Mbunge Wa Chadema Azomewa: TIT FOR TAT?!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Yaliyo wakuta viongozi kadhaa wa CCM hivi karibuni naona sasa yameanza kuwakuta wapinzani (walau huyu mmoja!), kama jinsi habari ifuatayo inavyosema. Je, demokrasia hapa inafanyakazi ipasavyo au...?!

Mbunge wa Chadema azomewa mkutanoni

Makubo Haruni, Tarime
HabariLeo; Thursday,October 18, 2007 @00:02

MBUNGE wa Jimbo la Tarime, Chacha Wangwe (Chadema), juzi alikumbana na wakati mgumu na kulazimika kukatisha mazungumzo yake na wananchi wa Kijiji cha Nyakunguru baada ya kumzomea wakimtaka ashuke jukwaani.

Wangwe alikumbana na dhahama hiyo katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Stanley Kolimba baada ya Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na kufunga ofisi. Aliitisha mkutano huo mahsusi kuelezea taratibu za kufuatwa wakati wa kumfukuza kiongozi wa serikali ya kijiji anapokuwa anatuhumiwa kwa jambo lolote.

Katika ufafanuzi, Mshauri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mkoani Mara, Laxford Miyaye alisema njia zilizotumiwa na Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyakunguru, Abel Maginga na kufunga ofisi yake kwa tuhuma mbalimbali, haukuwa sahihi.

Alisema kiongozi anapotuhumiwa ni lazima kwanza ajadiliwe na Kamati ya Serikali ya Kijiji na apewe nafasi ya kujitetea mbele ya Mkutano Mkuu wa kijiji ndipo uamuzi utatolewa. Miyaye alieleza kuwa mkutano wa Mbunge alioufanya Septemba 26, mwaka huu na kuamua kumfukuza mwenyekiti huyo uongozi na kufunga Ofisi ya Serikali ya Kijiji ni kinyume cha taratibu za uendeshaji.

Baadaye Wangwe alipata nafasi ya kutoa maoni yake na kueleza msimamo wake kwamba uamuzi alioufikia ni sahihi na ndipo wananchi walipomcharukia na kumtaka aache mazungumzo yake wakipiga kelele wakisema, “wewe ni mchochezi, hatutaki mambo yako, toka hapo hatuna haja na uongo wako.”

Licha ya Mbunge huyo kuwa mkali na kuwaambia wafunge midomo yao wamsikilize, walisisitiza hawamtaki na kamwe hawatamsikiliza. Hali hiyo ilimfanya Mbunge huyo wa Chadema atamke kwa hasira kuwa “msinibabaishe, kwanza mimi hamkunichagua.”

Baada ya kutoa kauli hiyo, aliketi chini kwa vile Mkuu wa Wilaya Kolimba aliingilia kati kuwatuliza wananchi hao walioonekana kuwa na jazba, huku Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Tarime, Constantine Bandola akisaidiana na Polisi wengine kutuliza ghasia, ingawa hakuna aliyejeruhiwa kwani vurugu zilizokuwapo zilikuwa za maneno ya kuzomea tu.

Mbunge Wangwe na wakili wa kujitegemea, Tundu Lisu, walilazimika kuondoka eneo hilo kwa gari kwenda katika uwanja wa ndege katika Kijiji cha Kewanja na kupanda ndege ya Kampuni ya Barrick Tanzania kurejea Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Trasias Kayenzi alikwenda kufungua ofisi ya mwenyekiti huyo wa kijiji na wananchi hao walimbeba juu mwenyekiti wao hadi ofisini hapo.

Hapo ndipo mkutano huo ulipofungwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime aliyewataka wananchi kufuata sheria katika uamuzi wa kuwaondoa viongozi madarakani. Tuhuma zilizokuwa zikimkabili mwenyekiti huyo ni pamoja na kutosoma mapato na matumizi ya kijiji, kuuza ardhi ya kijiji kwa Sh milioni 6.2 kwa Kampuni ya Barrick Tanzania.
Source link: HabariLEO.

SteveD.
 
Wananchi wa kijiji walimkataa mwenyekiti wao wa kijiji na kumuondoa kwa tuhuma za ufisadi. Mbunge wa CHADEMA akaunga mkono harakati zake. Mkuu wa wilaya ataapa atamrudisha. Akaitisha mkutano kwa ajili hiyo. Katikati ya tuhuma hizo za wanakijiji ipo kampuni ya Barrick. Mawakala wa serikali wakapanga watu wao wa kuvuruga mkutano. Kwa taarifa za baadhi ya wakazi wa huko kampuni ya Barick ilichangia uchinjaji wa ng'ombe na ugawaji wa pombe kwa kundi la wazomeaji. Kwa hiyo kijiji kikagawanyika, kikundi cha mkuu wa wilaya na umma kwa ujumla. Mkuu wa wilaya akaitisha mkutano wake. Mbunge akaalikwa, akajaribu kuelezea sakata lilivyokuwa, kikundi cha wazomeaji kikapiga kelele. Mkuu wa wilaya sasa akataka kutangaza kwamba anamrudisha mwenyekiti wa kijiji. Wananchi wakakataa na wakamwambia bayana kuwa hana mamlaka hayo. Mkutano ukavurugika na haukumalizika kwa suluhu. Kwa taarifa tu ni kuwa Mkurugenzi(ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kutangaza kiti wazi baada ya wananchi kuamua kumwondoa kiongozi wa kijiji au kiongozi kutoka kwa sababu yoyote) anaelekea kutangaza kwamba ndani ya siku saba zijazo atatangaza utaratibu wa kujaza nafasi wazi ya mwenyekiti wa kijiji hicho. Huu ni ushuhuda kwamba Mwenyekiti huyo ameondolewa ambalo ndilo hitaji la wananchi wa kijiji hicho lililoungwa mkono na Mbunge wa CHADEMA, kama taratibu zingekuwa zimekiukwa huyo Mwenyekiti si angeendelea kuwa katika nafasi yake? nawapongeza wananachi kijiji hicho kwa kuendeleza falsafa ya nguvu ya umma. Hakuna Kulala....

JJ
 
Mawakala wa serikali wakapanga watu wao wa kuvuruga mkutano. Kwa taarifa za baadhi ya wakazi wa huko kampuni ya Barick ilichangia uchinjaji wa ng'ombe na ugawaji wa pombe kwa kundi la wazomeaji


Mkuu Mnyika,

Heshima mbele, leo asubuhi tumeikataa ile article against Dr. Slaa, kuwa haina faida yoyote kwa taifa letu, na ni too low kuwepo hapa forum, imetolewa imetupwa mbali na haipo tena,

sasa usiturudishe tena kule kule kwenye nyepesi nyepesi, hapa hatutaki unazi au taarifa za vyama vya siasa, no! viongozi wa CCM wamezomewa, tumewapa heko wananchi, na ni leo tu ndio tumegundua kuwa kumbe huu mchezo wa kuzomewa viongozi ulianzia ndani ya CCM, kwa mujibu wa Butiku,

Kama kuna mbunge wa upinzani amezomewa, basi amezomewa, unless kama hakuzomewa, lakini hata wewe unakubali kuwa alizomewa. FULL STOP! Sisi tutaangalia hoja ndani ya hiyo article na kuamua kama kuzomewa kwake ilikuwa ni muhimu kwa maendeleo ya taifa letu, au hapana, anything less ni unazi hatuutaki tena siku hizi hapa, tumeamua ku-grow up na kukata ishus kiuhakika na in fairness, uonekane kwenye ishu zingine pia sio kusubiri tu kuja ku-spinn habari nyepesi nyepesi hapa,

Hapa sasa ni taifa kwanza, hivyo vyama vyenu na kuzomeana mpeleke huko, tunachohitaji kujua hapa ni mbunge aliyezomewa alikuwa na hoja gani muhimu kwa taifa?

Ahsante Mkuu!
 
