Mbeya: Dkt. Slaa akataa kuchukuliwa Sample ya Sauti yake

Mbeya: Dkt. Slaa akataa kuchukuliwa Sample ya Sauti yake

View attachment 2719269

Taarifa iliyotolewa na Wakili wa Dr Slaa inasema kwamba , kabla ya kufikishwa Mahakamani leo Polisi walitaka kuchukua Sample ya Sauti ya Dkt Slaa (Haifahamiki walitaka kuifanyia nini) , ambapo Dkt Slaa amekataa jambo hilo kufanyika , kwa vile tayari polisi walishasema wanayo sauti yake ambayo wanadai waliinasa akipanga Uhaini wake , basi ni vema wakiitumia hiyo waliyo nayo ili kufanyia mambo yao .

Vinginevyo Wakili wake amedai kwamba wakitaka sauti ya Dkt Slaa basi wafungue kesi mahakamani kuiomba sauti hiyo , inatajwa kwamba jambo hili ndilo limekwamisha Watuhumiwa hao kufikishwa Mahakamani siku ya leo kutokana na mabishano makali kuhusu Sauti hiyo .

========

Bali wadau wengi wanaona Polisi hawakujipanga na kesi hii wameburuzwa tu na Watawala ili kuwalinda Waarabu wa DP WORLD , na ndio maana wanaokoteza
na kuunga unga sauti ya Dkt Slaa ili kutengeneza ushahidi wa magumashi .

Lakini ni vema tukafahamu kwamba , Hakuna popote pale kwenye dunia hii ambako Shetani aliwahi kumshinda Mungu
eti anapanga kumpindua , jmn Hawa watu mbona wanaokoteza visa na vituko. hamuwezi kumziba mtu mdomo kwa staili hii ya kutengenezewa mikesi ya michongo. Wakumbuke 2025 NI kesho kutwa tu hapo, wapiga Kura wanawachora tu .
 
Mimi nilifuatilia Kesi ya Akina Hanspope 1982 na hasa Wakili Lakha alivyokuwa mjanja wa sheria

Nikafuatilia Kesi ya afande Zombe

Na hata Kesi ya Ugaidi ya Freeman

Sasa muangalie Sabaya alivyojinasua pamoja na CCTV

Mawakili wa mtaani wamewazidi sana wale wa kuajiriwa!
Sabaya alinaswa labda hao wengine
 

Sauti ya kwanza ni ya Slaa
 
eti anapanga kumpindua , jmn Hawa watu mbona wanaokoteza visa na vituko. hamuwezi kumziba mtu mdomo kwa staili hii ya kutengenezewa mikesi ya michongo. Wakumbuke 2025 NI kesho kutwa tu hapo, wapiga Kura wanawachora tu .
Huu muda CCM iliwapasa wawaandae mgambo wa kuiba maboksi ya kura mwaka 2024 uchaguzi wa serikali za mitaa na 2025 uchaguzi mkuu. .Ya nini kugombana na wanaharakati?Ni kama wanakula mishikaki kwa kahawa.Haiji kabisa!
 
Hujaelewa. Slaa sio kwamba anagoma sample zisichukuliwe but anataka zichukuliwe kwa kufuata utaratibu wa kimahakama.
Watakapo mpeleka waiombe mahakama ambayo nayo itauliza sababu ni zipi?
Nakumbuka hata Lissu aliwahi kugomea kuchukuliwa sample ya mkojo na wakakwama
Usiamshe hawa wajinga
 
Unadhibitishaje kuwa huyo ni Slaa? Utata unaanzia hapo! Ushahidi wa sauti mahakamani ni mgumu sana labda wa video.
Steve Nyerere anaweza kutuigizia sauti ya Mwl Nyerere na kila mtu akaamini ndiye, jee unadhani sauti hiyo inaweza kutumika mahakamani na kuita Agizo la Julius juu ya jambo fulani?
Swadakta
 
Chadema mtaacha lini ujinga? Polisi wanataka kukamilisha ushahidi wa sauti sasa Dr.mihogo anaogopa nini kuhojiwa kama yeye hausiki? Hii manaa yake ni kwamba Dr.mihogo anajuwa ni yeye alitamka maneno yale kwahiyo anaogopa ushahidi utakamilika kwajili ya kupeleka mashtaka kwa DPP. Slaa kwisha habari yakee hatunae tena.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
Mjinga sana wewe
 
Polisi wakitaka chochote kwa mtuhumiwa wanakipata, selo kuna mambo ya ajabu mule. Mtuhumiwa hawezi kataa kutoa ushirikiano wanaotaka polisi akiwa mikononi mwao.
Kama huna wakili, ukiwa naye wakikutesa wanavunja sheria
 
Nchi yetu ina vituko sana.

Haya mambo hayahiyaji hasira,wao walipaswa watafute ushahidi wao,kisha wamuite mahakamani
Nchi hii ina vituko kweli, imagine gaidi kbs mpaka anatangazwa kule BBC kwa Ugaidi halafu anaachiwa kimtindo 🤣🤣🤣🤣!! Sometimes ni kulichafua Taifa kwa mamb kama hayo.
 
Wanataka waitumie sauti kutengenezea voice note ya uhaini

Mtu anajirekodi voice note "Mimi Slaa nmeapa ntaipindua nchi " halafu hio sample ya sauti inawekwa juu ili isikike sauti ya Slaa.

wanachotaka ni ile sauti safi kutoka kwenye chumba kama kile cha kwenye studio .

View attachment 2719278
Wanatumia Ai( Artificial intelligence )
tu mzee kwisha kazi
Huko tunapokwendea USHAHIDI wa SAUTI utakuwa hauna nguvu tena
 
Back
Top Bottom