Donnie Charlie
JF-Expert Member
- Sep 16, 2009
- 15,167
- 16,254
DAR ES SALAAM: Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini (TCAA) imesema hakuna utoroshwaji wa wanyama pori kwenda Falme za Kiarabu kama taarifa za upotoshwaji zinavyodai.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari leo kuwa kama Mamlaka inayohusika na kutoa vibali kwa ndege za mizigo na abiria zinazoingia katika anga la Tanzania kuwa hakuna ndege ya mizigo iliyoingia nchini kwa kazi hiyo.“
Taarifa za utoroshaji wanyama pori kupitia ndege kubwa ya mizgo kutoka Loliondo kwenda nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) hazina ukweli wowote,” imesema taarifa hiyo. “Ndege ya mizigo ya Falme za Kiarabu ilifanya safari yake ya mwisho Julai 19, 2023 kinyume na taarifa kuwa kulikuwa na ndege hiyo Agosti 26, 2023.”
Hamza amesema Mamlaka ina mfumo wa kufuatilia ndege kwa wakati halisi na ndege zote za kimataifa huingia na kutoka kupitia viwanja vilivyoidhinishwa kuruhusu ndege kutoka nje ya nchi kutua na kuondoka kwenda nje ya nchi.
Viwanja vinavyohusika ni pamoja na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Kia, Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume (AAKIA) na vingine vilivyoidhinishwa.Imeandaliwa na Mwandishi Wetu
Habarileo
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari leo kuwa kama Mamlaka inayohusika na kutoa vibali kwa ndege za mizigo na abiria zinazoingia katika anga la Tanzania kuwa hakuna ndege ya mizigo iliyoingia nchini kwa kazi hiyo.“
Taarifa za utoroshaji wanyama pori kupitia ndege kubwa ya mizgo kutoka Loliondo kwenda nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) hazina ukweli wowote,” imesema taarifa hiyo. “Ndege ya mizigo ya Falme za Kiarabu ilifanya safari yake ya mwisho Julai 19, 2023 kinyume na taarifa kuwa kulikuwa na ndege hiyo Agosti 26, 2023.”
Hamza amesema Mamlaka ina mfumo wa kufuatilia ndege kwa wakati halisi na ndege zote za kimataifa huingia na kutoka kupitia viwanja vilivyoidhinishwa kuruhusu ndege kutoka nje ya nchi kutua na kuondoka kwenda nje ya nchi.
Viwanja vinavyohusika ni pamoja na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Kia, Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume (AAKIA) na vingine vilivyoidhinishwa.Imeandaliwa na Mwandishi Wetu
Habarileo