Uchaguzi 2020 Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Dkt. Christine Ishengoma anachunguzwa na TAKUKURU kwa tuhuma za kuwapa rushwa Wapiga Kura

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Morogoro inamchunguza Mbunge wa Viti MAALUM (CCM) Dk.Christine Ishengoma, kutokana na tuhuma za kugawa rushwa kwa wapiga kura huku ikiwahoji watu mbalimbali kutokana na tuhuma hizo.

Aidha TAKUKURU imewafikisha mahakamani aliyewahi kuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani Kata ya Boma, Amir Nondo, na wenzake watatu kutokana na makosa ya uhujumu uchumi baada ya kudaiwa kubadili matumizi ya kiwanja eneo la Msamvu bila kufuata taratibu za mipango miji, kosa analodaiwa kufanya wakati akiwa kwenye nafasi ya Uenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, Bi Janet Machulya wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo akaonya wananchi wanaotaka nafasi za uongozi kuacha kupitapita na kugawa rushwa au watumishi wanaoaminiwa wakiwemo wenye dhamana ya usimamizi wa ardhi kuacha kufanya udanganyifu.
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Morogoro inamchunguza Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Christine Ishengoma, kutokana na tuhuma za kutoa rushwa kwa wapiga kura, huku ikiwahoji watu mbalimbali kutokana na tuhuma hizo.

Aidha, Takukuru imewafikisha Mahakamani aliyewahi kuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani wa Boma, Amir Nondo, na wenzake watatu kutokana na makosa ya uhujumu uchumi baada ya kudaiwa kubadili matumizi ya kiwanja eneo la msamvu bila kufuata taratibu za mipango miji.

Nondo anadaiwa kufanya kosa hilo wakati akiwa kwenye nafasi ya uenyekiti wa kamati ya mipango miji na mazingira.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Morogoro, Janet Machulya, ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari na amewaonya wananchi wanaotaka nafasi za uongozi kuacha kupita pita na kutoa rushwa.

Pia amewataka watumishi wanaoaminiwa wakiwemo wenye dhamana ya usimamizi wa ardhi kuacha kufanya udanganyifu katika michakato ya kumilikisha ardhi na kusababisha migogoro kutokana na udanganyifu kitu ambacho kitwafanya kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika

NIPASHE
 
Dadeeeeki CCM mwaka huu hamtoboi, Watawekwa wagombea wa nanihii tu....sijamtaja mwenyekiti
 
Pongezi Kwa TAKUKURU Kwa kazi nzuri,
Nashauri kipindi hiki msilale wekeni shift, wananchi hatutaki viongozi wanao nunua vyeo/uongozi, mwaka huu 2020 tunataka viongozi wasafi.
Lkn pia tupieni macho rushwa ya ngono
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Morogoro inaufahamisha Umma kwamba leo siku ya Jumatano, tarehe 10/06/ 2020 itawafikisha mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro Meya Mstaafu ambaye kwa sasa ni Diwani wa Kata ya Boma Bw. Amir Juma Nondo kwa makosa ya udanganyifu ambayo kwa mujibu wa marekebisho yaliyofanywa na Sheria Na. 3/2016 makosa hayo ni ya Uhujumu Uchumi.

Pamoja na Meya huyo watashtakiwa wengine ni Bw. Simon Michael Mahundo aliyekuwa Afisa Mipangomiji, Bw. Athumani Leonard Juma aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Mipangomiji na Mazingira Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Bw. Dickson Steven Kesenha ambaye alikuwa ni Afisa Mipangomiji wa Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro.

Tuhuma zinazowakabili watuhumiwa hao zinatokana na uchunguzi wa TAKUKURU ambapo ilibainika kuwa Meya Mstaafu akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mipangomiji na Mazingira wa Halmashauri ya Manispaa Morogoro kwa kushirikiana na wataalam hao kwa mamlaka waliyokuwa nayo waliwasilisha

taarifa za upotoshaji zilizosababisha mfanyabiashara mmoja wa Mjini Morogoro kujipatia manufaa ya kubadili matumizi ya kiwanja Namba 138 Kitalu D kilichopo maeneo ya Msamvu B mjini Morogoro pasipokufuata taratibu za Mipango Miji.

TAKUKURU Mkoa wa Morogoro inatoa WITO kwa viongozi wa kisiasa na watumishi wenye dhamana ya usimamizi wa Ardhi kuacha kabisa mazoea ya udanganyifu katika mchakato wa umilikishaji wa rasilimali Ardhi unaosababisha uwepo wa migogoro katika Mkoa wa Morogoro. TAKUKURU haitasita kuwachunguza na kuwafikisha mbele ya Mahakama wale wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.

Imetolewa na:
Janeth Machulya
Mkuu wa TAKUKURU (M)
MOOROGORO
 
Hakuna kitu hapo,tupo makini kuangalia mammbo mazito yanayotukabili.Vp kuhusu Kangilugola nawemzie!
 
Ukishaona Mtu kaingizwa kwenye ishu za takukuru basi ndio kapunguzwa hivyo...kura za maoni ndio zimeanza hivyo.
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Morogoro inamchunguza Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Christine Ishengoma, kutokana na tuhuma za kutoa rushwa kwa wapiga kura, huku ikiwahoji watu mbalimbali kutokana na tuhuma hizo.

Aidha, Takukuru imewafikisha Mahakamani aliyewahi kuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani wa Boma, Amir Nondo, na wenzake watatu kutokana na makosa ya uhujumu uchumi baada ya kudaiwa kubadili matumizi ya kiwanja eneo la msamvu bila kufuata taratibu za mipango miji.

Nondo anadaiwa kufanya kosa hilo wakati akiwa kwenye nafasi ya uenyekiti wa kamati ya mipango miji na mazingira.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Morogoro, Janet Machulya, ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari na amewaonya wananchi wanaotaka nafasi za uongozi kuacha kupita pita na kutoa rushwa.

Pia amewataka watumishi wanaoaminiwa wakiwemo wenye dhamana ya usimamizi wa ardhi kuacha kufanya udanganyifu katika michakato ya kumilikisha ardhi na kusababisha migogoro kutokana na udanganyifu kitu ambacho kitwafanya kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika

NIPASHE
Ndio maana wanakuwa na viburi saana wakifika mjengon
 
Ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Morogoro inamchunguza Mbunge wa Viti MAALUM (CCM) Dk.Christine Ishengoma, kutokana na tuhuma za kugawa rushwa kwa wapiga kura huku ikiwahoji watu mbalimbali kutokana na tuhuma hizo.

Aidha TAKUKURU imewafikisha mahakamani aliyewahi kuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani Kata ya Boma, Amir Nondo, na wenzake watatu kutokana na makosa ya uhujumu uchumi baada ya kudaiwa kubadili matumizi ya kiwanja eneo la Msamvu bila kufuata taratibu za mipango miji, kosa analodaiwa kufanya wakati akiwa kwenye nafasi ya Uenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, Bi Janet Machulya wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo akaonya wananchi wanaotaka nafasi za uongozi kuacha kupitapita na kugawa rushwa au watumishi wanaoaminiwa wakiwemo wenye dhamana ya usimamizi wa ardhi kuacha kufanya udanganyifu.
Hivi maCCM huwa ayanshitakiana kwa rushwa au ni kiini macho tu???
 
Mlisema sio rushwa ni hela ya kiwi kwa maskari police, na hao wanatoa hela ya mboga kwa wajumbe/wapiga spana
 
Back
Top Bottom