Mauaji yaliyojaa utata

Mauaji yaliyojaa utata

NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Ishirini.
“Yupo wapi?”
“Nawaona vijana wawili wakiwa wamesimama, mmoja yupo ndani ya kibanda cha simu na mwingine yupo nje, Benjamin ni huyu aliyekuwa ndani, aliyekuwa nje simfahamu,” alisema kijana huyo aliyejiita Genius.
Alichokisema Bwana Swan ni kuunganishwa kwa kompyuta ile katika televisheni kubwa iliyokuwa ndani ya chumba hicho huku akimtaka kila ofisa wa FBI aliyekuwa humo ndani aangalie kile kilichokuwa kikiendelea.
Sehemu iliyoandikwa Location ikiwa na maana ya eneo ilionyesha kwamba ilikuwa ni Macberth 25W, sehemu ambayo ilikusanya watu wenye maisha ya kati katika Jiji la Boston, huko ndipo ambapo huyo Benjamin alipokuwa.
Kumuona tu hawakuridhika, waliamini kwamba wangeweza kutorokwa kwani huyo Benjamin hakuwa mtu wa kawaida hata kidogo. Walichokitaka ni kumfahamu mtu ambaye alikuwa naye, alikuwa nani na alikuwa akiishi wapi.
Hiyo wala haikuwa kazi kubwa, alichokifanya Genius ni kuivuta sura ya Harry, akaruhusu sura kadhaa zianze kupita katika kompyuta yake huku ikiitafuta sura ya mwanaume huyo aliyekuwa pamoja na Benjamin.
Ilikuwa kazi kubwa, kila mtu aliyekuwa ndani ya jengo hilo alikuwa kimya, Bwana Swan alibaki akiwa amesimama, mkono wake mmoja ulikuwa mfuko na mwingine aliupeleka katika shavu lake, alikuwa akifuatilia kwa ukaribu sana.
Zaidi ya sura milioni mbili zilipita kwa kasi kubwa mno, ndani ya dakika ishirini, kompyuta ikasimama katika sura moja na kujiandika 100 MATCH kwamba sura ya mtu huyo ilifanana na huyu aliyekuwa ametafutwa.
“Ni nani huyo?” aliuliza Bwana Swan, jamaa mwingine akachukua kalamu na karatasi.
“Anaitwa Harry Hoff, kijana mwenye asili ya Ujerumani, anaishi jijini Boston, nyuma namba 278 katika Mtaa wa Vivien View Barabara ya St. Peters, anasoma katika Chuo cha Kikuu cha Harvard,” alisema Genius, maelezo ya wananchi wote wa Marekani, data zao zilikuwa zimechukuliwa kutokana na vitambulisho wa taifa walivyokuwa wamepewa.
“Safi sana...ninahitaji maofisa kumi waende huko anapoishi Harry. Hakuna kuua, mnachotakiwa ni kuwapata wote wakiwa hai,” alisema Bwana Swan na maofisa wote kuitikia na hivyo kuanza kwenda huko.
****
Vivian hakuwa na raha, moyo wake ulikuwa na majonzi tele, hakuamini kile kilichotokea kwamba mpenzi wake alikuwa akitafutwa kila kona huku sababu kubwa ikiwa ni kufanya mauaji.
Alijua kwamba hakuwa muuaji bali kulikuwa na mtu ambaye alifanya mauaji, hakumfahamu na hivyo ndivyo alivyowaeleza maofisa wa FBI lakini hakukuwa na mtu aliyemuelewa.
Aliruhusiwa kwenda nyumbani, hakukukarika, kila alipokaa, alimkumbuka mpenzi wake tu. Maofisa wa FBI hawakutaka kumuacha, walihakikisha wanamfuatilia kila hatua.
Nje ya nyumba hiyo kulikuwa na gari lao, ndani ya gari hilo kulikuwa na kompyuta nyingi pamoja na kamera zilizokuwa na uwezo wa kupiga picha na kuona kile kilichokuwa kikiendelea ndani.
Mbali na hivyo, waliendelea kufuatilia mpaka mawasiliano ya simu zake, kuanzia ile ya mezani mpaka ya mkononi kwani waliamini kwamba msichana huyo alikuwa na nafasi ya kuwasiliana na mpenzi wake ambaye alikuwa akitafutwa kwa udi na uvumba kipindi hicho.
“Nini kinaendelea?” aliuliza Bwana Swan ambaye aliwagawa vijana wake sehemu mbalimbali.
“Bado tunaendelea kufuatilia, tunamuwekea ulinzi wa kutosha huyu msichana wake,” alijibu ofisa mmoja.
“Simu zake?”
“Tumeziwekea ulinzi pia.”
“Sawa.”
****
Maofisa wa FBI wakaelekea nyumbani kwa Harry, walikwenda na gari lao, ilikuwa asubuhi sana muda ambao waliamini kwamba hata watu hao hawakuwa wameamka, walitaka kuwavamia na kisha kumchukua mtu wao ambaye aliwatesa sana huku usiku uliopita tu akiwa amefanya mauaji katika hoteli moja huko Los Angeles.
Walifika katika nyumba hiyo huku wakiwa na bunduki zao mikononi mwao, waliamini kwamba wangeweza kumpata kwani kwa jinsi walivyoona siku iliyopita, wawili hao wangeendelea kuwa ndani ya hiyo nyumba na ilionyesha kwamba kwa kipindi kirefu Benjamin alikuwa mahali hapo ila tu hawakuwa wakijua hilo.
Walipofika nje ya nyumba hiyo, kitu cha kwanza kabisa walichokifanya ni kuizunguka nyumba hiyo na ndipo mmoja wao akaanza kuugonga mlango na kutaka kufunguliwa.
Nyumba ilikuwa kimya, japokuwa alipiga kelele na kusema “FBI, FBI” lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyefungua mlango. Hawakutaka kuendelea kubaki hapo ndani, walikuwa na hofu kwamba inawezekana Benjamin angekimbia hivyo walichokifanya ni kuingia ndani ya nyumba hiyo kwa kuuvunja mlango.
Bunduki zilikuwa mikononi mwao, walioingia hawakuwa wao peke yao bali kulikuwa na askari wa SWAT ambao kazi yao ilikuwa ni kuvamia sehemu zilizokuwa na hatari, yaani kule ambapo kulikuwa na watu waliokuwa na silaha nzito, walitumika hao kwa ajili ya kuwalegeza kwanza.
Ndani, hakukuwa na mtu, walijaribu kuingia humu na kule, walitembea huku na kule lakini hawakukuta mtu yeyote. Mwisho kabisa wakaamua kukifuata chumba kimoja, kilikuwa chumba cha Harry, walipokifikia, wakaingia ndani, hawakumuona Benjamin, mtu pekee waliyemuona humo alikuwa Harry.
“You are under arrest....” (Upo chini ya ulinzi...) alisema ofisa mmoja huku wote kwa pamoja wakimnyooshea bunduki Harry ambaye aliamka na kuanza kuwaangalia.
“What the hell is going on?” (Nini kinaendelea?) aliuliza huku akiwaangalia.
