Waziri Jerry Silaa awataka Watumishi wa Ardhi watoke ofisini waingie mtaani kuhudumia Wananchi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Silaa amewataka Watumishi wote wa Ardhi nchini kutoka maofisini na kwenda kutoa huduma ya wananchi kwa kuanzisha Kliniko ya Ardhi ambayo itafanua kazi kwa uwazi zaidi.

Jerry Slaa ametoa agizo hilo wakati akikabidhi Hati za viwanja katika Mtaa wa Rungwa, Kata ya Kazima Mkoani Katavi ambapo ametoa agizo la kila Mtumishi wa Ardhi nchini kuwa msuluhishi wa migogoro ambayo inajitokeza hasa kwa kuanzisha Kliniki ya Ardhi ambayo inawezesha Wananchi kupata uwazi zaidi kwa kuwafikia walipo.

Kamishina Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Katavi, Chediel Mrutu amesema jumla ya wakazi wanapaswa kupewa Hati za Viwanja ni 1997 huku Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi, Idd Kimanta akimpongeza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kutatua mgogoro huo ambao ulikuwa kikwazo kwa Wananchi na Serikali kwa jumla.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Jamila Yusuf ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda ameishukuru Serikali kwa kutatua mgogoro uliodumu zaidi ya miaka 10 ambapo amewasisitiza Wananchi kutoanzisha mgogoro mwingine wa ardhi katika maeneo hayo.

Mwelelwa Nkokwa na Sesilia Baltazar wameishukuru Serikali kwa kutatua mgogoro huo na kukabidhiwa Hati Miliki ambazo zitawanufaisha katika shughuli mbalimbali za kiuchimi.

Aidha, Slaa amewapiga marufuku viongozi wa vijiji na mitaa kutojihusisha na migogoro ya ardhi na badala yake wawe wasuluhishi.
 
Wanasikia sasa

Maana hiyo kauli anaisema mara kwa,mara

Ova
 
Waziri aangalie na suala la Watendaji wa Ardhi kukaa kituo kimoja kwa zaidi ya Miaka 10 watendaji hao wakizoeleka huo ni Chanzo kikubwa cha Migogoro Mkoa wa Dar es salaam Migogoro mingi inachangiwa na Hao Watendaji wa Manispaa.

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Wanasikia sasa

Maana hiyo kauli anaisema mara kwa,mara

Ova
Siasa hizo, tatizo watanzania tunashabikia vitu bila kuchunguza kwa undani. Inaonyesha system nzima ni mbovu,haiwezekani watu wasitimize wajibu wao wa kazi mpaka kiongozi mpya aje akumbushe. Tanzania tuna safari ndefu,viongozi wetu ni mifano mibovu, maana kiongozi anatakiw kuw mfano kw wale anaowaongoza.
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Slaa amewataka Watumishi wote wa Ardhi nchini kutoka maofisini na kwenda kutoa huduma ya wananchi kwa kuanzisha Kliniko ya Ardhi ambayo itafanua kazi kwa uwazi zaidi.

Jerry Slaa ametoa agizo hilo wakati akikabidhi Hati za viwanja katika Mtaa wa Rungwa, Kata ya Kazima Mkoani Katavi ambapo ametoa agizo la kila Mtumishi wa Ardhi nchini kuwa msuluhishi wa migogoro ambayo inajitokeza hasa kwa kuanzisha Kliniki ya Ardhi ambayo inawezesha Wananchi kupata uwazi zaidi kwa kuwafikia walipo.

Kamishina Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Katavi, Chediel Mrutu amesema jumla ya wakazi wanapaswa kupewa Hati za Viwanja ni 1997 huku Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi, Idd Kimanta akimpongeza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kutatua mgogoro huo ambao ulikuwa kikwazo kwa Wananchi na Serikali kwa jumla.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Jamila Yusuf ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda ameishukuru Serikali kwa kutatua mgogoro uliodumu zaidi ya miaka 10 ambapo amewasisitiza Wananchi kutoanzisha mgogoro mwingine wa ardhi katika maeneo hayo.

Mwelelwa Nkokwa na Sesilia Baltazar wameishukuru Serikali kwa kutatua mgogoro huo na kukabidhiwa Hati Miliki ambazo zitawanufaisha katika shughuli mbalimbali za kiuchimi.

Aidha, Slaa amewapiga marufuku viongozi wa vijiji na mitaa kutojihusisha na migogoro ya ardhi na badala yake wawe wasuluhishi.
Watumishi wa ardhi ndio watumishi walioiabgusha sana nchi hii yaani leo hii tumekuwa na miji mikubwa kama vijiji vyumba zipozipo tu hakuna mpangilio na hakuna feature yyte kwenye mipango miji..

Naona serikali ikienda kupata hasara kubwa kwa kuingia gharama kubwa sana za kuipanga miji yetu upya..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom