Mbunge Festo Sanga: Ripoti inaonyesha tumekopesha zaidi ya Trilioni 3.5 kwa vijana, na bado vijana wanalalamika hakuna ajira nani anakula hizo fedha?

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mbunge wa Jimbo la Makete, akichangia katika Bunge la 13, Mkutano wa Pili, Kikao cha 6, ameeleza kuwepo kwa mifuko ya vijana katika wizara mbalimbali licha ya kuwepo kwa Wizara rasmi ya Vijana. Amesema kuna zaidi ya mifuko 70 katika wizara tofauti inayopokea fedha kwa ajili ya vijana.

Amesisitiza umuhimu wa kuwepo kwa mfuko mmoja wa vijana ili kurahisisha ufuatiliaji wa matumizi ya fedha hizo, akibainisha kuwa ripoti zinaonyesha serikali imekopesha zaidi ya Shilingi trilioni 3.5 kupitia mifuko hiyo, lakini bado vijana wanalalamikia ukosefu wa ajira.


Your browser is not able to display this video.
 

Huyo mbunge ameongea point sana
Natamani ushauri wake uchukulkiwe mara moja; hela zote za vijana ziende Wizara ya vijana.
Kama kweli 3.5trillion zimetolewa, inaonekana kuna hela nyingi hazijafikia walengwa; ziko wapi?
 
Hizi script za ccm za kutafuta kiki TU
Ccm wenyewe waibe alafu wahoji upuuzi
 
Ukirejea speech za Polepole alizungumzia sana hili swala lakini "ccm" wenzake wakamteka

Leo makonda anakwambia "amepokea" biliini mbili kwa ajili ya watengeneza maudhui mitandaoni

Watz wanageuzwa geuzwa tu kama samaki
 
Walichukua vijana wa CCM kama zawadi.
 
Ukifatilia ripoti zinazotoka serikali unaweza ukasema mambo ni mazuri kumbe ukija field ni tofauti....Usikute Mkurugenzi ameeandaa vikundi hewa vya vijana wakapiga mabilioni.

Nina uhakika kwamba 10% kwa vijana haziendi kwa vijana ,hizo pesa wanakula madiwani na Ma DED.
 
Na watendaji wa kata na mitaa/vijiji. Ndio wanaokula hela hizo.
 
Wanakula mafisango
 
Na watendaji wa kata na mitaa/vijiji. Ndio wanaokula hela hizo.
Yap ,walio kwenye chain ya kuwasajili vijana ndiyo wanaopiga hizo pesa kwa kuaandaa vikundi vyao hewa ,serikali inajua imewapa pesa vijana na kuandaa pesa kumbe imeenda kwa WAHUNI wachache.
 
Mwambie festo sanga atafute zile nondo za polepole mbona altogether hili nani anakula hizo pesa au akumsikiliza
 
Hii ndio mbinu mpya wameambiwa wafanye kurudisha credibility ya bunge kufatiliwa...ukienda Yutubu unakuta 8 watching
 
Huyo mbunge ameongea point sana
Natamani ushauri wake uchukulkiwe mara moja; hela zote za vijana ziende Wizara ya vijana.
Kama kweli 3.5trillion zimetolewa, inaonekana kuna hela nyingi hazijafikia walengwa; ziko wapi?
Ziko wapi? Zimetumika kufanyia anasa umalaya na mengineyo ...hazijafika kwa vijana.
 
Huyo mbunge ameongea point sana
Natamani ushauri wake uchukulkiwe mara moja; hela zote za vijana ziende Wizara ya vijana.
Kama kweli 3.5trillion zimetolewa, inaonekana kuna hela nyingi hazijafikia walengwa; ziko wapi?
Nawewe unaamini kuwa ni kweli kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…