Wangwe alikumbana na dhahama hiyo katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Stanley Kolimba baada ya Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na kufunga ofisi. Aliitisha mkutano huo mahsusi kuelezea taratibu za kufuatwa wakati wa kumfukuza kiongozi wa serikali ya kijiji anapokuwa anatuhumiwa kwa jambo lolote.

Katika ufafanuzi, Mshauri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mkoani Mara, Laxford Miyaye alisema njia zilizotumiwa na Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyakunguru, Abel Maginga na kufunga ofisi yake kwa tuhuma mbalimbali, haukuwa sahihi. Alisema kiongozi anapotuhumiwa ni lazima kwanza ajadiliwe na Kamati ya Serikali ya Kijiji na apewe nafasi ya kujitetea mbele ya Mkutano Mkuu wa kijiji ndipo uamuzi utatolewa. Miyaye alieleza kuwa mkutano wa Mbunge alioufanya Septemba 26, mwaka huu na kuamua kumfukuza mwenyekiti huyo uongozi na kufunga Ofisi ya Serikali ya Kijiji ni kinyume cha taratibu za uendeshaji.

Baadaye Wangwe alipata nafasi ya kutoa maoni yake na kueleza msimamo wake kwamba uamuzi alioufikia ni sahihi na ndipo wananchi walipomcharukia na kumtaka aache mazungumzo yake wakipiga kelele wakisema, “wewe ni mchochezi, hatutaki mambo yako, toka hapo hatuna haja na uongo wako.”

Licha ya Mbunge huyo kuwa mkali na kuwaambia wafunge midomo yao wamsikilize, walisisitiza hawamtaki na kamwe hawatamsikiliza. Hali hiyo ilimfanya Mbunge huyo wa Chadema atamke kwa hasira kuwa “msinibabaishe, kwanza mimi hamkunichagua.”


Mkuu Mnyika,

Hebu soma vizuri hapa, utaona hoja na pumba ziko wapi, as opposed na taarifa zako za chama za spinning, wewe kweli huwezi kuona kuwa hapa wananchi walikuwa na haki ya kumzomea huyo mbunge asiyekuwa na heshima kwa wananchi anaowaongoza?

Hata mimi ningekuwepo ningemzomea huyo mpuuzi! Hawa ndio sasa wanachukulia heshima zetu kwa kina Zitto, na Dr. Slaa, for granted na wewe pia, hivi umeona kina Freeman na Zitto, hapa wakiandika na spinning kama wewe? Yaani wewe ishu yoyote ni spinning tu na unazi, mkuu grow up! Huu uwanja sasa sio wa unazi tena tunataka kukata serious ishus hapa, na ukweli ni kwamba mbunge amekosea ndio maana aezomewa na wananchi!
 
Mkuu Mnyika,

Heshima mbele, leo asubuhi tumeikataa ile article against Dr. Slaa, kuwa haina faida yoyote kwa taifa letu, na ni too low kuwepo hapa forum, imetolewa imetupwa mbali na haipo tena,

sasa usiturudishe tena kule kule kwenye nyepesi nyepesi, hapa hatutaki unazi au taarifa za vyama vya siasa, no! viongozi wa CCM wamezomewa, tumewapa heko wananchi, na ni leo tu ndio tumegundua kuwa kumbe huu mchezo wa kuzomewa viongozi ulianzia ndani ya CCM, kwa mujibu wa Butiku,

Kama kuna mbunge wa upinzani amezomewa, basi amezomewa, unless kama hakuzomewa, lakini hata wewe unakubali kuwa alizomewa. FULL STOP! Sisi tutaangalia hoja ndani ya hiyo article na kuamua kama kuzomewa kwake ilikuwa ni muhimu kwa maendeleo ya taifa letu, au hapana, anything less ni unazi hatuutaki tena siku hizi hapa, tumeamua ku-grow up na kukata ishus kiuhakika na in fairness, uonekane kwenye ishu zingine pia sio kusubiri tu kuja ku-spinn habari nyepesi nyepesi hapa,

Hapa sasa ni taifa kwanza, hivyo vyama vyenu na kuzomeana mpeleke huko, tunachohitaji kujua hapa ni mbunge aliyezomewa alikuwa na hoja gani muhimu kwa taifa?

Ahsante Mkuu!

Kaka:

Hapa sijaweka unazi. Nilichokifanya ni kutoa taarifa tu ya kilichojiri huko kijijini. Nimepiga simu kwa Mbunge Chacha Wangwe na nimezungumza pia na viongozi wengine wawili. Anyway, wakati utasema.

Nikipata taarifa tofauti na hizi ambazo nimepokea asubuhi hii niko tayari kuondoa hayo maelezo niliyoyatoa.

Tuendelee kumkoma nyani..

JJ
 
Naam, sasa hivi ni Tanzania kwanza kabla ya hivyo vyama vya upinzani. Wangekuwa makini hiki kipindi ni kizuri sana kwa wao kuweka mikakati ya kuvunja vyama vyao na kuunda chama kimoja chenye nguvu siyo kwa maslahi yao bali kwa maslahi ya Tanzania na Watanzania.
 
Wangwe alikumbana na dhahama hiyo katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Stanley Kolimba baada ya Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na kufunga ofisi. Aliitisha mkutano huo mahsusi kuelezea taratibu za kufuatwa wakati wa kumfukuza kiongozi wa serikali ya kijiji anapokuwa anatuhumiwa kwa jambo lolote.

Katika ufafanuzi, Mshauri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mkoani Mara, Laxford Miyaye alisema njia zilizotumiwa na Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyakunguru, Abel Maginga na kufunga ofisi yake kwa tuhuma mbalimbali, haukuwa sahihi. Alisema kiongozi anapotuhumiwa ni lazima kwanza ajadiliwe na Kamati ya Serikali ya Kijiji na apewe nafasi ya kujitetea mbele ya Mkutano Mkuu wa kijiji ndipo uamuzi utatolewa. Miyaye alieleza kuwa mkutano wa Mbunge alioufanya Septemba 26, mwaka huu na kuamua kumfukuza mwenyekiti huyo uongozi na kufunga Ofisi ya Serikali ya Kijiji ni kinyume cha taratibu za uendeshaji.

Baadaye Wangwe alipata nafasi ya kutoa maoni yake na kueleza msimamo wake kwamba uamuzi alioufikia ni sahihi na ndipo wananchi walipomcharukia na kumtaka aache mazungumzo yake wakipiga kelele wakisema, “wewe ni mchochezi, hatutaki mambo yako, toka hapo hatuna haja na uongo wako.”

Licha ya Mbunge huyo kuwa mkali na kuwaambia wafunge midomo yao wamsikilize, walisisitiza hawamtaki na kamwe hawatamsikiliza. Hali hiyo ilimfanya Mbunge huyo wa Chadema atamke kwa hasira kuwa “msinibabaishe, kwanza mimi hamkunichagua.”


Mkuu Mnyika,

Hebu soma vizuri hapa, utaona hoja na pumba ziko wapi, as opposed na taarifa zako za chama za spinning, wewe kweli huwezi kuona kuwa hapa wananchi walikuwa na haki ya kumzomea huyo mbunge asiyekuwa na heshima kwa wananchi anaowaongoza?

Hata mimi ningekuwepo ningemzomea huyo mpuuzi! Hawa ndio sasa wanachukulia heshima zetu kwa kina Zitto, na Dr. Slaa, for granted na wewe pia, hivi umeona kina Freeman na Zitto, hapa wakiandika na spinning kama wewe? Yaani wewe ishu yoyote ni spinning tu na unazi, mkuu grow up! Huu uwanja sasa sio wa unazi tena tunataka kukata serious ishus hapa, na ukweli ni kwamba mbunge amekosea ndio maana aezomewa na wananchi!

Es:

Tarime ina mambo mengi, hivyo ni vyema tusiende kwenye hitimisho haraka. Binafsi nisingependa kutimisha mjadala huo kwa kusema ni X na Y. Unakumbuka siku kadhaa nyuma lilizuka sakata kama hili na Habari leo ikataarifu kuwa Mbunge awatoa wahalifu na kueleza kuwa wananchi wamlalamkia kwa kitendo hicho. Again, it was chacha with lissu. Baada ya muda yaliyotokea ni tofauti kabisa. Na ilikuja kujulikana wazi ni nini chacha alikuwa akisimamia==syndicate ya yanayoitwa mabaraza ya jadi na genge la ufisadi kiasi kwamba ordinary justice system eg police and primary courts were ignored. Kuna mambo mengi sasa nyuma ya uwekezaji katika madini kule Tarime. Ombi langu tu-mwanakijiji afanye interview na Chacha Wangwe 0713488133, ni vyema katika hatua ya sasa kuzungumza na source moja kwa moja. Azungumzie suala hili la masuala ya madini kule kwa ujumla. Migogoro kati ya wananchi na makampuni ya madini nk. Nadhani hapo tutapata mahali pazuri pa kuendeleza mjadala huu.

Tuendelee kujadili

JJ
 
Katika ufafanuzi, Mshauri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mkoani Mara, Laxford Miyaye alisema njia zilizotumiwa na Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyakunguru, Abel Maginga na kufunga ofisi yake kwa tuhuma mbalimbali, haukuwa sahihi. Alisema kiongozi anapotuhumiwa ni lazima kwanza ajadiliwe na Kamati ya Serikali ya Kijiji na apewe nafasi ya kujitetea mbele ya Mkutano Mkuu wa kijiji ndipo uamuzi utatolewa. Miyaye alieleza kuwa mkutano wa Mbunge alioufanya Septemba 26, mwaka huu na kuamua kumfukuza mwenyekiti huyo uongozi na kufunga Ofisi ya Serikali ya Kijiji ni kinyume cha taratibu za uendeshaji.

Hii hoja ni very serious mkuu, kuhusiana na hii ishu!
 
Katika ufafanuzi, Mshauri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mkoani Mara, Laxford Miyaye alisema njia zilizotumiwa na Mbunge huyo kumfukuza Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyakunguru, Abel Maginga na kufunga ofisi yake kwa tuhuma mbalimbali, haukuwa sahihi. Alisema kiongozi anapotuhumiwa ni lazima kwanza ajadiliwe na Kamati ya Serikali ya Kijiji na apewe nafasi ya kujitetea mbele ya Mkutano Mkuu wa kijiji ndipo uamuzi utatolewa. Miyaye alieleza kuwa mkutano wa Mbunge alioufanya Septemba 26, mwaka huu na kuamua kumfukuza mwenyekiti huyo uongozi na kufunga Ofisi ya Serikali ya Kijiji ni kinyume cha taratibu za uendeshaji.

Hii hoja ni very serious mkuu, kuhusiana na hii ishu!

Kaka

I agree, as long as it is as it is!

Rule of Law Vs Law of the Ruler

JJ
 
Mkuu Mnyika,

Heshima mbele, leo asubuhi tumeikataa ile article against Dr. Slaa, kuwa haina faida yoyote kwa taifa letu, na ni too low kuwepo hapa forum, imetolewa imetupwa mbali na haipo tena,

sasa usiturudishe tena kule kule kwenye nyepesi nyepesi, hapa hatutaki unazi au taarifa za vyama vya siasa, no! viongozi wa CCM wamezomewa, tumewapa heko wananchi, na ni leo tu ndio tumegundua kuwa kumbe huu mchezo wa kuzomewa viongozi ulianzia ndani ya CCM, kwa mujibu wa Butiku,

Kama kuna mbunge wa upinzani amezomewa, basi amezomewa, unless kama hakuzomewa, lakini hata wewe unakubali kuwa alizomewa. FULL STOP! Sisi tutaangalia hoja ndani ya hiyo article na kuamua kama kuzomewa kwake ilikuwa ni muhimu kwa maendeleo ya taifa letu, au hapana, anything less ni unazi hatuutaki tena siku hizi hapa, tumeamua ku-grow up na kukata ishus kiuhakika na in fairness, uonekane kwenye ishu zingine pia sio kusubiri tu kuja ku-spinn habari nyepesi nyepesi hapa,

Hapa sasa ni taifa kwanza, hivyo vyama vyenu na kuzomeana mpeleke huko, tunachohitaji kujua hapa ni mbunge aliyezomewa alikuwa na hoja gani muhimu kwa taifa?

Ahsante Mkuu!

kumbe saa nyingine huwa tunaongea lugha moja ! great. hapo heshima tena GRADE A, !
 
Mia bana huwa sipendi kitu ambacho wananchi wanajitolea kufanya wenyewe (mfano kuzomea wapinzani) halafu watu wataanza kuruka na kusema ccm imekodisha watuwakamzomee, yaani hii kitu ni kama kidonda, wananchi wanajua nini pumba jamani sasa msione wapinzani leo wamezomewa mkaanza kukataa, kama utakubali utamu basi kubali chungu na chachu vile vile.

CCM TAKES THE GOOD AND THE BAD. sasa tuendelee kukata ishu, lakini kuzomea viongozi haitoleta maendeleo, bali kuamsha akili zao, hivyo kuongeza umakini wao katika wanayofanya. Viongozi wa ccm walivyozomewa, watu walikuwa wanafurahi kuliko, yaani utadhani ndio ulikuwa ulikuwa mwisho wa ccm, lakini wakachoka, ndio maana nikasema huwezi kuwa kwenye limelight milele, utakaa tu pale muda, utapenda raha utaondolewa. leo haya maneno yamewakuta chadema, sasa tuendelee kusukuma gurudumu la maendeleo, na tuache mapenzi na ushabiki wa vyama kupita kiasi !
 
Es:

Tarime ina mambo mengi, hivyo ni vyema tusiende kwenye hitimisho haraka. Binafsi nisingependa kutimisha mjadala huo kwa kusema ni X na Y. Unakumbuka siku kadhaa nyuma lilizuka sakata kama hili na Habari leo ikataarifu kuwa Mbunge awatoa wahalifu na kueleza kuwa wananchi wamlalamkia kwa kitendo hicho. Again, it was chacha with lissu. Baada ya muda yaliyotokea ni tofauti kabisa. Na ilikuja kujulikana wazi ni nini chacha alikuwa akisimamia==syndicate ya yanayoitwa mabaraza ya jadi na genge la ufisadi kiasi kwamba ordinary justice system eg police and primary courts were ignored. Kuna mambo mengi sasa nyuma ya uwekezaji katika madini kule Tarime. Ombi langu tu-mwanakijiji afanye interview na Chacha Wangwe 0713488133, ni vyema katika hatua ya sasa kuzungumza na source moja kwa moja. Azungumzie suala hili la masuala ya madini kule kwa ujumla. Migogoro kati ya wananchi na makampuni ya madini nk. Nadhani hapo tutapata mahali pazuri pa kuendeleza mjadala huu.

Tuendelee kujadili

JJ

mnyika sasa unaanza kuboa, you people ALWAYS HAVE EXCUSES tena pale mnapokuwa mambo yenu yameenda kombo, bora ungeuchuna kama hakijatokea kitu ! lakini hizi excuses bana hazina maana yoyote mie sitaki kuzisikia mkuu.
 
Licha ya Mbunge huyo kuwa mkali na kuwaambia wafunge midomo yao wamsikilize, walisisitiza hawamtaki na kamwe hawatamsikiliza. Hali hiyo ilimfanya Mbunge huyo wa Chadema atamke kwa hasira kuwa "msinibabaishe, kwanza mimi hamkunichagua."[/QUOTE]

hii ni dharau sana mkuu. mimi naamini kura ni siri na yeye alichaguliwa kwa wingi wa kura. Amejuaje hao hawakumchagua? hivi kweli hii sio kukosea heshima waajiri wako (wananchi) unajua huku ni kujisahau na wanasiasa wengi wanatabia hii. Wakienda kuomba kura kwa wananchi wanaenda mikono nyuma lakini wakishapata wanawatusi.
 