Hawakutaka kumjibu swali lake, walichokifanya ni kumshika na kumlaza chini kisha kumfunga pingu huku wakimtaka kuwaambia mahali alipokuwa Benjamin.
“Benjamin, I don’t know where he is,” (Benjamin, sijui yupo wapi) alisema Harry huku uso wake ukionyesha tabasamu pana.
“Tell us where he is,” (Tuambie yupo wapi)
“I dont know men, he left last night,” (Sijui jamani, aliondoka usiku uliopita) alijibu Benjamin, kwa kumwangalia tu, alionyesha dhahiri kwamba aliwadanganya.
****
Benjamin alikuwa kama mtu mwenye machale, usiku wa siku hiyo hakulala, alibaki macho huku akiwa na wasiwasi mno, alijua kama kulikuwa na kitu ambacho kingetokea hivyo asingeweza kulala kabisa.
Alikesha, mpaka mwanga unaanza kuchomoza asubuhi, alikuwa macho, akatoka kitandani na kwenda jikoni ambapo akaandaa kahawa na kisha kuelekea sebuleni kuangalia televisheni.
Kipindi hicho televisheni ndiyo ilikuwa faraja yake, hakuwa na cha kufanya, hakuwa na uhuru wa kufanya kitu chochote kile, alipokuwa kwenye televisheni, ndiyo ulikuwa muda wa kujua kitu gani kilikuwa kikiendelea katika ulimwengu aliokuwa akiuogopa.
Mara kwa mara alijiona kwenye televisheni, alikuwa mtu maarufu kwa sababu ya matukio yaliyokuwa yametokea. Watu wengi walihojiwa, kilio chao kilikuwa ni kumuona Benjamin akikamatwa na kufikishwa mahakamani na kisha kushtakiwa kwa makosa ambayo dunia nzima ilijua kwamba aliyafanya.
“Ila kwa nini huyu mzee anafanya hivi?” alijiuliza pasipo kupata jibu.
Akasimama, akaanza kutembea ndani ya sebule ile huku akiwa na mawazo lukuki, aliongea peke yake kama kichaa, akatoka pale alipokuwa mpaka katika dirisha kubwa, akafungua pazia na kuanza kuangalia nje.
Alitamani kuwa huru, aliwaona watu wakitembea barabarani huku wakiwa wamejiachia, alitamani na yeye kuwa vile lakini ilishindikana kabisa, hakuweza kuwa huru kama watu wale walivyokuwa huru kipindi kile.
Wakati akiwa amesimama katika dirisha lile ndipo alipoliona gari moja likija na kusimama karibu na eneo la nyumba ile barabarani. Kwanza akaanza kuwa na wasiwasi, hakutaka kujipa uhakika kwamba watu waliokuwa ndani ya gari hilo walikuwa watu wazuri, akagundua kwamba kulikuwa na kitu.
Hakutaka kuwa na wasiwasi mwingi, akasubiri kuona ni watu gani wangeteremka kutoka ndani ya gari lile. Wakati akiwa amelikodolea macho, likatokea gari jingine ambalo kwa ubavuni liliandikwa S.W.A.T.
Harakaharaka wanajeshi waliokuwa na mavazi yaliyoandikwa S.W.A.T wakatoka ndani ya gari lile, walikuwa na bunduki kubwa hasa AK 47 ambazo ndizo zilikuwa maalumu kwa kazi yao.
Mavazi yao, yalikuwa yale mazito ambapo tumboni mpaka kifuani walikuwa na vazi jingine lililokuwa na uwezo wa kuzuia risasi. Benjamin alipowaona watu hao, hakutaka kusubiri, alijua fika kwamba walikuwa mahali hapo kwa ajili yake.
Hakutaka kujiuliza, wanajeshi wale na FBI tayari walianza kuelekea kule ilipokuwa nyumba ile, aliamini kwamba kama angekwenda jikoni na kutoka nje kupitia mlango wa nyuma, angechelewa na hivyo kukamatwa, wazo pekee lililomjia kichwani ilikuwa ni lazima aingie ndani ya ‘chimney’.
Sebuleni hapo kulikuwa na sehemu maalumu ambayo nyumba nyingi za Marekani na Ulaya au hata sehemu zenye baridi kali huweka kama jiko kwa ajili ya kuchoma kuni na kuleta moto ambapo moshi wake ulipita katika bomba kubwa lililokwenda juu ya bati na kupotelea huko.
Yeye alitaka kuingia katika bomba hilo, halikuwa kubwa sana lakini lilitosha kwa mwili wake kuenea kwani hakuwa mnene ila alikuwa mrefu. Hakutaka kuchelewa, haraka sana akaelekea katika sehemu ile, kulikuwa na kuni, akazisogeza pembeni na kisha kuanza kujiingiza, hakuanza kukiingiza kichwa, alibinuka na kuanza kuiingiza miguu yake kwenda kwenye bomba lile kwa juu.
Ilikuwa kazi kubwa lakini haikumsumbua sana, hakuchukua sekunde nyingi, akafanikiwa kuingia ndani ya bomba lile na kutulia, masikio yake yalikuwa ni hapo sebuleni, tangu maofisa wa FBI walipoanza kuugonga mlango na kuuvunja, yeye alikuwa ndani ya bomba lile sebuleni pale huku akisikiliza kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Maofisa wa FBI walijua fika kwamba Harry alikuwa akijua mahali alipokuwa Benjamin ila hakutaka tu kuwaambia ukweli. Walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka kituoni.
Huko wakamuingiza ndani ya chumba cha mahojiano na kuanza kuzungumza naye, walitaka aeleze ukweli mahali alipokuwa Benjamin, vinginevyo wangemfanya kitu kibaya.
“Nina haki ya kusikilizwa pia,” alisema Benjamin kwani tayari aliona maofisa wale walikuwa wamekasirika.
“Sawa. Benjamin yupo wapi?”
“Sijui! Kwani nyie wa nini?”
“Amefanya mauaji!”
“Hapana! Benjamin hakuwahi kuua,” alisema Harry.
“Usibishane na sisi, aliua na hata jana aliua pia,” alisema ofisa huyo.
“Jana kuna mauaji yalitokea huko Los Angeles, wote mnasema kwamba Benjamin ndiye aliyehusika, si ndiyo?” aliuliza Harry.
“Ndiyo!”
“Sawa! Kwenye maelezo yenu mlisema kwamba jana usiku mliniona nikiwa naye, ilikuwa saa tano usiku, si ndiyo?”
“Ndiyo!”
“Mauaji yalitokea saa nne na nusu, si ndiyo?”
“Ndiyo!”
“Sasa jamani! Huyo Benjamin awe ameua saa nne na nusu usiku, atatumia usafiri gani kutoka Los Angeles mpaka hapa Boston kwa mwendo wa nusu saa? Kwa ndege haiwezekani, alitumia usafiri gani sasa?” aliuliza Harry huku akiwaangalia maofisa wawili aliokuwa nao humo ndani.
“Labda niwaulize kitu kimoja. Nyie mnaamini Benjamin ni yupi? Yule aliyefanya mauaji huko Los Angeles au huyu aliyekuwa pamoja nami?” aliuliza Harry. Maofisa wakabaki wakiangaliana tu.
Alichokisema Harry kilikuwa ni ukweli mtupu. Kutoka Los Angeles mpaka hapo Boston ilikuwa ni mwendo wa saa moja na nusu kwa ndege, sasa ilikuwaje huyo Benjamin afanye mauaji Los Angeles halafu ndani ya nusu saa aonekane jijini Boston? Hilo likawapa wakati mgumu maofisa hao, hawakujua washike lipi, kama Benjamin alionekana hapo Boston majira ya saa tano usiku, je aliyefanya mauaji saa nne na nusu usiku huko Los Angeles alikuwa nani? Wakabaki na maswali kibao.
****
Dunia ilikuwa ikijiandaa kwa ajili ya kumuona msichana mrembo ambaye angeibuka kidedea katika Mashindano ya Miss Dunia ambayo kwa kipindi hicho yalitegemewa kufanyika jijini Texas nchini Marekani.
Watu walitaka kushuhudia ni msichana yupi angeibuka mshindi kwani wasichana wote ambao walitegemewa kushiriki walikuwa wale warembo, waliowavutia watu wengi nchini mwao.
Kila mtu anawa na uhakika kwamba msichana Angelica Sanchez kutoka nchini Mexico angechukua taji hilo lililokuwa likishikiria na mrembo kutoka nchini Venezuel, Maria alejandro.
Kwa kumwangalia, Angelica alikuwa msichana mrembo mno, alikwenda juu, hipsi zake zilionekana vilivyo, alikuwa na sura nzuri uliopendezeshwa na vishimo viwili vilivyokuwa mashavuni mwake. Muda wote, alikuwa kwenye tabasamu pana kana kwamba hakujua maana ya kukasirika.
Huyo ndiye alikuwa gumzo kipindi hicho. Tangu alipochukua taji la urembo nchini Mexico, kila mtu alitokea kumpenda, kampuni mbalimbali zinazojihusisha na mambo ya mitindo ikamtafuta, yeye alijiona mrembo, watu wengine wakamuona mrembo lakini makampuni hayo yaliona fedha.
Walijua kwamba kama wangemtumia msichana huyo katika matangazo yao mbalimbali, wangepata fedha nyingi, hivyo wakaingia naye mikataba mingi kwa kutegemea kuwa angeweza kuchukua taji hilo.
Mbali na Angelica, pia kulikuwa na msichana aliyeitwa Jenny Chu, msichana kutoka nchini China, alikuwa mrembo, alisoma na kuwa na PhD ya udaktari, hakuangalia elimu yake, alichokuwa akikiangalia kilikuwa ni masuala ya urembo tu, tangu zamani aliwaahidi wazazi wake kwamba kuna siku angekuwa mrembo wa dunia, na muda huo, aliona ndiyo kipindi chenyewe.
Kulikuwa na wasichana wengi, japokuwa wengi waliwafikiria wasichana hao warembo lakini wakasahau kwamba mbali na wasichana hao kulikuwa na msichana mmoja aliyekuwa mrembo mno, inawezekana kuliko wote hao, msichana huyo aliitwa Stacie Lawrence.
Kwa kumwangalia msichana huyo kutoka nchini Australia, alikuwa mrembo haswa, sura ya kitoto, lipsi pana kidogo, macho ya goroli, shingo ya upanga, aliumbika, alijua kutembea, yaani kwa kumwangalia harakaharaka, ingekufanya kudhani kwamba umekutana na mzimu wa mwanamke mrembo kuliko wote, Cleopatra.
Stacie hakuwa mzungumzaji, alikuwa kimya, alionekana kama kuwa na wasiwasi, hakuonekana kujiamini kabisa. Alikuwa msomi, alikuwa na PhD ya mambo ya uandishi, alitamani kusoma lakini pia alipenda sana mambo ya urembo na huo ukawa ndiyo muda wake wa kukamilisha kile alichokuwa akikiota kila siku.
Alimuogopa msichana Angelica kwa kuwa alitangazwa sana, hakuwa na uhakika kama angeweza kushinda kinyang’anyiro hicho, kila wakati alipokuwa akimuona Angelica, alitamani kumsogelea na kumsalimia kisha kumwambia kwamba alitamani sana kuwa kama yeye.
Hakujua watu walimfikiria vipi. Wasichana wengi waliokuwa katika kinyang’anyiro hicho walimpa ushindi, alionekana kustahili hata zaidi ya Angelica ambaye mara kwa mara alikuwa akipigiwa promo kutoka sehemu mbalimbali.
Wasichana wengine wakashindwa kujizuia, walimsogelea na kumwambiia wazi kwamba alikuwa mrembo, kila msichana alitamani kuwa kama yeye lakini kila alipoambiwa, aliwajibu kitu kimoja kwamba inawezekana hawakumuona Angelica.
“Unajua wewe mzuri sana,” aliambiwa na msichana Priscilia, mrembo kutoka nchini Italia.
“Nani? Mimi?”
“Ndiyo! U mrembo sana...”
“Hapana! Labda hujamuona Angelica...”
“Nimemuona lakini wewe, hakika unastahili kuwa mshindi katika shindano hili,” alisema msichana Priscilia.
Kwa kumwangalia, alionekana kutokutania, alimaanisha kile alichokuwa akikizungumza. Hiyo haikuwa kwa msichana huyo tu, alipoondoka walimfuata wasichana wengine na kumwambia jinsi alivyokuwa mrembo.
Alipoambiwa, alijisikia aibu, hakujiamini hata kidogo. Kwa Angelica, tayari alianza kuona wivu, jinsi wasichana wengine walivyokuwa wakimzungumzia Stacie, moyo wake uliuma kupita kawaida.
Walikaa kambini huku wakiendelea na mazoezi kama kawaida, saa zilizidi kukatika, siku zikaenda mbele mpaka siku ya tukio kufika. Kila mtu alitaka kuona msichana Angelica akichukua taji hilo na kuwa mrembo wa kwanza kushinda kutoka nchini Mexico.
Wakati Angelica akiendelea kuwa gumzo ndipo watu wakafanikiwa kumona msichana Stacie. Kwanza kila mmoja akashtuka, hawakuamini kile walichokiona, hawakuamini kama kulikuwa na msichana mwingine mrembo hata zaidi ya Angelica ambaye alikuwa gumzo.
Mioyo ya watu ikaanza kubadilika, ikatoka kwa msichana Angelica na kuhamia kwa Stacie, watu wakaanza kumtafuta katika mitandao mbalimbali, picha zake, urembo wake ukawadatisha sana, hakukuwa na aliyeamini kama dunia hiihii ingekuwa na msichana mrembo kama alivyokuwa Stacie.
Watu wakaanza kutumiana picha za msichana huyo katika mitandao ya kijamii, kila mtu aliyemuona Stacie katika picha zile, alitaka kumuona uso kwa uso kwani mioyo yao ilikataa kabisa kwamba katika dunia hiihii, kipindi hikihiki kungekuwa na msichana mrembo kama Stacie.
“Ni lazima nitakwenda kutazama kinyang’anyiro,” alisema jamaa mmoja, alikuwa ameshika simu yake akimwangalia Stacie.
“Si ulisema hauendi!”
“Nitakwenda, nimebadili mawazo,” alisema jamaa huyo.
Watu walitaka kuona ushindani mkubwa kutoka kwa wasichana wawili warembo, mmoja kutoka nchini Australia na mwingine kutoka nchini Mexico. Kila kona, wawili hao walawa gumzo, japokuwa kipindi cha nyuma Angelica alikuwa akizungumziwa sana lakini katika kipindi hicho upepo ukabadilika kabisa, hakuzungumziwa Angelica peke yake bali alizungumziwa Stacie, tena kadiri muda ulivyokuwa ukizidi kwenda mbele, aliendelea kusikika zaidi.
“Unahisi nani atachukua ushindi?”
“Mmh! Wala sijui manake nishanchanganyikiwa!”
Watu walisubiri mpaka pale kinyang’anyiro kilipoanza. Mwana huo, watu walifuatilia kinyang’anyiro hicho kuliko vipindi vingine vyote, kila kona, watu walikuwa wakifuatilia katika televisheni zao na kitu kilichokuwa kikiwavuta zaidi ni urembo wa wasichana hao wawili.
Vipengele vyote vikapita na mwisho wa siku mshindi kutarajiwa kutangazwa. Katika tatu bora alibaki Stacie, Angelica na mrembo mwingine kutoka Afrika Kusini, ThandiMbokani.
Ukumbi mzima ulibaki kimya, mtu aliyetakiwa kutangaza matokeo, akasimama, akachukua matokeo kutoka kwa majaji na kisha kusimama, hakuanza na mtu wa kwanza, alianza na mtu wa tatu.
Lilipotajwa jina la Thandi, kila mtu alikaa kimya, walilitegemea hilo, walijua kwamba msichana huyo angeshika nafasi hiyo na mbili za juu zingekuwa kwa hao warembo waliowafanya watu wengi kujaa ndani ya ukumbi huo.
Mtangazaji, hakutaka kutangaza kwa pupa, alitaka kila mtu awe na presha mahali hapo, kwanza akarekebisha tai yake, akajikoholesha, akafanya mambo mengi yasiyokuwa na msingi ili kuwafanya watu kuwa na presha ndani ya ukumbi huo.
Kila mmoja alikuwa akimwangalia, mapigo yao ya moyo yalikuwa yakidunda sana, wote walikuwa na mshindi wao mioyoni mwao, walitaka kumsikia mtangazaji huyo alikuwa nani kwani kama ni urembo, wote walikuwa warembo japokuwa msichana Stacie alizidi kidogo.
Je, nini kitaendelea
Thanks

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii riwaya kila nikisoma natamani episode isifike mwisho. Thanks anyway Madame
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Ishirini na Moja.
Moyo wa Bwana Seppy ulikuwa mweupe kabisa, alichokuwa akitaka kukiona ni kuwa peke yake katika penzi la msichana Maria, kuua, kwake hakukuwa na tatizo lolote lile, kitu pekee alichokitaka ni kuwa na furaha kipindi chote.
Alipata taarifa kutoka kwa watu wengine kwamba yule mchezaji wa mpira wa kikapu aliyekuwa akitamba sana kipindi hicho, Paul alikuwa amekufa chumbani katika hoteli moja huko Los Angeles, hakutaka kujali sana kwani yeye ndiye aliyekuwa nyuma ya mpango wake.
Hakutaka kumuuliza Maria kuhusu Paul, alijua kwamba msichana huyo alikuwa na hofu kubwa kwa kuhisi kwamba angejua, akamuacha na uzuri ni kwamba kila taarifa iliyokuwa ikiandikwa, hakutajwa msichana, ilitajwa kwamba kama kawaida Benjamin alikuwa amekwenda chumbani humo na kumuua kijana huyo.
“Hakikisheni huyo msichana anakuwa huru, si mnajua kwamba huyo ni msichana wangu?” alizungumza Bwana Seppy katika simu, alikuwa akizungumza na polisi.
“Ndiyo mkuu!”
“Basi fanyeni hivyo!”
Hela zilikuwa kila kitu, alikuwa miongoni mwa matajiri wakubwa, aliheshimika kila kona, polisi wengi waliokuwa na tamaa ya fedha walikuwa chini yake na ndiyo maana wakati mwingine alikuwa huru kufanya kitu chochote alichotaka kukifanya kwa kuwa alijua hakukuwa na mtu aliyekuwa akimbabaisha hata mara moja.
Polisi walipewa maelekezo juu ya nini cha kufanya na wao walitakiwa kufanya vilevile, harakaharaka wakamuita Maria katika chumba cha mahojiano, wakaanza kuzungumza naye, hawakuchukua muda mrefu wakaamua kumwachia huku wakimwambia kwamba angehitajika kituoni hapo mara kwa mara.
Hilo ndilo alilolitaka Bwana Seppy, akawasiliana na Maria ambaye alimwambia kwamba yupo nyumbani, akamwambia kuwa alitaka kumuona wiki hiyo lakini msichana huyo akasema kwamba hakujisikia vizuri, alihitaji muda wa kupumzika.
“Si utakuja kupumzika huku mpenzi!” alisema Bwana Seppy.
“Hapana mpenzi! Naomba wiki moja ya mapumziko!”
“Sawa. Upo poa lakini?”
“Ndiyo! Najisikia kuchoka tu,” alisema Maria.
Bwana Seppy aliusoma mchezo, alijua fika kwamba msichana huyo alikuwa katika kipindi cha majonzi, alimpenda sana Paul na hakuona kama kungekuwa na mtu ambaye angelivuruga penzi lake, hata mapenzi aliyokuwa nayo juu ya Bwana Seppyy alipungua kwa kiasi kikubwa kwani hata kama fedha, Paul alikuwa nazo japokuwa hazikuwa nyingi kama za Bwana Seppy.
Siku zikaendelea kukatika, wiki ikakatika lakini msichana Maria hakufika nchini Marekani, kila alipopigiwa simu, alisema kwamba alikuwa kwenye kipindi kigumu, matatizo ya kifamilia yalikuwa yakimwandama hivyo asingeweza kabisa kwenda nchini Marekani.
Kwake, hayo yalikuwa majibu makali, yaliyouumiza moyo wake kupita kawaida, hakutaka kuona akishindwa, alichokifanya ni kuondoka Marekani na kuelekea nchini Mexico kwa kuamini kwamba uwepo wake mbele ya msichana huyo ungeweza kubadilisha kila kitu.
“Kisa nini Maria?” aliuliza Bwana Seppy huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Sipo vizuri kiafya,” alisema.
“Najua na ndiyo maana naona umekonda sana. Tafadhali mpenzi, kama kuna tatizo, naomba uniambie.”
“Hakuna tatizo lolote lile.”
“Kweli?”
“Hakika!”
Siku hiyo Bwana Seppy alitumia muda wake wote kuwa chumbani na msichana Maria, hata walipofanya mapenzi, haikuwa kama kipindi cha nyuma, hakupewa ushirikiano kama ilivyokuwa kipindi kingine. Moyoni mwake aliumia lakini hakuwa na jinsi, alimpenda msichana Maria na kama kuzunguka, alizunguka sehemu nyingi, aliwaona wasichana wengi lakini alikiri kwamba hakuwahi kumuona msichana kama Maria kwa jinsi alivyokuwa mzuri.
