Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,880
- 12,320
Napenda kuwasalimu kwa jina la alietuumba. Ndugu zangu, ingawa inafahamika kuwa CCM na Serikali yake wana uzoefu, ujuzi na uwezo wa kucheza na saikolojia ya wapinzan wao kwa kuanzisha jambo baada ya jambo, lkn safari hii aisee wameweza kufanya jambo ambalo wengi hatukulitarajia hata kidogo katika kipindi hiki ambacho mh Mbowe analala mchongoma na masela mbali mbali kule keko.
Ni kweli tumezoea kuyaona baadhi ya mambo ambayo CCM na serikali yake huyafanya kwa lengo la kuwapoteza maboya wapinzani wao, mfano halisi ni mwaka 2015 ambapo CCM ya mzee Kikwete walikuja na style ya "mchawi mpe mtoto akulelee".
Na kweli style hii ilizaa matunda baada ya wapinzani kuingia mkenge kwa kumpokea mtoto huyo ili wamlee na matokeo yake ilikuwa ni ushindi mtamu kwa CCM, huku wapinzani wakishikana uchawi wenyewe kwa wenyewe.
Sasa baada ya CCM kufanya yale iliyofanya mwaka 2015, safari hii tulijua hali ingekuwa tofauti. Lakini kwa weledi mkubwa CCM imekuja na Mbinu nyingine ya kutuliza hali kuhusu kukamatwa kwa mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani mh Mbowe. Kwanza walikuja na swala la gazeti fulan kuleta taharuki, na pili wakamalizia na picha la Sabaya akimuhusisha hayati Magufuli katika kesi yake.
Na kwahili naweza kusema wamefanikiwa maana wanaharakati wote waliokuwa wanampigania Mbowe aachiwe huku mitandaoni washaonekana kumtelekeza mwenyekiti wao na kuvalia njuga swala la Sabaya.
Hii ndo CCM iliyomshinda hata Nyerere mwenyewe bwana!!
Ni kweli tumezoea kuyaona baadhi ya mambo ambayo CCM na serikali yake huyafanya kwa lengo la kuwapoteza maboya wapinzani wao, mfano halisi ni mwaka 2015 ambapo CCM ya mzee Kikwete walikuja na style ya "mchawi mpe mtoto akulelee".
Na kweli style hii ilizaa matunda baada ya wapinzani kuingia mkenge kwa kumpokea mtoto huyo ili wamlee na matokeo yake ilikuwa ni ushindi mtamu kwa CCM, huku wapinzani wakishikana uchawi wenyewe kwa wenyewe.
Sasa baada ya CCM kufanya yale iliyofanya mwaka 2015, safari hii tulijua hali ingekuwa tofauti. Lakini kwa weledi mkubwa CCM imekuja na Mbinu nyingine ya kutuliza hali kuhusu kukamatwa kwa mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani mh Mbowe. Kwanza walikuja na swala la gazeti fulan kuleta taharuki, na pili wakamalizia na picha la Sabaya akimuhusisha hayati Magufuli katika kesi yake.
Na kwahili naweza kusema wamefanikiwa maana wanaharakati wote waliokuwa wanampigania Mbowe aachiwe huku mitandaoni washaonekana kumtelekeza mwenyekiti wao na kuvalia njuga swala la Sabaya.
Hii ndo CCM iliyomshinda hata Nyerere mwenyewe bwana!!