Atakuwa ni mtu mjinga tu ndio anaweza kuto kujua nini kinafuata nyuma baada ya Kansa Mbarouk kupata air time ya hizi propaganda kwenye Mtanzania, Jambo leo, Uhuru na Habari leo.
Kwa nini?
1. Kansa Mbarouk anaye jitokeza na sababu za ukomo wa madaraka yeye mwenyewe anajua kwenye katiba ya chama kuna kipengele (6.3.2 (c), kinasema "kiongozi aliye maliza muda wa uongozi ana haki ya kugombea na kuchaguliwa tena mradi awe anatimiza masharti ya kuchaguliwa kuwa kiongozi"
Kupitia kipengele hichohicho mtu huyohuyo Kansa Mbarouk amekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Tabora kwa vipindi zaidi ya viwili. Amekuwa mwenyekiti kwa vipindi vitatu mfululizo yaani amekuwa mwenyekiti wa Tabora kwa miaka 15. Leo hii aliye kuwa mwenyekiti wa mkoa, aliye kuwa miongoni mwa wajumbe wa Baraza kuu waliopitisha katiba yenye kipengele hicho anaweka pingamizi! Ana tofauti gani na Samson Mwigamba aliyetumia hoja hizo hizo huku naye akiwa miongoni mwa waliopitisha kifungu hicho?!
2. Kama yeye katiba ilimruhusu kugombea kwa vipindi vitatu mfululilo nini leo kinamkuna kuipinga katiba hiyo hiyo ambayo yeye ilimuwezesha kugombea vipindi vitatu na akawa mwenyekiti wa mkoa wa Tabora?!
Kama unawaza mambo kwa 3D na kuhusisha milango 6 ya fahamu utajua kuna mazingira yanaandaliwa. Mazingira yapi?
1. Kansa Mbarouk na Athuman Balozi yule aliye ongoza maandamano fake kwenda kwa msajili na CAG akishirikiana na Yona ni mtu na mjomba wake, kipindi cha mwezi juni wakati wa hekaheka za Athumani Balozi ambaye nae alikuwa kaimu katibu wa Tabora walikuwa wote hapa Dar es salaam, Athuman akitoa matamko ya kukikashifu chama na miongoni mwa hoja ikiwa ni hii hii ya mjomba wake na baadae akajiunga na ACT.
2. Kansa Mbarouk mara kadhaa amelalamikiwa kuwa amekuwa anatumia ofisi za chama kule Tabora kufanya shughuri za ACT hakuwahi kukanusha, alipoitwa kwenye kikao ajieleze alikuwa yuko Dar es salaam kwa madai anauguliwa lakini wakati huohuo akiwa DSM na watu ACT. Baadae mtu huyohuyo anachukua fomu ya uwenyekiti wa chama (ni haki yake) halafu anatangaza kuwasamehe na kuwarejesha chamani watu walio anzisha chama kingine (ACT).
3. Kuna juhudi tunazozijua za kutaka kuvuruga uchaguzi mkuu wa Taifa, tunajua role ya wapinzani wa chama wanao fadhiriwa na watu ambao tuna majina yao. Kansa Mbarouku amesha anza kazi hii na analipwa, na kuna mlolongo wa magazeti yameanza kuandika leo, si kosa lao kuandika; Cha kujiuliza mbona magazeti hayohayo hayaja hoji uhalali wa yeye kuwa mwenyekiti wa mkoa kwa miaka mitatu na iwe nogwa kwa Mbowe wakati kifungu cha katiba ni kile kile?!
KAMA ULIKUWA HUJUI.
Kansa Mbarouk anatafuta kick ya kwenda ACT lakini walau anataka aonyeshe kuwa amepambana, na hapo atakuja na viroja na uzishi kama aliokuja nao mjomba wake Athumani Balozi wa kuandaa maandamano kwenda kwa msajili na CAG kukituhumu chama kwa propaganda zilezile halafu wiki moja baadae akajiunga na muungano wa usaliti wa waziwazi (ACT).
Tutaona na kusikia mengi.