Dr. Slaa katika hotuba yake pale Serena Hoteli sikusikia kabisaaa, akiongelea Ujio wa Lowassa ndani ya UKAWA, bali ndani ya CHadema. Bado napata tabu kujua sababu ya Mbatia kuwa mtu wa kwanza kujitokeza live kwenye Tv na kupinga yaliyozungumzwa na Dr. Slaa kuhusu ujio wa LOWASSA ndani ya Chadema. Isiwe tabu, labda kuna lililojificha nyuma ya pazia.
Sababu kubwa iliyonifanya niandike Uzi huu ni yale aliyoyasema Mbatia kama moja ya majibu kwa Dr. Slaa
1. Unataka kulipeleka wapi taifa hili, unapowahusisha Maaskofu na kuhongwa pesa? Unataka waumini wao wasiwaamini? Kwanini uwahusishe Maaskofu na siasa nyepesinyepesi za maji taka?
Duh! Mbatia, kwa sababu ni MAASKOFU, wawe mafisadi, wakubali kuhongwa kwa sababu hawatassemwa popote kuepuka kutoaminiwa na waumini wao? Je tuamini kwamba viongozi wengi wa dini ni mafisadi, wala rushwa lakini kwa sababu wana WAUMINI nyuma yao, hakuna wa kuwaumbua kwao?
2. Tuachache na Siasa za uongo, siasa nyepesinyepesi kwa kwa sababu tunapigania kupata KATIBA MPYA KWANZA, na hicho ndicho kipaumbele cha kwanza cha LOWASSA. Mamaaaa, tangu Chadema wamezindua Kampeni zao, ni wapi LOWASSA amesema kipaumbele chake cha kwanza ni kupata KatibaMpya? nakumbuka alisema, ELIMU, ELIMU, ELIMU. Hii Katiba mpya kaisemea wapi, Mbatia naomba andiko, picha, sauti au hata video na hili.
3. Chadema walishamptisha Dr. Slaa kuwa mgombea urais wao na ni yeye(Dr. Slaa) aliyewakataza wasimtangaze kwanza ili kuandaa mbwembwe za kumtangaza. Kwa sababu inaonekana Mbatia unayajua ya Chadema kuliko Chadema wenyewe, tuambie kikao gani kilichobadili mgombea urais wa CHADEMA kutoka Dr. Slaa kwenda Edward Lowassa?