Safi sana jeshi la polisi,kamata magaidi wote
Soma alama za nyakati. Kama ujui lema kakamatwa kwa sababu gani. Basi wewe ni kilaza wa kutupwa. Wahehe atupo kama wewe, unatudhalilisha sana ndugu. Kila mtanzania anasubiri mageuzi 2015 sasa wewe endelea kujipendekeza itakukosti.Tunaomba updates na pia kama unajua sababu zozote za Llema kukamatwa
Na.inasikitisha sana tuna wanasiasa magaidi na wahuni
Mlioko Arusha hali ikoje na nini kinajiri ?
kwa kweli walio karibu na lema wanatakiwa wamuweke kitako na kumshauri kuhusu mwendo anaenda nao. siasa sio ugomvi na kutengeneza matatizo kila siku
kuna njia nyingi za kupita kufanya siasa. hii njia aliochagua inashangaza sana tena sana. mbona kuna wabunge wengi wa chadema na vyama vyengine hawabehave kama yy? hata wenziwe mwisho watamchoka
Kwenye nchi hii kukamatwa hakutegemei mtu kuwa na kosa la jinai. Kama ni hivyo Kamanda Kamuhanda angekuwa amekamatwa kwa kuwa tume ya haki za binadamu ilimuona amehusika katika mauaji ya Mwangosi. Akili ya kawaida inaweza kukutuma kuamini kuwa kushinda kwake ubunge na kauuli zake za hivi karibuni dhidi ya mkuu wa nchi zinatosha kuwafanya wasaidizi wake kumkamata. Kama tatizo ni yaliyotokea chuoni kulikuwa na sababu gani kwa mfano ya kulichukua gari lake kituoni? Na kama anahusishwa na vurugu za wanachuo ni mtu gani mwenye weledi wa kawaida tu asiyeona ukosefu wa kusoma saikolojia ya watu ulivyosababisha kauli za mkuu wa mkoa kuzua tafrani iliyotokea. Lema anachukiwa, Lema anawindwa, na wanaofanya hivyo wamekosa busara ya kufanya matendo hayo bila kujulikana. Nguvu inayotumika kwa Lema haifanani na kosa linalotajwa. Polisi wetu lini wataacha kushughulika mambo madogo ya kudhaniwa tu na kuanza kushughulikia mamabo halisi yenye ushahidi. Wameshindwa "kuwatambua" na kuwashughulikia wang'oa kucha na meno wa Ulimboka na Kibanda na kuanza kushughulikia video za kwenye Youtube, Wameacha kushughulikia vifo vyenye utata vya wanachuo wawili - (ambalo ndilo dai la wanachuo lililozua yote haya), wanamshughulikia Lema, kana kwamba hiyo ndiyo inayojibu hitaji la wanachuo. Kama wanachuo wasingezuiwa na Lema wakaandamana hadi kwa Mkuu wa mkoa wangekuwa na kosa lipi la kumkamatia Lema? Wangemkamata kwa sababu hakuwazuia waandamanaji? Au kwa kuwa mauaji yametokea kwenye eneo lake? Hawa viongozi wetu kwa nini wanatumia nguvu kubwa zaidi kwa mambo yenye sababu dhaifu na kuacha yenye sababu nzito zilizo wazi? Mungu ibariki Tanzania
Bado unahasira za kuuwawa kwa Osama Bin Laden.aliyemuua ni rais OBANA sio LEMA.Nakukumbusha tu.Kwenye Laptop Yake Zimekutwa Vidio Za Mipango Ya Kigaid,pamoja Na Siraha Yakivita Na Kofia Za Kininja Mia 2 Alikua Amepanga Kufanya 2kio Na Vijana Baaz Yao Alipanga Nao Mipango Hiyo Alipokua Jela Kisongo Na Ndo Mana Alikua Anapenda Kwenda Jela Kumbe Alikua Anaagenda Yake Ya Kigaid,naomba Polc Mcmwachie Gaid Huyo
Sema mwalimu,utaangaika sana mwaka huu.anamakosa ya uchochez ambao umesababisha kifo cha mwanafunzi.shame on you cdm.
Hakuna kitu kama hicho lema hajashika amani ya nchi