Cannibal OX
JF-Expert Member
- Aug 27, 2014
- 3,096
- 3,478
Wanatakiwa kulipa kodi, wanathubutuje kuitaka Serikali iongeze ukusanyaji wa mapato mengi wakati wao wenyewe hawalipi kodi? HAKI NA WAJIBU NA USAWA UKO WAPI?
Pamoja na hayo mkuu wabunge huchangia pesa nyingi kwenye majimbo yao kuanzia misiba,wenye shida mbalimbali sasa unadhani hiyo michango mikubwa bila hiyo pesa wataiweza, labda utakuwa huishi kwenye majimbo yaliyo nje ya Darisalama,kama ungekuwa huku vijijini ungeona jinsi wabunge wanavyotoa michango yao kwenye shughuli nyingi za wapiga kura wao, naamini pia kama una uwezo watu wanaokupiga mizinga kila siku ni wengi ,huyu atakuomba hiki na mwingine kile. Watu wengi wanaolaumu ndio hao hao kila siku wamekuwa ombaomba kwa watu wenye vipato wakiwemo wabunge.Mbunge analipwa mshahara wa 3.8M kwa mwezi, anapata posho 8M kila mwezi, jumla 11.8M. Akiwa kwenye kikao analipwa posho ya kikao 240K kwa siku na posho ya kujikimu 120K, jumla 360K. Bunge la bajeti litakaa kwa miezi mitatu, akihudhuria vikao vyote atapata 32M, wastani wa 10M kwa mwezi. Kwahiyo hii miezi mitatu ya bunge la bajeti Mbunge ana uhakika wa kukunja 22M kila mwezi.
Sambamba na hayo anapewa mkopo wa 90M kwa ajili ya gari na bima ya afya daraja la kwanza inayomruhusu kutibiwa yeye na familia yake ndani na nje ya nchi. Anapewa lita 1,000 za mafuta kila mwezi. Vyote hivyo havikatwi kodi. Mtumishi mwenye mshahara wa laki mbili, anakatwa kodi, anakatwa mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF/PSSSF), anakatwa bima ya afya, LAKINI Mbunge mwenye karibu 12M kwa mwezi, na marupurupu kibao hachangii chochote kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, hachangii kodi, wala hachangii bima ya afya.
Baada ya miaka mitano, Mbunge huyohuyo anapewa kiinua mgongo cha 240M, ambacho hakuwahi kukatwa kuchangia hata mwezi mmoja. Je pesa hizi za kiinua mgongo anazolipwa zinatoka wapi kama alikua hakatwi? Jibu ni.kwamba zinatoka kwa watanzania maskini including wale wanaolipwa laki mbili kwa mwezi.Halafu Mbunge mmoja bila aibu anademka eti watanzania walipe tena kodi kwa kutumia simu zao. Yeye anaiita kodi ya uzalendo na ameshauri ilipwe kila siku. Yani kila ukiamka unakatwa kiasi fulani cha pesa kwenye simu yako kama kodi ya uzalendo.
Wabunge walipaswa kuonesha mfano wa uzalendo. Wakatwe kodi kwenye mishahara yao na posho zao zote. Mbunge akiangalia salary slip yake aone Gross salary ni 11.8M lakini Net saalary ni 7M. Akatwe Bima ya afya, akatwe pensheni pia. Hapo atakua na adabu na ataongea lugha moja na wananchi, maana atakua anafeel kile wananchi wake wanafeel.
Na akipoteza ubunge akiwa na miaka 30 asubirie hadi afikishe miaka 60 ndipo apate mafao yake. Wale wanaopoteza ubunge wakiwa na mika zaidi ya 60 ndio wapewe mafao yao kwa wakati. Na wapewe kwa kadri walivyochangia kwenye mifuko ya hifadhi za jamii. Kama alikua anakatwa 500K kwa mwezi kwa ajili ya pensheni means baada ya miaka mitano atakua amechangia 30M. Hiyo ndio haki yake, lakini asipewe hadi afikishe miaka 60.
Hapa ndio tutaona kweli ni wazalendo. Sio wanatunga sheria za kiiimla kukandamiza wanyonge, halafu wao wanajiondoa kwenye sheria hizo. Wanaishi kwenye dunia yao halafu wakishavimbiwa nyama choma na Dompo wine, wanabweka kuhusu uzalendo. Uzalendo gani wakati umezuia fao la kujitoa kwa vijana maskini, while wewe unavuta mshiko kila baada ya miaka mitano?
Unatunga sheria kuwa kijana maskini aliyetoka chuo akapata ka mkataba ka miaka miwili, akimaliza mkataba wake eti asilipwe mafao yake hadi afikishe miaka 60. Lakini wewe ukipoteza ubunge na miaka 35 unataka uvute mafao yako fasta. Hutaki kusubiri ufikishe miaka 60. Huu ndio uzalendo mnaohubiri?
Halafu hawa watanzania unaotaka walipe kodi ya uzalendo kupitia simu zao ni wapi? Hawahawa maskini au kuna wengine? Tanzania ina watumiaji wa simu za mkononi milioni 40. Kati yao watanzania milioni 8 matumizi yao kwenye simu hayafiki TZS 1,000/= kwa mwezi. Yani kuna watanzania milioni 8 ambao ndani ya mwezi mzima hawawezi kutumia "buku" kwenye simu. Hawa ndio wanataka kukamuliwa kodi ya uzalendo na watu wanaolipwa 12M kwa mwezi.
Mwizi huyuashukuriwe Malissa GJ kwa uandishi makini japo hujampa credit...
Hiyo ni hoja nzuri. Kwa nini wao was iwe mstari wa mbele kuwa mfano... Badala ya kuhubiri Uzalendo bila vitendo. Hakuna justification yeyote kwa nini wasikatwe kodi hasa kwenye mshahara wao.Nasikia kuwa wabunge wako kwenye kundi la wasiokatwa kodi. Kama ni kweli ni kwanini?
Nchi yetu bado ni changa, kama kweli tuko serious tunataka kuijenga nchi yetu wabunge lazima waonyeshe uzalendo kwa kukatwa kodi ya mapato.
Hakuna mahali duniani ambapo posho inazidi mshahara... Only in TZ.Mbunge analipwa mshahara wa 3.8M kwa mwezi, anapata posho 8M kila mwezi, jumla 11.8M. Akiwa kwenye kikao analipwa posho ya kikao 240K kwa siku na posho ya kujikimu 120K, jumla 360K. Bunge la bajeti litakaa kwa miezi mitatu, akihudhuria vikao vyote atapata 32M, wastani wa 10M kwa mwezi. Kwahiyo hii miezi mitatu ya bunge la bajeti Mbunge ana uhakika wa kukunja 22M kila mwezi.
Sambamba na hayo anapewa mkopo wa 90M kwa ajili ya gari na bima ya afya daraja la kwanza inayomruhusu kutibiwa yeye na familia yake ndani na nje ya nchi. Anapewa lita 1,000 za mafuta kila mwezi. Vyote hivyo havikatwi kodi. Mtumishi mwenye mshahara wa laki mbili, anakatwa kodi, anakatwa mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF/PSSSF), anakatwa bima ya afya, LAKINI Mbunge mwenye karibu 12M kwa mwezi, na marupurupu kibao hachangii chochote kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, hachangii kodi, wala hachangii bima ya afya.
Baada ya miaka mitano, Mbunge huyohuyo anapewa kiinua mgongo cha 240M, ambacho hakuwahi kukatwa kuchangia hata mwezi mmoja. Je pesa hizi za kiinua mgongo anazolipwa zinatoka wapi kama alikua hakatwi? Jibu ni.kwamba zinatoka kwa watanzania maskini including wale wanaolipwa laki mbili kwa mwezi.Halafu Mbunge mmoja bila aibu anademka eti watanzania walipe tena kodi kwa kutumia simu zao. Yeye anaiita kodi ya uzalendo na ameshauri ilipwe kila siku. Yani kila ukiamka unakatwa kiasi fulani cha pesa kwenye simu yako kama kodi ya uzalendo.
Wabunge walipaswa kuonesha mfano wa uzalendo. Wakatwe kodi kwenye mishahara yao na posho zao zote. Mbunge akiangalia salary slip yake aone Gross salary ni 11.8M lakini Net saalary ni 7M. Akatwe Bima ya afya, akatwe pensheni pia. Hapo atakua na adabu na ataongea lugha moja na wananchi, maana atakua anafeel kile wananchi wake wanafeel.
Na akipoteza ubunge akiwa na miaka 30 asubirie hadi afikishe miaka 60 ndipo apate mafao yake. Wale wanaopoteza ubunge wakiwa na mika zaidi ya 60 ndio wapewe mafao yao kwa wakati. Na wapewe kwa kadri walivyochangia kwenye mifuko ya hifadhi za jamii. Kama alikua anakatwa 500K kwa mwezi kwa ajili ya pensheni means baada ya miaka mitano atakua amechangia 30M. Hiyo ndio haki yake, lakini asipewe hadi afikishe miaka 60.
Hapa ndio tutaona kweli ni wazalendo. Sio wanatunga sheria za kiiimla kukandamiza wanyonge, halafu wao wanajiondoa kwenye sheria hizo. Wanaishi kwenye dunia yao halafu wakishavimbiwa nyama choma na Dompo wine, wanabweka kuhusu uzalendo. Uzalendo gani wakati umezuia fao la kujitoa kwa vijana maskini, while wewe unavuta mshiko kila baada ya miaka mitano?
Unatunga sheria kuwa kijana maskini aliyetoka chuo akapata ka mkataba ka miaka miwili, akimaliza mkataba wake eti asilipwe mafao yake hadi afikishe miaka 60. Lakini wewe ukipoteza ubunge na miaka 35 unataka uvute mafao yako fasta. Hutaki kusubiri ufikishe miaka 60. Huu ndio uzalendo mnaohubiri?
Halafu hawa watanzania unaotaka walipe kodi ya uzalendo kupitia simu zao ni wapi? Hawahawa maskini au kuna wengine? Tanzania ina watumiaji wa simu za mkononi milioni 40. Kati yao watanzania milioni 8 matumizi yao kwenye simu hayafiki TZS 1,000/= kwa mwezi. Yani kuna watanzania milioni 8 ambao ndani ya mwezi mzima hawawezi kutumia "buku" kwenye simu. Hawa ndio wanataka kukamuliwa kodi ya uzalendo na watu wanaolipwa 12M kwa mwezi.
Hapo ukiwagusa mkuu unaambiwa wanaombwa hela mno na wananchi mtaani ndio maana wanatunishiwa mfuko..Nimesikiliza hotuba ya mama Samia. Ni bla bla kama bla bla nyingine tu za wakati wa kampeni. Kufanya mabadiliko kwenye hii system tuliyonayo ni kama kujidanganya. Hebu ona mbunge anavyomega pato la nchi. Na bado kuna maeneo mengine mengi sana amabyo fedha zinamegwa sana. Rais atakayeleta mabadiliko ni rais atakayekubali kufumua system na kuondoa mianya kama hii. Taifa letu linaingiza pato zuri tu ila vipaumbele imekuwa mifuko ya wanasiasa. NB: Na hapo hujaweka usafiri wa daraja la pili kwenye ndege.
Tutanue wigo wa kukusanya kodi kwa wabunge pia kutozwa kodi kwenye mapato yao, huo ndio uzalendo kwa taifa. Uzalendo sio kuvaa tai, bags, skafu au shati lenye rangi za bendera.Na Rais nae alipe kodi! Haiwezekani na yeye anatuletea maneno matamu ya kulipa kodi kwa hiyari, huku yeye mwenyewe pamoja na hao Wabunge wakiishi maisha ya peponi, haafu hawalipi kodi!..
Mwe sasa uzalendo unatoka wapi kama wao wenyewe hawalipi kodi.Sio wabunge tu
Rais halipi kodi
Mawaziri hawalipi kodi..