Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,814
- 11,991
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kuzuia na kudhibiti ajali za barabarani kwa kushirikiana na mamlaka na wadau mbalimbali wa usafirishaji katika Mkoa wa Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamini Kuzaga amesema Jeshi hilo linaendelea kuimarisha na kufanya misako na doria katika maeneo ya barabara kuu ili kuzuia uhalifu na ajali zinazotokana na uzembe na sababu nyingine za kibinadamu.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya katika kuzuia na kudhibiti makosa ya barabarani pamoja na ajali za barabarani kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari 2023 hadi Juni 2023 limefanikiwa kuchukua hatua mbalimbali kwa madereva wa vyombo vya moto hususani mabasi ya abiria.
Kwa kipindi hicho, jumla ya madereva saba (07) wa mabasi ya abiria wa Kampuni ya New Force, Zanuni, Rungwe Express, Super Rojas, Abood Bus Service na Kyela Express walikamatwa na kuchukulia hatua za kufungiwa leseni zao za udereva kwa kipindi cha miezi miwili, mitatu na wengine kufikishwa Mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
Aidha, miongoni mwa makosa ya usalama barabarani yaliyoripotiwa kufanywa na madereva hao ni pamoja na kuendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi, kusababisha ajali ya kifo, kusababisha ajali ya majeruhi na uharibifu wa magari na miundombinu ya barabara.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa madereva kufuata sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya litaendelea kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo madereva kwa kushirikiana na vyuo vya udereva pamoja na kuwakumbusha madereva sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamini Kuzaga amesema Jeshi hilo linaendelea kuimarisha na kufanya misako na doria katika maeneo ya barabara kuu ili kuzuia uhalifu na ajali zinazotokana na uzembe na sababu nyingine za kibinadamu.
Kwa kipindi hicho, jumla ya madereva saba (07) wa mabasi ya abiria wa Kampuni ya New Force, Zanuni, Rungwe Express, Super Rojas, Abood Bus Service na Kyela Express walikamatwa na kuchukulia hatua za kufungiwa leseni zao za udereva kwa kipindi cha miezi miwili, mitatu na wengine kufikishwa Mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
Aidha, miongoni mwa makosa ya usalama barabarani yaliyoripotiwa kufanywa na madereva hao ni pamoja na kuendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi, kusababisha ajali ya kifo, kusababisha ajali ya majeruhi na uharibifu wa magari na miundombinu ya barabara.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa madereva kufuata sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya litaendelea kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo madereva kwa kushirikiana na vyuo vya udereva pamoja na kuwakumbusha madereva sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani.