Mauaji ya watu 3 Ilala - Dar

Mauaji ya watu 3 Ilala - Dar

Nimepita hapa maeneo ya ilala karibu na club ya wazee, kuna mauaji yametokea kwa watu wawili kupigwa risasi na muuaji nae kajiua,pia wawil wamejeruhiwa. Taarifa zaid ntawajuza.


Kwa mujibu wa shuhuda wa Clouds FM.

Mauaji hayo yamefanyika maeneo ya Ilala, kataja maeneo kwa jina lake maarufu (bahati mbaya sikudaka vizuri). Inadaiwa kuna gari ilikua inatoka ndani ya geti kutoka ikiwa na dereva mwanaume, abiria mwanamke mbele, na abiria wengine wawili wakiwa seat ya nyuma.

Pembeni hapo kulikua na jamaa kasimama. Inadaiwa alishushwa hapo dakika chache toka katika tax, walipotokeza abiria hao kupitia gari yao alitoa silaha yake na kupiga risasi gari akilenga zaidi abiria wa mbele pande zote kisha na nyuma. Baada ya kumaliza hapo muuaji huyo naye alijipiga risasi na kufariki hapo hapo.

Dereva na abiria wake wa mbele wamefariki dunia, huku abiria wa nyuma mmoja mama mtu mzima kajeruhiwa na risasi mgongoni na dada mwingine kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni.

hakuna kitu kibaya kama kula jasho la mtu au kumuibia muke yake ndio huwa inaishia hivyo..
 
Binafsi najiepusha kumiliki silaha japo zapatikana kirahisi.
 
wiv wa kimapenzi?pambav za huyo muuwaji angekuja kunipenda mie nipo hapa ona kaenda moton sasa
 
yaani mie nlijua westgate imehamia Ilala boma.
na ule msongamano sikutaka hata kuuliza nani huyo bada ya tu ya kuskia ni madada na mkaka wameuawa hapo getini na huyo muuaji mwenyewe kajiua

Hiyo ya Ilala Boma labda ni nyingine ila hii ya saubuhi ya leo kwenye saa moja unusu hivi imetokea karibu na klabu ya wazee, eneo kati ya Amana na Bungoni, na sidhani kama kuna benki ya CRDB hapo.
 
Sikuwahi kuwaza kulipiza kisasi kwa mambo ya wivu wa kimapenzi - ikitokea nikahisi kuibiwa naomba mungu aniepushe na hasira
 
Binafsi najiepusha kumiliki silaha japo zapatikana kirahisi.

Hongera sana mkuu, tena na kusihi kabisa usifikirie kuimiliki make utaishi Butimba. Yule ni Shetani kamili namba mbili baada ya pesa!!!
 
unamaanisha morogoro au kule kwa waliochagua kuwekewa lami badala ya umeme miaka ile alafu wakawa wanatembea peku pekua ili lami yao isichafuke??!!!!

Nadhani atakuwa anatoka kule kwa mazuzu yanayolima msimu mzima halafu mavuno wanayatumia kwa ajili ya ngoma na wengi wao miguu imeenda kushoto kwa kushambuliwa na funza.
 
Daah RIP Gabriel Munisi

Aisee, ni mchaga tena huyu!!!!!???? Nilichojifunza kwa wachaga ni kwamba hata kama utaona kuwa hawaelewani kati ya mke na mume then utumie fursa hiyo kumpata mke wake. Nakuambia akifahamu tu ni lazima akumalize. Wachaga wana wivu sana na wake zao, hata wakiachana kwa talaka au kutengana huwa wanaume wale hawafurahi sana wakisikia kuwa mke yule ana mwanaume mwingine. Nimeshuhudia incidence nyingi za hawa jamaa, hata kama hawakuua lakini huwa ni lazima mwanaume upate vitisho au kufanyiwa visa. Sasa huyu sijui huyo dada mtu ndiye aliyesababisha wawili hao kukosana au? Maana dada mtu kauwa na dereva na anayedhaniwa kuwa mchumba kajeruhiwa. Nafikiri alitaka awamalize wote akaona sasa atakamatwa akaamua kujimaliza. Rest in peace shemeji na dereva, na wewe muuaji Mungu anajua atakapokupumzisha!!!! Tujitahidi hata kama unampenda mwanamke/mwanaume kiasi gani, kuachana kunauma ila jua kuwa wanawake/wanaume are like buses, you missed one, you get another (the next) one. Why killing yourself? huyu jamaa anabiashara ya magari, siamini kama vihela havimtembelei, achana naye, wako wanawake wengine wazuri tu. Na mwanamke au mwanaume akianza kukudengulia jua kuwa hata mkifunga ndoa hamtaishi au kudumu. Bora dalili za kuachana zionekane mapema na kila mtu achukue ustaarabu wake.
 
Nadhani atakuwa anatoka kule kwa mazuzu yanayolima msimu mzima halafu mavuno wanayatumia kwa ajili ya ngoma na wengi wao miguu imeenda kushoto kwa kushambuliwa na funza.

Mazuzu akina nani hebu futa hiyo kai
 
Sikuwahi kuwaza kulipiza kisasi kwa mambo ya wivu wa kimapenzi - ikitokea nikahisi kuibiwa naomba mungu aniepushe na hasira
Mkuu makitu inauma sana pale ambapo umewekeza kila kitu juu yake alafu kaharibia chumba na kitanda kilekile mnacholalia...
 
hapa mimi nahisi harufu ya dhuluma, kuua dada na shemeji, pole sana majeluhi na mliokufa Mungu awaweke mahala stahiki amina ,ngoja tusubili habari kamili kwa walio karibu na tukio
 
enz za mwalim silaha za moto tlikuwa tnaziona kwenye movie tu.. na mpaka uimiliki ni ngumu ckuhz hata kina adam mchomvu wa clauz wanazo na vichaa wengnd weng sasa mnategemea nn?mt kalewa zake amekorofishwa kidogo anaenda kuuua ,serikal itazame upya habar za kugawa silaha hovyohovyo,
 
Back
Top Bottom