mnajidanganya sana.Mambo hayapo sawa kabisa
Kwa sasa Mbowe haaminiki, tunataka kumsikia dr slaa mwenyewe
Nyie watu wengine unashabiki umewaathiri sana, umeharibu hadi akili zenu, hata kusoma kwa makini ili uelewe kilichoandikwa unashindwa, unakurupuka tu na kusema hajasema anapumzika. Iruhusu akili yako ijitegemee
kamanda mboye na yeye amekosea.
Yani mtu ameharibu chama cha watu kwa kuwachukulia mtu wao. Waliochukuliwa mtu wakaona wasitake shari na wamwachie mboe aondoke na jembe lao na wao kuamua kujifariji na propaganda kuwa dr. Slaa anahama chadema.
Tumaini hili pekee la ccm kujifariji kuwa dr. Slaa anahama chadema, mboe kaja tena na kuliondoa na kuusema ukweli.
Mimi binafsi huu uonevu unaofanywa na kamanda mbowe siukubali na naupinga kabisa. Maana nimeshagundua nia ya kamanda mbowe ni kutaka kukiuwa kabisa chama cha mapinduzi. Na kwakuwa mm ni mkristo safi na ninaamiani kuwa kuuwa ni dhambi, basi sina budi kumpinga kamanda mbowe.
Akizungumza na redio one mda huu saa 4, mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema Freeman Mbowe, amesema Dr Slaa hawezi kuhama chama hicho na hafikirii kamwe.kwa sasa anapumzika kwa likizo ya wiki moja .
Alipo ulizwa kuhusu Slaa kutokubaliana na ujio Wa Lowassa amejibu kila kitu tulikubaliana na Slaa mwenyewe aliunga mkono suala hilo.
Mbowe amesema wananchi na wanachadema kwa ujumla wasiwe na wasiwasi kwani hiki chama ni makini na hakiwezi fanya maamuzi bila maridhiano na akasisitiza kuwapuuza wanaoeneza habari kuwa Slaa amejiuzulu siasa.
Alipo ulizwa mara ya mwisho kuwasiliana na Dr Slaa ni lini akajibu jana saa kumi na mbili jioni.
alipoulizwa walizungumza nini akajibu anajua yeye na Slaa.
walipo muuliza hasa mbona sisi tukimpigia hapatikani akajibu sijui lakini mimi nimewasiliana nae jana.
sourse.
Radio one,
Shost
Mbowe ni muongo tu na hilo kishajidhihirisha siku nyingi.
Ngoja daktari wa kanoni padri Dr.W.Slaa amshukie kama alivyomshukia anaejiita Yericko Nyerere kwa uongo.
Ndani ya siku 10 CHADEMA wameshatoa kauli zaidi ya tatu tofauti kuhusu Dr. Slaa. Mwanzo walisema wamegawana majukumu hivyo Dr Slaa yuko ofisini anaendelea na kazi. Baadaye ikaja kauli kwa mtindo wa tuhuma dhidi ya Mke wa Dr Slaa, Josephine kuwa ameshikilia mateka mumewe. Wakati huo huo 'wakereketwa' sana wa CHADEMA 'mpya' wamekuwa wanasisitiza kuwa Dr Slaa anaanda mkutano wa CC. Sasa inakuja kauli kwamba Dr Slaa anapumzika!
Watanzania walalahoi wamepotea maisha, na wengine wamepata vilema vya maisha wakitetea CHADEMA na misingi yake ya kukataa ufisadi. Leo hii vipande thelathini vimewafanya Mbowe na wakubwa wenziwe waamini kuwa wanaweza kuwageuza-geuza Watanzania wote kama chapati! Haiwezekani.
Slaa siyo strategist mzuri .... amepunguza kasi ya magamba kujivua magamba yao
Pro Baregu hakuwepo nchini,nimekutana naye Jana Addis Ababa na tulikuja nae kwenye ndege moja kurudi Bongo,tulifika Bongo saa tisa Kasoro usiku wa leoVipi kuhusu mnyika na baregu?hawakuuliziwa?
Angalieni maelezo ya hii clip na haya ambayo mmeweka hapa! Ukweli ni upi na uongo ni upi? ??
Ni bora kuweka wazi mapema ili kama solution ipatikane mapema kuliko kuwa na uongo mtakatifu.
Hii taarifa ina majibu yote ya SLAAAngalia menyewe.https://www.youtube.com/watch?v=Onyr_4by0UM
mtaisoma namba T ccm 2015-2015 ni vumbi tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu