Maziwa ya Azam siyaelewi!

Maziwa ya Azam siyaelewi!

Someni maelezo kwenye box la maziwa mjue mnakunywa nini,
Nilinunua hayo maziwa nikabaini sio kabisa, sasa kuja kusoma maelezo kwenye box ndio nikajiona mjinga kama watanzania wengi hatusomi maelezo kwenye bidhaa tunazotumia.
Sasa hivi hata bure hayo maziwa situmii
 
Nishakunywa kama mara tatu, lakini kila nikinywa najiskia hovyo kama naumwa, vipi jamani haya Maziwa yana ubora kweli au ndio tunalishwa sumu kiaina?
😀 😀 😀 😀 😀 babaaa vp ww ulikuwa una umwa tu na kupoteza ladha milk ya Azamu mbona yako safi tuuu tena matam hayoooooo
 
Yale ni maziwa ya unga, sijui wanayatoa wapi. wajanja sana, wanaongezea maji tu. kwanza ng'ombe wenyewe wako wapi
He he hee! Umenichekesha kwa kweli. Mi mwenyewe nilipoangalia eti maziwa yanazalishwa Zanzibar nikashangaa sana na kuwaza kama Zanzibar kuna ng'ombe wengi kiasi cha kuweza kuzalisha maziwa yote yale...
 
Soma unachoandika Prondo.
Hakuna bidhaa yenye kiwango cha chini ikapasishwa na TBS.
Au huelewi maana Ya Tbs?
Tanzania bureau of standard kazi yake ni kuhakiki UBORA WA BIDHAA na kila bidhaa yenye Nembo ya TBS basi kiwango chake Ni LZM kiwe juu.

Ulimi wako au tumbo lako haliwezi kupima UBORA wa Bidhaa.

Watu wengine ukiwalisha Biriani ya mbuzi wanahara ovyo na wengine km mimi tukila mapera ni balaa.

Jifunze hili kwanza
Ubora unatofautiana....maji ya mlimani ubora wake huwezi kulinganisha na maji ya 'kuishi'
 
Kweli binadamu tunatofautiana, nayapenda sana azam milk ya box la blue, na toka nimeanza kuyatumia hayajawahi kuniletea shida yoyote
 
Nishakunywa kama mara tatu, lakini kila nikinywa najiskia hovyo kama naumwa, vipi jamani haya Maziwa yana ubora kweli au ndio tunalishwa sumu kiaina?


Pole sana Munsolin
Mm niljdai mtanzania kununua bidhaa za nyumban nkaachana na Brookside ila kila nkitumia Yale maziwa ya azam cpati radha ya maziwa,nayasikia kama yana Mafuta mengi sana yaan hayaelewek kabisa hasa kwetu sie wafugaji. Kuna kipnd nilienda Zanzibar pia nkanywa maziwa furan ya ajabu sana cjui maziwa ya Samaki Yale?

Ila kuna siku nmekunywa haya ya azam niljsikia vbaya nkayaacha had kesho stak kuyanunua tenaaaa

Nmehamia Mara Milk na Tanga Fresh na mtind tatzo tanga fresh ukiyachemsha yanaganda apo tuuuu ndo wanakosea
 
Maziwa ni yale ya kenya tu brokxide
Waambie jombaa,kampuni ya Uhuru Kenyatta hiyo,si kampuni aliyorithi,kampuni yake mwenyewe kaikuza miaka nyingi hadi ikawa kampuni kubwa.Maziwa ya brookside matamuuu ng'ombe wao wako kule Njoro,Nakuru.Ng'ombe wanalala kwenye magodoro na wana hadi 'swimming pool' wanachezewa hadi mziki wanatoa maziwa mazuuri tena sana.Si utani aisee!Acheni maneno ya azam hadi mnataka kupiga marufuku brookside huko tz,mtanyeshwa sumu bure!
 
Nishakunywa kama mara tatu, lakini kila nikinywa najiskia hovyo kama naumwa, vipi jamani haya Maziwa yana ubora kweli au ndio tunalishwa sumu kiaina?
Maziwa ya unga yanatokana na maziwa ya ng'ombe yaliyokaushwa ili kupata Dried Skimmed milk powder (DSMP) ama Dried whole milk powder ambayo yanakuwa na kiwango cha juu cha mafuta ( Butter fat ) Miaka ya nyuma hadi 1994 Tanzania ilikuwa inazalisha maziwa ya unga huko Utegi Musoma hali kadhalika Long life milk ( UHT) . Uzalishaji huu hufanyika hasa wakati wa msimu wa maziwa mengi ili kuepusha hasara ya maziwa kuharibika
 
kunyweni asas diaries kama vp ila mbona azam tv hua wanaonyesha jinsi maziwa yao yanavotengenezwa na wanaonyesha ng'ombe kabisa wakikamua?
Ulitaka wakuoneshe na wanavyochanganya unga na maji? Naye aache ujanja ujanja! Kama uko Morogoro kunywa maziwa ya SUA DASP, hayo ni maziwa halisi ya ng'ombe!
 
YA KITIMOTO DIARY MILK MMESHA JARIBU........
 
Tatizo la wabongo ni lilelile miaka nenda miaka rudi,yaani hatupendi kusoma tunanunuanunua vitu bila kusoma written information kwenye bidhaa,Azama milk ametowa maelezo yote kwenye bidhaa yake so read it and if you decide to buy ,you buy and drink at your own ....and never complain.
 
Toka siku yalipoingia sokoni sikuyakubali haya maziwa
 
Last edited:
Hayo Tanga fresh yenyewe si halisi...Umeme.ukikatika nayo yameganda au yanakatika...
Siku zote maziwa halisi hayawezi kukaa zaidi ya siku moja bila kuganda au kukatika kama hujayaweka kwenye friji. Ulichokieleza hapo juu ni uthibitisho kuwa tangafresh ni maziwa halisi. Maziwa ya azam yanakaa muda mrefu tena hata juani na hayaharibiki, nn kinafanya yasiharibike? Bila shaka utakibaliana na mm kuwa wameweka preservatives, kama ndivyo, je unafahamu madhara ya preservatives? Kifupi maziwa haya yapo mbali sana na ubora ambao Tangafresh na Asas wanao.
Kwakweli ulimwengu ujao ni ulimwengu wa maradhi yatakayotokana na ulaji wetu, Time will tell.
 
Hayo Tanga fresh yenyewe si halisi...Umeme.ukikatika nayo yameganda au yanakatika...
Maziwa halisi huganda yanapokuwa exposed kwenye room temperature na sio kwa kutegemea umeme.

Ila kwa wafugaji kama mimi hakuna maziwa processed ambayo ni mazuri kushinda yale niliyogandishia kwenye ndoo chumbani bila kutoa natural mik cream, au niliyotoka kukamua zizini.
 
Pole sana Munsolin
Mm niljdai mtanzania kununua bidhaa za nyumban nkaachana na Brookside ila kila nkitumia Yale maziwa ya azam cpati radha ya maziwa,nayasikia kama yana Mafuta mengi sana yaan hayaelewek kabisa hasa kwetu sie wafugaji. Kuna kipnd nilienda Zanzibar pia nkanywa maziwa furan ya ajabu sana cjui maziwa ya Samaki Yale?

Ila kuna siku nmekunywa haya ya azam niljsikia vbaya nkayaacha had kesho stak kuyanunua tenaaaa

Nmehamia Mara Milk na Tanga Fresh na mtind tatzo tanga fresh ukiyachemsha yanaganda apo tuuuu ndo wanakosea
Maziwa ya tanga hayahitaji kuchemsha. Yale yamefanyiwa kitu inaitwa" pesturaization" ukichemsha protein yote inakuwa denatured. Ila hongera kwa kuona kasoro kwenye kitu ya azam
 
Tatizo wabongo mmeanza tabia ya kufakamia kila kitu ambacho ni packed huku mkidharau kutumia vyakula halisi.
Hali hii inasababisha magonjwa ya kansa na shinikizo la damu kuzid kuongezeka hapa Tanzania
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom