Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,866
- 4,253
Mola anasikia kilio cha wabongo sasa. Enyi ndugu zetu wabunge endeleeni kukaza buti. Na huyo Pinda kwa nini asijiiweke kwenye hiyo list?
Phillemon Mikael, nami nahisi jamaa watakuwa hawafanya analysis vema katika hili!
Kamanda mi sijalala nilikuwa nasubiria hii habari hebu weka nyama kidogo eleza kwa kina kilichojiri dodoma kwenye cocus ya ccm
mahakama ya umma ndiyo eventually itaamua thru ballot papersHuu ni upuuzi hii inaonyesha serikali jinsi gani ilivyojaa upendeleo kwenye matumbo yao naomba niweke wazi laiti raisi kikwete angesikia mawazo ya watu na hao wabunge mwaka jana mwaka huu tusingekuwa na wizi waa kiasi kwa hiyo soln sio tu hao waliojizulu pamoja na huyu bwana na naamini hata anaoenda kuwachagua nao wanakauja kula na kuwaumiza kichwa tena mnaomba wajiuzulu why????na baada ya kujiuzulu what next??
FULL LIST
Mkulo
Mponda
Nkya
Magembe
Nundu
Mkuchika
Chami
Maige
Ngeleja
KWA HISANI YA https://www.jamiiforums.com/members/ghost-ryder.html
Wanamjua mkuu wa kaya anaweza kuwageuzia kibao, haeleweki huyu na pasi zake za kusakizia.
Pamoja na hao mawaziri kuondoka hoja ha kutokuwa na imani na Waziri Mkuu iwepo pale pale.
Sijawahi kuona Waziri Mkuu wa aina hii. Alitakiwa yeye aweza wa kwanza kuondoka.
Waziri Mkuu amepewa madaraka lakini anashindwa kufanya maamuzi magumu. Hatufai huyu.
CCM inajimaliza kwa kila upenyo inaopata, na kuongeza maadui kila ikiamka usingizini.
Jk akirudi atapinga kujiuzulu kwao kwenye kikao cha wazee wa Dar es salaam na kuwalaani walioanzisha chokochoko. Bonge la presid! Saa hizi anapanga ratiba ya mazishi kule Malawi na anaandaa b/fast na Maximo
Infact huu ndio mzizi wenyewe. Sidhani kama JK anaweza kuapisha mawaziri safi, wasio na scandal yeyote kutokana na sababu zifuatazo 1)kupata uwaziri lazima uwe mshkaji wa Kikwete au mtu wa ndio mzee 2) Kikwete anapenda watu ambao hawajamzidi kumfikiri (not very smart) 3) wanachama wa CCM walio safi/wazalendo wengi wao hawajapewa nafasi zozote za uongozi, so mpaka kuja kutambulika una-exist ni kazi saana etc. Kwa uwezo wakufikiri wa rais wetu lazima atafanya recycling tu. Akienda mbali sana atachukua wale wa awamu zilizopita akina Meghji.Lakini bado naamini kuwajibika kwa mawaziri ni hatua nzuri whether wamekuwa-pressured or not.
Nadhani analysis yao ili-focus zaidi kwenye hii report ya CAG, lakini ukweli ni kwamba Baraza la Mawaziri la JK limejaa vimeo, wana kashfa za kufa mtu na wengi wao ni mzigo
Kweli Tanzania raha sana. Unaiba mali ya umma unapewa ushauri u-step down au ujipime. Tena kizuri zaidi hulazimishwi kurudisha ulichochukua so una options nyingi tu. Argh!:A S angry: