Mawaziri wanane watakiwa kung'oka...!

Mawaziri wanane watakiwa kung'oka...!

[h=6]BREAKING NEWS: Mawaziri NANE waliojiuzulu ni; Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),George Mkuchika, Waziri wa Kilimo Jumanne Maghembe na Afya, Dk. Haji Mponda.[/h]
 
kwa muujibu wa Joseph selasin mbunge wa rombo(CHADEMA) mawaziri chami,nundu,mkulo na mponda wameeandika barua jioni ya ijumaa ya tarehe 20 kuomba kujiuzuru
 
Kutokana na kuchachamaa kwa hoja kali ya uwajibishwaji ikiongozwa na Mh. Zitto yaani mawaziri wahusika hawana njia nyingine bora kujiulu. Pia natamani wafikishwe kwenye vyombo vya dola.
 
Tatizo ni bigger than individuals kwa kweli..... A system overhaul seems the way to go ladies & gentlemen
 
Tufike mahali Nguvu ya uma tujue hawa ccm wanajuana kwani, sokoine alipata wapi nguvu au sheria ya kuwakata wahujumu uchumi? kwani wale wanatofauti gani na hawa watendaji wa kikwete? kama filisi mpaka kijiko bila kesi yoyote ushahidi ni huo kutowajibika unatosha

tuwaige wenzentu wachina boss wa kiteng akikosea kwa wachina Adhabu yake ni kisu tu
tukifanya hivyo wote watakuwa waoga wewe fikria leo hii Mdaktari wanaacha tiba wanaenda kweny siasa
Ma profesor wanakimbilia siasa ni masilahi huko. WANYONGWE HAWA IWE FUNDISHO WANAJUA KILA KITU.
 
[h=3]Chanzo: Mpayukaji blog[/h]


[h=3][/h][h=3]
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
thumbnail.aspx
[/h]Habari tulizopokea toka kwa ripota wetu toka Dodoma ni kwamba Tanzania imeanza kukomaa ambapo mawaziri nane wameachia ngazi baada ya wabunge kuwatolea uvivu. Ingawa habari hii hajathibitika toka serikalini, wanaotajwa ni ;na Uchukuzi Omar Nundu,Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja , Dk. Haji Mponda (Afya), Jumanne Maghembe ( Kilimo Chakula na Ushurika) , George Mkuchika (Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Mustafa Mkulo (Fedha) na Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii)
 
Hivi wakishajiuzulu hawa mtaridhika? au mtasema "angalau tumeanza mahali" na hivyo kuonesha kuwa mmesahau kabisayaliyiotokea 2008 au ya kina Kiula miaka kadhaa nyuma?

Kaka,

Hili ndilo tatizo letu Watanzania la kutoa hazina zetu zote kubadilishana na peremende...

Nashangaa kwa nini hawataki kushughulisha akili zao ili wamalizane na tatizo lenyewe??

Ndani ya CCM hakuna msafi (By Sophia Simba), kwa hiyo hakuna baraza lolote linaweza kuundwa likafanya kazi...

Kama thinking ndiyo hii, this time next year, tutakuwa tujadili kuvunjwa tena kwa baraza la mawaziri
 
Hii ni nguvu ya umma. CCM wamekiona cha moto. Wanadhani Zitto yuko peke yake au CHADEMA wako pekee yao?? Wamechemsha, Zitto alitoa hoja ya watanzania na wala haikuwa hoja yao. Tembelea Twitter, facebook, jamiiforums, simu za watanzania, vijiweni n.k., hoja ilikuwa ni kushinikiza wabunge wao kukubali kuweka saini. Sasa CCM itaponaje????

Watanzania tukiamua tunaweza lolote. Tena nimegundua Serikali yetu inaogopa sana, hata fujo hazistahili tena. Ni maneno tu na hoja. Big up Zitto, Big up JF, Facebook, Tanzanians...
 
Watanzania tuweke nani bado anatakiwa kujiuzulu pengine mpaka jumatatu wakisoma watakuwa wameongezeka humu kujiuzulu

Hawa gasia na watumishi wake hewa. Selina kombani na katiba yake feki
 
Tufike mahali Nguvu ya uma tujue hawa ccm wanajuana kwani, sokoine alipata wapi nguvu au sheria ya kuwakata wahujumu uchumi? kwani wale wanatofauti gani na hawa watendaji wa kikwete? kama filisi mpaka kijiko bila kesi yoyote ushahidi ni huo kutowajibika unatosha

tuwaige wenzentu wachina boss wa kiteng akikosea kwa wachina Adhabu yake ni kisu tu
tukifanya hivyo wote watakuwa waoga wewe fikria leo hii Mdaktari wanaacha tiba wanaenda kweny siasa
Ma profesor wanakimbilia siasa ni masilahi huko. WANYONGWE HAWA IWE FUNDISHO WANAJUA KILA KITU.


Hayo unayosema yakifanywa na serikali yoyote ya CCM katika zama hizi basi nidai chochote hata kama dhamani yake itakaribia kuwa sawa na pumzi yangu!!
 
Usisahau kusali na kumshukuru kwa mambo makuu kama haya kutokea nchini na kuomba mengi zaidi ya haya yandelee kutokea na zaid watu wafikshwe mbele ya sheria
mungu awalinde muamke salama
 
Dogo makamba anazidi kuropoka kwenye twitter yake tu....

Sitting with someone in a room & telling him to his face that he has messed & must go for the good of the country.
#Courage. I can sleep now
 
Yaani madudu yanaiba tu nchi hii, kila ka-senti kanakokatiza wanakwapua. Yani utakuta wizara moja imetafuna bilioni 5 au trilioni moja wakati watoto wa masikini vyuoni ati wanaandamana kudai milioni 500 tu na hizo zinafanywa wapigwe mabomu na kufukuzwa chuo, ati watukutu na wakorofi na watovu wa nidhamu. Mukandala na ma-vc wenzako mnawaona wezi na watukutu! Mnaona namna mtu mmoja anavyoweza kutafuna bilioni 2 huku nyie mnatoka jasho kufukuza vijana masikini wanaodai kulipiwa na serikali ada yenye thamani ya shilingi milioni 500? Nchi hii kama ikiendelea hivi nasisitiza pana siku maskini watakuwa mitaani na majeshi hayatatosha...tucheze na masikini....

Tatizo kubwa zaidi katika nchi hii ni kuwa ili upate uwaziri lazima uwe rafiki ya rais, mwanamtandao(ulimsaidia rais kuingia madarakani),ndugu ya rais na vinginevyo. Majuzi nilikuwa tandahimba, pale pana Mkuu wa wilaya anaitwa HUSNA MWILIMA, huyu zamani alikuwa mpambaji wa saloon wa mama salma kikwete.... baadaye kikwete akamuchukua na kumpa kaposti ka kuongoza CCM wilaya(sijui walikuwa na deal gani)...baadaye kampa ukuu wa wilaya... a stupid leadership ever.....nchi inaendeshwa kihunihuni tu... sasa yule mama anafanya madudu tu pale tandahimba, wananchi wameandamana kudai pesa zao za malipo ya korosho ambayo wamekopwa na hawajalipwa karibu mwaka unatimia. Yan mwilima anawajibu wananchi utumbo, matusi na ujinga mtupu huku anamshinikiza OCD awapige mabomu. Nikasema this mum is crazy...we have crazy leaders in this country, lazima tushikamane na tuchukue hatua za kuokoa taifa letu.... hili siyo taifa la CCM, ni la watanzania.
"julius mtatiro"
 
Hivi wakishajiuzulu hawa mtaridhika? au mtasema "angalau tumeanza mahali" na hivyo kuonesha kuwa mmesahau kabisayaliyiotokea 2008 au ya kina Kiula miaka kadhaa nyuma?

asilimia 0.0000 bora waondoke, huyu kikwete mkitaka kumtoa atatumia udini atasema kwa vile yeye ni muislam. Wananchi wenyewe ndio hawajionei huruma kuiipigia ccm kura kila siku
 
sio wafikishwe kwenye vyombo vya dola wafilisiwe ngeleja mwaka 2005 alikuwa anakaa kimara
mabondeni kule kilungule leo hii hata kwenda kuangalia gofu lake haendi


wataifishwe kila kitu iwe fundisho kwa wengine




wa
 
Wanachezea Tanzania! Ya leo siyo ya jana,watu wameamka hivi sasa;
Ningemshauri Bwana mdogo Jakaya Kikwete,avunje baraza lote la mawaziri na kuunda baraza dogo la kumalizia kipindi cha MPITO cha uongozi wa C C M madarakani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom