Mbunge Jerry Slaa akataliwa na Wananchi wa Jimbo la Ukonga mbele ya Waziri Ulega

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wafanyabiashara wa Ukonga, aliwaambia wananchi hao kuwa wanasalimiwa na Mbunge wao, ambaye pia ni waziri wa Ardhi, Jerry Slaa, lakini wananchi hao walionesha kutokubaliana na salamu hizo.


Baadhi ya wananchi walionesha kuwa wanataka kumuona, ambapo Ulega aliwaambia mbunge huyo atafika kuwasilimia. Japo hakueleza kwa nini kwa safari hiyo hakuja naye ambapo yeye ndio mbunge wa jimbo husika.

Katika Video hiyo hapo juu ni zaidi ya dakika nne Ulega amekuwa akitaka kuzitua salamu za Slaa kwa wananchi ambao wamegoma kupokea salamu hizo.
 
Ukonga kuna barabara mbovu na maji ya shida. Hata Segerea maji tatizo. Wananchi wa majimbo hayo mawili hawaogi na ni wachafu hasa kwenye daladala, tena ukutane na wanawake wa Kitunda weusi tii, wamepiga mkorogo alafu wana mawigi yanatema.
Mtu anakazana kupita kwenye vumbi akifika kwake maji ya kuoga hamna.

Atakayesema nimetukana basi aende Banana ajionee vipanya vya kwenda Kitunda uko.
 
Nimesema tafuta vitabu ujisomee.

Kazi ya mbunge ni uwakilishi . Anachukua maoni, shida, mipango na matamanio ya wananchi wa jimboni kwake halafu anayatumia kutungwa sheria, kupanga bajeti na kuisimamia serikali bungeni.
Huwa pesa za bajeti zikitoka kwa ajili ya Jimbo Fulani mbunge anafahamu na anasimamia au anakuwa yupo pembeni kabisa na hausishwi?

Nipo kujifunza
 
Huwa pesa za bajeti zikitoka kwa ajili ya Jimbo Fulani mbunge anafahamu na anasimamia au anakuwa yupo pembeni kabisa na hausishwi?

Nipo kujifunza
Hakuna pesa za bajeti kwa ajili ya Jimbo kwasabb Jimbo siyo eneo la kiutawala (administrative area/region).

Usichanganye na mfuko wa maendeleo ya Jimbo (ambayo ni kama 100M kwa kila Jimbo). Sasa pesa hii inaweza kujenga barabara ya lami? Kujenga km moja ya barabara ya lami ni Tshs 1.2 bilion (milioni 1200)

Hizi fedha kimsingi wabunge walizipanga kisiasa ili kupunguza kero kwao ya kuombwa ombwa misaada na wananchi ktk Jimbo lake. Wakajikuta wanatumia posho zao mpk wanafulia..

Kabla ya kuwekewa utaratibu mzuri wa matumizi wabunge wengi walikuwa wanazipiga kimya kimya. Lkn hv Sasa mbunge ni mwenyekiti wa mfuko, wajumbe wa mfuko ni madiwani.

Kwahiyo bajeti hupangwa kwa ajili ya majiji, mikoa na wilaya. Na kuna wilaya zina majimbo zaidi ya moja.

Kuhusu kuhusishwa na usimamizi.

Mbunge anahudhuria vikao vya baraza la madiwani linalohusika ktk kubuni, kuanzisha na kutekeleza miradi ya maendeleo ktk halmashauri ama jiji lake.

Kazi ya usimamizi hufanywa na mkuu wa wilaya akishirikiana na wakurugenzi ambaye anasaidiana na engineer wa wilaya. Ndiyo maana hujawahi kusikia mbunge anatumbuliwa kwasabb mradi fulani haujakamilika ama kuna ufisadi. Wanaotumbuliwa ni wakuu wa wilaya, wakurugenzi na wahandisi.
 
Back
Top Bottom