Mbowe awekewa pingamizi CHADEMA

Mbowe awekewa pingamizi CHADEMA

mtoto wa mbwaaaa hiyo ID yako tu inakutoa kwenye ulingo!!
Katika kipindi hiki Mbowe anahitajika saana, kuelekea Uchaguzi, hatutasikiliza kelele zenu!!
 
Last edited by a moderator:
Watu kwa kujikweza hamjambo, hivi na wewe huwa unajihesabu kuwa ni muona mbali!
well niliyasema yote yametokea kipi kikubwa? Chadema sasa hivi maji ya shingo, ni swala la muda tu maana Maalim Seif naye anapanga mkakati dhidi ya chama- Utanikumbuka.
 
huyo mbaruku,nimeshamsikia akiongea.jamaa anaongeaga pumba tu,na kama akipewa uenyekiti,basi cdm itakuwa imekufa.UONGOZI WA CHADEMA SI WA MAJARIBIO.
 
huyo mbaruku,nimeshamsikia akiongea.jamaa anaongeaga pumba tu,na kama akipewa uenyekiti,basi cdm itakuwa imekufa.UONGOZI WA CHADEMA SI WA MAJARIBIO.

cdm walipuuza ushauri wa msajili wa vyama, sasa inawagharimu.
 
well niliyasema yote yametokea kipi kikubwa? Chadema sasa hivi maji ya shingo, ni swala la muda tu maana Maalim Seif naye anapanga mkakati dhidi ya chama- Utanikumbuka.

chagadema bila mwenyekiti kutoka kaskazini, kwishney.
 
Mbowe akiondoka pengine pesa ya walipa kodi(ruzuku) inaweza kusalimika.
 
Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo, CHADEMA mh Freeman Mbowe, amewekewa pingamizi kugombea nafasi ya uenyekiti Taifa kutokana na madai kuwa, amekiuka katiba ya chama hicho pamoja na maagizo ya msajili wa vyama nchini.

Freeman-Mbowe.jpg

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amewekewa pingamizi la kutogombea nafasi hiyo kwa awamu ya tatu kwa madai ya kukiuka katiba ya chama hicho na maagizo ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.

Pingamizi hilo limewekwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Tabora, Kansa Mbarouk, ambaye pia ni mgombea wa nafasi hiyo.

Barua ya Mbarouk yenye kumbukumbu namba Mbarouk/UCH/14 kwenda kwa Katibu Mkuu wa Chadema na Msajili wa Vyama vya Siasa, iliyoandikwa Septemba tano, inasema kufikia Septemba 14 siku ya uchaguzi mkuu wa chama hicho, Mbowe atakuwa ametumikia vipindi viwili katika nafasi ya mwenyekiti wa taifa.

Barua ya Mbarouk inasema kwa mujibu wa katiba ya Chadema, kama ilivyothibitishwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, hakuna mwanachama anayeruhusiwa kuchaguliwa kuongoza kwa zaidi ya vipindi viwili katika cheo kimoja kwa ngazi moja.

“Msajili wa Vyama alikuwa ametoa maelekezo kwamba chama kiitishe Baraza Kuu na Mkutano Mkuu Maalumu kwa lengo la kubadilisha kipengele kinachoweka ukomo wa uongozi kama litaona kuna haja hiyo kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu. Hata hivyo hadi naandika barua hii hakuna dalili zozote kwamba mkutano mkuu maalumu utaitishwa na maandalizi ya uchaguzi yanaendelea bila kujali agizo la msajili wa vyama,”alisema Mbarouk katika barua hiyo.

Alisema katika kipindi chake cha uongozi Mbowe alisimamia vikao vya chama vilivyofanya maamuzi ya kuvunja katiba waziwazi.

“Mfano Novemba 2013, Mbowe alisimamia kikao cha kamati kuu kilichomvua nafasi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama, Zitto Kabwe na wenzake bila kuzingatia mamlaka ya kikao hicho. Kwa mujibu wa Sura ya Sita ibara ya 6.3.6(b) ya katiba ya Chadema toleo la mwaka 2006 ‘kiongozi aliyeteuliwa na vikao vya uongozi ataweza kusimamishwa au kuachishwa uongozi na kikao kilichomteua’,”alisema.

Alisema baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 chama kilipata nafasi tano za kuteua nafasi wabunge wa viti maalumu kuingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano, ambapo Kamati Kuu kilipitisha majina ya Suzan Kiwanga, Chiku Abwao, Halima Mdee, Mhonga Ruhanywa na Grace Kiwelu lakini Mbowe alibadilisha majina hayo.

“Mbowe alibadilisha majina ya Chiku Abwao na Susan Kiwanga huku akiwapachika Susan Lyimo na Lucy Uwenya. Baadaye Mbowe alikiri kosa na kuomba msamaha katika kikao cha Kamati Kuu,”alisema.

Alisema hayo yote yanadhihirisha pasipo shaka kwamba mwenyekiti huyo amekosa uaminifu hivyo anapaswa kunyang’anywa nafasi hiyo ya uenyekiti.

“Ninatambua kuwa kwa mujibu wa katiba ya chama Sura ya Saba ibara ya 7.3.1, uchaguzi ngazi ya taifa unapaswa kusimamiwa na wazee wastaafu wa chama hata hivyo hadi naandika barua hii sina taarifa kuhusu kuteuliwa kwa kamati hii. Hivyo basi nimelazimika kuandika barua yangu ya pingamizi kwako nikiamini kwamba utaifikisha katika chombo husika kinachoshughulikia uchaguzi,”alisema Mbarouka.

Alipotafutwa na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani kuzungumzia barua hiyo, Mbarouk alisema ni kweli ameandika barua hiyo na kwamba aliikabidhi juzi Septemba 6 katika ofisi ya Katibu Mkuu wa Chama.

“Ni kweli nimeiandika mimi na nilikabidhi jana (juzi) katika ofisi ya katibu mkuu wa chama,”alisema Mbarouk.

Kwa upande wake Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene alipoulizwa na gazeti hili endapo ni kweli barua hiyo imewafikia, alimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa atampigia baadaye.

Hata hivyo baada ya Makene kumpigia simu mwandishi alimtaka amtajie lengo la Mbarouk kumpinga Mbowe, baada ya mwandishi kufanya hivyo aliahidi angepiga tena simu, lakini hadi gazeti linakwenda mtamboni hakupiga simu.



CHANZO: Mtanzania

Vyovyote itakavyokuwa ila hatuwezi kuongozwa na Kansa, Chadema sio Ocean Road Hospital
 
Jaji Mutungi alishawashauri kwanza muitishe mkutano kamati kuu ili kurekebisha katiba iliyochakachuliwa kwanza kabla ya kuitisha uchaguzi.
 
Wanajamvi!

Kumekuwa na tabia ya CCM kila wanapoona wanabanwa na vyama vingine vya siasa, wao wanakuja na mbinu ya kupandikiza mamluki. Hali hii imeendelea miaka nenda rudi sasa!

Kipindi hiki wamegonga mwamba kwa kukutana na mwamba wa kaskazini Mh. Mbowe asiyekuwa na bei katika ununuliwaji wa viongozi wa vyama vya siasa unaofanywa na CCM.

Baada ya CCM katika kuona kuwa plan "A" ya kutaka kibalaka wao Zitto awe mwenyekiti wa CHADEMA kugonga mwamba wakaja na plan "B" ya kuunda chama cha siasa cha ACT – Tanzania huku kikiwa na viongozi bila ya waongozwa. Wengi wa viongozi hao ni wasaliti waliofukuzwa CHADEMA.

Plan "B" nayo imeonekana kushindwa, ili kutimiza kauli ya Wassira kuwa CHADEMA haifiki 2014 wamekuja na plan "C" ya kumpachika Kansa Mbaruku (Mzimu wa Zitto) kwenye kinyang'anyiro cha kugombea nafasi ya uenyekiti wa CHADEMA Taifa. (hapa ndipo ninapojikita katika mada hii)

Siku chache kabla ya Kansa Mbaruku kutangaza kuchkua fomu ya kuomba uenyekiti wa CHADEMA Taifa akaunti yake ilikuwa Dormant lakini siku tatu baadae akaunti hiyo ilionekana kuwa na shilingi milioni tatu (3,000,000/=) huku wachambuzi wakijiuliza amezitoa wapi ili hali Mbaruku hana kazi ya kumuingizia kipato na anaishi kwa kulishwa na mkewe ambaye mfanyakazi wa CCM ofisi ya mkoa.

Katika kuonesha na kutekeleza masharti ya mdhamini wake (CCM) Mbaruku alikwenda kwenye kituo cha redio kinachomilikiwa na Msomali wa CCM Aden Rage kilichpo Tabora na kuanza kuporomosha matusi na vijembe dhidi ya CHADEMA na Viongozi wake. Pia alitangaza kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa CHADEMA ngazi ya mkoa.

