Mbowe atuhumiwa kuhamisha mabilioni

Mbowe atuhumiwa kuhamisha mabilioni

Propaganda Za LUMUMBA KITENGO CHA IT!! Tehe! Tehe! Tehe!! Eti Wamegawana Mabilioni!! Kama Hizo Taarifa Sio Propaganda, Mtoa UZI Na MNAOSAPOT Huo Upuuzi!! Waambieni Hao Wahariri Wa UHURU Na RAIA!! Wataje Hizo Benki Zilizohusika Na Kupitisha Au Kuhifadhi Hayo Mabilioni!!! KAMA KWELI Ni Wanaume Wayataje Ktk. Magazeti Yao, Sio KUPEWA Taarifa Hizo Nusu!!! Mbona Wale WALIOFANYA Miamala Yao Ktk. Benki Yenu Ya Kigeni, IMEGOMA Kutoa Ripot Ya Miamala Ya Wale Waliogawana Mabilioni Ya ESCROW Hadi Leo!! Na NINYI Kama KWELI Wazalendo, Mbona Hamthubutu KUWATAJA HAO Waliogawana, Au KUWAAMBIA Hiyo Benki Itoe Taarifa Zake Za Miamala!!! Wabunge Wa Upinzani Wamedai Mno BUNGENI, Lkn SERIKALI Ya CCM Imekaa Kimyaa!! Hata WAHUSIKA Wa MEREMETA, DEEP GREEN N.k . Semeni Na Hayo Pia!!!

Tatizo mkiambiwa ukweli mnaanza kumbwela mbwela
 
baada ya uchaguzi,mbowe ndo atakua tajiri namba moja tanzania,akifuatiwa na mbatia......
Angalau nikikujibu wewe taarifa zitafika kitengo cha propaganda na mjuwe ndio mzidi kujinyima kura, unajuwa kwa nini?

Sababu ni hii, kwamba Tanzania hakuna serikali mtu yeyote ana uwezo wa kuhujumu uchumi wa nchi, je kile kitengo cha pesa chafu kimefungwa? ni bank gani inaweza kutransfer pesa nyingi bila kutoa LC? HII NI SABABU TOSHA YA KUWAPIGA CHINI CCM MAANA INACHEKA NA WAHUJUMU UCHUMI HUKU IKIWAJUWA KWA MAJINA MPAKA TRANSACTION ZAO. kiama chenu tarehe 25.

ELIMU
ELIMU
ELIMU.
 
Huku majuzi mlisema amefilisika,haya magazeti uhuru raia mwema hata kuchambia hayafai!uharo mtupu yanaandika.Fuatilieni kwanza mabilioni aliyoyasema Zitto yapo uswiss
 
Magazeti ya leo yameandika jamaa wapiga dili wanafanya miamala ya kufa mtu kupitia hongkong na dubai. Kweli kura ni mali.

Muamala Wa kwenda kununua ferari mbona hausemwi??
 

Attachments

  • 1445235546483.jpg
    1445235546483.jpg
    77.4 KB · Views: 575
Magazeti ya tz hayajui kutengeneza headline za kijanja huku unamponda mbowe pembeni unasifia ccm hapo unapata jibu moja...hatubadiliki ngooo
 
