Mbunge wa Mbalari CCM ahamia CHADEMA

Mbunge wa Mbalari CCM ahamia CHADEMA

possibly, maana walikuwa na mivutano ya mara kwa mara na DC na watu/viongozi wengine ndani ya ccm ngazi ya Wilaya kaona "gutter politics" zinamzingua acha tusubiri uthibitisho
 
Pipozz Power si mchezo watu wenye mapenzi mema na nchi hii lazima wahamie CHADEMA. Huyu mbunge anapinga wizi unaofanywa na maburushi na ndugu yao yule msafirisha wanyama hai kwenda Qatar kwa kusaidiwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya Bw. Nawabu Mullah ambayea ni Mburushi wa Pakistan wa kufanya ujangili kwenye bonde la Ihefu na jinsi mashamba ya wananchi ya mpunga yalivyoporwa na kupewa wahamiaji hao wa Kiburushi toka Pakistan huku wananchi wakiwa hawana sehemu ya kulima
 
Pipooooz power! source: amplifaya ya milard ayo.

mkuu ng'wanangwa make sure habari kama hizi una uhakika nazo
unajua mimi binafsi naheshimu sana comment zako,kama sio kweli nitaongea na mods private
 
Pipooooz power! source: amplifaya ya milard ayo.

Mimi nakuamini sana .Na siamini kwamba Nape anaweza kukutumia kuja kupima upepo hapa .Natoa heshima kwenye tetesi zako lakini .......................................
 
Kama sikosei huyu mbunge alijitahidi sana kuwasilisha kero za wananchi wake kwenye kikao cha bunge la bajeti mwaka huu, lakini kukawa na usanii wa kiaina akazimwa! Na kuna kipindi aliweka wazi kuwa wananchi wake walimwambia kama hakupata ufumbuzi wa kero zao basi asirudi. Sasa, ameamua kusimama na wananchi, tatizo ukiwa ccm unatakiwa usimame na wawekezaji na sio wananchi!

Hofu yangu kwenye hili ni kwamba kama ccm na serikali yake hawakuwa makini, Mbarali kunaweza kuwa kubaya kuliko Nyamongo. Matatizo ya Mbaralali ni ya muda ,mrefu lakini cha ajabu badala ya serikali kutatua wamezidi kupalilia mgogoro kwa kuwapa nguvu wawekezaji. Huyu Mbunge ana kesi na ccm wanaweza kumuewekea mizengwe (kupitia mahakama au tume ya uchaguzi) ili asiweze kugombea (kama ni kweli kahama chama inabidi uchaguzi mdogo ufanyike maana ubunge kupitia ccm unakuwa umekoma).
 
Mullah? Majina mengine bana . . . utata mtupu.


Mkuu Nawabu Mullah ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya. Huyu jamaa ni Mpakistani wa kabila la Ki-Balouch(burushi). Alitumia nafasi yake kujipatia mashamba ya Kapunga Rice kwa bei chee kupitia kampuni ya Export Trading. Sasa wanaua wananchi na kuwapiga kama wanavyoua digi digi.
 
karibu sana uungane na wapambanaji wenzako!!! but mkuu hizi habari ni za kweli?? be carefull
 
Na Ni Mbarali na Sio Mbalari

Kama amehamia CHADEMA lazima Uchaguzi Ufanyike kwahiyo hakuna Furaha Mpaka Uchaguzi
 
Majid Mjengwa kama umo humu tupe uhakika, ww kule una jamaa kibao wa kutoa japo kaukweli.
 
twndeni taratibu.....ngoja kwanza nivute waya mahali ili kuhakiki
 
Acha aende kwa wauaji wenzake cdm; maana ccm c mahala pa kutishia kuwaua wananchi!

Jamaa si muuwaji kama wewe unavyodhani. Wauwaji ni kina Aeshi wa Rukwa, Esther Bulaya na Rage sio Kilufi. Huyu mbunge wa Mbarali Modestus Kilufi amesimama kidete kuwatetea wananchi wake kuhusu shamba la mpunga ambalo magamba walimuuzia mwekezaji wa kiburushi na JK akiwa na ubia humo. Sasa wawekezaji hawa wanawanyanyasa sana wakulima ikiwa ni pamoja na kupandisha gharama za kukodi shamba na kuvamia mashamba yao yaliyo jirani na hilo shamba la wawekezaji. Kilufi yuko upande wa wananchi na ndio maana magamba hawamtaki wanasema anatekeleza sera za CDM za kutetea wanyonge badala ya zile za magamba. Hakuna cha kesi ya mauwaji wala kuwasifia polisi kwamba wamemkamata mbunge wa CCM. Issue ni kwamba jamaa hatakiwi kwasababu anatetea hao wakulima na Jakaya Kikwete ana ubia kwenye hilo shamba!! Upo hapo?
 
Huu utakuwa ni ujasiri unaopaswa kuonyeshwa na wabunge makini. Wale wote wasio makini wanapaswa kuachwa wajifie kwenye ligamba lao.
Tunasubiri uthibitisho wa habari hizi.
 
Acha aende kwa wauaji wenzake cdm; maana ccm c mahala pa kutishia kuwaua wananchi!

Mmeua Ilemela, mmeua Igunga, mliua Kombe, Shija, KOLIMBA, SOKOINE, Baba wa Taifa, na wale unaowajua NI WAUAJI PERIOD. Ila kila muuaji na yeye atakufa
 
Back
Top Bottom