Mbowe atolewa nje ya bunge

Mbowe atolewa nje ya bunge

Ndugai hovyo sana,kwa nini asimsikilize anataka kusema nini Mbowe?

Anaogopa atakachosema kamanda Mbowe hana ubavu au uwezo wa kujibu, kwa hiyo "Kinga ni bora kuliko Tiba".
Afadhali aonekane mbabe kuliko adhalilishwe kwa kushindwa kukabili hoja za Mbowe.
Kweli sasa matunda ya CCM kutuwekea Bi Kiroboto na huyu naibu wake ndiyo haya, aibu kubwa sana kwa Bunge hili la kumi.
 
Wabunge wanapojadili Mswada wa kuwezesha kua Sheria ni jambo ambao linahitaji umakini wa hali ya Juu bila kufata ushabiki wa Itikadi za Vyama,kwa Kua Sheria inapotungwa Tayari inakua Na impact kubwa mahali itakapotumika,Wabunge wanapotofautiana katika Kutunga sheria inaonesha kuna Mapungufu ambayo yanahitajika KUfanyiwa Marekebisho,Hatutegemei kuona Wabunge wanatofautiana katika Jambo la Kutunga Sheria kufikia Kiasi cha Kutoelewana jambo hili linadhirisha wazi kua Kuna Kundi mojawapo lina Maslahi Binafsi hivyo kuwahadaa wananchi,ni vema Wabunge wanapotofauiana wakapeana muda wa Kusikiliza Hoja za Kila Upande na Kufikia Hitimisho kwa Hoja zenye Maslahi ya Nchi yetu.Kwa jambo hili Naibu Spika Kulazimisha Maoni ya Idadi ya Walio Wengi kutoka Chama Tawala kua Ni Uamuzi wa Jambo hilo bila Kuzingatia Kwa Makini hoja za Pande Mbili katika Jambo hili ni Kupwaya ki Uamuzi.
 
wapinzani 50 na ccm 200 ni huko bungeni lakini nje ya bunge wanaounga mkono wapinzani wanaweza kuwa wengi kuliko wale walioko upande wa ccm. nataka hili ccm walielewe. kama ni hivo basi ni bora kujiandaa kiakili.
 
Ili kuepukana na fedhea kama hizi si vibaya jokery mbowe akajiendeleza hata kwa elimu kwa njia posta itamfungua kiakili na upeo
 
ili kuepukana na fedhea kama hizi si vibaya jokery mbowe akajiendeleza hata kwa elimu kwa njia posta itamfungua kiakili na upeo

aliyekuambia mbowe hajasoma ni nani.mpeleke shule,vinginevyo una pepo la wivu na utumwa...!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
aliyekuambia mbowe hajasoma ni nani.mpeleke shule,vinginevyo una pepo la wivu na utumwa...!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Elimu tunayozungumzia si ya uDJ kwenye uDJ amefuzu mpk ngazi ya taifa kwengine ni mzungu wa reli
 
Naangalia bunge sasa,wabunge wa ccm hawajadili tena hoja bali wanaijadili cdm na upinzani kwa ujumla.pure ccm na wabunge wake wasio na uelewa.
 
Nimefarijika sana jioni baada ya kuzima tv punde baada ya kigwangala kunichefua na kukutana na mzee wa mako na mkewe wakiniambia wamezima tv kwa kusononeshwa na wabunge wa ccm kuacha kujadili mswada husika na kum-attack mh.mbowe hadi kufikia hatua ya kumtaja mke wake mbowe asiehusika na hoja inayojadiliwa bungeni.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Duh kumbe Vita inaanzia humu humu ndani afu mnasingizia Rwanda ona Bunge lenu Full aibu
Mkuu hata mimi nilikuwa nafikilia hivyo hivyo, ni aibu tupu - nilishapendekeza kwamba kama Taifa letu linaona tuendelee na chama kimoja basi watangazie dunia hivyo. Haya mambo ya kudhani vyama vya upinzani ni maadui, wakosa uzalendo na mambo mengine chungu mzima ya kutunga tu! Watu wazima wana-behave kama watoto wa shule, zomea zomea ovyo, maneno ya kashfa, kupiga makofi ambako hakuitajiki - yaani mtu unaona wazi wazi kwamba sio kujali sana chama tawala bali ni watu kutaka kujipendekeza tu, wengi wao hawana moyo wa dhati wa kujali maslahi ya taifa letu; kama wangekuwa wazalendo kweli mbona hawakomalii biashara ya madawa ya kulevya ambayo yanalitia aibu kubwa Taifa letu, yaani mtu ukiwa na passport ya Tanzania una angaliwa mara mbili mbili unapokuwa kwenye viwanja vya Ulaya na Merikani, cha ajabu Taifa letu alifanyi effort zozote ya kukamata Kingpins wa upuuzi huu, wana wahacha wa roam streets scotch free au kutoa visingizio mbali mbali ili wasifikishwe mbele ya PILATO!! Jana kwa mfano niliangalia kwenye playback mtandaoni wabunge wa upinzani wakiondoka Bungeni wakipinga masuala fulani, ili ni jambo la kawaida kwa nchi zinazo jali demokrasia - ajabu wabunge wa chama tawala wanaona huo ni uhasi au sijui kukosa shukrani! Wanafika hatua ya kuwasimanga eti walikaribishwa chai na JK Ikulu sasa kwa nini wanapinga sijui mapendekezo gani? Mambo ya ajabu kweli kweli!! Kwani leo naibu wa Spika angemuhacha Mh.Mbowe akasema alichotaka kusema alafu akapewa onyo baadae baada ya kugundulika kwamba Mh.Mbowe hakuwa na hoja ya maana - kwa nini Kiongozi wa Upinzani Bungeni hachukuliwe lightly?? Hivi Bunge au naibu Spika wangemsikiliza mbowe wangepoteza nini? Ni vizuri tuwe wastaarabu kidogo, hakuna sababu za kuvurumisha Viongozi wa vyama vya upinzani na kuwadhalilisha nao they deserve heshima, hata kama hawapo madarakani - wote ni Watanzania, tofauti za itikadi za vyama zisitufanye kutoana macho na masikio. Hivi wabunge wetu na maspika wanapokwenda kuangalia Bunge za wenzetu Ulaya na kuketi kwenye mabunge ya wenzetu wanajifunza nini. Narudia kusema Bunge jana jioni linapoteza muda mwingi wakitoa hotuba za kulaani kitendo cha wabunge wa upinzani kususia kikao, hata wabunge ambao waliwahi kupata bahati ya kutembelea mabunge ya Ulaya na Merikani na kuona nini maana ya Demokrasia Bungeni nao wakaingia mkumbo huo huo wa kulaani wapinzani - tubadilike jamani, upinzani si uhaini!!
 
Kiongozi makini yu tayari kusikia asichotaka kusikia,uvumilia sana na kutumia busara zaidi kuliko mamlaka yake kuongoza.....kuna kazi kubwa sana ya kupata viongozi bora na sahihi...binafsi namwona Ndugai kukosa sifa za kuwa kiongozi mwenye kuweza kuunganisha makundi yenye mtazamo tofauti bali ni mtu mwenye kuegemea upande mmoja na anayesahau kuwa kiti cha spika kinahitaji busara nyingi zaidi kuliko hasira.
 
Angesubiri bwana Mrema amalize kuongea kwanza. Mbona ustaarabu hauuzwi..
 
Mbowe wananchi tupo nyuma yako mwanzo mwisho, 2015 sio mbali kiasi hicho na kila jambo na wakati wake, tunakuamini sana tena sana!!!!!!!
 
Ooovyo! chukua chako Mapema (CCM) kilichotokea Bungeni ni aibu ya naibu spika na serikali yake kukosa staha ya kuongoza Bunge na kusikiliza hoja za wapinzani.Oovyo mtu mzima hovyooo mbaya hatari aibu shida ziro
 
Dah! kama ndo kumekucha vile, kwa hakika tunakoelekea huko..... mmmh sijui.
Na vip kuhusu uzalendo, amani na upendo?
 
Bunge la Tanzania limegeuka Kichen Party.

Mkuu bila shaka wewe ni mhudhuriaji wa hizo kitchen party maana ni vigumu mtu kuzungumza au kufananisha kitu usichokijua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom