Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, Priscus Tarimo unatambua uhitaji wa wananchi wako?

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,828
21,461
Mh mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini Heri ya kwaresma.

Nije kwenye hoja, kuna uwezekano mkubwa wananchi wa Jimbo la moshi mjini tena kupitia ticket ya ccm kukosa Kura Za maoni kama walivyofanya awali au kukosa ubunge 2025.

Tatizo ulilonalo ni kutokutambua wananchi wako wanahitaji nini na unatakiwa ufanye nini.

Umekuwa ukizungumzia ujenz wa Hospital ya wilaya kila kona ninaomba nikujulishe kuwa agend a hiyo Sio kipaumbele cha wananchi wako Kwani , Moshi imezingukwa na ma hospitali makubwa mengi na vituo vya afya vya kutosha.

2. Umekuwa ukapiga debe ujenzi wa barabara Za lami , Pia hicho Sio kipaumbele cha wananchi wako Kwani mji huo umezungukwa na lami kila kona hadi umepeleka lami kwenye hotel ya tajiri Ameg hotel Ili kumfurahisha Sijui.

3. Ujenzi wa vyumba vya madarasa na shule mpya Sio kipaumbele.

Vipaumbele vya wananchi wa Moshi mjini, ni ujenzi au Kufufua viwanda Ili wananchi wapate ajira, kubuni miradi ya kijamii Ili kuingia vipato vya wananchi, kusaidia vijana kuweza kujikomboa na umaskini badala ya sasa vijana wa ccm wanaendesha boda boda kama ajira rasmi, kufungua stand mpya ya mabasi ambayo Kwa sasa imekuwa gofu, kufanya mji wa Moshi kuwa Jiji, ujenzi wa Soko la mitumba la memorial, kujenga Soko la mbuyuni kuwa la kisasa na ujenzi wa Soko la kuuzwa Samaki.

Ukifanya hayo utakuwa unanijenga kuomba tena ubunge 2025, vinginevyo endelea kusimamia miradi ya familia yenu.

Pia Ukumbuke Wewe ni mbinafsi, mchoyo na usiyejua Mfumo wa ccm japo ni mbunge wa ccm.
 
Mh mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini Heri ya kwaresma.
Nije kwenye hoja,kuna uwezekano mkubwa wananchi wa Jimbo la moshi mjini tena kupitia ticket ya ccm kukosa Kura Za maoni kama walivyofanya awali au kukosa ubunge 2025.
Wabunge wa mchongo mwisho wao ni 2025 watafute kaz za kufanya mapema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom