aisee, ni mchaga tena huyu!!!!!???? Nilichojifunza kwa wachaga ni kwamba hata kama utaona kuwa hawaelewani kati ya mke na mume then utumie fursa hiyo kumpata mke wake. Nakuambia akifahamu tu ni lazima akumalize. Wachaga wana wivu sana na wake zao, hata wakiachana kwa talaka au kutengana huwa wanaume wale hawafurahi sana wakisikia kuwa mke yule ana mwanaume mwingine. Nimeshuhudia incidence nyingi za hawa jamaa, hata kama hawakuua lakini huwa ni lazima mwanaume upate vitisho au kufanyiwa visa. Sasa huyu sijui huyo dada mtu ndiye aliyesababisha wawili hao kukosana au? Maana dada mtu kauwa na dereva na anayedhaniwa kuwa mchumba kajeruhiwa. Nafikiri alitaka awamalize wote akaona sasa atakamatwa akaamua kujimaliza. Rest in peace shemeji na dereva, na wewe muuaji mungu anajua atakapokupumzisha!!!! Tujitahidi hata kama unampenda mwanamke/mwanaume kiasi gani, kuachana kunauma ila jua kuwa wanawake/wanaume are like buses, you missed one, you get another (the next) one. Why killing yourself? Huyu jamaa anabiashara ya magari, siamini kama vihela havimtembelei, achana naye, wako wanawake wengine wazuri tu. Na mwanamke au mwanaume akianza kukudengulia jua kuwa hata mkifunga ndoa hamtaishi au kudumu. Bora dalili za kuachana zionekane mapema na kila mtu achukue ustaarabu wake.