Mbowe atolewa nje ya bunge

Mbowe atolewa nje ya bunge

Chanzo cha yote haya ni bunge ni kuongozwa na huyu Naibu Spika ambae kitaaluma zaidi amesomea wanyama pori sasa sheria na yeye wapi na wapi? Katiba mpya ilitizame hili pia kwa kweli kua SPIKA NA wenyeviti wao wawe watu walosoma sheria
 
ndugai anataka msimu ujao awe spika wa bunge na kigezo anatakiwa akandamize uoinzani. sasa kuna sababu gani ya kumzuia kiongozi wa kambi ya upinzani asitoe hoja?, haya bwana kidumu chama cha maoinduzi na utawala wa ndugai bungeni.
 
kwa mara nyingine kiti cha spika kinazidi kudhihirisha ubabe na ukandamizaji wa serikali ya ccm dhidi ya WAPINZANI.

kumtoa Mbowe bungeni Ndugai na CCM kwa ujumla watajuta.

nb;
Ndugai ameshanza kujuta kwa kumuomba Mbowe arudi bungeni saa 11.

paradiso hapo blue ya kweli hayo??
 
Last edited by a moderator:
Leo bunge la JMT limegeuka kioja,huku naibu spika wa bunge akionesha kukitumikia chama tawala,na si kutumikia watanzania.kitendo cha kumtoa Mbowe nje kwanza ni kumpa ujiko mkubwa Mbowe,ambae kimsingi anasimama muda wowote bungeni na kuzungumza kama ilivyo kwa waziri mkuu.
Sasa kitendo cha Ndungai kuamuru kutumika nguvu kumtoa kiongozi huyo wa kambi ya upinzani bungeni,kitendo kilichoprove "Upumbavu" wa naibu spika.
C
Kioja Kingine ni kwa shirikisho la utangazaji Tanzania,tbc kufanya kazi kitumwa kwa kuacha kuwaonesha watanzania ngumi zilivyopigwa pale chini,badala yake kutuonesha sura mbaya ya Job Ndungai ambae kimsingi ndio chanzo cha haya yote.
Kwa mtu atakaewashabikia ccm kwa hili la leo,apimwe akili,na kiukweli,leo Ndungai kakivua ccm nguo,na wabunge wote waliobaki bungeni leo ni watumwa,ila namshukuru Mrema kuleta burudani Bungeni,na kuongea mambo ambayo hakuwa ameulizwa,acha akae humo bungeni maana akitoka atakufa.
 
bila kung'oa kiti cha spika na kutoka nacho nje au kubeba siwa na kutoka nayo miccm haitojitambua, esp mchawi Ndugai.
 
kwa mara nyingine kiti cha spika kinazidi kudhihirisha ubabe na ukandamizaji wa serikali ya ccm dhidi ya WAPINZANI.

kumtoa Mbowe bungeni Ndugai na CCM kwa ujumla watajuta.

nb;
Ndugai ameshanza kujuta kwa kumuomba Mbowe arudi bungeni saa 11.
Really! Nilidhani wangemfungia hadi kikao cha Novemba kama walivyomfanyia Zitto miaka ile.
 
Mkuu, kwani kuna wabunge wangapi wameongea? si wawili tu yaani mzee Mrema na huyu anayeongea sasa ANNE KILANGO MALECELA? acha kukurupuka
aka mama wa karo-lite.
 
Mkuu Profesa, wakat mwingine huwa inanichanganya mtu wa namna kuwa naibu spika ni aibu yaani hata busara hana.. muda uliotumika kwa fujo hivi huku yeye mimeno kaitoa kufurahi order yake ikitekelezwa ilitosha kabsa kwa mh.Mbowe kutoa hoja yake na bunge kujua alichotaka kusema hasa nin..

Mim naona Makinda ni bora na huwa anafanya kazi vizuri sana na upinzani kulinganisha na viongozi wengine wa bunge hasa naibu spika na wale wenyeviti wawili ukimwacha Zungu.. Bila shaka ni aibu kwa Ndugai na kwa Bunge kuwa na kiongozi mjinga kama Ndugai.
Jana wakati wa walkout ya wapinzani nilimsikia akisema 'waacheni tuwaone nafikiri hawanitambui' ni maneno ya ubabe wa mitaani ambayo hayatakiwi kutolewa hadharani na kiongozi kama yeye, lakini kwa akili ya wabunge wa CCM wanayafurahia bila kujua madhara yake, in short Ndugai ha-fit pale kwa vigezo vyovyote.
 
hujui chadema ni tanuri la uongo? Lema kakimbia bunge toka alivyoambiwa atoe ushahidi. wabunge wa Ccm walisema kama askari wa bunge wameshindwa waachiwe wao,si unajua tena waliberali mikono imewalegea
wabunge wa chadema ni wachache ingetokea mauaji.
 
Hiki ni kishooiya....Hakiwezi kupata tena kura kule vunjo.

Mkuu Mkirua
Niliposema tunamambo mengi makubwa ya msingi hili ni moja wapo, huku ndiko tunatakiwa kuweka nguvu zetu mengine yote yatanyooka yenyewe.
 
Ndugai,ndugai,ndugai,ndugai, nammiss sana samweli sitta kuliko hiki kiazi cha ccm!!!!!!!!!!
 
paradiso hapo blue ya kweli hayo??

ni kweli kabisa, Ndugai akifunga bunge kwa unyonge mkubwa amesema Mbowe na wenzake wanaruhusiwa kurudi bungeni kuendelea na mjadala. tena akasema eti tumsmeheni tu uyu Mbowe na tuendelee na kazi kwa pamoja(sijaonaKOSA la Mbowe hasa)
Ndugai anajuta sasa.
 
Sikuwa nafuatilia toka mwanzo ila Lyatonga Mrema ameniacha hoi kwa kusema kuwa yeye hawezi kutoka kwa kuwa CDM haijamshirikisha kwenye kambi rasmi ya upinzani! Kana kwamba pembe ya ng'ombe haijifichi akaanza kumfagilia Rais kwa kumteu Mbatia na kupeleka maendeleo jimboni kwake...ghafla akamuomba PM msamaha kwa kusaini ule wa waraka wa kumuondoa eti alikuwa anajipendekeza kwa CDM lakini walimtosa! akasema "you scatch my back I'll scratch yours"!!!
Safari ni ndefu sana kuelekea kwenye maendeleo na demokrasia ya kweli Tanzania...

mkuu usiumize kichwa chako na huyu mzee,he is a zombie,he came back reincarnated.
 
Mkuundu-gai nafikiri hatagombea tena mwaka 2015 kwa namna anavyoliendesha Bunge hadi aibu sidhani kama hata CCM watampitisha kugombea kwani ni dhahiri wapiga kura wake watampiga chini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom