Meko Junior
Senior Member
- Mar 23, 2018
- 159
- 362
Kisa cha pili
Mauaji Mbezi Siku ya uzinduzi wa nyumba
Jamaa mmoia mwenyeji wa Moshi kwa akina Mamndenyi mtani wangu na Asprin babu kijana.. Huyu mwana alipiga dili ndefu na wenzake ila kwenye mgao akawazima wenzake akasepa na mzigo wote akapotea mazima..
Akaibukia Mbezi akanunua kiwanja akajenga nyumba nzuri kubwa ya kisasa kwa ile pesa ya dili aliyodhulumu wenzake! Akaandaa na sherehe ya kuizindua siku ya Jumapili.. Akamualika mama yake mzazi toka Moshi na ndugu na jamaa na marafiki wengine
Siku ya uzinduzi asubuhi ile ya Jumapili watu wengine wakiws wameenda kanisani, wengine waliobaki nyumbani wakiandaa vyakula nk.. Mama mzazi akawa yuko sebuleni anaangalia TV jamaa kalala ndani
Walifika watu watatu rika la mwanae wakaingia mpaka sebuleni na kumsalimia mama kwa heshima zote kisha wakamuulizia jamaa
Mama mzazi akidhani ni wageni waalikwa akamuita mwanae! Jamaa akatoka ndani akiwa na uchovu mwingi.. Ghafla uso kwa uso anakutana na wale jamaa zake aliowapiga
Jamaa bila kupoteza muda wakamwambia mama yake kwamba kilichowaleta pale ni roho ya mtoto wake! Jamaa akajaribu kuwaomba wasimdhuru atawapatia chao, lakini wakamwambia siku hiyo hawakuhitaji hela tena bali roho yake tuu..
Akala risasi tatu akafa palepale jamaa wakasepa bila kuchukua hata sindano..! Walioenda kanisani na wageni waalikwa wengine walikuta msiba badala ya sherehe za uzinduzi wa nyumba
Mkuu samahani hiki kisa ni kile cha miaka ya 2008 kurudi nyumba, mbezi beach, alipigwa risasi mbele ya familia yake na watoto walikuepo, au nakosea ndugu Mshana
