Mazda CX 5 inanifilisi!

Mazda CX 5 inanifilisi!

Mkuu, jamaa kwenye uzi wake hajasema kuwa gari lina shida ila amesema linamfilisi kwa kuwa vipuri vyake na service ni vya gharama sana. Mfano hiyo service, ni kama amewatahadharisha wengine wataotaka kununua CX5, wajue wanachokiingia
Nimemuelewa hoja yangu ni kwamba kwanini aseme gari inashida kwasababu spare ni gharama? Kwanini zile taa walimtengenezea ili akazivunje au azitumie barabarani kuangaza mwanga wa kuona akiendesha gari?
 
Nimemuelewa hoja yangu ni kwamba kwanini aseme gari inashida kwasababu spare ni gharama? Kwanini zile taa walimtengenezea ili akazivunje au azitumie barabarani kuangaza mwanga wa kuona akiendesha gari?
Mkuu kwenye bandiko lake hakuna mahali amesema gari ina shida. Kuhusu ughali wa spea, chukulia kuwa taa ingevunjika kwa kugongwa jiwe lililoruka baada ya kukanyagwa na gari lingine - bado bei ingekua ni Tshs. 1.5m ndio anayoisema sasa kuwa ni ghali sana.

Ishu ya service nayo ameisema hapo kuwa bila laki 7 hujafanya service,

Lawama hajazielekeza kwa hali ya uimara gari, bali kwa gharama za maintanance, zipo juu ya kiwango chake au anaona kuwa haziendani na hadhi ya gari.
 
Chombo chochote cha moto huwaga akuna ugumu wa kuinunua hata kama ni pikipiki. Linapokuja sual la service ndio watu huchanganyikiwa.

Nmeletewa hapa quotation nataka badili drive belt, nmesema ngoja nimalize chai ndio nijibu text yake, vingine na hii asira plus njaa naweza mtukana fundi
😂😂😂😂😂😂😂😂 Jibu tu kama mmiliki wa chombo.
 
Ukiweza uza mapema sana itakufilisiiii.....engine itakufa soon.....nasikia ya petrolnzuri zaidi kulikp diesel....zinachemsha anytime
 
Ni vile wafanyabiashara wameamua kutuumiza. Bei ya taa ya mazda nikiagiza mpaka kunifikia haizidi Laki nne kwa zote mbili, ikijumuisha na usafiri

It will only take two weeks mzigo kunifikia

Screenshot_20250502-145021.png
 
Unahisi hizo zilizokuwa madukani zinatokea wapi
Sihisi kwa sababu parts ndio sehemu yangu zipo za China na Nchi zingine ambazo nao wanatengeneza kwa ubora zaidi na zilizotumika pia.
 
Njoo nipe hio nikupe rumion yangu vipuri sio ghali
 
ni kweli gari kimeo sana hiyo. pole sana kiongozi kwa usumbufu.

ukitaka kuiondoa nicheki aisee tayari 6.5m iko apa mezani kiongozi.

=mapigo na mwendo=
 
Back
Top Bottom