“Hii yote ni kwa sababu nakupenda Maria?” aliuliza Bwana Seppy ilipofika asubuhi.
“Kivipi?”
“Kwa unavyonifanyia!”
“Kwani nimekufanyaje mpenzi?”
“Sawa. Si umesema una matatizo ya kifamilia, ngoja nikuache uendelee nayo,” alisema Bwana Seppy.
Moyo wake ulikasirika, alimfahamu Maria, hakuwa namna ile, alijua kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikimuuma, kitendo cha mwanaume aliyekuwa akimpenda kuuawa, ndicho kilichomfanya kuwa katika hali ile.
Alikasirika kwa kuwa yeye kama yeye alikuwa na nafasi yake lakini pia hakutakiwa kukasirikiwa au kuonyeshewa hali yoyote ya kutokujali kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa akimuweka mjini msichana huyo.
Uamuzi wa mwisho kabisa kuupanga ulikuwa ni kuondoka mahali hapo, hakutaka kurudi tena, kama kuumia, aliumia vya kutosha na huo ulikuwa muda wa kuulizwa moyo wake huku akijitahidi kutafuta msichana mzuri ambaye angempenda kama alivyokuwa akimpenda Maria.
****
Hakukuwa na aliyeamini kama Stacie alikuwa amembwaga Angelica katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Miss World ambacho kilifanyika nchini Marekani katika jiji la Texas.
Ukumbi mzima ulipiga makofi, watu wengine walibaki midomo wazi, wapo wengine waliocheza kamari na kubashiri kwamba msichana Angelica angeibuka mshindi kutokana na kunyakua taji hilo.
Stacie alikuwa na furaha kubwa moyoni mwake, alipita huku na kule akiwapungia watu mikono, ndoto yake aliyokuwa nayo tangu kipindi cha nyuma hatimaye Mungu aliifanikisha na kuwa kweli.
Machozi ya furaha yalimbubujika, kuna kipindi hakuwa akiamini, alihisi kwamba alikuwa katika moja ya ndoto yenye msisimko ambapo baada ya kipindi fulani angeamka na kujikuta akiwa kutandani kitu ambacho hakikuwa kweli, kila kitu kilichokuwa kikitokea, kilikuwa katika maisha halisi.
Jina lake siku hiyo likapata umaarufu, waandishi wa habari wakampiga sana picha na wengine kuiweka habari yake katika mitandao ya kijamii, jina lake, yaani kwa kipindi cha dakika kadhaa, lilikuwa maarufu mno.
Uzuri wake uliendelea kuwatetemesha wanaume wengi, hawakuwa wakiamini kama kweli duniani kulikuwa na msichana aliyekuwa na sura nzuri kama alivyokuwa Stacie, wanaume wenye fedha wakajipanga, kila mtu alihitaji kuwa na msichana huyo, hawakujua kama angekubaliana nao au la, kitu walichokihitaji ni kuwa naye kimapenzi, yaani hata kama ni kutumia fedha, watumie lakini mwisho wa siku wampate msichana huyo.
Siku hiyo Stacie akapelekwa katika hoteli kubwa ya nyota saba na kukaa huko. Usiku mzima alikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli angefanikiwa kunyakua taji hilo lililokuwa na heshima kubwa duniani katika masuala ya urembo.
Siku iliyofuata akawasiliana na rafiki yake wa kipindi kirefu, Robert Steph ili awe meneja wake kwani mbele yake aliyaona mafanikio makubwa hasa ya kuingia mikataba minono.
Kama alivyohisi ndivyo ilivyotokea, siku hiyihiyo akapigiwa simu na watu wa Jarida kubwa la Forbes ambao walitaka kuonana naye na kuzungumza naye kuhusu masuala ya kibiashara, hilo wala halikuwa tatizo, alichoangalia kwanza ni kupiga pesa tu.
****
Fedha zikaanza kunukia kwa msichana Stacie, hakukuwa na kitu alichokiona mbele yake zaidi ya mafanikio makubwa, alijiona akiwa mtu mkubwa, mwenye fedha na heshima kubwa.
Kitendo cha kunyakua tuzo na kuwa mrembo wa dunia kilimpa uhakika wa kuishi maisha ya kuwa na fedha mpaka anakufa, kupitia uzuri wake, alishinda tuzo hiyo na hivyo kumshukuru Mungu kila siku kwa kile alichokuwa amempa.
Baada ya kusaini mkataba na Jarida la Forbes na kulipwa kiasi cha dola milioni mbili ambazo zilikuwa zaidi ya bilioni nne za Kitanzania, makampuni mengi yakamfuata, hakuwa na hiyana, alichokifanya ni kuendelea kukusanya fedha kama kawaida.
Jina lake halikushuka, liliendelea kuwa juu na kwa sababu tayari alikuwa na jina, aliona kuwa na umuhimu wa kuwa na mbunifu wake wa mavazi. Kulikuwa na watu wengi walioomba nafasi hiyo, kila siku alipokea barua pepe, watu walikuwa wakimuomba nafasi ya kuwa mbunifu wake wa mavazi kiasi kwamba akachanganyikiwa amchukue yupi kwani kila mmoja alionekana kuwa mtaalamu kwa kazi hiyo.
“Kwa hiyo utamchukua nani?” aliuliza Robert.
“Labda huyu Muitaliano, Alejandro Petrescu,” alijibu Stacie.
Alichokifanya ni kuwasiliana na mbunifu huyo wa mavazi na kumtaka kufika nchini Marekani haraka iwezekanavyo, alimtumia tiketi ya ndege, gharama za kukaa hotelini lakini mwisho wa siku walitaka kuona kila kitu kinakuwa kama kinavyotakiwa.
Tangu achukue taji hilo alikwenda nyumbani kwao Australia mara mbili tu, baada ya hapo, maisha yake yakaendelea kuwa nchini Marekani ambapo aliishi kwa kuheshimika kupita kawaida.
Alejandro ndiye aliyemfanya Stacie kupendeza zaidi, kila siku alikuwa mtu wa kumbunia mavazi mbalimbali, na kila alipovaa, alivutia kiasi kwamba wanaume wengi wakazidi kumpenda.
Jina lake lilikuwa kubwa, ni ndani ya miezi sita tu tayari aliingiza kiasi kikubwa cha fedha kwa sababu tu alikuwa mrembo na hata mastaa wa filamu walitamani kuigiza naye kitu kilichowafanya kuwaomba waongozaji wafanye kitu.
“Hakuna tatizo, nitamuita kwenye hii filamu!”
Muongozaji kutoka katika Kampuni ya Filamu ya Marvel alikuwa akizungumza na muigizaji wake mwenye jina kubwa, Tom Hardy ambaye alikuwa akihitaji kuigiza na msichana Stacie.
Hilo wala halikuwa tatizo, kwa sababu wao wenyewe walikuwa wakitafuta fedha, waliamini kuwa kama wangemruhusu msichana huyo ashiriki katika muvi yao hakika wangepata kiasi kikubwa cha fedha, hivyo bila ubishi, wakawasiliana naye na kumuita.
Stacie hakuamini, hakuwahi kufikiria hata mara moja kwamba ingetokea siku angepokea simu kutoka kwa mmoja wa waongozaji katika kampuni hiyo na kumtaka kuigiza filamu, hakukataa, kwa kuwa naye alizitaka hizo fedha na kuwa maarufu zaidi, akakubaliana nao.
Baada ya siku kadhaa, wakaanza kuigiza filamu mpya ya Black Panther. Japokuwa alikuwa muigizaji mchanga lakini alifanya vizuri sana kitu kilichoonyesha kwamba angekuwa muigizaji mkubwa sana hapo baadaye.
Hayo ndiyo yalikuwa mwanzo wa mafanikio makubwa aliyoanza kuyapata. Kila siku akawa mtu wa kuingiza fedha, uzuri wake uliwachanganya watu wengi na hivyo kuanza kumfutailia bila mafanikio makubwa.
Miongoni mwa watu wengi waliokuwa wakimfuatilia alikuwa Bwana Seppy. Mzee huyu alimpigia simu Stacie na kumwambia kwamba alitaka kuonana naye kwa kuwa kulikuwa na mambo mengi ya kuzungumza.
Jina la Bwana Seppy halikuwa geni, alimfahamu mzee huyo, alikuwa miongoni mwa watu wenye fedha ambao waliitetemesha Marekani kipindi hicho. Kwake ilikuwa furaha tele hivyo kupanga mipango ya kuonana.
Siku mbili zilizofuata, walikuwa katika Mgahawa wa SamSam ambapo hapo Bwana Seppy alikuwa na walinzi wake waliokuwa kimya kila wakati.
Bwana Seppy alibaki akimwangalia msichana huyo, alikuwa mrembo sana, tangu aachane na mpenzi wake, Maria miezi kadhaa iliyopita hakupata mtu ambaye angeziba pengo kubwa lililoachwa na msichana Maria.
Alimtafuta msichana wa kuziba pengo hilo ila kwa kipindi chote hicho, hakufanikiwa kabisa. Kila alipomwangalia Stacie, aliona kabisa kwamba msichana huyo alikuwa akielekea katika kuliziba pengo hilo lililomtesa kwa kipindi kirefu.
Kuhusu kutumia fedha, kwake halikuwa na tatizo lolote lile, kitu pekee alichokihitaji kilikuwa ni mapenzi kutoka kwa msichana huyo tu. Macho yake tu yalionyesha kila kitu, mapenzi aliyokuwa nayo moyoni hayakubaki huko bali yalizunguka mpaka machoni mwake.
Alitaka kumwambia ukweli lakini hakujua mahali pa kuanzia, alivuta pumzi huku akiagiza kahawa, kipindi chote hicho msichana Stacie alikuwa akimwangalia tu machoni mwake.
“Nashukuru sana kwa kuitikia wito wangu,” alisema mzee huyo huku akimwangalia msichana huyo.
“Usijali...”
“Nimekuita kwa jambo moja...”
“Lipi hilo? Biashara?”
“Ndiyo! Lakini sidhani kama la biashara linatakiwa kuzungumzwa leo, nadhani leo tunatakiwa kuzungumzia jambo jingine kabisa,” alisema mzee huyo.
“Lipi hilo?”
Bwana Seppy akashusha pumzi ndefu na kuangalia pembeni kama kulikuwa na watu waliokuwa wakiyafuatilia mazungumzo yao, alipoona hakukuwa na mtu aliyekuwa akifanya hivyo, hapo ndipo alipoamua kutumbua jipu.
Hakutaka kuteseka moyoni mwake, ilikuwa ni vigumu mno kuendelea kuumia, kuwa na mawazo na wakati alikuwa na uwezo mkubwa wa kumwambia msichana huyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Hakutaka kuficha, kama ni siri, aliamua kuitoa na hivyo kumwambia jinsi alivyokuwa akimpenda. Muda wote msichana Stacie alikuwa kimya, alibaki akimwangalia mzee huyo usoni, uso wa Stacie ulikuwa kwenye tabasamu pana ambalo lilimpa matumaini mzee huyo kwamba angefanikiwa kile alichokuwa akikitaka.
“Umemaliza?” aliuliza Stacie baada ya kumsikiliza mzee huyo kwa dakika tatu.
“Ndiyo!”
“Haitowezekana!” alijibu kwa kifupi.
“Kwa nini tena jamani?”
“Jua kwamba haitowezekana, hakuna sababu, jua tu kwamba haitowezekana,” alisema Stacie na hapohapo kusimama, hakutaka kusubiri, japokuwa mzee huyo alionyesha muonekano uliomtia huruma, hakutaka kujali, akachukua kila kilicho chake na kuondoka zake huku Bwana Seppy akiishia kula kwa macho tu.
Je, nini kitaendelea?
 
Baada ya mauaji ya Stacie, Benjamin atakamatwa, siku za bwana sappy zinahesabika
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Ishirini na Moja.
Moyo wa Bwana Seppy ulikuwa mweupe kabisa, alichokuwa akitaka kukiona ni kuwa peke yake katika penzi la msichana Maria, kuua, kwake hakukuwa na tatizo lolote lile, kitu pekee alichokitaka ni kuwa na furaha kipindi chote.
Alipata taarifa kutoka kwa watu wengine kwamba yule mchezaji wa mpira wa kikapu aliyekuwa akitamba sana kipindi hicho, Paul alikuwa amekufa chumbani katika hoteli moja huko Los Angeles, hakutaka kujali sana kwani yeye ndiye aliyekuwa nyuma ya mpango wake.
Hakutaka kumuuliza Maria kuhusu Paul, alijua kwamba msichana huyo alikuwa na hofu kubwa kwa kuhisi kwamba angejua, akamuacha na uzuri ni kwamba kila taarifa iliyokuwa ikiandikwa, hakutajwa msichana, ilitajwa kwamba kama kawaida Benjamin alikuwa amekwenda chumbani humo na kumuua kijana huyo.
“Hakikisheni huyo msichana anakuwa huru, si mnajua kwamba huyo ni msichana wangu?” alizungumza Bwana Seppy katika simu, alikuwa akizungumza na polisi.
“Ndiyo mkuu!”
“Basi fanyeni hivyo!”
Hela zilikuwa kila kitu, alikuwa miongoni mwa matajiri wakubwa, aliheshimika kila kona, polisi wengi waliokuwa na tamaa ya fedha walikuwa chini yake na ndiyo maana wakati mwingine alikuwa huru kufanya kitu chochote alichotaka kukifanya kwa kuwa alijua hakukuwa na mtu aliyekuwa akimbabaisha hata mara moja.
Polisi walipewa maelekezo juu ya nini cha kufanya na wao walitakiwa kufanya vilevile, harakaharaka wakamuita Maria katika chumba cha mahojiano, wakaanza kuzungumza naye, hawakuchukua muda mrefu wakaamua kumwachia huku wakimwambia kwamba angehitajika kituoni hapo mara kwa mara.
Hilo ndilo alilolitaka Bwana Seppy, akawasiliana na Maria ambaye alimwambia kwamba yupo nyumbani, akamwambia kuwa alitaka kumuona wiki hiyo lakini msichana huyo akasema kwamba hakujisikia vizuri, alihitaji muda wa kupumzika.
