Mi naona hata mama yake Lulu nae wa kuwekwa ndani,kwani yeye akiwa mlezi wa lulu alikuwa haoni anayofanya mwanae akamkanya? na je huyo mtoto anayedai ni wa miaka 17 alikuwa anafanya nini usiku mnene kwenye chumba cha mwanaume? unajua ngoma ikilia sana hupasuka,sasa hii ya lulu ndio imefika wakati wake. Ngoja ajifunze kwa vitendo kwamba asiyefunzwa na mama yake hufunzwa na ulimwengu. Na kuhusu hili la Komba kutembea na watoto wadogo nashauri kama kuna ushaidi nae afunguliwe mashtaka,maan mafataki kama haya ndio yanayotuharibia watoto wetu. Alafu tunamuita muheshimiwa,mpaka naskia kutapika kwa jinsi anavyonitia kichefuchefu,sijui hana mshipa wa aibu.