Mazingaombwe (Jugglery) ni Sayansi au Uchawi?

Mi niliona nyingi sana... Moja jamaa alitafuna nyembe nyingi na kuzimeza.. Baadaye akatoa mdomoni roll ndefu ya karatasi,ndefu sana!

Jamaa aliwahi kuwasha moto kwenye kichwa cha mtu na yakapikwa maandazi matatu..!
 
mi nakumbuka tulikua na rafiki yetu mmoja home yeye alikua anajua haya mambo, alikua anatuambia ila tulilkua hatumuamini, basi siku 1 akatuweka duara, halafu akachukua makaratasi na kuyachana madodo madogo akampa kila mmoja wete atafune, ameze halafu anywe na maji gilasi moja moja, tukafanya km alivotuagiza. Basi akasema maneneo yake ya puche na seto, baada ya muda alitoa sindano za kushonea mdomoni mwake kibaoo zaidi ya mia tena mpya mpya.
Akatupa na tulizitumia mpk. Siku nyengine alichukua ya wifi yangu akaitia ndani ya mkoba wa karatasi akampa afungue kufungua akatoka jongoo.
Wana uchawi wanafanya
 
Lakini nilisikia kuwa mtu akiingia na mkaa au ndimu kwenye chumba cha maonyesho wanamsitukia na kumfukuza!
PIa ikumbukwe kuwa walikuwa enzi hizo wakija na sanduku la mbao, ambapo kwa wakati huo lilikuwa likionekana la fasheni ya kawaida tu!

Umenikumbusha mbali mkuu! Hii ilikuwa miaka ya 1980; alikuja mwanamazingaombwe mmoja na sanduku la mbao, akiitwa Profesa Eyesso. Kabla ya mchezo kuanza, alipiga mkwara kuwa mwanafunzi yeyote aliyeingia na ndimu ukumbini atoke nje la sivyo atampofua macho. Nakumbuka vijana wawili walitoka nje kwa aibu kubwa.
 
Ahahhahahaah wengine walikua waongo sana ! niliwahi kuhusika na mchezo mchafu alikuja Mwanamazingaombwe simkumbuki jina , akaomba vijana watatu wajanja , nami nikala shavu ! kumbe anaenda kutufundisha uwongo wake.

Mimi alinifundisha akipuliza dawa yake nijidai sioni amenipofusha kwa dawa zake !

Mwisho wa siku nikapewa Tsh. 20
 
Ahahhahahaah wengine walikua waongo sana ! niliwahi kuhusika na mchezo mchafu alikuja Mwanamazingaombwe simkumbuki jina , akaomba vijana watatu wajanja , nami nikala shavu ! kumbe anaenda kutufundisha uwongo wake.

Mimi alinifundisha akipuliza dawa yake nijidai sioni amenipofusha kwa dawa zake !

Mwisho wa siku nikapewa Tsh. 20


tehteh...hope ilikuwa ni 1980's ....manake hiyo 20sh ili ufiche siri si mchezo!
 
Umenikumbusha mbali mkuu! Hii ilikuwa miaka ya 1980; alikuja mwanamazingaombwe mmoja na sanduku la mbao, akiitwa Profesa Eyesso. Kabla ya mchezo kuanza, alipiga mkwara kuwa mwanafunzi yeyote aliyeingia na ndimu ukumbini atoke nje la sivyo atampofua macho. Nakumbuka vijana wawili walitoka nje kwa aibu kubwa.



Hivi ni kweli ndimu ilikuwa na uwezo wa kuzuia mazingaombwe kutokea?
 
nakumbuka kuna mmoja aliwahi kuja shuleni akawa kama kakatwa na panga afu likatokezea upande wa pili na damu zinamvujia. bdae alikwenda nyuma ya pazia ile kurudi hakuwa na jeraha hata kidgo. lakini ukimwangalia unaona upande wa mpini uko kulia na makali yapo kushoto. duh,yan mpaka leo sijawahi kuelewa huwa wanatumia mbinu gani?
 
mwaka jana kwenye East Africa trade fair kulikuwa na mazingaombwe ya kichwa kisicho na kiwiliwili lakini kinaongea. kilikuwa kimewekwa mezani. me nilikwenda kushuhudia lakin ile naingia tu nikaona kama kimenipiga kope kikaogopa nikatoka. dah cjui ni ufundi gani jamani?
 
Hawa jamaa sijui huwa wanatumia na ushirikina!

mwaka jana kwenye East Africa trade fair kulikuwa na mazingaombwe ya kichwa kisicho na kiwiliwili lakini kinaongea. kilikuwa kimewekwa mezani. me nilikwenda kushuhudia lakin ile naingia tu nikaona kama kimenipiga kope kikaogopa nikatoka. dah cjui ni ufundi gani jamani?
 
kweli mazingaombwe yalikuwa na raha zake. Wadada walikuwa wanadondosha hela kwa nyuma
 
Hivi wale ma POWER wa Mazingaombwe wa zamani walikuwa wanatembelea mashule wako wapi siku hizi?
Namkumbuka Power Mabula
 
Dah!umenikumbusha mbali sana,miaka ile ya tisini akija mtu wa mazingaombwe masomo yanasimama mnaingia kwa kulipa kiingilio kuanzia sh moja mpaka sh.tano.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom