Mchakato Katiba Mpya: 44% wanasema maoni yao hayakuwekwa kwenye Katiba iliyopendekezwa

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138


Utangulizi Mchakato wa kurekebisha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulianza baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Vyama viwili vikuu vya upinzani nchini, CHADEMA na CUF ndivyo vilivyoanzisha vugu vugu ya kudai katiba mpya.

Umuhimu wa katiba mpya ndio ulikuwa msingi wa kampeni za uchaguzi za vyama hivyo. Rais Jakaya Mrisho Kikwete, aliitikia wito huo kwa kuanzisha mchakato wa marekebisho ya Katiba. Hata hivyo mchakato huo ulisimama mwaka 2015, kupisha uchaguzi mkuu wa 2015, na haujaendelea tena tangu kipindi hicho. Mchakato wa marekebisho ya katiba ulipitia awamu kuu tatu.

Awamu ya kwanza ilikuwa ya kuundwa kwa Tume ya marekebisho ya Katiba. Hii iliundwa chini ya uongozi wa Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba na Tume hii ilisafiri nchi nzima kukusanya maoni ya wananchi kuhusu muundo wa katiba mpya na ikachapisha rasimu yake ya kwanza baada ya kupata maoni ya wananchi.

Rasimu hii ilijulikana kama “rasimu ya Warioba” na ilichapishwa mwezi Disemba mwaka 2013. Miongoni mwa mambo yaliyopendekezwa katika rasimu hii ni kubadilisha muundo wa sasa wa serikali mbili (Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibari) na kuanzisha muundo wa serikali tatu (Serikali ya Muungano, Serikali ya Tanzania Bara, Serikali ya Zanzibari).

Taasisi ya TWAWEZA kupitia Sauti za Wananchi, ambao hukusanya maoni ya wananchi kupitia simu za mkononi kuhusu kinachoendelea nchini katika nyanja zote za maisha, inakuja kwa mara nyingine na Ripoti ya maoni ya wananchi yenye kichwa Zege limelala? Maoni ya Watanzania kuhusu kukwama kwa mchakato wa marekebisho ya katiba.

Ripoti hiyo ambayo itazinduliwa leo tarehe 19.10.2017 kuanzia saa 5 asubuhi hadi 7 mchana pale Makumbusho ya Taifa (Posta, Mkabala na chuo cha IFM), itabainisha maoni ya wananchi.
 

Attachments

  • SzW-TZ-2017-Katiba-KIS-FINAL-web.pdf
    1.1 MB · Views: 101
  • SzW-TZ-2017-Constitution-EN-FINAL-web.pdf
    1.1 MB · Views: 91
Christina Kamili(Jukwaa la Katiba): Katiba ya Warioba ilibeba maslahi mapana ya wananchi hasa mgawanyo wa mihimili 3 ya Serikali [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

IMG_20171019_114240.jpg
Mchakato wa marekebisho ya Katiba ulipitia awamu 3. Awamu ya kwanza ilikuwa ya kuundwa Tume ya marekebisho chini ya Jaji Warioba
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Miongoni mwa mambo yaliyopendekezwa ktk rasimu hii ni kubadilisha muundo wa sasa wa Serikali 2 na kuanzisha muundo wa Serikali 3
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Bunge Maalumu la [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] lilipitisha rasimu hii Oktoba 2014, pasipo kujali kujiondoa kwa wajumbe waliounda umoja uliojulikana kama UKAWA

93% ya Watanzania wameshawahi kusikia kuhusu Katiba, lakini kati yao 58% hawafahamu Katiba ni nini
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

22% - Ni mkusanyiko wa kanuni zitumikazo kuongoza nchi
12% - Ni azimio la kisheria litumikalo kuongoza nchi
1% - Azimio la haki za wananchi

IMG_20171019_114633.jpg

Uelewa wa Katiba ni mkubwa miongoni mwa wenye elimu ya Sekondari na ya juu(49%) kuliko ambao hawajahitimu elimu ya msingi(22%)

Uelewa wa Katiba ni mkubwa miongoni mwa wenye umri > miaka 50(45%) kuliko wenye < miaka 30(29%) - Matajiri(40%); masikini (28%)

Uelewa wa Katiba kati ya wanaume na wanawake: 47% ya wanaume waliweza kueleza maana ya Katiba, ukilinganisha na 22% ya wanawake

44% wanasema [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] iliyopo inatekelezwa ipasavyo, 46% wanasema inatekelezwa “kwa kiwango fulani”. 4% tu wanasema “haitekelezwi ipasavyo”

IMG_20171019_115623.jpg

Waliosema [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] inatekelezwa ipasavyo walisema ni kwa sababu sheria zinafuatwa (22%) au kutokana na kwamba uongozi ni mzuri (12%)
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Waliosema “inatekelezwa kwa kiwango fulani” walieleza kuwa kuna baadhi ya vipengele vya Katiba(15%) au Sheria(12%) ambavyo havifuatwi
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

71% ya wananchi wanafahamu kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa [HASHTAG]#Tanzania[/HASHTAG] ilianzisha mchakato wa mabadiliko ya [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] yake
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Uelewa wa mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] ni mkubwa miongoni mwa wanaume (81%) ukilinganisha na wanawake (61%) [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

IMG_20171019_120109.jpg

Uelewa wa mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] ni mkubwa miongoni mwa wenye miaka zaidi ya 50 (81%) kuliko wenye umri chini ya miaka 30 (63%)
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Wananchi 2 kati ya 3(67%) wanasema maoni ya wananchi hayajatokea kwenye rasimu ya [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] iliyoandaliwa na Bunge Maalum la Katiba [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

IMG_20171019_120224.jpg

23% ya wananchi wanasema mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] kwa kiasi kikubwa ulikuwa ni
kuwapa taarifa kuliko kuruhusu wananchi kutoa maoni yao
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

44% ya wananchi waliona mchakato huo uliwapa fursa wananchi kutoa maoni yao, lakini hayakutumika kwenye rasimu ya [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

59% ya wananchi wanasema Bunge Maalumu la [HASHTAG]#Katiba[/HASHTAG] liliwawakilisha vema watanzania ktk mchakato huo
- 38% hawakubaliani na kauli hiyo
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Mwananchi mmoja kati ya wanne(23%) wanaunga mkono UKAWA kususia Bunge Maalumu la Katiba na kugomea mchakato wa kupitia [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]
[HASHTAG]#szw[/HASHTAG]

IMG_20171019_120359.jpg

56% ya wananchi wanasema kutoka nje kwa UKAWA hakubatilishi mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] ; 41% wanasema kitendo hicho kinabatilisha mchakato
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

48% ya wananchi wanasema njia nzuri ya kufufua mchakato wa mabadiliko ya Katiba ni kuanza mchakato huo upya na tume mpya
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

IMG_20171019_120447.jpg

Wananchi hawakubaliani na mabadiliko mengi yaliyofanywa na Bunge la katiba chini ya M/Kiti kamati ya uandishi [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG], Ndugu Chenge
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

79% hawakubaliani na kuondolewa kifungu kinachotaka mawaziri kupitishwa/kukataliwa kwa kura bungeni baada ya kuteuliwa na Rais
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

IMG_20171019_121915.jpg

Ado Shaibu kutoka Chama cha ACT-Wazalendo: Kwa Ripoti hii ya Sauti za Wananchi iliyotolewa na TWAWEZA ni dhahiri kuwa wananchi wanahitaji [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

IMG_20171019_122012.jpg

Ado Shaibu(ACT): Rais Magufuli hakusema mchakato wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] haufai bali alionesha wazi kuwa si kipaumbele cha Serikali Awamu ya 5
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Ado Shaibu: Utafiti huu umebainisha kuwa kuna pengo kubwa kati ya Wanawake na Wanaume katika uelewa wa mambo nchini
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG] [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Ado Shaibu: Mchakato mzima wa [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] unaonesha [HASHTAG]#SautiZaWananchi[/HASHTAG] zimezimwa
- Wananchi wametaja vipengele walivyopendekeza na vikatolewa

Ado Shaibu: Wapinzani tunafanya makosa ktk kujifungamanisha na Wadau wakuu ambao ni wananchi
-Wananchi wengi hawaijui UKAWA
[HASHTAG]#SzW[/HASHTAG] [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

IMG_20171019_122255.jpg

Polepole(CCM): Watanzania kwa takwimu hizi za Twaweza wanataka kuona Ukatiba(constitutionalism) kuliko Katiba(constitution) nchini

Polepole: Watu wa kawaida wanataka viongozi waadilifu, wasiokula rushwa, wanaojua cheo ni dhamana; huo ndio Ukatiba [HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG]

Polepole: Ukatiba ni kuwekeana mifumo hata kama haikuandikwa mahali. Kila mtu akielewa hii mifumo hakutokuwa na tatizo
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

Polepole: Tunaweza kuandaa Katiba na kuiweka kwenye kitabu lakini bila Ukatiba hakuna atakayeifuata
[HASHTAG]#KatibaMpya[/HASHTAG] [HASHTAG]#SzW[/HASHTAG]

IMG_20171019_122412.jpg
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!
Kuto kupiga kura ndio utaratibu wa wapi? Korea Kaskazini?
 
Rasimu ya katiba hii ni bora kuliko katiba ya sasa. Tatizo Rais Magufuli haitaki sababu anajua itambana na yeye pia kwenye majukumu yake na yeye hataki. Yuko hiari mabilioni ya pesa za walipa kodi zipotee kuliko kupatatika na kwa katiba hii. Sasa yeye kama mzalendo na uchungu wa rasilimali za watanzania. Kwa nini hana uchungu wa mabilioni ya haya yaliyotumika kwa mchakato wa katiba mpya?? Tena ni ya kwao CCM wenyewe?
 
Rasimu ya katiba hii ni bora kuliko katiba ya sasa. Tatizo Rais Magufuli haitaki sababu anajua itambana na yeye pia kwenye majukumu yake na yeye hataki. Yuko hiari mabilioni ya pesa za walipa kodi zipotee kuliko kupatatika na kwa katiba hii. Sasa yeye kama mzalendo na uchungu wa rasilimali za watanzania. Kwa nini hana uchungu wa mabilioni ya haya yaliyotumika kwa mchakato wa katiba mpya?? Tena ni ya kwao CCM wenyewe?
Kumpunguzia madaraka Rais ni kuruhusu nchi 'kuliwa' zaidi... Leo hii nchi imefikia pabaya sio kwa sababu ya udhaifu wa katiba bali ubinafsi.. Acha kidogo hiki chuma kinyooshe mambo then tutazungumza upya kuhusu hiyo rasimu pendwa tukishakaa mguu sawa!
 
Katiba ni sasa kama siyo sasa ni sasa hivi.

CCM Tuna option mbili tuu Kurekebisha Katiba au Kurekebisha Katiba.
 
Watanzania bhana watu wa ajabu sana! Sasa mmeandaliwa Katiba nzuri, mkapendekezewa.. Hamtaki! Mnakuwa kama Raila Odinga bhana..

Kimsingi sioni haja ya kurudia mchakato........ Kama tunataka katiba mpya, ipo iliyopendekezwa, tuipigie kura, finish!
Kinyume na hapo, basi tuendelee tu na hii..

Tusipoteze muda na pesa kwa mambo yasoisha, ebo!

baby mama jipigie makofi
 
Kumpunguzia madaraka Rais ni kuruhusu nchi 'kuliwa' zaidi... Leo hii nchi imefikia pabaya sio kwa sababu ya udhaifu wa katiba bali ubinafsi.. Acha kidogo hiki chuma kinyooshe mambo then tutazungumza upya kuhusu hiyo rasimu pendwa tukishakaa mguu sawa!

chuma my ass, ungepewa macho hata kwa dakika ungeona. asantemwenyezi
 
Conclusion


This brief looks both backwards and forwards. It provides valuable detail on how the public view the Constitution-making process that took place between 2010 and 2015, and how they appraise these efforts. But the most valuable insights are those that help up to move forward.

What lessons can be learned? Is there a public appetite to restart the review process? And if so, how should this be done? Looking back, the most useful findings are those that provide pointers for anyone thinking of taking Tanzania through a similar process again.

Here, four things stand out. First, the level of public awareness and understanding of the constitution and the review process is not very high. 93% of citizens have heard of the constitution, but just 35% can confidently explain what it is, and a quarter of the population are not aware that a review process took place.

Second, there is a real challenge with ensuring inclusion, most particularly of women. Understanding of the Constitution, awareness of the review process overall and in detail, and participation in that process are all much lower among women than among men.