“Si utakuja kupumzika huku mpenzi!” alisema Bwana Seppy.
“Hapana mpenzi! Naomba wiki moja ya mapumziko!”
“Sawa. Upo poa lakini?”
“Ndiyo! Najisikia kuchoka tu,” alisema Maria.
Bwana Seppy aliusoma mchezo, alijua fika kwamba msichana huyo alikuwa katika kipindi cha majonzi, alimpenda sana Paul na hakuona kama kungekuwa na mtu ambaye angelivuruga penzi lake, hata mapenzi aliyokuwa nayo juu ya Bwana Seppyy alipungua kwa kiasi kikubwa kwani hata kama fedha, Paul alikuwa nazo japokuwa hazikuwa nyingi kama za Bwana Seppy.
Siku zikaendelea kukatika, wiki ikakatika lakini msichana Maria hakufika nchini Marekani, kila alipopigiwa simu, alisema kwamba alikuwa kwenye kipindi kigumu, matatizo ya kifamilia yalikuwa yakimwandama hivyo asingeweza kabisa kwenda nchini Marekani.
Kwake, hayo yalikuwa majibu makali, yaliyouumiza moyo wake kupita kawaida, hakutaka kuona akishindwa, alichokifanya ni kuondoka Marekani na kuelekea nchini Mexico kwa kuamini kwamba uwepo wake mbele ya msichana huyo ungeweza kubadilisha kila kitu.
“Kisa nini Maria?” aliuliza Bwana Seppy huku akimwangalia msichana huyo usoni.
“Sipo vizuri kiafya,” alisema.
“Najua na ndiyo maana naona umekonda sana. Tafadhali mpenzi, kama kuna tatizo, naomba uniambie.”
“Hakuna tatizo lolote lile.”
“Kweli?”
“Hakika!”
Siku hiyo Bwana Seppy alitumia muda wake wote kuwa chumbani na msichana Maria, hata walipofanya mapenzi, haikuwa kama kipindi cha nyuma, hakupewa ushirikiano kama ilivyokuwa kipindi kingine. Moyoni mwake aliumia lakini hakuwa na jinsi, alimpenda msichana Maria na kama kuzunguka, alizunguka sehemu nyingi, aliwaona wasichana wengi lakini alikiri kwamba hakuwahi kumuona msichana kama Maria kwa jinsi alivyokuwa mzuri.
“Hii yote ni kwa sababu nakupenda Maria?” aliuliza Bwana Seppy ilipofika asubuhi.
“Kivipi?”
“Kwa unavyonifanyia!”
“Kwani nimekufanyaje mpenzi?”
“Sawa. Si umesema una matatizo ya kifamilia, ngoja nikuache uendelee nayo,” alisema Bwana Seppy.
Moyo wake ulikasirika, alimfahamu Maria, hakuwa namna ile, alijua kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikimuuma, kitendo cha mwanaume aliyekuwa akimpenda kuuawa, ndicho kilichomfanya kuwa katika hali ile.
Alikasirika kwa kuwa yeye kama yeye alikuwa na nafasi yake lakini pia hakutakiwa kukasirikiwa au kuonyeshewa hali yoyote ya kutokujali kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa akimuweka mjini msichana huyo.
Uamuzi wa mwisho kabisa kuupanga ulikuwa ni kuondoka mahali hapo, hakutaka kurudi tena, kama kuumia, aliumia vya kutosha na huo ulikuwa muda wa kuulizwa moyo wake huku akijitahidi kutafuta msichana mzuri ambaye angempenda kama alivyokuwa akimpenda Maria.
****
Hakukuwa na aliyeamini kama Stacie alikuwa amembwaga Angelica katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Miss World ambacho kilifanyika nchini Marekani katika jiji la Texas.
Ukumbi mzima ulipiga makofi, watu wengine walibaki midomo wazi, wapo wengine waliocheza kamari na kubashiri kwamba msichana Angelica angeibuka mshindi kutokana na kunyakua taji hilo.
Stacie alikuwa na furaha kubwa moyoni mwake, alipita huku na kule akiwapungia watu mikono, ndoto yake aliyokuwa nayo tangu kipindi cha nyuma hatimaye Mungu aliifanikisha na kuwa kweli.
Machozi ya furaha yalimbubujika, kuna kipindi hakuwa akiamini, alihisi kwamba alikuwa katika moja ya ndoto yenye msisimko ambapo baada ya kipindi fulani angeamka na kujikuta akiwa kutandani kitu ambacho hakikuwa kweli, kila kitu kilichokuwa kikitokea, kilikuwa katika maisha halisi.
Jina lake siku hiyo likapata umaarufu, waandishi wa habari wakampiga sana picha na wengine kuiweka habari yake katika mitandao ya kijamii, jina lake, yaani kwa kipindi cha dakika kadhaa, lilikuwa maarufu mno.
Uzuri wake uliendelea kuwatetemesha wanaume wengi, hawakuwa wakiamini kama kweli duniani kulikuwa na msichana aliyekuwa na sura nzuri kama alivyokuwa Stacie, wanaume wenye fedha wakajipanga, kila mtu alihitaji kuwa na msichana huyo, hawakujua kama angekubaliana nao au la, kitu walichokihitaji ni kuwa naye kimapenzi, yaani hata kama ni kutumia fedha, watumie lakini mwisho wa siku wampate msichana huyo.
Siku hiyo Stacie akapelekwa katika hoteli kubwa ya nyota saba na kukaa huko. Usiku mzima alikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli angefanikiwa kunyakua taji hilo lililokuwa na heshima kubwa duniani katika masuala ya urembo.
Siku iliyofuata akawasiliana na rafiki yake wa kipindi kirefu, Robert Steph ili awe meneja wake kwani mbele yake aliyaona mafanikio makubwa hasa ya kuingia mikataba minono.
Kama alivyohisi ndivyo ilivyotokea, siku hiyihiyo akapigiwa simu na watu wa Jarida kubwa la Forbes ambao walitaka kuonana naye na kuzungumza naye kuhusu masuala ya kibiashara, hilo wala halikuwa tatizo, alichoangalia kwanza ni kupiga pesa tu.
****
Fedha zikaanza kunukia kwa msichana Stacie, hakukuwa na kitu alichokiona mbele yake zaidi ya mafanikio makubwa, alijiona akiwa mtu mkubwa, mwenye fedha na heshima kubwa.
Kitendo cha kunyakua tuzo na kuwa mrembo wa dunia kilimpa uhakika wa kuishi maisha ya kuwa na fedha mpaka anakufa, kupitia uzuri wake, alishinda tuzo hiyo na hivyo kumshukuru Mungu kila siku kwa kile alichokuwa amempa.
Baada ya kusaini mkataba na Jarida la Forbes na kulipwa kiasi cha dola milioni mbili ambazo zilikuwa zaidi ya bilioni nne za Kitanzania, makampuni mengi yakamfuata, hakuwa na hiyana, alichokifanya ni kuendelea kukusanya fedha kama kawaida.
