Mbowe: Slaa anapumzika, msiwe na hofu

Mbowe: Slaa anapumzika, msiwe na hofu

Msitake kumshushia hadhi yake Dr Slaa aliyojijengea katika nchi na jamii kiujumla, leo hii eti Slaa akae meza moja na Lowassa mnadhani ye mroho wa madaraka? Niliahidi kura yangu kwa Slaa kwani naamin ndiye sahihi wa kututoa wa Tanzania tulipo sitaacha kupiga kura ntaweka box pembeni naandika Slaa naweka tiki. Lakin si kwa CCM wala fisadi Lowassa
 
dkmagupombe.jpg


Teh! Tehe! Teheee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Huyu anaumwa nini?mbona alienda kugonga kikombe cha utatu mtakatifu?teh teh
 
hadi mwenyekiti wa chama naye anaingia mkenge kwenye hizi propaganda hchi chama kinaenda wapi..?
 
Bado nina tatizo na Dk Slaa unless ani-prove wrong. Huu sio wakati wa kufanya haya anayoyafanya otherwise naamini Dk Slaa anatumika na CCM kutudhoofisha. Sikubaliani nae kama kweli makelele yake jipindi kile yalikuwa kuitoa CCM madarakani leo nafasi inapatikana anaipa mgongo. Kipi kitanifanya nisiamini ni munafiki! He is so selfish this old man!

Yeye anapinga ufisadi na mafisadi na huo nadhani ndio msimamo wake daima haijalishi ni ndani ya CCM au CDM au kwingineko. Hakubaliani na tabia ya kubadili gia angani, anataka wananchi waamini anachokisema leo ndio hicho hicho atakisema kesho na kuendelea.
 
​Hivi huyu Slaa anachoshindwa kutoa neno tu na roho za watu zitulie shida ni nni???huu ni upuzi kwakweli
 
Mbona mbowe ni kama kachanganyikiwa kwanini slaa asiongee mwenyewe na vyombo vya habari?acha kudanganya nyerere alisema ukifanya Zambi haitakuacha Zambi ya kumtoa zitto kabwe eti msaliti hiyo ni zambi na ndo hayo ya slaa eti yupo likizo

Zambi** dhambi
 
Msitake kumshushia hadhi yake Dr Slaa aliyojijengea katika nchi na jamii kiujumla, leo hii eti Slaa akae meza moja na Lowassa mnadhani ye mroho wa madaraka? Niliahidi kura yangu kwa Slaa kwani naamin ndiye sahihi wa kututoa wa Tanzania tulipo sitaacha kupiga kura ntaweka box pembeni naandika Slaa naweka tiki. Lakin si kwa CCM wala fisadi Lowassa

umeongea point nzuri sana mkuu. Tatizo humu ndani kuna mijitu inapelekwa kama punda. Leo utawasikia wanasema pia rosti tamu, karamagi na mzee wa vijisenti nao ni watu safi na hawana doa la ufisadi. Much respect to dr. Slaa endelea na kuuchubua tu.
 
Akizungumza na Radio one mda huu saa 4, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Freeman Mbowe, amesema Dr Slaa hawezi kuhama chama hicho na hafikirii kamwe, kwa sasa anapumzika kwa likizo ya wiki moja.

Alipoulizwa kuhusu Slaa kutokubaliana na ujio Wa Lowassa amejibu kila kitu tulikubaliana na Slaa mwenyewe aliunga mkono suala hilo.

Mbowe amesema wananchi na wanachadema kwa ujumla wasiwe na wasiwasi kwani hiki chama ni makini na hakiwezi fanya maamuzi bila maridhiano na akasisitiza kuwapuuza wanaoeneza habari kuwa Slaa amejiuzulu siasa.

Alipoulizwa mara ya mwisho kuwasiliana na Dr Slaa ni lini akajibu jana saa kumi na mbili jioni.

Alipoulizwa walizungumza nini akajibu anajua yeye na Slaa.

Walipomuuliza hasa mbona sisi tukimpigia hapatikani akajibu sijui lakini mimi nimewasiliana nae jana.


Chanzo: Radio one

Ee mungu saidia dr.slaa asiondoke CDM
 
Kachukuwa likizo baada ya Lowassa kujiunga na Chadema Mbowe bana unadhani watu wote Bavicha.
 
Huyu mbowe anataniya wanachama wake lakini anejua thamani ya Dr slaa hawezi kukuelewa!kwani jibu halijitoshekezi
 
Mwisho wa siku wote mtanyooka tu Chadema/Slaa wanajua nini wanachokifanya
 
Back
Top Bottom