One out of four men (25%) participated in the CRC consultations, for example, compared to just 10% of women. There are also signs that younger, poorer and less educated citizens were excluded, though these cases are less stark than the gender imbalance.

Third, there is widespread public scepticism about whether the opportunities they were given to contribute were genuine or not. While a massive 91% agree that both process and content are important in Constitution-making, just 33% of citizens think the public’s views were actually listened to and reflected in the various drafts.

The remaining two-thirds think the process of consultation was only for creating an impression of consultation or for sharing information. Fourth, public opinion on the UKAWA walkout and boycott is divided. The majority do not back UKAWA’s actions.

But asked in general terms, without mentioning UKAWA by name, a majority say that if a significant group decides not to participate, the whole process lacks legitimacy as a result. Public opinion on the content of the Constitution is worth noting. Many of the changes made by the Constituent Assembly to the draft that relate to accountability are unpopular.

There are strong majorities against the decisions to drop provisions for parliamentary confirmation of Ministers and for voters to “recall” failing MPs, and smaller majorities against dropping the prohibition on overseas bank accounts for senior government figures and dropping 15-year term limits for MPs.

On the issue that dominated debate and headlines around the Constitution – the Union question – this brief suggests the most popular structure among mainlanders is the current two-government structure, as proposed by the CA. Only 16% of mainlanders prefer the idea of a three-government structure, as put forward by the CRC.

However, these figures in particular must be treated with 16 caution, as they do not include opinion from Zanzibar. A survey in 2014 found that support for the three-government idea among Zanzibaris was high, at 46%.

Looking forward, the public are very clear on two points: there is a strong appetite for a new Constitution and a strong preference for starting afresh with a blank page, a new commission, and new consultations. Further, if any existing document is to be used as a starting point for discussions, the public would prefer it to be the CRC / Warioba.

Putting all of this together, future Constitution-making processes in Tanzania will need to resolve three key challenges: (i) awareness and inclusion, (ii) popular legitimacy, and (iii) consensus on content.

The first of these should be the easiest to address, through awareness raising efforts that specifically target women and other disadvantaged groups and specific efforts to address the gender participation gap.

The legitimacy challenge is harder, but it can be addressed through the kind of leadership that prevents the process breaking down into partisan battles, and that solves disagreements through dialogue instead of the weight of numbers.

Finding consensus on content is perhaps the hardest challenge of all. It requires a fine balance between listening to public opinion while providing sage leadership and guidance on some of the more thorny issues. Restarting the process from where it stalled risks reigniting the battles that were fought during the last round.

Following the public’s guidance and starting again with new consultations and a blank page could help build trust and defuse tension. Developing a draft that reflects public opinion on accountability measures should be relatively straightforward, but the union question is much harder. And this issue must be approached with great care.

A simple of tyranny of numbers whereby the mainland can always effectively veto Zanzibari voices does not hold to the spirit of the union and will create significant issues down the line. Countries all over the world find it hard to reach agreement on arrangements for similar, semiautonomous areas – Scotland and the UK, Hong Kong and China, Puerto Rico and the US, are three examples.

For those Zanzibaris who resent the perceived lower status of Zanzibar in the Union, putting the three-government option onto the agenda through the CRC then taking it away again through the CA, is like putting a cake on the table then telling people they can’t eat it.

Frustration and even anger are the natural result. The best chance of finding a solution comes from addressing the other two challenges mentioned here: inclusion and legitimacy.

With an open, inclusive process that solves disagreements through dialogue, consensus is possible. With open, inclusive leadership, such a process should be achievable.
 
. Hitimisho:

Muhtasari huu unatupa maelezo muhimu juu ya mitazamo ya wananchi kuhusu mchakato mzima wa mabadiliko ya katiba uliofanyika kati ya mwaka 2010 na 2015, na tathmini yao kuhusu jitihada hizo. Lakini maoni ya msingi zaidi ni yale ambayo yatatusaidia kusonga mbele.

Je, tunajifunza nini? Je, wananchi wana hamu ya kuanza tena upya mchakato wa mabadiliko ya katiba? Na kama ndivyo, je, ufanyike vipi? Tukitazama tulikotoka, matokeo muhimu ni yale yanayotoa maelekezo kwa yeyote anayewaza kuanza tena mchakato wa mabadiliko ya katiba nchini Tanzania. Hapa, vinajitokeza vitu vitatu.

