Mi mi
JF-Expert Member
- Jul 14, 2024
- 5,752
- 10,523
Israel imekua ikitumia mbinu wa kuua viongozi wa juu kisiasa au kijeshi katika serikali[ Iran ] na makundi hasimu kama Hamas,Hezbollah,Houthi je, mbinu hii ina faida kimedani kwao au ipo tu katika kujizolea ujiko kwa jeshi lake ?
Toka Israel imeanza kuua viongozi hao ni kipi kilicho badilika katika serikali[ Iran ] na makundi kama Hamas,Hezbollah na Houthi ?
Je, misimamo yao imebadilika juu ya Israel ?
Je, makundi hayo yameingia katika migogoro ya ndani ya kiutawala ?
Je, kumetokea kuto kuelewana katika utoaji wa amri za kimashambulizi katika makundi hayo ?
Israel katika vita vya siku 12 na Iran ilianza kwa kuua viongozi wa ngazi za juu za kiutawala katika jeshi na serikali ya Iran. Je, Israel ilipata faida gani baada ya kufanya hivyo ?
Mbinu ile ile wameirudia tena katika vita vya sasa kwa kumuua kiongozi mkuu wa kidini wa Iran. Je, shambulizi hilo limebadili nini mpaka sasa kwa Iran au limeipa faida gani Israel mpaka sasa ?
Bado Israel ina sisitiza itaendelea kuwaua viongozi wote wa kidini watakao chaguliwa Iran sasa je, Israel inapata faida gani kwa maamuzi haya kama wataendelea kuua kila kiongozi atakae chaguliwa je, maamuzi yao haya yana badili nini katika utawala wa Iran kiasi kwamba iwe faida kwa Israel.
Jambo la kukumbusha Israel imeua viongozi wa Hamas karibu wote lakini mwisho wa siku ili rudi mezani kuzungumza na Hamas juu ya mahitaji yao kwa maana nyepesi mbinu yao ya kuua viongozi wa Hamas imeshindwa kufanikisha wao kuyatimiza malengo yao yote katika vita vya Gaza mpaka sasa.
Hivyo hivyo kwa Hezbollah tunaiona Hezbollah leo ipo na inaendelea kupambana na Israel huko mpakani pamoja ya kwamba viongozi wao wakuu huuawa mara kwa mara.
Pia kwa Houthi licha ya kuuawa viongozi wao ila bado kundi hili lipo na misimamo yake ile ile.
Hiki ndicho nacho kiona kwa Iran mpaka sasa.
Sasa kwanini Israel inaendelea kuamini katika mbinu hii ambayo ijaleta matunda kwao mpaka sasa kwa makundi yote aliyo pambana nayo na kwa serikali ya Iran mpaka sasa ?
Toka Israel imeanza kuua viongozi hao ni kipi kilicho badilika katika serikali[ Iran ] na makundi kama Hamas,Hezbollah na Houthi ?
Je, misimamo yao imebadilika juu ya Israel ?
Je, makundi hayo yameingia katika migogoro ya ndani ya kiutawala ?
Je, kumetokea kuto kuelewana katika utoaji wa amri za kimashambulizi katika makundi hayo ?
Israel katika vita vya siku 12 na Iran ilianza kwa kuua viongozi wa ngazi za juu za kiutawala katika jeshi na serikali ya Iran. Je, Israel ilipata faida gani baada ya kufanya hivyo ?
Mbinu ile ile wameirudia tena katika vita vya sasa kwa kumuua kiongozi mkuu wa kidini wa Iran. Je, shambulizi hilo limebadili nini mpaka sasa kwa Iran au limeipa faida gani Israel mpaka sasa ?
Bado Israel ina sisitiza itaendelea kuwaua viongozi wote wa kidini watakao chaguliwa Iran sasa je, Israel inapata faida gani kwa maamuzi haya kama wataendelea kuua kila kiongozi atakae chaguliwa je, maamuzi yao haya yana badili nini katika utawala wa Iran kiasi kwamba iwe faida kwa Israel.
Jambo la kukumbusha Israel imeua viongozi wa Hamas karibu wote lakini mwisho wa siku ili rudi mezani kuzungumza na Hamas juu ya mahitaji yao kwa maana nyepesi mbinu yao ya kuua viongozi wa Hamas imeshindwa kufanikisha wao kuyatimiza malengo yao yote katika vita vya Gaza mpaka sasa.
Hivyo hivyo kwa Hezbollah tunaiona Hezbollah leo ipo na inaendelea kupambana na Israel huko mpakani pamoja ya kwamba viongozi wao wakuu huuawa mara kwa mara.
Pia kwa Houthi licha ya kuuawa viongozi wao ila bado kundi hili lipo na misimamo yake ile ile.
Hiki ndicho nacho kiona kwa Iran mpaka sasa.
Sasa kwanini Israel inaendelea kuamini katika mbinu hii ambayo ijaleta matunda kwao mpaka sasa kwa makundi yote aliyo pambana nayo na kwa serikali ya Iran mpaka sasa ?