halafu ndio watu wanapiga kelele na kubase points zao kwa kutumia chama, kama ni hivyo basi huyu mtu amekiuma chama chake, lakini kwa watu tunaotaka maendeleo, we wont sweat, kakosea yeye binafsi na sio chadema, akikosea kiongozi wa ccm vile vile msiseme ccm haifai !

lakini jamaa ameboronga yaani ile pure kuboronga big taimu tu !
 
heee heee ya father Dito kujibizana na wanatabora yalikuwa mapana hapa, sasa na huyu chacha nae jaziba zimezidi mno ndio maneno gani ya kujibishana na wananchi, fikiria kidogo angekuwa waziri wa madini au rais wa jamhuri majibu yake yangekuwa yepio kwa wananchi?

nnaaamini angeamuru wakatiwe viboko wote, ukweli chadema bado chelema tena sana
 
heee heee ya father Dito kujibizana na wanatabora yalikuwa mapana hapa, sasa na huyu chacha nae jaziba zimezidi mno ndio maneno gani ya kujibishana na wananchi, fikiria kidogo angekuwa waziri wa madini au rais wa jamhuri majibu yake yangekuwa yepio kwa wananchi?

nnaaamini angeamuru wakatiwe viboko wote, ukweli chadema bado chelema tena sana


Natumaini huyu jamaa nae hamiliki silaa maana kwa hasira hizi anaweza aka Ditto mwananchi hivihivi. Hapa naona watu wamekaa kimya njooni hapa mseme. Kuzomewa ni kuzomewa tuu nakumbuka waziri alisema hiyo ni sehemu ya siasa sasa hasira za nini?
 
hii ni dharau sana mkuu. mimi naamini kura ni siri na yeye alichaguliwa kwa wingi wa kura. Amejuaje hao hawakumchagua? hivi kweli hii sio kukosea heshima waajiri wako (wananchi) unajua huku ni kujisahau na wanasiasa wengi wanatabia hii. Wakienda kuomba kura kwa wananchi wanaenda mikono nyuma lakini wakishapata wanawatusi.
Bila shaka amejua hao ni ccm akang'aka "Kwanza ninyi hamkunichagua..." Hata hivyo lazima katika sukari iliyo tamu kuwe na chungu yake japo kidogoooo. Alipanda ndege ya Barrick au helicopter, sijaelewa kapanda ndege ya mawakala wa ufisadi?
 
Bila shaka amejua hao ni ccm akang'aka "Kwanza ninyi hamkunichagua..." Hata hivyo lazima katika sukari iliyo tamu kuwe na chungu yake japo kidogoooo. Alipanda ndege ya Barrick au helicopter, sijaelewa

Kwa taarifa hiyo ni kuwa alipanda ndege ya Barrick. Yeah kweli nadhani nayeye hakutegemea kuzomewa ndio maana aling'aka nadhani kidogo angewaambia kazomeeni wake zenu kama Ditto.

Duh lakini kwenye hiyo picha yako unaonekana mrembo kichizi yaani AFrican Queen sio utani hata mie nimekolea hapo.
 
Natumaini huyu jamaa nae hamiliki silaa maana kwa hasira hizi anaweza aka Ditto mwananchi hivihivi. Hapa naona watu wamekaa kimya njooni hapa mseme. Kuzomewa ni kuzomewa tuu nakumbuka waziri alisema hiyo ni sehemu ya siasa sasa hasira za nini?

wale waliokuwa wanazomewa na wananchi INAFAHAMIKA kwamba walikuwa wanazomewa hapa JF kwa kuwa walikuwa ccm. yah that is a statement niliyosema. kwa nini nasema hivyo ?
kama kweli sio sababu ya chama chao, leo hii mbona wamezomewa hawa jamaa wa upinzani na wale waliokuwa wanawazomea viongozi wa ccm JF hawaji kuja kumzomea huyu jamaa wa chadema ? ITS CLEAR AND SIMPLE, yaani PURE SIMPLICITY kwamba makosa ya waliokuwa wanazomewa viongozi wa mwanzo ni sababu za kichama na si vinginevyo !
 
Back
Top Bottom