Kwanza, kiwango cha uelewa na ufahamu wa wananchi kuhusu mchakato wa mabadiliko ya katiba si kikubwa sana. Asilimia 93 ya wananchi wamesikia kuhusu katiba, lakini ni asilimia 35 tu waonaweza kueleza maana ya katiba kwa kujiamini, na robo ya wananchi hawafahamu kama mchakato wa mabadiliko ya katiba ulifanyika.

Pili, kuna changamoto kubwa katika kuhakikisha wananchi wote wanashirikishwa, hususani wanawake. Uelewa wa katiba, na uelewa wa mchakato mzima wa mabadiliko ya katiba, pamoja na ushiriki katika mchakato huo ni mdogo miongoni mwa wanawake kuliko wanaume. Kuna dalili pia kwamba vijana, wananchi masikini na wasiokuwa na elimu hawakuhusishwa ipasavyo.

Tatu, wananchi wana maoni tofauti kuhusu kujiondoa kwa UKAWA katika Bunge maalumu la Katiba. Idadi kubwa hawaungi mkono maamuzi ya UKAWA. Lakini walipoulizwa kwa kauli ya ujumla, bila ya kutaja jina UKAWA, idadi kubwa walisema kama kikundi fulani kikiamua kutoshiriki, matokeo yake mchakato mzima unakosa uhalali. Maoni ya wananchi kuhusu maudhui ya katiba yanafaa kuzingatiwa.

Mabadiliko mengi yaliyofanywa na Bunge Maalumu la Katiba yanayoendana na uwajibikaji hayafahamiki. Kuna idadi kubwa ya wananchi wanaotofautiana na maamuzi ya kuondoa vifungu vilivyotaka bunge kupitisha mawaziri walioteuliwa na Rais na wapiga kura kuwavua madaraka wabunge walioshindwa kutekeleza majukumu yao.

Vile vile idadi ndogo ya wananchi wanapinga kuondolewa kwa kipengele kinachokataza viongozi wakubwa wa serikali kumiliki akaunti za benki nje ya nchi na kuondolewa kwa kipengele kinachotaka ukomo wa ubunge uwe miaka 15.

Katika suala ambalo lilitawala mjadala na vichwa vya habari kuhusu katiba mpya – ni suala la muungano – muhtasari huu unabainisha muundo unaopendwa zaidi miongoni mwa wananchi wa Tanzania Bara ambao ni muundo wa serikali mbili, kama ulivyopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba.

16% pekee ya watanzania bara wanapendelea wazo la kuwa na muundo wa serikali tatu, kama ulivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Hata hivyo, takwimu hizi zinapaswa kuangaliwa kwa tahadhari, kwa kuwa hazihusishi maoni ya wazanzibari.

Utafiti uliofanyika mwaka 16 2014 ulionesha kuwa uungaji mkono wa muundo wa serikali tatu miongoni mwa wazanzibari ulikuwa mkubwa, kwa asilimia 46. Tukiangalia mbele, wananchi wapo wazi kwenye mambo mawili: wana hamu kubwa ya kupata katiba mpya na wangependa kuanza mchakato huo upya na tume mpya, pamoja na ukusanyaji upya wa maoni.

Zaidi, endapo litatumika andiko la zamani kama sehemu ya kuanzia majadiliano, wananchi wangependa itumike rasimu iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba (rasimu ya Warioba).

Kwa kuweka haya yote pamoja, mchakato ujao wa kutengeneza katiba mpya nchini Tanzania utapaswa kutatua changamoto kuu tatu: (i) ufahamu na ushirikishwaji, (ii) uhalali miongoni mwa wanachi, na (iii) makubaliano ya maudhui ya katiba.

Suala la kwanza ni rahisi zaidi kutekelezwa, kwa kutumia jitihada mbalimbali za kuwafahamisha wananchi hususani wanawake na makundi mengine yaliyoko pembezoni pamoja na kufanya jitihada mahususi za kuondoa changamoto ya usawa wa kijinsia.

Suala la uhalali ni gumu, lakini linaweza kufanyiwa kazi kupitia aina ya uongozi ambayo itazuia mchakato wa katiba kuingia kwenye vita za ushabiki wa kisiasa na hivyo kutatua tofauti zinazojitokeza kupitia mijadala badala ya kutumia wingi wa idadi ya watu.

Kufikia makubaliano kwenye suala la maudhui ya katiba pengine ndiyo changamoto kubwa kuliko zote. Suala hili linahitaji usawa kamili katika kusikiliza maoni ya wananchi na wakati huo huo kutoa mwongozo wenye busara kwenye baadhi ya masuala mazito.

Kuendeleza mchakato pale ulipokomea kuna hatari ya kurejesha vita vilivyokuwepo wakati wa awamu ya mwisho. Kwa kufuata mwongozo wa wananchi wa kuanza ukurasa upya na kuanza tena mchakato wa kukusanya maoni utasaidia kujenga uaminifu na kuondoa wasiwasi.

Kutengeneza rasimu inayoendana na maoni ya wananchi kwenye suala la uwajibikaji ni rahisi, lakini suala la muungano ni gumu zaidi. Na linapaswa kujadiliwa kwa uangalifu mkubwa. Suala la kutumia idadi kubwa ya watu ambapo Tanzania bara itaizidi Zanzibari halifai na litaleta shida.

Nchi mbalimbali duniani huwawia vigumu kufikia muafaka kwenye suala linalofanana na hili la Tanzania – Scotland na Uingereza, Hong Kong na China, Puerto Rico na Marekani, ni mifano mitatu inayoendana.

Kwa wazanzibari ambao hawapendezwi na hadhi ya Zanzibar inayoonekana kuwa ndogo kwenye muungano, kuondoa kipengele cha muundo wa serikali tatu kilichowekwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ni kama kuweka keki mezani na kisha kuwaambiwa watu wasile.

Fursa nzuri ya kutafuta suluhisho ni kwa kutatua changamoto mbili kubwa: ushirikishwaji na uhalali. Kwa kutumia mchakato ulio wazi, unaoshirikisha wananchi na kutatua tofauti zinazojitokeza kwa njia ya mazungumzo, tunaweza kabisa kufikia muafaka. Kwa kutumia mchakato wa wazi na uongozi jumuishi tutafanikiwa.
 
Matokeo muhimu ni:

1• Karibu wananchi wote wamesikia kuhusu katiba, lakini ni mwananchi 1 tu kati ya 3 anayeweza kueleza katiba ni nini.

2• Wananchi 7 kati ya 10 wanafahamu kuhusu mchakato wa mabadiliko ya katiba.

3• Mwananchi 1 kati ya 5 alishiriki katika kutoa maoni yake kwenye zoezi lililoratibiwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

4• Uelewa wa katiba na mchakato wa mabadiliko, na pia ushiriki kwenye mchakato huo ni 3 mdogo zaidi miongoni mwa wanawake kuliko wanaume.

5• Wananchi 2 kati ya 3 wanasema mchakato huo haukuruhusu maoni ya wananchi kuingizwa kwenye katiba

6• Wananchi wanapinga mabadiliko mengi yaliyofanywa na Bunge Maalumu la Katiba, ikiwemo uamuzi wa kuondoa mamlaka ya bunge kupitisha mawaziri walioteuliwa.

7• Miongoni mwa wananchi wa Tanzania Bara, muundo wa serikali unaokubalika zaidi ni wa serikali mbili.

8• Mwananchi 1 kati ya 4 anaunga mkono UKAWA kulisusia Bunge Maalumu la Katiba na kuugomea mchakato wa mabadiliko ya katiba.

9• Chaguo la wananchi la kurudia mchakato wa mabadiliko ya katiba ni kuanza upya kabisa na kuunda tume mpya.

10• Kama mchakato utaanzishwa upya, wananchi wangependa ukurasa mpya kabisa ufunguliwe au uanzie kwenye rasimu ya Warioba.

11• Wananchi 2 kati ya 3 wanasema Tanzania inahitaji katiba mpya na wananchi 3 kati ya 10 wanasema hili litafanikiwa ndani ya miaka mitatu ijayo.
 
Kumpunguzia madaraka Rais ni kuruhusu nchi 'kuliwa' zaidi... Leo hii nchi imefikia pabaya sio kwa sababu ya udhaifu wa katiba bali ubinafsi.. Acha kidogo hiki chuma kinyooshe mambo then tutazungumza upya kuhusu hiyo rasimu pendwa tukishakaa mguu sawa!
Hiyo siyo sahihi! Kumpunguzia rais madaraka kunamfanya rais afanye kazi kwa weledi na uaminifu zaidi. Sababu akifanya kinyume, wawakilishi wa wananchi na wananchi wenyewe waliomchagua ndiyo watamwajibisha. Hata kwa katiba mpya ataendelea kufanya vizuri kama rais ilimradi atafanya kazi yake kwa misingi ya sheria na katiba. Siyo kukurupuka tu hatutaki mambo hayo.
 
Rasimu ya katiba hii ni bora kuliko katiba ya sasa. Tatizo Rais Magufuli haitaki sababu anajua itambana na yeye pia kwenye majukumu yake na yeye hataki. Yuko hiari mabilioni ya pesa za walipa kodi zipotee kuliko kupatatika na kwa katiba hii. Sasa yeye kama mzalendo na uchungu wa rasilimali za watanzania. Kwa nini hana uchungu wa mabilioni ya haya yaliyotumika kwa mchakato wa katiba mpya?? Tena ni ya kwao CCM wenyewe?
Hivi Rais Magufuli amehusikaje kukwamisha mchakato wa Katiba?
 
. Hitimisho:

Muhtasari huu unatupa maelezo muhimu juu ya mitazamo ya wananchi kuhusu mchakato mzima wa mabadiliko ya katiba uliofanyika kati ya mwaka 2010 na 2015, na tathmini yao kuhusu jitihada hizo. Lakini maoni ya msingi zaidi ni yale ambayo yatatusaidia kusonga mbele. Je, tunajifunza nini? Je, wananchi wana hamu ya kuanza tena upya mchakato wa mabadiliko ya katiba? Na kama ndivyo, je, ufanyike vipi? Tukitazama tulikotoka, matokeo muhimu ni yale yanayotoa maelekezo kwa yeyote anayewaza kuanza tena mchakato wa mabadiliko ya katiba nchini Tanzania. Hapa, vinajitokeza vitu vitatu. Kwanza, kiwango cha uelewa na ufahamu wa wananchi kuhusu mchakato wa mabadiliko ya katiba si kikubwa sana. Asilimia 93 ya wananchi wamesikia kuhusu katiba, lakini ni asilimia 35 tu waonaweza kueleza maana ya katiba kwa kujiamini, na robo ya wananchi hawafahamu kama mchakato wa mabadiliko ya katiba ulifanyika. Pili, kuna changamoto kubwa katika kuhakikisha wananchi wote wanashirikishwa, hususani wanawake. Uelewa wa katiba, na uelewa wa mchakato mzima wa mabadiliko ya katiba, pamoja na ushiriki katika mchakato huo ni mdogo miongoni mwa wanawake kuliko wanaume. Kuna dalili pia kwamba vijana, wananchi masikini na wasiokuwa na elimu hawakuhusishwa ipasavyo. Tatu, wananchi wana maoni tofauti kuhusu kujiondoa kwa UKAWA katika Bunge maalumu la Katiba. Idadi kubwa hawaungi mkono maamuzi ya UKAWA. Lakini walipoulizwa kwa kauli ya ujumla, bila ya kutaja jina UKAWA, idadi kubwa walisema kama kikundi fulani kikiamua kutoshiriki, matokeo yake mchakato mzima unakosa uhalali. Maoni ya wananchi kuhusu maudhui ya katiba yanafaa kuzingatiwa. Mabadiliko mengi yaliyofanywa na Bunge Maalumu la Katiba yanayoendana na uwajibikaji hayafahamiki. Kuna idadi kubwa ya wananchi wanaotofautiana na maamuzi ya kuondoa vifungu vilivyotaka bunge kupitisha mawaziri walioteuliwa na Rais na wapiga kura kuwavua madaraka wabunge walioshindwa kutekeleza majukumu yao. Vile vile idadi ndogo ya wananchi wanapinga kuondolewa kwa kipengele kinachokataza viongozi wakubwa wa serikali kumiliki akaunti za benki nje ya nchi na kuondolewa kwa kipengele kinachotaka ukomo wa ubunge uwe miaka 15. Katika suala ambalo lilitawala mjadala na vichwa vya habari kuhusu katiba mpya – ni suala la muungano – muhtasari huu unabainisha muundo unaopendwa zaidi miongoni mwa wananchi wa Tanzania Bara ambao ni muundo wa serikali mbili, kama ulivyopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba. 16% pekee ya watanzania bara wanapendelea wazo la kuwa na muundo wa serikali tatu, kama ulivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Hata hivyo, takwimu hizi zinapaswa kuangaliwa kwa tahadhari, kwa kuwa hazihusishi maoni ya wazanzibari. Utafiti uliofanyika mwaka 16 2014 ulionesha kuwa uungaji mkono wa muundo wa serikali tatu miongoni mwa wazanzibari ulikuwa mkubwa, kwa asilimia 46. Tukiangalia mbele, wananchi wapo wazi kwenye mambo mawili: wana hamu kubwa ya kupata katiba mpya na wangependa kuanza mchakato huo upya na tume mpya, pamoja na ukusanyaji upya wa maoni. Zaidi, endapo litatumika andiko la zamani kama sehemu ya kuanzia majadiliano, wananchi wangependa itumike rasimu iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba (rasimu ya Warioba). Kwa kuweka haya yote pamoja, mchakato ujao wa kutengeneza katiba mpya nchini Tanzania utapaswa kutatua changamoto kuu tatu: (i) ufahamu na ushirikishwaji, (ii) uhalali miongoni mwa wanachi, na (iii) makubaliano ya maudhui ya katiba. Suala la kwanza ni rahisi zaidi kutekelezwa, kwa kutumia jitihada mbalimbali za kuwafahamisha wananchi hususani wanawake na makundi mengine yaliyoko pembezoni pamoja na kufanya jitihada mahususi za kuondoa changamoto ya usawa wa kijinsia. Suala la uhalali ni gumu, lakini linaweza kufanyiwa kazi kupitia aina ya uongozi ambayo itazuia mchakato wa katiba kuingia kwenye vita za ushabiki wa kisiasa na hivyo kutatua tofauti zinazojitokeza kupitia mijadala badala ya kutumia wingi wa idadi ya watu. Kufikia makubaliano kwenye suala la maudhui ya katiba pengine ndiyo changamoto kubwa kuliko zote. Suala hili linahitaji usawa kamili katika kusikiliza maoni ya wananchi na wakati huo huo kutoa mwongozo wenye busara kwenye baadhi ya masuala mazito. Kuendeleza mchakato pale ulipokomea kuna hatari ya kurejesha vita vilivyokuwepo wakati wa awamu ya mwisho. Kwa kufuata mwongozo wa wananchi wa kuanza ukurasa upya na kuanza tena mchakato wa kukusanya maoni utasaidia kujenga uaminifu na kuondoa wasiwasi. Kutengeneza rasimu inayoendana na maoni ya wananchi kwenye suala la uwajibikaji ni rahisi, lakini suala la muungano ni gumu zaidi. Na linapaswa kujadiliwa kwa uangalifu mkubwa. Suala la kutumia idadi kubwa ya watu ambapo Tanzania bara itaizidi Zanzibari halifai na litaleta shida. Nchi mbalimbali duniani huwawia vigumu kufikia muafaka kwenye suala linalofanana na hili la Tanzania – Scotland na Uingereza, Hong Kong na China, Puerto Rico na Marekani, ni mifano mitatu inayoendana. Kwa wazanzibari ambao hawapendezwi na hadhi ya Zanzibar inayoonekana kuwa ndogo kwenye muungano, kuondoa kipengele cha muundo wa serikali tatu kilichowekwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ni kama kuweka keki mezani na kisha kuwaambiwa watu wasile. Fursa nzuri ya kutafuta suluhisho ni kwa kutatua changamoto mbili kubwa: ushirikishwaji na uhalali. Kwa kutumia mchakato ulio wazi, unaoshirikisha wananchi na kutatua tofauti zinazojitokeza kwa njia ya mazungumzo, tunaweza kabisa kufikia muafaka. Kwa kutumia mchakato wa wazi na uongozi jumuishi tutafanikiwa.
Sijui umekopi wapi
 
Kadri simba anavyokuwa Mzee ndivyo uwezo wake Wa kuwinda unavyopungua. Yaani siku hizi umekuwa kauzu kuliko dagaa. Samahani Joseverest.
 
Back
Top Bottom