Mbeya na mambo yao

Wasomi ma Tanzania One wengi wametoka mbeya
Mbeya kuna ziwa moja sio maarufu sana linaitwa ziwa Gosi, hilo lilivokaa kaa linawatisha watu, inadaiwa lilihamishwa Tukuyu likaja huku mbelembele na Igawilo, hilo ziwa ukiongea kinyakyusa eti linakulamba, mwenye detail kidogo atupe kuhusu hilo ziwa.
Tuliwahi kuzulu hilo ziwa tukakuta kuna mawe mengi ya majina ya watu kama wa nne hivi sio watanzania waliokuwa wanafanya utafiti walipotelea humo humo.
Mbeya kweli kwa Tofauti.
Wanaoumwa magonjwa ya ajabu wanatoka Mbeya (Mwakyembe & Mwandosya)

Mbeya, pia iliitwa Moon Bay na wazungu!
 
Wasomi ma Tanzania One wengi wametoka mbeya
Mbeya kuna ziwa moja sio maarufu sana linaitwa ziwa Gosi, hilo lilivokaa kaa linawatisha watu, inadaiwa lilihamishwa Tukuyu likaja huku mbelembele na Igawilo, hilo ziwa ukiongea kinyakyusa eti linakulamba, mwenye detail kidogo atupe kuhusu hilo ziwa.
Tuliwahi kuzulu hilo ziwa tukakuta kuna mawe mengi ya majina ya watu kama wa nne hivi sio watanzania waliokuwa wanafanya utafiti walipotelea humo humo.
Mbeya kweli kwa Tofauti.
Wanaoumwa magonjwa ya ajabu wanatoka Mbeya (Mwakyembe & Mwandosya)
According to Nyakyusa ancients ni kuwa ziwa hilo lilikuwa maeneo ya Mwakaleli, ikatokea watu wakipeleka mifugo kunywa maji kwenye hilo ziwa ikawa inazamishwa na kupotezwa kimaajabu ajabu, baadaye watu pia wakaanza kuzamishwa katika hilo ziwa.
Ndipo machifu walipoitana na kufanya kikao kirefu na maamuzi waliyokuja nayo ni kuwa inabidi either walifukuze au walihamishe ziwa hilo.
Baadaye wakakubaliana kulihamisha na taratibu za kijadi kuhamisha ziwa hilo zikafanyika ambapo walichukua mawe na kuyachoma moto mpaka yalipoapata moto sana na kubadirika rangi. Hapo machifu wakaanza kuchukua yale mawe na kuanza kuyarushia katika lile ziwa, kwa maajabu ya wote wakaona maji yanajikusanya na kuinuka juu na kuondoka kama wingu la mvua, maji hayo yakaenda kutua katika mlima unaouongelea na mpaka sasa yapo pale.
Simulizi zinasema kuwa ziwa lile lilikuwa 'limekasirika' kwa kuondolewa sehemu yake ya asili na kupelekwa 'ukimbizini' hivyo ikawa ukifika katika vilima na misitu ile izungukayo lile ziwa halafu ukaongea kinyakyusa unapotea.
Hapo ikabidi machifu wakae tena vikao vyao kujua kwanini wanyakyusa wanapotea kule na si wasafwa (Ieleweke kuwa eneo lile wengi ni wasafwa), ndipo wakagundua kuwa ni lille ziwa 'lililofukuzwa' kule miaka iliyopita limehamia pale na lina 'hasira' na wanyakyusa, ikabidi machifu wafanye tena utaratibu kuondoa hali ile na walifananikiwa japo mpaka sasa kuna hako kahofu ka kuongea kinyakyusa ndani ya vilima vile.

Nawasilisha
 
Haya ni baadhi tu ya mambo yaliyowahi kutokea huko Mbeya.
  • Eneo la Forest kulikuwa na msitu mkubwa ambako mauji yalikuwa yakifanyika kila uchao.
  • Eneo la soweto kulikuwa na wachinjaji, kila mara miili ya watu waliochinjwa ilikuwa ikukutwa eneo hilo.
  • Nonde ni kitongoji kilichopo Mbeya mjini, ila kimekaa kama kiko maili elfu tatu kutoka mjini. Bangi inavutwa hadharani kuanzia kwenye ngazi ya familia. Huko kazi yao kubwa, kinababa ni kuchinja ng'ombe na wanawake kufanya biashara ndogondogo soko la Mabatini. Kiongozi asiye rasmi aliyewahi kusimika bendera na kudai kuwa Nonde ni nchi yake alikuwa ni Baunsa mchinja ng'ombe maarufu akiitwa Mwasimba.
  • Jombi alikuwa ni jambazi maarufu zambia na tanzania akiteka magari, kupora magari na mali za watu.Alikuwa akitoa taarifa kabla hajafanya uhalifu wake. Wazungu wa Denmark waliokuwa wakifadhili mradi wa maji danida walikatisha msaada wao baada ya Jombi kuua na kubaka mke wa mkurugenzi wa mradi huo. Mkapa akatoa amri kuwa jombi akamatwe. Vikosi maalum ndio vilivyoenda kumkamata jombi.
  • Mbeya kuna makanisa mengi sana yenye majina ya Kiingereza, Kiswahili, Kinyiha, Kisafwa, Kimalila na Kikimbu. Makanisa mengi na uovu mwingi vyaenda sambamba.
  • Waimbaji wa nyimbo za injili wanaovuma wengi wao wana asili ya Mbeya.
  • Pombe ya kadansana ilikuwa maarufu sana mwaka 2000, haijuulikani ilikokuwa ikitokea. Ilikuwa ikiua sana watu, na watu waliendelea kuishabikia hadi ilipogundulika kuwa inatoka Malawi, ikapigwa marufuku kabisa.
  • Mauaji na uchunaji wa ngozi uliwatisha sana watu waishio nje ya mkoa wa Mbeya, Mbeya hali ilikuwa shwari kabisa.
  • matukio ya kupigana na nondo ilikuwa gumzo sana mwaka juzi na mwaka jana, wengi walijeruhiwa.
  • Leo Mbeya kuku na nguruwe wananenepeshwa kwa dawa za kuzuia makali ya ugonjwa wa ukimwi.
  • Pombe inayoitwa kiduchu ndio sasa iko kwenye midomo ya watu. lmeacha gumzo kwa kuwa ukiiweka kwenye chupa inavimbisha chupa hadi inapasuka. pombe hiyo inahifadhiwa kwenye vyungu.Ni ya hatari lakini wana Mbeya wanaendelea tu kuinywa.
  • Kuna vivutio kibao vya utalii lakini havitangazwi, sijui ni kwanini.
  • Pichani ni kijana Peter muongoza watalii akijipumzisha baada ya kazi ngumu ya kutwa nzima.
  • 2338502-Peter_after_a_hard_days_work-Mbeya.jpg



...wakuu naomba mnijuze, hivi jina Mbeya lina maana gani? ni nani aliupa mkoa huu jina hilo? je jina hilo limeanza kutumika mwaka gani?
 
Hapo kwenye hiyo pombe kiduchu me ndo nimewakuli wambeya, au mna matumbo ya chuma nini! Pombe inayovimbisha chupa tumboni inakuwaje?
 
...wakuu naomba mnijuze, hivi jina Mbeya lina maana gani? ni nani aliupa mkoa huu jina hilo? je jina hilo limeanza kutumika mwaka gani?
Jina Mbeya linatokana na lugha ya kisafwa ambacho kinafanana na kindali, likiwa na maana ya chumvi, yaani imbeeje. Miaka ya nyuma palikuwa na soko na chumvi iliuzwa pale. Wazungu, kama walivyotohoa majina ya maeneo mengi, wakapaita Mbeya. Mwaka gani, really, sijui. Loli nine kokukaja, gwe nakumis sana.
 
Jina Mbeya linatokana na lugha ya kisafwa ambacho kinafanana na kindali, likiwa na maana ya chumvi, yaani imbeeje. Miaka ya nyuma palikuwa na soko na chumvi iliuzwa pale. Wazungu, kama walivyotohoa majina ya maeneo mengi, wakapaita Mbeya. Mwaka gani, really, sijui. Loli nine kokukaja, gwe nakumis sana.
kama kindali hukijui ni bora unyamaze kimya KINDALI HAKIFANANI NA KISAFWA HATA KIDOGO. KINYAKYUSA SIO KINDALI, KISUKUMA SIO KINYAMWEZI. take that to the bank
 
According to Nyakyusa ancients ni kuwa ziwa hilo lilikuwa maeneo ya Mwakaleli, ikatokea watu wakipeleka mifugo kunywa maji kwenye hilo ziwa ikawa inazamishwa na kupotezwa kimaajabu ajabu, baadaye watu pia wakaanza kuzamishwa katika hilo ziwa.
Ndipo machifu walipoitana na kufanya kikao kirefu na maamuzi waliyokuja nayo ni kuwa inabidi either walifukuze au walihamishe ziwa hilo.
Baadaye wakakubaliana kulihamisha na taratibu za kijadi kuhamisha ziwa hilo zikafanyika ambapo walichukua mawe na kuyachoma moto mpaka yalipoapata moto sana na kubadirika rangi. Hapo machifu wakaanza kuchukua yale mawe na kuanza kuyarushia katika lile ziwa, kwa maajabu ya wote wakaona maji yanajikusanya na kuinuka juu na kuondoka kama wingu la mvua, maji hayo yakaenda kutua katika mlima unaouongelea na mpaka sasa yapo pale.
Simulizi zinasema kuwa ziwa lile lilikuwa 'limekasirika' kwa kuondolewa sehemu yake ya asili na kupelekwa 'ukimbizini' hivyo ikawa ukifika katika vilima na misitu ile izungukayo lile ziwa halafu ukaongea kinyakyusa unapotea.
Hapo ikabidi machifu wakae tena vikao vyao kujua kwanini wanyakyusa wanapotea kule na si wasafwa (Ieleweke kuwa eneo lile wengi ni wasafwa), ndipo wakagundua kuwa ni lille ziwa 'lililofukuzwa' kule miaka iliyopita limehamia pale na lina 'hasira' na wanyakyusa, ikabidi machifu wafanye tena utaratibu kuondoa hali ile na walifananikiwa japo mpaka sasa kuna hako kahofu ka kuongea kinyakyusa ndani ya vilima vile.

Nawasilisha

Aisee historia tamu sana.....ukiwa unaangalia isidingo haya utajulia wapi?
 
Wasanii wakubwa wametoka Mbeya japo wamejikausha. Kama AY {Ambwene Yesaya}, GK {Gwamaka Kaighula}. Rais wa Kongo Joseph Kabila kasoma Mbeya, Wasanii kama vile Prof. Jay, Soggy Dog, Jay Moe wamesoma Mbeya pamoja na wengineo kibao. Hata wasomi wengi wenye uelewa mzuri wametoka Mbeya.
 
Thread imenikuna kweli, nimepitia post zote. Hata miye natokea Mbeya tena Kyela>kikubwa tunajazana ujinga tu hapa, ktk wilaya zilizoshindwa kutumia fursa basi kyela inaongoza, huko watu wanavuavua badala ya kuvua samaki, badala ya kulima wao wanalimalima, wakati Tukuyu wanafuga huko Kyela wanafugafuga> mboga za majani na maziwa vyote vinatoka Tukuyu.
 
Back
Top Bottom