Jina lake halikushuka, liliendelea kuwa juu na kwa sababu tayari alikuwa na jina, aliona kuwa na umuhimu wa kuwa na mbunifu wake wa mavazi. Kulikuwa na watu wengi walioomba nafasi hiyo, kila siku alipokea barua pepe, watu walikuwa wakimuomba nafasi ya kuwa mbunifu wake wa mavazi kiasi kwamba akachanganyikiwa amchukue yupi kwani kila mmoja alionekana kuwa mtaalamu kwa kazi hiyo.
“Kwa hiyo utamchukua nani?” aliuliza Robert.
“Labda huyu Muitaliano, Alejandro Petrescu,” alijibu Stacie.
Alichokifanya ni kuwasiliana na mbunifu huyo wa mavazi na kumtaka kufika nchini Marekani haraka iwezekanavyo, alimtumia tiketi ya ndege, gharama za kukaa hotelini lakini mwisho wa siku walitaka kuona kila kitu kinakuwa kama kinavyotakiwa.
Tangu achukue taji hilo alikwenda nyumbani kwao Australia mara mbili tu, baada ya hapo, maisha yake yakaendelea kuwa nchini Marekani ambapo aliishi kwa kuheshimika kupita kawaida.
Alejandro ndiye aliyemfanya Stacie kupendeza zaidi, kila siku alikuwa mtu wa kumbunia mavazi mbalimbali, na kila alipovaa, alivutia kiasi kwamba wanaume wengi wakazidi kumpenda.
Jina lake lilikuwa kubwa, ni ndani ya miezi sita tu tayari aliingiza kiasi kikubwa cha fedha kwa sababu tu alikuwa mrembo na hata mastaa wa filamu walitamani kuigiza naye kitu kilichowafanya kuwaomba waongozaji wafanye kitu.
“Hakuna tatizo, nitamuita kwenye hii filamu!”
Muongozaji kutoka katika Kampuni ya Filamu ya Marvel alikuwa akizungumza na muigizaji wake mwenye jina kubwa, Tom Hardy ambaye alikuwa akihitaji kuigiza na msichana Stacie.
Hilo wala halikuwa tatizo, kwa sababu wao wenyewe walikuwa wakitafuta fedha, waliamini kuwa kama wangemruhusu msichana huyo ashiriki katika muvi yao hakika wangepata kiasi kikubwa cha fedha, hivyo bila ubishi, wakawasiliana naye na kumuita.
Stacie hakuamini, hakuwahi kufikiria hata mara moja kwamba ingetokea siku angepokea simu kutoka kwa mmoja wa waongozaji katika kampuni hiyo na kumtaka kuigiza filamu, hakukataa, kwa kuwa naye alizitaka hizo fedha na kuwa maarufu zaidi, akakubaliana nao.
Baada ya siku kadhaa, wakaanza kuigiza filamu mpya ya Black Panther. Japokuwa alikuwa muigizaji mchanga lakini alifanya vizuri sana kitu kilichoonyesha kwamba angekuwa muigizaji mkubwa sana hapo baadaye.
Hayo ndiyo yalikuwa mwanzo wa mafanikio makubwa aliyoanza kuyapata. Kila siku akawa mtu wa kuingiza fedha, uzuri wake uliwachanganya watu wengi na hivyo kuanza kumfutailia bila mafanikio makubwa.
Miongoni mwa watu wengi waliokuwa wakimfuatilia alikuwa Bwana Seppy. Mzee huyu alimpigia simu Stacie na kumwambia kwamba alitaka kuonana naye kwa kuwa kulikuwa na mambo mengi ya kuzungumza.
Jina la Bwana Seppy halikuwa geni, alimfahamu mzee huyo, alikuwa miongoni mwa watu wenye fedha ambao waliitetemesha Marekani kipindi hicho. Kwake ilikuwa furaha tele hivyo kupanga mipango ya kuonana.
Siku mbili zilizofuata, walikuwa katika Mgahawa wa SamSam ambapo hapo Bwana Seppy alikuwa na walinzi wake waliokuwa kimya kila wakati.
Bwana Seppy alibaki akimwangalia msichana huyo, alikuwa mrembo sana, tangu aachane na mpenzi wake, Maria miezi kadhaa iliyopita hakupata mtu ambaye angeziba pengo kubwa lililoachwa na msichana Maria.
Alimtafuta msichana wa kuziba pengo hilo ila kwa kipindi chote hicho, hakufanikiwa kabisa. Kila alipomwangalia Stacie, aliona kabisa kwamba msichana huyo alikuwa akielekea katika kuliziba pengo hilo lililomtesa kwa kipindi kirefu.
Kuhusu kutumia fedha, kwake halikuwa na tatizo lolote lile, kitu pekee alichokihitaji kilikuwa ni mapenzi kutoka kwa msichana huyo tu. Macho yake tu yalionyesha kila kitu, mapenzi aliyokuwa nayo moyoni hayakubaki huko bali yalizunguka mpaka machoni mwake.
Alitaka kumwambia ukweli lakini hakujua mahali pa kuanzia, alivuta pumzi huku akiagiza kahawa, kipindi chote hicho msichana Stacie alikuwa akimwangalia tu machoni mwake.
“Nashukuru sana kwa kuitikia wito wangu,” alisema mzee huyo huku akimwangalia msichana huyo.
“Usijali...”
“Nimekuita kwa jambo moja...”
“Lipi hilo? Biashara?”
“Ndiyo! Lakini sidhani kama la biashara linatakiwa kuzungumzwa leo, nadhani leo tunatakiwa kuzungumzia jambo jingine kabisa,” alisema mzee huyo.
“Lipi hilo?”
Bwana Seppy akashusha pumzi ndefu na kuangalia pembeni kama kulikuwa na watu waliokuwa wakiyafuatilia mazungumzo yao, alipoona hakukuwa na mtu aliyekuwa akifanya hivyo, hapo ndipo alipoamua kutumbua jipu.
Hakutaka kuteseka moyoni mwake, ilikuwa ni vigumu mno kuendelea kuumia, kuwa na mawazo na wakati alikuwa na uwezo mkubwa wa kumwambia msichana huyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Hakutaka kuficha, kama ni siri, aliamua kuitoa na hivyo kumwambia jinsi alivyokuwa akimpenda. Muda wote msichana Stacie alikuwa kimya, alibaki akimwangalia mzee huyo usoni, uso wa Stacie ulikuwa kwenye tabasamu pana ambalo lilimpa matumaini mzee huyo kwamba angefanikiwa kile alichokuwa akikitaka.
“Umemaliza?” aliuliza Stacie baada ya kumsikiliza mzee huyo kwa dakika tatu.
“Ndiyo!”
“Haitowezekana!” alijibu kwa kifupi.
“Kwa nini tena jamani?”
“Jua kwamba haitowezekana, hakuna sababu, jua tu kwamba haitowezekana,” alisema Stacie na hapohapo kusimama, hakutaka kusubiri, japokuwa mzee huyo alionyesha muonekano uliomtia huruma, hakutaka kujali, akachukua kila kilicho chake na kuondoka zake huku Bwana Seppy akiishia kula kwa macho tu.
Je, nini kitaendelea?
Thanks again

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom