Mavazi ya Mchungaji Tony Kapola yachunguzwe

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
22,325
19,109
Nilipohoji kuhusu uvaaji wa mchungaji Tony Kapola kuna watu hususan wanawake walinivaa kwa ukali kwamba nina wivu niwaachie mchungaji wao, kwamba uvaaji wake ni wa kawaida, kwamba uvaaji wa kisasa kwa Watumishi wa Mungu sio tatizo. Binafsi niwaambie UTUMISHI WA MUNGU ni mgumu na unahitaji usiriaz kuliko wengi mnavyofikiri, Yohana alijinyima hadi kuvaa magunia na kula nzige jangwani mnafikiri utumishi ni mwepesi?
1716400833543.png

Tunarahisisha mno utumishi wa Mungu miaka hii ndio maana wahubiri nao wanahubiri injili mpya nyepesi ya kisasa iliyopakwa maneno matamu ya miujiza, utajiri na mafanikio, hawaihubiri ile injili pure ya Ufalme wa Mungu, ile ya kukemea dhambi kwa ukali wake.

Ndio maana tunaskia Watumishi wengine wanasema hata dukani sigara weka biashara sio ibada, wengine wanasema ndoa sikuiz sio mwili mmoja, wengine wameenda mbali na kusema pesa za majini sio haramu. Utumishi wa Mungu umeonekana ni simple tu hadi kina Irene Uwoya wanataka kufungua makanisa sasa huku bado miili imejaa tattoo.

Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi anahitaji Watumishi VIELELEZO KWAO WAAMINIO. Katika uvaaji, unenaji, utendaji na mwenendo mzima wa maisha kwa ujumla

Kwa Mungu hakuna usasa, sheria zake ni zile zile WAACHE DHAMBI NA KUNIABUBU

Mahubiri ya utajiri, pesa, miujiza na mahusiano yasitutoe kwenye mstari, Mungu sio mrahisi kama tunavyoaminishwa na Watumishi hawa wa kisasa

Tunapaswa kusali kwa imani, kutubu, kufunga na kuomba, Tunapaswa kumuogopa Mungu na kumuabudu kweli. Tunapaswa kuyaheshimu madhabahu yake. Tunapaswa kutambua Mungu ni mtakatifu hadhihakiwi wala kuchanganywa na aina yoyote ya uchafu

Nawasilisha.
 
Nilipohoji kuhusu uvaaji wa mchungaji Tony Kapola kuna watu hususan wanawake walinivaa kwa ukali kwamba nina wivu niwaachie mchungaji wao, kwamba uvaaji wake ni wa kawaida, kwamba uvaaji wa kisasa kwa Watumishi wa Mungu sio tatizo. Binafsi niwaambie UTUMISHI WA MUNGU ni mgumu na unahitaji usiriaz kuliko wengi mnavyofikiri, Yohana alijinyima hadi kuvaa magunia na kula nzige jangwani mnafikiri utumishi ni mwepesi?

Tunarahisisha mno utumishi wa Mungu miaka hii ndio maana wahubiri nao wanahubiri injili mpya nyepesi ya kisasa iliyopakwa maneno matamu ya miujiza, utajiri na mafanikio, hawaihubiri ile injili pure ya Ufalme wa Mungu, ile ya kukemea dhambi kwa ukali wake.

Ndio maana tunaskia Watumishi wengine wanasema hata dukani sigara weka biashara sio ibada, wengine wanasema ndoa sikuiz sio mwili mmoja, wengine wameenda mbali na kusema pesa za majini sio haramu. Utumishi wa Mungu umeonekana ni simple tu hadi kina Irene Uwoya wanataka kufungua makanisa sasa huku bado miili imejaa tattoo.

Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi anahitaji Watumishi VIELELEZO KWAO WAAMINIO. Katika uvaaji, unenaji, utendaji na mwenendo mzima wa maisha kwa ujumla

Kwa Mungu hakuna usasa, sheria zake ni zile zile WAACHE DHAMBI NA KUNIABUBU

Mahubiri ya utajiri, pesa, miujiza na mahusiano yasitutoe kwenye mstari, Mungu sio mrahisi kama tunavyoaminishwa na Watumishi hawa wa kisasa

Tunapaswa kusali kwa imani, kutubu, kufunga na kuomba, Tunapaswa kumuogopa Mungu na kumuabudu kweli. Tunapaswa kuyaheshimu madhabahu yake. Tunapaswa kutambua Mungu ni mtakatifu hadhihakiwi wala kuchanganywa na aina yoyote ya uchafu

Nawasilisha.
The bible says, “Do not look at his appearance or at his physical stature, because I have refused him. For the LORD does not see as man sees; for man looks at the outward appearance, but the LORD looks at the heart.” It's the heart issue that is important, not the clothes.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom