Mauaji yaliyojaa utata

Mauaji yaliyojaa utata

Masikini Paul. Kifo kinamwita. Ila huyo sappy ni mbinafsi mtoto mbichi huyo awe nae yeye tu wakati yeye ana mke wake
 
Sehemu ya Kwanza.

Ilikuwa ni taarifa mbaya, iliyoshtua ambayo ilianza kwa kusikika katika sehemu mbalimbali jijini Las Vegas nchini Marekani kabla ya kuwafikia polisi. Kila aliyezisikia taarifa hizo, hakuamini, wengi wakahisi kwamba hazikuwa taarifa za kweli, labda kulikuwa na mtu mwingine aliyetaka kuivumisha habari hiyo ambayo ilimsisimua kila mtu aliyeisikia.
Msichana mrembo aliyeitwa kwa jina la Stacie Lawrence, msichana aliyebahatika kunyakua taji la Urembo wa Dunia, alikutwa amekufa ndani ya chumba kimoja cha Hoteli ya Vikings Hill iliyokuwa Las Vegas, Nevada nchini Marekani alipokuwa amepanga huku akisubiri kuonana na Mkurugenzi wa Tovuti ya Google kwa ajili ya kusaini mkataba wa picha zake kutumika katika programu moja ambayo ingetumiwa katika simu zote zinazotumia system ya android.
Stacie aliyekuwa gumzo kwa kipindi hicho duniani kutoka na uzuriwake, alikutwa amekufa baada ya kujiovadosi madawa ya kulevya aina ya Heroine kwa kujichoma sindano katika mkono wake wa kulia wakati kitandani ndani ya hoteli hiyo.
Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya mjini, kila aliyeisikia, hakuamini, swali la kwanza kabisa walilojiuliza watu ni juu ya utumiaji wa madawa ya kulevya. Kila mtu alijua kwamba Stacie hakuwahi kutumia madawa hayo, si kipindi hicho tu, hata kabla ya kutwaataji hilo, hakuwa mtumiaji, sasa ilikuwaje mpaka leo hii akutwe chumbani kitandani akiwa amejidunga madawa hayo? Hilo lilikuwa swali lisilokuwa na majibu.
Waandishi wa habari kutoka katika mashirika mbalimbali ya habari kama CNN, BBC, Sky News na hata wale wa kujitegemea tayari walikuwa nje ya hoteli hiyo, vitendea kazi vyao vyote vilikuwa mikononi mwao, walitaka kupiga picha na kupata habari kuhusu kifo cha msichana huyo mrembo ambaye bado uzuri wake ulikuwa gumzo duniani.
Polisi walitanda kila sehemu nje ya hoteli hiyo, mkanda wa njano ulioandikwa Do Not Cross yaani ‘Usivuke’ulizungushiwa katika hoteli hiyo kwa muda. Magari ya wagonjwa mawili yalikuwa yamekwishafika katika hoteli hiyo, kilichosubiriwa ni kuingia ndani na kuuchukua mwili huo.
Waandishi hawakuruhusiwa kabisa kuingia ndani ya hoteli hiyo, waliambiwa wasubiri hapo nje wakati polisi wakiingia ndani kwa ajili ya kufanya kazi yao, hawakuwa na la kufanya zaidi ya kusubiri.
Polisi wakaingia ndani ya chumba kile. Huko wakaukuta mwili wa Stacie ukiwa kitandani, katika mkono wake wa kushoto kulikuwa na sindano iliyochoma mshipa wake, aliishikilia kwa kutumia mkono wake wa kulia mbali na hivyo, pembeni yake kulikuwa na noti za Dola, Paundi, Yeni na Euro.
Udenda ulikuwa ukimtoka, pale alipokuwa, hakutingishika, kilikuwa kifo kibaya, kilichozua maswali mengi kwa watu wengi, maswali hayo yote, hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya Stacie mwenyewe ambaye kipindi hicho alikuwa marehemu.
“This is the fifth one, what the hell with the drugs?” (huyu ni mtu wa tano, kuna nini na haya madawa?) alisikika akiuliza mwanaume mmoja huku akionekana kushangaa.
“I don’t know. What the hell with these teenagers, they like to try each and every goddamn thing, why?” (sifahamu. Nini kinaendelea kwa hawa vijana, wanapenda kujaribu kila kitu, kwa nini?) aliuliza mzee mmoja huku akionekana kukasirika.
Kila mmoja alishangaa, huyo hakuwa mtu wa kwanza, supastaa aliyejiua baada ya kujiovadozi kwa madawa ya kulevya, huyo alikuwa mtu wa tano, kijana supastaa ambaye aliamua kujiua kwa kujidunga sindano ya madawa ya kulevya.
Mtu wa kwanza kabisa kujiua kwa kujidunga shindano alikuwa Paul McKenz. Huyu alikuwa mcheza kikapu aliyekuwa akichipukia, mwenye sura nzuri, alijitengenezea jina kubwa katika Timu ya La Lakers, akaanza kupata mashabiki wengi, alipendwa na kila mtu aliyekuwa akiupenda mchezo huo, jina lake likaanza kuwa kubwa, akapata mikataba mingi lakini mwisho wa siku, Paul akaja kujidunga sindano yenye madawa ya kulevya aina ya Methamphetamine chumbani kwake.
Watu wengi walisikitika kwani ndiye alikuwa kijana aliyekuwa akichipukia katika mafanikio makubwa. Hiyo haikuishia hapo, pia kulikuwa na kijana mwingine aliyekuwa na kipaji cha uigizaji. Katika filamu yake ya kwanza ya Fallen Tree, alishinda Tuzo ya Oscar, Global na nyingine nyingi, huyu aliitwa Todd Lewis.
Bahati ikaanza kuonekana upande wake, akapendwa sana, kila kona alisikika yeye tu. Kadiri jina lake lilivyovuma ndivyo alivyozidi kujitengenezea mashabiki. Wakati akiwa amenunua gari yake ya kwanza ya thamani kabisa aina ya Ferrari Testarossa nyekundu, akakutwa naye akiwa amejidunga madawa ya kulevya ndani ya gari lake nje ya klabu moja huku pembeni kukiwa na noti ya dola, paundi, Yuan na Euro. Watu walisikitika na kulia, vilio vyao, huzuni zao hazikuweza kuwarudisha watu hao duniani.
Mtu mwingine kabla ya Stacie kujiua kwa madawa ya kulevya alikuwa kijana aliyeitwa kwa jina la Carter Phillip. Huyu alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakichipukia katika muziki wa Pop. Alikuwa na sauti kali, yenye nguvu ambapo kila alipokuwa akiitumia katika nyimbo zake, wanawake walichanganyikiwa.
Alikuwa mzuri wa sura, mwili uliojengeka. Kibao chake cha kwanza kabisa cha Come and Get Me Shawty alichokitoa kilitingisha kila kona duniani. Uwezo wake ulionekana, si hapo tu hata kwenye Shindano la American Got Talent, mpaka aliposhinda, watu waliona kipaji kikubwa ndani yake.
Wengi wakatabiri kwamba Carter ndiye angekuwa mrithi sahihi wa Michael Jackson, wengi wakamtabiria mema, njozi njema ikaonekana mapema kabisa kwani ngoma zake mbili alizozitoa, zote zilishika nafasi za juu kabisa katika orodha ya Billboard.
Akatengeneza fedha nyingi huku ndiyo kwanza akiwa na miaka kumi na tisa. Akapendwa, akawa kipenzi kikubwa cha watu ila baada ya kwenda nchini Uingereza kwenye Tamasha la UKIMWI lililokuwa likifanyika katika Jiji la Southampton, akakutwa akiwa amejiua ndani ya chumba alichochukua hotelini baada ya kujidunga sindano iliyokuwa na madawa ya kulevya aina ya Dextromethorphan huku pembeni kukiwa na noti za dola, paundi, yuan na euro.
Hakukuwa na aliyejua sababu ya vijana hao kujidunga madawa hayo ya kulevya, kila mtu aliyepata habari za vijana hao alishtuka. Mpaka katika kipindi ambacho msichana mrembo, Stacie kujiovadozi madawa hayo, bado watu hawakujua sababu ilikuwa nini, ni afadhali kama wangekuwa wamepigika katika maisha yao, ila kilichoshangaza, walikuwa wakianza kupata umaarufu, kupata fedha, na ndipo kipindi hichohicho nao waliamua kujidunga madawa ya kulevya.
Dunia ikatetemeka, watu wakaogopa kuwa mastaa, wengi walisikia kwamba unapokuwa staa, ilikuwa ni lazima kutumia madawa ya kulevya. Wazazi walipowaona vijana wao wanaanza harakati kupitia vipaji vyao, waliwazuia kwa kuona kwamba mwisho wa siku wangejiua kama hao wengine.
Swali kubwa ambalo waandishi wa habari walihoji, mitaani ni sababu gani zilizopelekea vijana hao kujidunga madawa ya kulevya? Kila aliyeuliza swali hilo, alikosa jibu kabisa.

Je, nini kitaendelea?
Nini kilipelekea watu hao, mastaa wakubwa kujimaliza kwa kujiovadozi madawa ya kulevya?
Tukutane kesho hapahapa
Asante mkuu unaeza ukatuchambulia mauaji yaliyojaa utata ya bongo/Africa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Namwonea huruma Paul kwa kitendo atakachofanyiwa na bwana seppy
 
Sehemu ya Kwanza.

Ilikuwa ni taarifa mbaya, iliyoshtua ambayo ilianza kwa kusikika katika sehemu mbalimbali jijini Las Vegas nchini Marekani kabla ya kuwafikia polisi. Kila aliyezisikia taarifa hizo, hakuamini, wengi wakahisi kwamba hazikuwa taarifa za kweli, labda kulikuwa na mtu mwingine aliyetaka kuivumisha habari hiyo ambayo ilimsisimua kila mtu aliyeisikia.
Msichana mrembo aliyeitwa kwa jina la Stacie Lawrence, msichana aliyebahatika kunyakua taji la Urembo wa Dunia, alikutwa amekufa ndani ya chumba kimoja cha Hoteli ya Vikings Hill iliyokuwa Las Vegas, Nevada nchini Marekani alipokuwa amepanga huku akisubiri kuonana na Mkurugenzi wa Tovuti ya Google kwa ajili ya kusaini mkataba wa picha zake kutumika katika programu moja ambayo ingetumiwa katika simu zote zinazotumia system ya android.
Stacie aliyekuwa gumzo kwa kipindi hicho duniani kutoka na uzuriwake, alikutwa amekufa baada ya kujiovadosi madawa ya kulevya aina ya Heroine kwa kujichoma sindano katika mkono wake wa kulia wakati kitandani ndani ya hoteli hiyo.
Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya mjini, kila aliyeisikia, hakuamini, swali la kwanza kabisa walilojiuliza watu ni juu ya utumiaji wa madawa ya kulevya. Kila mtu alijua kwamba Stacie hakuwahi kutumia madawa hayo, si kipindi hicho tu, hata kabla ya kutwaataji hilo, hakuwa mtumiaji, sasa ilikuwaje mpaka leo hii akutwe chumbani kitandani akiwa amejidunga madawa hayo? Hilo lilikuwa swali lisilokuwa na majibu.
Waandishi wa habari kutoka katika mashirika mbalimbali ya habari kama CNN, BBC, Sky News na hata wale wa kujitegemea tayari walikuwa nje ya hoteli hiyo, vitendea kazi vyao vyote vilikuwa mikononi mwao, walitaka kupiga picha na kupata habari kuhusu kifo cha msichana huyo mrembo ambaye bado uzuri wake ulikuwa gumzo duniani.
Polisi walitanda kila sehemu nje ya hoteli hiyo, mkanda wa njano ulioandikwa Do Not Cross yaani ‘Usivuke’ulizungushiwa katika hoteli hiyo kwa muda. Magari ya wagonjwa mawili yalikuwa yamekwishafika katika hoteli hiyo, kilichosubiriwa ni kuingia ndani na kuuchukua mwili huo.
Waandishi hawakuruhusiwa kabisa kuingia ndani ya hoteli hiyo, waliambiwa wasubiri hapo nje wakati polisi wakiingia ndani kwa ajili ya kufanya kazi yao, hawakuwa na la kufanya zaidi ya kusubiri.
Polisi wakaingia ndani ya chumba kile. Huko wakaukuta mwili wa Stacie ukiwa kitandani, katika mkono wake wa kushoto kulikuwa na sindano iliyochoma mshipa wake, aliishikilia kwa kutumia mkono wake wa kulia mbali na hivyo, pembeni yake kulikuwa na noti za Dola, Paundi, Yeni na Euro.
Udenda ulikuwa ukimtoka, pale alipokuwa, hakutingishika, kilikuwa kifo kibaya, kilichozua maswali mengi kwa watu wengi, maswali hayo yote, hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu zaidi ya Stacie mwenyewe ambaye kipindi hicho alikuwa marehemu.
“This is the fifth one, what the hell with the drugs?” (huyu ni mtu wa tano, kuna nini na haya madawa?) alisikika akiuliza mwanaume mmoja huku akionekana kushangaa.
“I don’t know. What the hell with these teenagers, they like to try each and every goddamn thing, why?” (sifahamu. Nini kinaendelea kwa hawa vijana, wanapenda kujaribu kila kitu, kwa nini?) aliuliza mzee mmoja huku akionekana kukasirika.
Kila mmoja alishangaa, huyo hakuwa mtu wa kwanza, supastaa aliyejiua baada ya kujiovadozi kwa madawa ya kulevya, huyo alikuwa mtu wa tano, kijana supastaa ambaye aliamua kujiua kwa kujidunga sindano ya madawa ya kulevya.
Mtu wa kwanza kabisa kujiua kwa kujidunga shindano alikuwa Paul McKenz. Huyu alikuwa mcheza kikapu aliyekuwa akichipukia, mwenye sura nzuri, alijitengenezea jina kubwa katika Timu ya La Lakers, akaanza kupata mashabiki wengi, alipendwa na kila mtu aliyekuwa akiupenda mchezo huo, jina lake likaanza kuwa kubwa, akapata mikataba mingi lakini mwisho wa siku, Paul akaja kujidunga sindano yenye madawa ya kulevya aina ya Methamphetamine chumbani kwake.
Watu wengi walisikitika kwani ndiye alikuwa kijana aliyekuwa akichipukia katika mafanikio makubwa. Hiyo haikuishia hapo, pia kulikuwa na kijana mwingine aliyekuwa na kipaji cha uigizaji. Katika filamu yake ya kwanza ya Fallen Tree, alishinda Tuzo ya Oscar, Global na nyingine nyingi, huyu aliitwa Todd Lewis.
Bahati ikaanza kuonekana upande wake, akapendwa sana, kila kona alisikika yeye tu. Kadiri jina lake lilivyovuma ndivyo alivyozidi kujitengenezea mashabiki. Wakati akiwa amenunua gari yake ya kwanza ya thamani kabisa aina ya Ferrari Testarossa nyekundu, akakutwa naye akiwa amejidunga madawa ya kulevya ndani ya gari lake nje ya klabu moja huku pembeni kukiwa na noti ya dola, paundi, Yuan na Euro. Watu walisikitika na kulia, vilio vyao, huzuni zao hazikuweza kuwarudisha watu hao duniani.
Mtu mwingine kabla ya Stacie kujiua kwa madawa ya kulevya alikuwa kijana aliyeitwa kwa jina la Carter Phillip. Huyu alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakichipukia katika muziki wa Pop. Alikuwa na sauti kali, yenye nguvu ambapo kila alipokuwa akiitumia katika nyimbo zake, wanawake walichanganyikiwa.
Alikuwa mzuri wa sura, mwili uliojengeka. Kibao chake cha kwanza kabisa cha Come and Get Me Shawty alichokitoa kilitingisha kila kona duniani. Uwezo wake ulionekana, si hapo tu hata kwenye Shindano la American Got Talent, mpaka aliposhinda, watu waliona kipaji kikubwa ndani yake.
Wengi wakatabiri kwamba Carter ndiye angekuwa mrithi sahihi wa Michael Jackson, wengi wakamtabiria mema, njozi njema ikaonekana mapema kabisa kwani ngoma zake mbili alizozitoa, zote zilishika nafasi za juu kabisa katika orodha ya Billboard.
Akatengeneza fedha nyingi huku ndiyo kwanza akiwa na miaka kumi na tisa. Akapendwa, akawa kipenzi kikubwa cha watu ila baada ya kwenda nchini Uingereza kwenye Tamasha la UKIMWI lililokuwa likifanyika katika Jiji la Southampton, akakutwa akiwa amejiua ndani ya chumba alichochukua hotelini baada ya kujidunga sindano iliyokuwa na madawa ya kulevya aina ya Dextromethorphan huku pembeni kukiwa na noti za dola, paundi, yuan na euro.
Hakukuwa na aliyejua sababu ya vijana hao kujidunga madawa hayo ya kulevya, kila mtu aliyepata habari za vijana hao alishtuka. Mpaka katika kipindi ambacho msichana mrembo, Stacie kujiovadozi madawa hayo, bado watu hawakujua sababu ilikuwa nini, ni afadhali kama wangekuwa wamepigika katika maisha yao, ila kilichoshangaza, walikuwa wakianza kupata umaarufu, kupata fedha, na ndipo kipindi hichohicho nao waliamua kujidunga madawa ya kulevya.
Dunia ikatetemeka, watu wakaogopa kuwa mastaa, wengi walisikia kwamba unapokuwa staa, ilikuwa ni lazima kutumia madawa ya kulevya. Wazazi walipowaona vijana wao wanaanza harakati kupitia vipaji vyao, waliwazuia kwa kuona kwamba mwisho wa siku wangejiua kama hao wengine.
Swali kubwa ambalo waandishi wa habari walihoji, mitaani ni sababu gani zilizopelekea vijana hao kujidunga madawa ya kulevya? Kila aliyeuliza swali hilo, alikosa jibu kabisa.

Je, nini kitaendelea?
Nini kilipelekea watu hao, mastaa wakubwa kujimaliza kwa kujiovadozi madawa ya kulevya?
Tukutane kesho hapahapa
Na hizo noti je mbona hajiulizi kila anayekufa anakutwa nazo pembeni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NYEMO CHILONGANI
MAUAJI YALIYOJAA UTATA
Sehemu ya Kumi na Nane.
“David, niambie nini kinaendelea,” alisema Benjamin kwenye simu.
“Nimeendelea kufuatilia mawasiliano kwa njia ya simu,” alijibu David.
“Umegundua nini?”
“Kuhusu nini?”
“Juu ya hizo fedha, unajua hizi zitakuwa na maana yake, nini umegundua?” aliuliza Benjamin huku siku ikiwa sikioni mwake, Harry alikuwa pembeni akimsikiliza.
“Bado! Nitaendelea kufuatilia, hata mimi ninahisi kwamba kuna kitu,” alisema David.
Hilo ndilo lililowasumbua kichwa kipindi hicho, hawakujua ni kitu gani walitakiwa kufanya kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa, ilionyesha kabisa kwamba huyo muuaji ambaye waliamini ni Bwana Seppy alitumia noti zile za fedha huku akiwa na maana yake.
Benjamin akakata simu na kisha kwenda kutulia kwenye kochi, kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi, moyo wake ulimwambia wazi kwamba kulikuwa na maana kubwa juu ya zile noti lakini hakujua zilikuwa na maana gani.
Alisimama kutoka pale alipokuwa na kuanza kutembea huku na kule, alikuwa na akili nyingi, alitumia muda wake mwingi kufikiria maana ya fedha zile lakini bado hakupata jibu lolote lile.
Alichokifanya ni kuchukua kalamu na karatasi na kisha kuziandika fedha zile kwa majina, alikumbuka, ilikuwa ni noti ya Yen, Dola, Paundi na Euro. Akaziandika zote na kisha kuanza kuziangalia kwa makini.
“Umegundua nini?” alimuuliza Harry.
“Bado sijagundua lolote lile,” alijibu Harry.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Mtu aliyekuwa akihusika na mauaji walikuwa wakimfahamu, alikuwa Bwana Seppy lakini tatizo lilitokea ni kwamba hawakujua sababu iliyompelekea kutumia fedha zile kuficha kilichokuwa kikiendelea.
Kitu cha kwanza kabisa alichokifanya Benjamin ni kuandika jina la mzee huyo, tena yote mawili, David Seppy na kisha kuanza kuyaangalia kwa umakini kabisa.
“Harry, hebu yaangalie haya majina vizuri,” alisema Benjamin, akayatumbulia macho.
“Umegundua lolote?”
“Hapana!”
“Kweli?”
Alichokifanya Harry ni kuyaangalia tena majina yale, tena kwa wakati huu kwa umakini mkubwa kabisa, aliangalia vya kutosha lakini hakubahatika kitu. Alichokifanya Benjamin ni kulifuta jina la David, likabaki jina la Seppy.
“Na hapo?”
“Bado sijapata kitu.”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Benjamin akatoa tabasamu pana, hakuamini kama mwisho wa siku angepata jibu kutokana na zile fedha zilizokuwa zikiwekwa kila tukio lilipokuwa likifanyika. Harry alikuwa kimya, kila alipomwangalia rafiki yake, alikuwa akitabasamu tu kitu kilichompa wakati mgumu kama kweli alijua maana ya fedha zile au la.
“Inamaanisha nini?” aliuliza Harry.
“Ni jina lake, alitaka kila mtu ajue kwamba yeye ndiye anafanya mauaji haya,” alijibu Benjamin.
“Unamaanisha Bwana Seppy?”
“Ndiyo!”
“Hebu nifafanulie...”
“Sawa. Hebu niandikie hizi alama za fedha kwenye karatasi...”
“Alama kivipi?”
“Kama dola ina alama gani?”
Alichokifanya Harry ni kuandika kama alivyoambiwa, fedha zote, yaani dola, euro, rubui na paundi, na alama zake zote kisha kumuonyeshea Benjamin. Benjamin akaichukua karatasi hiyo, akachukua kalamu na kuanza kumuonyesha.
“Alama hii ni alama ya dola ($), ukitoka hapa, kuna alama hii pia (£) ambayo ni paundi, ukiachana na hiyo, kuna hii (₽), hii ni fedha ya Urusi, ila pia kuna (¥) hii ni fedha kutoka nchini Urusi, hizi zimekuwa fedha ambazo amekuwa akizitumia mara kwa mara. Sasa ziunganishe, yaani $+£+₽+¥ ambayo unapata $£₽¥, yaani SEPPY. Bado hujapata kitu hapo?” aliuliza Benjamin baada ya kutoa maelezo ya kutosha.
Harry alipigwa na mshangao, hakuamini kile kilichokuwa kimemaanishwa juu ya fedha zile zilizokuwa zikiwekwa kila tukio lilipokuwa likitokea. Moyoni mwake, aliamini kwamba Benjamin alikuwa na akili sana kwani kugundua kitu kama hicho, kwamba mtu alikuwa akifanya mauaji na kuweka fedha kama alama ya jina lake, hakika ilimshangaza sana.
“Mmh! Nimekuelewa, na hii noti ya euro vipi?” aliuliza Harry.
“Aliiweka kwa kuwa kitambo jina lake lilikuwa Seepy, ila baadaye akaamua kutoa E moja na kubaki Seppy, kwa hiyo alitumia euro kama kuongezea alama yake ambayo ni € ili watu wasielewe kile alichokimaanisha,” alijibu Benjamin huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.
“Nimekuelewa. Kilichobaki?”
“Ni kuwataarifu polisi tu, akamatwe na afungwe gerezani,” alijibu Benjamin. Wakagongesheana mikono na kuahidiana kwamba asubuhi ya siku inayofuatia, ilikuwa ni lazima kwenda katika kituo cha polisi kutoa taarifa.
****
Moyo wa Bwana Seppy uliwaka kwa hasira, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea kwamba msichana aliyekuwa akimpenda, alikuwa akitembea na mwanaume mwingine.
Hakuamini, alichanganyikiwa, kila wakati alikuwa akitembea peke yake ndani ya nyumba yake huku akizungumza kama kichaa. Hakumjua mwanaume aliyekuwa akitembea na mpenzi wake ila aliambiwa kwamba mara kwa mara wawili hao walikutana katika hoteli moja iitwayo Greenland iliyokuwa huko New York.
Alichokifanya ni kuwaandaa vijana wake, ilikuwa ni lazima mwanaume huyo ajulikane ili kama kumuua amuue kwani asingeweza kumuua msichana Maria kwa kuwa alikuwa akimpenda mno kutoka ndani ya moyo wake.
Siku ziliendelea kusogea mbele, alijua ukweli lakini kila alipomwambia Maria kwamba alikuwa mdanganyifu katika uhusiano wao msichana huyo alimwambia wazi kwamba hakuwa akimdanganya kabisa na alimpenda yeye tu, nyuma yake hakukuwa na mwanaume yeyote yule.
Bwana Seppy akajipanga, ilikuwa ni lazima ajue ukweli wa kile kilichokuwa kikiendelea. Kijana wake wa kompyuta bado alikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha anafahamu mahali anapokuwa msichana huyo ili aweze kutoa taarifa inayotakiwa kutolewa.
“Mkuu! Maria amekuja tena Marekani,” Tim, kijana wa kompyuta alimwambia bosi wake.
“Amekuja lini?”
“Leo hii! Ila hayupo New York.”
“Yupo wapi?”
“Los Angeles kwenye hoteli iitwayo Scandnavia Hill,” alijibu Tim.
Bwana Seppy hakutaka kuchelewa, harakaharaka akawatuma vijana wake waliokuwa Los Angeles kwenda kuhakikisha kile walichokuwa ameambiwa. Huku nyumbani, moyo wake ulizidi kuuma, alimpenda sana Maria, hakutaka kumpoteza, aliuburudisha moyo wake vilivyo hivyo kumuwia vigumu sana kumfanya lolote baya.
Alijua kwamba msichana huyo alihitaji uhuru wake, alitakiwa kuwa na mwanaume mwingine kwani yeye, kwa jinsi alivyokuwa na umri mkubwa, kitandani hakuwa na uwezo mkubwa wa kufanya mapenzi, kama msichana ambaye damu inachemka, ilikuwa ni lazima kutafuta kijana machachari, mwenye nguvu ya kufanya mapenzi hata kwa zaidi ya saa mbili kitandani.
Yote hayo alikubaliana nayo lakini tatizo likawa ni kusalitiwa huku akijua kwamba anasalitiwa. Hakutaka kuona hilo likitokea na hivyo alikuwa tayari kwa kila kitu, alimgharamia sana msichana huyo, hakukuwa na mtu mwingine aliyeingiza mkono katika kumpa fedha na kumjengea nyumba, sasa iweje mwanaume mwingine amchukulie msichana huyo?
Kitu alichokuwa akikisubiria ni kuhusu mwanaume aliyekwenda na mpenzi wake hotelini, hakujua kama alikuwa na fedha kuzidi yeye, hakujua kitu chochote kile, kitu alichokisubiri kilikuwa ni taarifa tu.
Vijana hao walifanya uchunguzi wao katika hoteli hiyo tena kwa kutumia wahudumu ambao walilipwa vizuri na kutoa jibu kwamba msichana Maria alikuwa na mwanaume, supastaa wa mchezo wa kikapu, Paul McKenzie, hivyo kumpa taarifa mzee huyo.
“Nani? Paul?” aliuliza mzee huyo huku akionekana kutokuamini.
“Ndiyo!”
“Hapana!”
“Ndiyo mzee, tumeangalia vizuri! Ni yeye,” alisema kijana wake.
Bwana Seppy alipigwa na butwaa, hakuamini alichokisikia, alikuwa shabiki namba moja wa Paul, alimpenda sana kwa kuwa alionyesha kuwa kijana anayesaka mafanikio kwa nguvu kubwa, kila siku katika maisha yake alipambana, alimpenda lakini mwisho wa siku ndiye huyohuyo aliyekuwa akitembea na mpenzi wake.
Kabla ya kutoa uamuzi wa nini cha kufanya, akatulia kwenye kochi lake, akaanza kufikiria kitu kwamba ni uamuzi gani alitakiwa kuuchukua, machozi yalikuwa yakimbubujika, alijifikiria kwa muda na mwisho wa siku, akaamua kutoa uamuzi wake.
“Muueni kama wengine,” alisema mzee huyo.
“Hakuna tatizo!”
“Kesho, Dracula atasafiri mpaka huko kuja kuwasaidia kukamilisha kazi hiyo,” alisema Bwana Seppy.
“Sawa bosi.”
****
Hawakuwa wakijua kama walikuwa wakifuatiliwa, Paul na Maria walikuwa chumbani huku wakiyafurahia maisha kama kawaida yao. Hawakutaka kwenda katika Hoteli ya Greenland jijini New York bali walichokifanya ni kubadilisha hoteli na kwenda Los Angeles na kuingia katika Hoteli ya Scandnavia Hill.
Huko, walikuwa huru, waliamini kwamba kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angefahamu kama walikuwa humo. Hawakujua kama wahudumu wa humohumo ndiyo waliwapa taarifa vijana wa Bwana Seppy hasa baada ya kupewa kiasi kikubwa cha fedha.
Walijiachia usiku kucha na ilipofika asubuhi, Paul hakutaka kuondoka, bado alitamani kuwa na mpenzi wake huyo kwa kuwa hakukuwa na mechi yoyote na hata mazoezi hayakuwepo pia.
