Mbowe atuhumiwa kuhamisha mabilioni

Mbowe atuhumiwa kuhamisha mabilioni

Eti sitomuamini uliposikia alipokea bil 10, dah sasa hii kazi. Kusikia tuu bila ushaidi, basi chuki na ku kosa kabisa kumuamini.
Ungeonyesha ushaidi, hapo sawa, lakini bila ushaidi, basi ninamashaka na uwezo wako wa kudadavua mambo. Kama hizi ndo akili za watanzania wengi, basi nchi ina safari ndefu ya ukombozi.
Ccm wameuza nchi kwa wawekezaji hulioni? Wanyama pori kutorosha huoni? Watu kupiga dili ESCROW, hulioni? Wanafunzi kukaa chini hulioni? Huduma duni za afya kwa wazee, akina mama na watoto, huyaoni hao.
Wachache kua matajiri, na wengi kuwa masikini kwenye nchi yenye kilakitu, hayo huyaoni? Ila bado waiamini ccm kuku letea maendeleo. Dah! Majanga kweli. Ila unauchungu wa hisia eti kapewa hela na sio kua na uchunga na hali halisi ya nilioataja hapo juu. Amakweli alio waroga watanzania kafaa. Badilikeni jamani, tuanze ukurasa mpya. Tanzania bila ccm inawezekana kama vile tanzania bila nyerere inasonga mbele.

Tanzania bila ccm haiwezekani, Mbowe ni mzee wa dili na kibaya zaidi Lowasa katembeza pesa ndani ya chadema na wenzake, ss wote wamekaa kimya, hawa huwezi kuwaamini kuwapa nchi, wao imekuwa sanaa hadi kwenye kampeni, mgombea hawezi kuongea wanasingizia mitambo mibovu, wakati huo wao wote wameongea bila shida ila Dk5 za Lowasa ndo mic
Mbovu,, tutawapa nafasi za ubunge na udiwani si urais, ni bora kumpatia simba mmoja aliyeshiba kuliko kuwapatia simba wengi wenye njaa, kama kaanza kuhamisha pesa kwenda nje na ndo wana mipango ya kufumua mikataba ss ndo itakuwa bara 2pu.
 
Magazeti ya leo yameandika jamaa wapiga dili wanafanya miamala ya kufa mtu kupitia hongkong na dubai. Kweli kura ni mali.
View attachment 300421
View attachment 300420

Mbowe ameshaanza kukimbiza pesa sasa daah haya ndio madhara ya kuwaamini wafanyabiashara, Mwisho wa Siku wanakuumiza kama hivi... Ila wajidanganye hivyo hivyo maana oktoba 25 tutawanyoosha tuu.Na nitamchagua Magufuli Ili aje kuwashughulikia na mahakama ya Mafisadi
 
Ah2lBJcZJ0bhmRKtT7K7rZ3wvjokorIDyZZvEKSpI4X5.jpg

hii uzushi hamna tarehe wala saa ya iyo transaction kufanyika?
 
hii uzushi hamna tarehe wala saa ya iyo transaction kufanyika?

Hata kama sio uzushi, unapofanya biashara ni lazima ufanye transfer, na ni lazima uweke request

PUKU ni kampuni ya power banks na ina mtanznia ndani, TanChin pia

as a businessman, the amount he transfer ni kidogo, i think Mbowe should have done bigger business, especially after being in business for over 30 years
 
Sema kweli, wametoa wapi huo utajiri chap chap hivyo? Au ndiyo dil zao zimetick

Jamani kuweni makini hizi ni propaganda katika lala salama ya kampeini. Lengo la Magazeti ya Uhuru na Raia Tanzania ni kuwalisha watu wasio na uwezo mkubwa wa kuchambua pumba na mchele upuuzi ili kubadili nia. Siku hizi baada ya sakata la Escrow hakuna benki inaweza kupeleka nje hivi hivi.
 
Ndiyo maana huwa sioni tofauti ya wanaoshabikia ccm na wanaoshabikia ukawa.
Yani wote wanatetea viongozi wao hata pale penye makosa kweli,ila ajabu hao viongozi watakapotoka kwenye vyao ndio huanza kuyasema mapungufu na maovu ya viongozi hao ambayo mwanzo waliyatetea.

Leo Dr.slaa anaonekana wa maana ccm ila ukawa anaonekana hana maana,msaliti,na mambo kibao ambayo walikuwa wakiyatetea.
Ccm nao wanaeleza ufisadi wa watu wanaohama ccm wakati wakiwa bado ccm hawakuwa wakisema.
 
Hata kama sio uzushi, unapofanya biashara ni lazima ufanye transfer, na ni lazima uweke request

PUKU ni kampuni ya power banks na ina mtanznia ndani, TanChin pia

as a businessman, the amount he transfer ni kidogo, i think Mbowe should have done bigger business, especially after being in business for over 30 years


Mkuu hiyo Document ya PDF wameitoa mahali then wakaedit kuanzia hapo kwenye Freeman Mbowe na Location ya hiyo ofisi.. Mbowe hana wala hausiki na hiyo kampuni inayoitwa ARETRA na wala hiyo kampuni nimejaribu kuitafuta inaonekana ni kampuni hewa tu...

Lakini pia hapo katikati ya Kind regards na Jina la Mbowe kulitakiwa kuwe na Signature ya kuidhinisha hizo pesa zitoke, sasa sahihi iko wapi?? Au wameshindwa kuigilizia au hawaijui signature ya Mbowe wakaona wataumbuka?? This is a forgery document to please some stupid people ambao hawawezi kujiongeza
 
Hakuna kitu kibaya kama wanachama wa chama kushindwa kukosoa wanayoyafanya viongozi wao.
 
Mbowe nae ni mpiga kura tu, mgombea urais ni mzee mamvi. Kichwa cheupe, roho nyupe, njia nyeupe na ikulu nyeupe. Mambo ya mbowe msubiri watu wamalize kupiga kura ndo mlete habari zake.
 
magazeti ya leo yameandika jamaa wapiga dili wanafanya miamala ya kufa mtu kupitia hongkong na dubai. Kweli kura ni mali.
View attachment 300421
View attachment 300420
i mambo ya kuunga unga ambayo hayana ukweli wowote.kwanza hakuna uhusiano wowote kati ya kichwa cha habari yako na viambatanishi ulivyoweka!na pia hakuna uhusiano wowote kati ya kiambatanishi cha kwanza na cha pili.kiambatanishi cha kwanza,soma vizuri ,ni instruction ya tarehe 20/04/2015.ambapo hata lowassa alikuwa "hafikirii kujiunga na ukawa".sasa hayo mabilioni unayosemayako wapi?pili ili chama kijiendeshe lazima kuwe na watu wanafadhili(vinaitwa vyama rafiki au taasisi rafiki),huwezi kushika dola bila kuwa na ushirikiano ya kidpomasia na nchi nyingine.hilo ni jambo la kawaida sana.taasisi hizi hutoa misaada kusaidia ukuaji wa chama husika.sasa si rahisi kila chama kuweka kila kitu "uchi"kama unavyotaka wewe hasa kwa wapinzani wako!kinachoitwa mabiliano ni shilingi milioni 600 ambayo ni pesa ndogo sana kwa uendeshaji wa chama na hasa kipindi cha uchaguzi.ningefurahi hoja yako ingejikita kwamba "hakuna kitu/vitu vinavyofanyika "kwa maendeleo ya chama!transfer za mabilioni ya pesa kwenda nje "benki kuu"kama msimamizi wa mabenki inapaswa kujua!!hivyo si vizuri kuandika mambo ambayo pengine huna "uelewa"nayo sawaa sawa.
Unapotaka kuhamisha mabilioni kwenda "nje"hilo ni dili kati ya serikali na mhusika si kitu cha "ku-transfer"tu kama unavyotaka kuaminisha umma.
Mwandishi wa habari hii pamoja wa wewe umeonyesha uelewa mdogo wa masuala ya "kipesa"na "kibenki"kwa ujumla.nadhani mkajipange upya mje na taarifa nzuri isiyo na chembe ya shaka,otherwise,habari hii taka taka kama habari nyingine la magazeti ya uhuru na mzalendo!!
 
Katika hali isiyotarajiwa viongozi wanaounda umoja wa katiba wa wananchi waanaza kuhamisha mali zao ikiwamo ni

pamoja na pesa taslim za kitanzania katika mataifa ambayo wamepanga kwenda kumalizia maisha yao mara baada ya

kushindwa kwa aibu baada ya uchaguzi wa mwaka huu viongozi hao ni pamoja na mwenyekiti wa chadema na mgombea

wao pamoja na meneja kampeni wa mgombea wao
 
Hustler mtoto wa mjini DJ huyoo katika ubora wake! Siasa inalipa haki ya nani. Halafu iko mijitu inaambiwa ikae kituoni ilinde kura ile mkong'oto na kutupwa jela mambo yabumburuke wajanja akina Mbowe wakati huo wametulia zao Dubai wanatanua. Shit!

Mbona siku nyingi?
 
Sasa si muende mahakamani kufungua kesi dhidi ya Mbowe kuwa anafanya miamala kinyume na sheria!! Nchi ya propaganda na walalamikaji.

Waandishi wa habari wao wamefanya kazi yao kutupasha habari wananchi. Suala la kwenda mahakamani kufungua kesi hiyo ni kazi ya serikali kumchukulia hatua Mbowe.
 
Back
Top Bottom