samora10
JF-Expert Member
- Jul 21, 2010
- 7,607
- 4,818
Mbatia hajui lolote kuhusu lini, wapi na nini viongozi wa chadema walikubaliana kuhusu LOWASSA kuhamia kwao. Hana sifa ya kujibu tuhuma za Dr. Slaa. Tundu Lissu ni mwanasheria wa Chadema, lakini kwa kinywa chake anakiri Dr. Slaa hakumshirikisha kuhusu Lowassa kwenda CHADEMA na hata SLAA amesema kuwa alipigiwa simu na Mshenga(Gwajima) wakaenda kwa Mwenyekiti na hapo ndipo hoja za LOWASSA NI ASSET AU LIABILITY ilipoanzia. Kwa mantiki hiyo, Lissu amepoteza sifa ya kumjibu Dr. Slaa. Prof. Safari alijua ujio wa Lowassa kuhamia Chadema, pale Slaa alipompelekea barua ya kujiuzulu, barua ambayo , Safari ameiita KIMEMO TU kana kwamba kuna masharti kwamba barua ya kujiuzulu lazima iwe GAZETI ZIMA. Kwa mantiki hii, Safari hawezi kujua chimbuko la LOWASSA NI ASSET AU LIABILITY. Gwajima ni mbali na kwamba ni MSHENGA TU, pia ni kiongozi wa DINI, viongozi wa dini wanaaswa kuwahamasisha waumini wao umuhimu wa kuwachagua viongozi wanaofaa kwa njia ya amani, kitendo cha yeye kuwa MSHENGA(kuweka kumbukumbu sawa, mshenga hafanyikazi bila malipo) ni kuwadhalilisha waumini wake, kulidhalilisha dhehebu lake na kukidhalilisha chama ambacho ANAKISHENGEA.
Dr. Slaa ajibiwe na MBOWE aliyempeleka Lowassa Chadema.
Shida yako ni Mbowe tu.. haya jisomee hapo chini,
https://www.jamiiforums.com/uchaguz...oa-msimamo-mzito-kuhusu-wanaoasi-mageuzi.html