi, majadiliano yanaweza kupunguza, kuongeza au kuondoa baadhi ya vitu. Hivi mnawezaje watu zaidi ya 300 kujadili kitu kimoja mkawa na mawazo sawa?
Kweli tunahitaji katiba mpya, ila kama mchakato utakuwa ni uleule wa kuwa na bunge, basi ni lazima tuheshimu mawazo ya bunge sababu kupeleka maoni yetu kule ina maanisha mawazo ya wananchi sio ya mwisho ila ya bunge la katiba.

Kwahiyo tusijitoe ufahamu wakujifanya kutokujua nafasi ya bunge la katiba.
NARUDIA TENA, KAMA TUNATAKA KATIBA YENYE MAWAZO YA WANANCHI PEKE YAO, BASI KUSIWEPO NA BUNGE LA KATIBA.
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!
Uwelewa wako ndogo au ni kibaraka wa kina Chenge unatetea ufisadi!!
 
Hiyo siyo sahihi! Kumpunguzia rais madaraka kunamfanya rais afanye kazi kwa weledi na uaminifu zaidi. Sababu akifanya kinyume, wawakilishi wa wananchi na wananchi wenyewe waliomchagua ndiyo watamwajibisha. Hata kwa katiba mpya ataendelea kufanya vizuri kama rais ilimradi atafanya kazi yake kwa misingi ya sheria na katiba. Siyo kukurupuka tu hatutaki mambo hayo.
Mkuu maoni mazuri .
CCM wasinyakuwe madaraka ya mchakato kama walivyofanya.
Mchakato uwe huru kwa maslahi ya taifa sio mtu au kundi la watu.
Rasimu bora ya Warioba ni jibu!!
 
Binafsi naona mchakato wa katiba ulianza kupotezwa na jaji warioba mwenyewe kwa kuto heshimu maoni ya wengine. Mchakato ulikuwa na vipengele muhimu kadhaa, baadhi ni ukusanyaji wa maoni ya wananchi, kuyachambua, na lililokuwa la mwisho, ambalo ni muhimu kabla ya kupiga kura, ni bunge la katiba. Hapa ndipo babu alipotuyumbisha. Kazi kubwa ya bunge la katiba ilikuwa kuijadili rasimu ya katiba na SI KUIPITISHA. Sasa mzee Warioba na ukawa walitaka ipitishwe, jambo ambalo lilikuwa halileti maana ya kuwa na bunge la katiba. Ninavyojua mimi, majadiliano yanaweza kupunguza, kuongeza au kuondoa baadhi ya vitu. Hivi mnawezaje watu zaidi ya 300 kujadili kitu kimoja mkawa na mawazo sawa?
Kweli tunahitaji katiba mpya, ila kama mchakato utakuwa ni uleule wa kuwa na bunge, basi ni lazima tuheshimu mawazo ya bunge sababu kupeleka maoni yetu kule ina maanisha mawazo ya wananchi sio ya mwisho ila ya bunge la katiba.

Kwahiyo tusijitoe ufahamu wakujifanya kutokujua nafasi ya bunge la katiba.
NARUDIA TENA, KAMA TUNATAKA KATIBA YENYE MAWAZO YA WANANCHI PEKE YAO, BASI KUSIWEPO NA BUNGE LA KATIBA.
Hilo bunge lilikuwa mkusanyiko wa taasisi na mafisadi wa CCM, wakitetea wizi wao kina Chenge.
Polepole leta mezani rasimu bora ya Mzee Warioba.
Tengeneza katiba bora ya Watanzania.
Hila mbinu chafuu
hazitatusaidia!!
 
Back
Top Bottom