Moja ya sababu alizozisema kuwa zimemchosha na anataka azidhibiti pindi atakapo kuwa mwenyekiti wa Taifa ni kuondoa udini, kuwekana kidungu na kiongozi kukaa madarakani kwa muda mrefu bila ya kuleta mafaniko katika chama.

Kansa Mbaruku (mzimu wa Zitto) kama alivyotambulishwa na baadhi ya magazeti ya tare 31/08/2014 amekuwa ni kikwazo cha kuingia kwa wanachama wengine kujiunga na chama. Huyu huyu Mbaruku alimkaimisha ukatibu ndugu yake Athuman Balozi na kumpa umwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) ndugu Halima Katundu pia kumpa Uenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) ndugu yake Hussein Kundecha na pia kumuweka ndugu yake mwingine kuwa mpiga mashine (PS) wa ofisi ya mkoa ndugu Reheme Ulaya. Ambao wote wametangulia ACT kwa sasa na yeye atafuata baada ya mbinu zake chafu kushindikana.

Katika kuzamilia kukamilisha plan "C", Kansa Mbaruku alikuja na pingamizi la kutaka Mh. Mbowe asigombee uenyekiti kwa lengo kutimiza matakwa ya mdhamini wake (CCM). Jana magazeti ya UHURU, JAMBO LEO na MTANZANIA ambayo ni mali ya CCM na vigogo wake yaliandika kuwa MBOWE awekewa pingamizi. Leo tena katika kuashiria kuwa wasaliti na CCM jumlisha na MCHEPUKO wake wameonekana kushindwa katika hatua yao baada ya mapitio ya magazeti kutangaza kuwa pingamizi lao limetupiliwa mbali hivyo kumfanya Mh. Mbowe kuwa mgombea halali wa uenyekiti ndani ya CHADEMA.

Nimefuatilia ili kujua katika mfumo wanaoufuata wanachama wa CHADEMA hivi sasa wa CHADEMA NI MSINGI, huyu Kansa Mbaruku anatokea Msingi gani, Tawi gani na ni Kata gani. Nilichoambulia ni kuwa Kansa Mbaruku anatokea kata ya Ipuli na anakaa kwenye nyumba zilizoibwa na wanaCCM zilizopo jirani na Bohari ya Madawa au Kituo cha Gari moshi (Station) zinazoitwa URBAN QUARTER.

Kwa sasa Kansa Mbaruku yupo Dar es Salaam tokea siku aliporudisha fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA ngazi ya Taifa huku akiwa na wahuni wabeba mizigo wa standi ya mabasi ya mikoani almaarufu UBUNGO. Ambapo wahuni hao waliishia getini bila ya kuingia ndani ya ofisi ya CHADEMA makao makuu.

Mwisho itoshe kusema kuwa KANSA MBARUKU ndiye mtunza vifaa vya uenezi (kadi, bendera na vipeperushi) vya ACT - Tanzania kwa mkoa wa Tabora.

Tusubiri plan "D"! inayosukwa na vijana wa CCM wakiongozwa na Msalani na Vijana wa ACT wenye ofisi mitandaoni wakiongozwa na Mwl. Kaijage
 
Wanajamvi!

Kumekuwa na tabia ya CCM kila wanapoona wanabanwa na vyama vingine vya siasa, wao wanakuja na mbinu ya kupandikiza mamluki. Hali hii imeendelea miaka nenda rudi sasa!

Kipindi hiki wamegonga mwamba kwa kukutana na mwamba wa kaskazini Mh. Mbowe asiyekuwa na bei katika ununuliwaji wa viongozi wa vyama vya siasa unaofanywa na CCM.

Baada ya CCM katika kuona kuwa plan “A” ya kutaka kibalaka wao Zitto awe mwenyekiti wa CHADEMA kugonga mwamba wakaja na plan “B” ya kuunda chama cha siasa cha ACT – Tanzania huku kikiwa na viongozi bila ya waongozwa. Wengi wa viongozi hao ni wasaliti waliofukuzwa CHADEMA.

Plan “B” nayo imeonekana kushindwa, ili kutimiza kauli ya Wassira kuwa CHADEMA haifiki 2014 wamekuja na plan “C” ya kumpachika Kansa Mbaruku (Mzimu wa Zitto) kwenye kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya uenyekiti wa CHADEMA Taifa. (hapa ndipo ninapojikita katika mada hii)

Siku chache kabla ya Kansa Mbaruku kutangaza kuchkua fomu ya kuomba uenyekiti wa CHADEMA Taifa akaunti yake ilikuwa Dormant lakini siku tatu baadae akaunti hiyo ilionekana kuwa na shilingi milioni tatu (3,000,000/=) huku wachambuzi wakijiuliza amezitoa wapi ili hali Mbaruku hana kazi ya kumuingizia kipato na anaishi kwa kulishwa na mkewe ambaye mfanyakazi wa CCM ofisi ya mkoa.

Katika kuonesha na kutekeleza masharti ya mdhamini wake (CCM) Mbaruku alikwenda kwenye kituo cha redio kinachomilikiwa na Msomali wa CCM Aden Rage kilichpo Tabora na kuanza kuporomosha matusi na vijembe dhidi ya CHADEMA na Viongozi wake. Pia alitangaza kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa CHADEMA ngazi ya mkoa.

Moja ya sababu alizozisema kuwa zimemchosha na anataka azidhibiti pindi atakapo kuwa mwenyekiti wa Taifa ni kuondoa udini, kuwekana kidungu na kiongozi kukaa madarakani kwa muda mrefu bila ya kuleta mafaniko katika chama.

Kansa Mbaruku (mzimu wa Zitto) kama alivyotambulishwa na baadhi ya magazeti ya tare 31/08/2014 amekuwa ni kikwazo cha kuingia kwa wanachama wengine kujiunga na chama. Huyu huyu Mbaruku alimkaimisha ukatibu ndugu yake Athuman Balozi na kumpa umwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) ndugu Halima Katundu pia kumpa Uenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) ndugu yake Hussein Kundecha na pia kumuweka ndugu yake mwingine kuwa mpiga mashine (PS) wa ofisi ya mkoa ndugu Reheme Ulaya. Ambao wote wametangulia ACT kwa sasa na yeye atafuata baada ya mbinu zake chafu kushindikana.

Katika kuzamilia kukamilisha plan “C”, Kansa Mbaruku alikuja na pingamizi la kutaka Mh. Mbowe asigombee uenyekiti kwa lengo kutimiza matakwa ya mdhamini wake (CCM). Jana magazeti ya UHURU, JAMBO LEO na MTANZANIA ambayo ni mali ya CCM na vigogo wake yaliandika kuwa MBOWE awekewa pingamizi. Leo tena katika kuashiria kuwa wasaliti na CCM jumlisha na MCHEPUKO wake wameonekana kushindwa katika hatua yao baada ya mapitio ya magazeti kutangaza kuwa pingamizi lao limetupiliwa mbali hivyo kumfanya Mh. Mbowe kuwa mgombea halali wa uenyekiti ndani ya CHADEMA.

Nimefuatilia ili kujua katika mfumo wanaoufuata wanachama wa CHADEMA hivi sasa wa CHADEMA NI MSINGI, huyu Kansa Mbaruku anatokea Msingi gani, Tawi gani na ni Kata gani. Nilichoambulia ni kuwa Kansa Mbaruku anatokea kata ya Ipuli na anakaa kwenye nyumba zilizoibwa na wanaCCM zilizopo jirani na Bohari ya Madawa au Kituo cha Gari moshi (Station) zinazoitwa URBAN QUARTER.

Kwa sasa Kansa Mbaruku yupo Dar es Salaam tokea siku aliporudisha fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA ngazi ya Taifa huku akiwa na wahuni wabeba mizigo wa standi ya mabasi ya mikoani almaarufu UBUNGO. Ambapo wahuni hao waliishia getini bila ya kuingia ndani ya ofisi ya CHADEMA makao makuu.

Mwisho itoshe kusema kuwa KANSA MBARUKU ndiye mtunza vifaa vya uenezi (kadi, bendera na vipeperushi) vya ACT - Tanzania kwa mkoa wa Tabora.

Tusubiri plan “D”! inayosukwa na vijana wa CCM wakiongozwa na Msalani na Vijana wa ACT wenye ofisi mitandaoni wakiongozwa na Mwl. Kaijage

Umenifurahisha sana mkuu.
Tunataka watu kama wew mnaoandika baada ya kujisumbua kufsnya utafiti wa kina.
 
Umenifurahisha sana mkuu.
Tunataka watu kama wew mnaoandika baada ya kujisumbua kufsnya utafiti wa kina.

ametumia nguvu nyingi wakati inahitajika akili kidogo!
 
Back
Top Bottom