Mbunge Musukuma: Walioambiwa wale kwa urefu wa kamba zao hawanunui kamba za katani wanatumia manati, likijaa linatanuka

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626

Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku 'Musukuma'

Vikao vya bunge vimefunguliwa rasmi leo tarehe 4/4/2023. Katika kikao cha leo, shughuli za Bunge zilisimamishwa kwa ajili ya Azimio la kumpogeza Rais, ambapo Wabunge walipata nafasi ya kutoa pongezi zao.

Kwa upande wa Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku 'Musukuma' amesema kwenye madudu yaliyoibuliwa na CAG, kuna viongozi wanaiba sehemu moja na kuhamishwa sehemu nyingine wanaenda kuendeleza wizi sehemu nyingine

Akisema kuwa TAKUKURU ina mrundikano wa kesi kutoka CAG na kama TAKUKURU kuna madudu pia basi waundiwe tume ya kuwachunguza. Akisema haiwezakani watu hao watajwe mwaka jana na mwaka huu pia bila kushughulikiwa.

Akasema Rais alisema kama wanakula basi wale kwa urefu wa kamba zao lakini hao hananunui kamba za katani, wananunua manati likijaa linatanuka.

Msukuma pia amesema hawataki tena kupiga swaga kwani kila CAG wanaongea lakini watu hawachukuliwi hatua. Amedai mwaka jana wameyajadili na mwaka huu watu hao hao wamepata hati chafu.
 
Thanks discassants

Ukweli ni kuwa sio kilichotajwa na CAG kipo kama kinavyozungumzwa

Ngoja waje hao wataalam wanaosemwa humu wanapangua hoja moja baada ya nyingine

Maana hao wanaosemwa wezi sometimes ni kukosekana kwa viambata au risiti tu lakini kila kitu kipo Ofisini labda wakati CAG anapita vilikuwa havipo

Ngoma hii huwa inaanzaga kwa vigeregere nderemo na vifijo ila itaisha kimya kimya kila mtu ataondoka kwa njia yake

Taarifa ya CAG inaonesha upotevu wa fedha na matumizi ya hovyo lakini haiainishi kabisa udhaifu wa taratibu kanuni na sheria za manunuzi ya umma.

Ila ngoja tuone ila hayo masheria na makanuni na mataratibu ya manunuzi ya umma mamifumo n.k ndio kwa kiasi vikubwa yanachangia kutokea kwa haya yanayoonekana
 
Au Mimi kichwani ni mweupe? Wabunge ni wajumbe wa mabaraza ya madiwani kwenye halmashauri zao. Inakuwaje wawalaumu wakurugenzi wa halmashauri zao kwa matumizi ambayo wao walishiriki kuyapitisha kwenye vikao vya kanseli walivyoshiriki? Huu nao ni unafiki uliokubuhu ambao unawadhalilisha Sana Ila kwa kuwa wamekuwa na ngozi ngumu wanaona sawa tu kuwalaumu wakurugenzi na hii siyo sawa!
Nashauri tu kuwa cag akiikagua halmashauri na kuipa hati chafu au yenye mashaka Basi impendeze mbunge, madiwani na mkurugenzi waachishwe nafasi zao na wafunguliwe mashitaka ya ufisadi Mara moja. Njia hii itakomesha mchwa wote waliojaa kwenye halmashauri zetu na kwenye ofisi za umma. Nawasilisha.
 
View attachment 2576181
Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku 'Musukuma'

Vikao vya bunge vimefunguliwa rasmi leo tarehe 4/4/2023. Katika kikao cha leo, shughuli za Bunge zilisimamishwa kwa ajili ya Azimio la kumpogeza Rais, ambapo Wabunge walipata nafasi ya kutoa pongezi zao.

Kwa upande wa Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku 'Musukuma' amesema kwenye madudu yaliyoibuliwa na CAG, kuna viongozi wanaiba sehemu moja na kuhamishwa sehemu nyingine wanaenda kuendeleza wizi sehemu nyingine

Akisema kuwa TAKUKURU ina mrundikano wa kesi kutoka CAG na kama TAKUKURU kuna madudu pia basi waundiwe tume ya kuwachunguza. Akisema haiwezakani watu hao watajwe mwaka jana na mwaka huu pia bila kushughulikiwa.

Akasema Rais alisema kama wanakula basi wale kwa urefu wa kamba zao lakini hao hananunui kamba za katani, wananunua manati likijaa linatanuka.

Msukuma pia amesema hawataki tena kupiga swaga kwani kila CAG wanaongea lakini watu hawachukuliwi hatua. Amedai mwaka jana wameyajadili na mwaka huu watu hao hao wamepata hati chafu.
sasa kama maza alisema mwenyewe analalamika nini et...
 
Back
Top Bottom