“Naomba ukae huku wiki nzima,” alisema Paul huku akimwangalia Maria usoni.
“Kwa ajili yako tu, hakuna tatizo!”
Kweli, hicho ndicho alichokifanya, hakutaka kurudi nchini Mexico, aliamua kukaa humohumo hotelini huku Bwana Seppy akiwasiliana naye kwa kutumia Whatsapp tu, tena huku akiwa ameifunga simu yake.
Hakujua kama mzee huyo alifahamu kila kitu, tayari Dracula ambaye alikuwa akisubiriwa alikwishafika na hivyo ni mipango ya mauaji ndiyo yaliyotakiwa kufanyika.
“Hakuna taarifa zilizosambaa kwamba tunakuja?” aliuliza Dracula, alikuwa akimuuliza dada wa mapokezi.
“Hakuna!”
“Sawa. Chukua kwanza hii,” alisema Dracula huku akimpa bahasha iliyokuwa na dola elfu ishirini.
Wakapewa kadi iliyokuwa na uwezo wa kufungua kila mlango ndani ya hoteli hiyo, kitu kingine walichokifanya ni kuwasiliana na watu wa IT ambao walikuwa wakisimamia kamera zote zilizokuwa humo hotelini, kuhitaji ulinzi wa hali na mali ili wasiweze kukamatwa, kwani walitaka kuingia ndani wakati msichana Maria alipokwenda bafuni kuoga.
Walichokifanya ni kuondoka na kwenda katika korido iliyokuwa na chumba hicho, walipoifikia, kwa kuwa kwenye mlango kwa chini kulikuwa na nafasi fulani hivyo wakachukua kamera ndogo waliyokuja nayo na kuipitisha kwa chini ambayo iliunganishwa na kichuma kirefu, kamera ile ambayo kama zilizokuwa zikitumiwa na FBI, zikaanza kuonyesha kilichokuwa kikiendelea ndani, tena huku wao wakifuatilia kila kitu kwa nje.
“Wamelala....” alisema jamaa mmoja.
“Usingizi?”
“Hapana! Wamekumbatiana,” alijibu jamaa huyo, baada ya dakika kadhaa, wakamuona msichana Maria akiamka, akachukua taulo lake, akampiga Paul kibao cha kimahaba na kuelekea bafuni kuoga.
“Amekwenda kuoga.”
“Nani?”
“Msichana...”
“Basi tuingieni,” alisema Dracula huku kila kitu alichokuwa ameambiwa awe nacho akiwa nacho. Hakukuwa na muda wa kupoteza, hicho ndicho walichokuwa wakikitaka, kwa haraka sana, wakaingia ndani kwa kutumia kadi ile waliyopewa na mhudumu kama funguo ya kuingia katika chumba chochote kile.
****
Hawakutaka kupoteza muda hapo mlangoni, walishakubaliana kuingia ndani hivyo wakaingia. Paul aliyekuwa kitandani, akakurupuka lakini Dracula akamuwahi palepale kitandani na kumbana vilivyo, akauziba mdomo wake, kijana mwingine akasogea na kumshikilia miguu ili asilete purukushani kitandani pale.
Walipoona wameweza kumzuia, mwingine akaufuata mlango wa bafuni na kuufunga kwa nje ili Maria asiweze kutoka ndani ya bafu lile. Huku kitandani, Dracula akachukua mto na kisha kuufunika uso wa Paul ili amuue kwa kumziba pua na mdomo, akose hewa na kufa, ndivyo ilivyotokea.
Paul alikukuruka na kukuruka lakini ilishindikana kabisa, hakuweza kujinasua kutoka katika mikono ya wanaume hao waliokuwa wamemkandamiza vilivyo kitandani pale, zoezi hilo lilifanyika kwa dakika tano mpaka walipohakikisha amekufa hapo kitandani ndipo Dracula alipotoa mto ule na kumwangalia Paul.
“He is gone,” (Amekufa) alisema Dracula huku uso wake ukianza kutoa tabasamu pana.
Kama kawaida yao, Dracula akachukua bomba la sindano lililokuwa kwenye mfuko aliokuwa nao, akalitoa, akachomeka sindano, akavuta madawa ya kulevya yaliyokuwa katika majimaji na kisha kumchoma Paul huku akimshikiza kwa mkono wake mwingine, alipohakikisha imekuwa poa, akachukua kiplastiki kilichokuwa na alama za vidole vya Benjamin na kisha kumuwekea katika shingo ya mwili wa Paul na katika sehemu zingine za mwili, kabla ya kuondoka, pia wakaweza zile noti ambazo zilikuwa ni kwa ajili ya utambulisho wa mauaji yale.
Hawakutaka kupoteza muda, waliingia harakaharaka na kufanya kazi yao haraka sana, walipomaliza, wakaondoka zao huku wakiwa wamekamilisha kazi hiyo kwa mafanikio makubwa.
“How was the work?” (Kazi ilikwendaje?) aliuliza Bwana Seppy kwenye simu.
“Simple as usual,” (Nyepesi kama kawaida) alijibu Dracula.
Ndani ya bafu lile, wakati mlango ukifungwa, Maria hakuwa akijua kitu chochote kile, hakujua kama kulikuwa na watu walikuwa wameingia na kumuua mpenzi wake.
Aliendelea kuoga huku akiimba, alipomaliza, akachukua taulo lake akajifuta na kisha kuufuata mlango. Akakishika kitasa ili aufungue, mlango haukuwa ukifunguka, ulionyesha kwamba ulifungwa kwa nje.
Akaanza kuugonga huku akiliita jina la Paul, mara ya kwanza alifikiri ni utani na hata uitaji wake ulikuwa ni wa kiutani sana lakini mlango haukufunguliwa na wala hakusikia sauti yoyote ile kutoka ndani ya chumba hicho.
“Paul, just open the door,” (Paul, fungua mlango) alisema Maria huku akiugonga mlango ule lakini hali iliendelea kuwa kimya.
Aliendelea kusubiri kwa dakika thelathini, alipoona Paul hafungui mlango ndipo alipoanza kuugonga kwa nguvu huku akikitekenya kitasa kile. Ilikuwa kazi kubwa lakini hakuacha kwani pasipo kufanya hivyo, basi angeendelea kuwa ndani ya chumba kile tu.
Alichukua dakika zaidi ya thelathini nyingine, kukipiga kitasa kile mpaka kilipovunjika ndipo akafanikiwa kutoka ndani ya bafu lile. Alichokutana nacho kitandani, hakuamini, mwili wa mpenzi wake, Paul ulikuwa tuli kitandani.
Maria hakuweza kuvumilia, akaanza kupiga kelele, wala hazikupita dakika nyingi, mlango ukafunguliwa, watu wa kwanza kuufungua mlango hawakuwa wahudumu bali walikuwa wageni kutoka katika vyumba vingine ndani ya hoteli hiyo.
Wao wenyewe wakapigwa na butwaa, walichokutana nacho, hawakuamini hata mara moja, mwili wa Paul ulikuwa kitandani, alivyoonekana, ni kama mtu aliyejiovadozi madawa ya kulevya kwani sindano ilikuwa mwilini mwake, katika mkono wake wa kushoto, udenda ulikuwa ukimtoka.
Hakukuwa na mtu aliyeugusa mwili ule, wakapiga simu mapokezini ambapo wahudumu wakafika haraka sana. Wao wenyewe hawakuamini kile walichokiona, wakaona jambo la busara kumuita meneja wa hoteli ile ambaye haraka sana akafika.
“Mungu wangu!” alisema meneja huku akionekana kutokuamini, hivyo kupiga simu polisi.
Japokuwa hoteli hiyo ilikuwa na wahudumu wengi, lakini kulikuwa na mhudumu mmoja ambaye alihusika, yeye ndiye aliyewapa kadi ya kufungulia mlango na hata kuwaelekeza chumba alichochukua Paul na Maria.
Muda wote wakati watu wapo hapo chumbani, Maria alikuwa akilia tu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makubwa.
Hakutoa maelezo yoyote yale kwani aliamini chochote kile ambacho angekisema mahali hapo, kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angemuelewa.
Baada ya dakika kumi, polisi wakafika hotelini hapo, moja kwa moja wakapandisha ngazi na kuanza kuelekea kule kilipokuwa chumba kile, kwa kuwa kilikuwa ghorofa ya tatu, hawakuchukua muda mrefu, wkaafika.
“Nani alikuwa humu chumbani tofauti na marehemu?” aliuliza polisi mmoja.
“Mimi hapa!” alijibu Maria huku akijifuta machozi.
“Hakuwepo mwingine?”
“Hakuwepo.”
“Nini kilitokea?”
“Hata mimi sijui, nilikuwa naoga, nilipotoka, nikakuta hiki kilichotokea,” alisema Maria.
Walichokifanya ni kumfunga pingu kwani yeye ndiye alikuwa mshukiwa namba moja wa mauaji yale. Wakamchukua na kuondoka naye kwenda kituoni huku polisi wengine wakiangalia kitu cha kufanya.
Waandishi wa habarai tayari walikuwa wamefika, hawakuamini kile kilichokuwa kimetokea, mtu aliyekuwa amekufa chumbani humo, walimfahamu, alikuwa staa mkubwa wa kikapu, alipendwa na wasichana wengi kutokana na uzuri wa sura yake.
Hakuwa mtu wa kashfa, aliishi na watu vizuri, alipendwa kutokana na upole wake pia. Siku hiyo, hakukuwa na aliyeamini kama kweli Paul alikuwa amekufa, majonzi yasiyokwisha yakaikumba mioyo yao na hivyo watu haohao waliokuwa ndani ya chumba hicho, wakaanza kusambaza taarifa hizo katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
Njia nzima Maria alikuwa akilia, polisi hawakutaka kusikia lolote lile, kilichowaambia ni kwamba msichana Maria alikuwa akijua kilichotokea hivyo walitaka kushirikiana naye ili kujua nini kilitokea.
Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom