Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Juma Homera, ameliagiza Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama mkoani humo kumsaka na kumtia nguvuni, Andrea Ngomeni, mkazi wa Kijiji cha Kambikatoto wilayani Chunya kwa tuhuma za kuuza eneo la pori la akiba la hifadhi ya msitu wa asili Rungwa.
Homera ametoa agizo hilo akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mbeya baada ya kufika katika hifadhi na pori la Rungwa Two na kukuta sehemu ya hifadhi imefyekwa kwa ajili ya kilimo na mifugo na kujulishwa kuwa eneo hilo limeuzwa kwa wafugaji kutoka wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
"Nawaagiza polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kumsaka huyu bwana Andrea akamatwe ili hatua zichukuliwe, maana haiwezekani watu wanajifanyia wanavyotaka," amesema RC Homera
Homera ametoa agizo hilo akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mbeya baada ya kufika katika hifadhi na pori la Rungwa Two na kukuta sehemu ya hifadhi imefyekwa kwa ajili ya kilimo na mifugo na kujulishwa kuwa eneo hilo limeuzwa kwa wafugaji kutoka wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
"Nawaagiza polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kumsaka huyu bwana Andrea akamatwe ili hatua zichukuliwe, maana haiwezekani watu wanajifanyia wanavyotaka," amesema RC Homera