hata awe na miamala ya trilion haisumbui tunataka mabadiliko tu

Mabadiliko yalishaanza siku nyingi baada ya kugundua lowasa hafai, anayefaa ni Dk. JPM. Mgufuli hoyeeeee. lowasa ziiiiiiiiiiiiii. Wanaosumbuliwa na mabadiliko wanakimbia huku na huko ili wawafunge na kuwaziba mdomo wanaweza kumkemea: 1. Nina ushahidi wa kutosha kuhusiana na Wizi na Ufisadi wa Lowassa na Rostam -John Mnyika.
2. CCM wamempatia Fisadi Lowassa fomu ya kugombea urais. Ni hatari sana -Tundu Lissu.
3. Nimesema kama UKAWA tutamsimamisha fisadi , mna haki ya kututosa -Halima mdee
6. I thought safari ya Matumaini was poorly organized, imekuwa safari ya marumizi
4. Taarifa kwa Umma: Serikali iache kumlinda Lowassa , ni mmoja wa mizizi ya ufisadi wa Richmond. Akamatwe, ahojiwe na achukuliwe hatua za kisheria - Yeriko Nyerere
5. Wakati Mwakyembe na Magufuli wakiwajibika kulitumikia taifa , kuna Mapaka shume yanatembea Makanisani na Misikitini yakisaka urais -Yeriko Nyerere
6. Ni heshima kwa Mungu kumzomea na kumtukana mtu FISADI kama Lowassa -Godbless Lema
7. Pamoja na haki ya kila mtu kugombea urais ,kwa hawa walioomba kutoka CCM, I don't *see talent , kwangu mimi wote ni average brain-Peter Msigwa' s *tweet 09/06/2015
8. Mtu anayetaka nafasi urais, lazima awe tayari kujipima, kujitafakari, kujiridhisha kuwa anatosha, yeye mwenyewe kwanza, afanye hayo, ajipime , ajitafakari na ajiridhishe kuwa anatosha:
* * * *¡ * kiafya
* * * *¡¡ *kiakili
* * * *¡¡¡ *kimaadili
* * * *¡v kidhamira
Lazima ujipime hayo kama unapungukiwa na mojawapo kati ya hayo, hufai, lakini la pili uwe tayari Umma kukupima katika hayo niliyoyataja, uwe tayari Umma ukupime kiafya, kiakili, kimaadili na kidhamira, siyo unajipima tu mwenyewe na unasema , mimi sawasawa, A a a *a, na Umma nao ukupime - Fredrick Tluwaye Sumaye
9. CCM mkimpitisha Lowassa nahama Chama –Sumaye
10. Njaa hadi kwenye nyumba za ibada, Wachungaji wa makanisa mbalimbali ya Kikristo wakiandamana muda huu kwenda nyumbani kwa Edward Lowassa kumshinikiza achukue fomu ya kugombea urais. I hope Mapadre hawamo humo. Mungu atuepushe.*
11. Yaani Kanchi ketu haka kanaendeshwa kwa ujanja ujanja na wiziwizi tu. Mtu akiwa na hela zake basi anafanya jambo lolote tu -Julius Mtatiro
12. Lowassa ni dhaifu -MBOWE
 
sitomuamini mbowe tangu nliposikia alipokea bil 10 ili lowassa aingie, walanguzi wakubwa, laana iko juu yao ngoja uchaguzi utakapoisha tutajua ukweli

Eti sitomuamini uliposikia alipokea bil 10, dah sasa hii kazi. Kusikia tuu bila ushaidi, basi chuki na ku kosa kabisa kumuamini.
Ungeonyesha ushaidi, hapo sawa, lakini bila ushaidi, basi ninamashaka na uwezo wako wa kudadavua mambo. Kama hizi ndo akili za watanzania wengi, basi nchi ina safari ndefu ya ukombozi.
Ccm wameuza nchi kwa wawekezaji hulioni? Wanyama pori kutorosha huoni? Watu kupiga dili ESCROW, hulioni? Wanafunzi kukaa chini hulioni? Huduma duni za afya kwa wazee, akina mama na watoto, huyaoni hao.
Wachache kua matajiri, na wengi kuwa masikini kwenye nchi yenye kilakitu, hayo huyaoni? Ila bado waiamini ccm kuku letea maendeleo. Dah! Majanga kweli. Ila unauchungu wa hisia eti kapewa hela na sio kua na uchunga na hali halisi ya nilioataja hapo juu. Amakweli alio waroga watanzania kafaa. Badilikeni jamani, tuanze ukurasa mpya. Tanzania bila ccm inawezekana kama vile tanzania bila nyerere inasonga mbele.
 
Hizi taarifa tumezichoka, wasitutoe kwenye mada ya msingi dakika hizi za mwisho kuelekea kupiga kura, mbinu nyingi zitatumika sasa hivi kuwatoa wapiga kura kwenye mada.
 
Duhh hata ningekuwa mimi mahela yote hayo niyaachie mwe
 
Back
Top Bottom