Hizi habari umezipata wapi ? Kujengea ni dhambi na ukifanya hivyo ni madhambi kinachotakiwa kufanywa ni kuweka alama ambayo ndugu au jamaa akienda muda wowote anajua ndugu yao alizikwa wapi.Kujengea sio DHAMBI, ila inashauriwa yasijengewe ili kuweza kupata eneo la kuzika watu wengine.
Usipoteshe watu na usitengeze nafasi ya kuwaona waislam wenzako wamekosea bali toa elimu watu waelewe.
Na nukuu :
Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kaburi kutiwa chokaa (liwe imara), kuketiwa juu yake na kujengewa. [Muslim]
Kutokana na Hadithi hii, swahaba Ali bin Abi Twalib kipindi cha utawala alipata habari kuna sehemu watu wanajengea makaburi, akatuma mtu au watu na kuwaamuru wakikuta kaburi lolote limeinuka kwa kujengewa basi wavunje hichi kilichojengwa.
Sasa unaposema inafaa kujengewa unatumia mafundisho ya nani katika Uislamu ?