Mauaji holela ya waendesha boda boda:

Mauaji holela ya waendesha boda boda:

Dr PL

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2024
Posts
682
Reaction score
1,031
Usafiri wa boda boda umekuwa kipimbilio la vijana wengi kupata kipato.

Wengi wanaofeli shuleni na wale wanaohitimu na kukosa ajira hukimbilia kwenye shughuli hii ya kusafirisha watu na/au mizigo.

Usafiri wa boda boda una changamoto nyingi ambazo humpata mwendesha boda boda na abiria wake pia.

Mojawapo ya changamoto hizo ni mauaji holela na ya kikatili ya waendesha boda boda (mbali na ulemavu na vifo vitokanavyo na ajali). Katika sehemu mbalimbali ya nchi yetu kumekuwa na kesi nyingi za vijana waendesha boda kujeruhiwa au kuuawa na pikipiki zao kupotea.

Matukio mengi ya mauaji hufanyika nyakati za usiku kwenye vichochoro, misituni nk.

Simulizi nyingi ni za boda kupata abiria ambao huwaomba kupelekwa sehemu fulani ambapo mtego huwekwa wa kufanya uporaji wa chombo kwa kumjeruhi au kumtoa uhai mhusika.

Miili yao hutelekezwa ikiwa na majeraha ya kutisha ya vitu vyenye ncha kali, alama za kunyongwa au ikiwa imefungwa kwa kamba.

Kwenye matukio hayo ya uporaji waathirika wengi miongoni mwa waendesha boda boda ni wale ambao wana vyombo vipya, wanaoanza kazi hiyo kwa mara ya kwanza nk.

Mbali na mambo mengi yanayosababisha matukio haya kuna la waendesha boda boda kuchongeana wao kwa wao.

Ukilitafakari jambo hili utaona kwamba hata baadhi ya waendesha boda boda wenyewe kwa wenyewe hushiriki kuwapora, kuwajeruhi au kuua wenzao na kutoweka na vyombo vyao.

Unakuta kwenye vijiwe wenye vyombo vipya ndiyo waathirika wakubwa. Sasa utaujiuliza hao waporaji au wauaji wanajuaje kwamba kwenye kijiwe kuna pikipiki mpya na hivyo kuanza kumfuatilia au kumwinda mhusika?

Jamii sasa inashuhudia umwagaji wa damu na mauaji ya kikatili ya waendesha boda boda wasio na hatia na mwisho wake ni laana kwa jamii.

Matukio mengi ya mauaji ya waendesha boda boda hayafuatiliwi au kuchunguzwa kwa kina ili kubaini wahusika hivyo kukomesha kabisa matukio hayo.

Tusipochukua hatua tutaendelea kuwapoteza vijana wetu na kuijaza nchi yetu laana ya damu.

Tupendane, tulindane, tudumishe haki, tudumishe amani na usawa kwa watu wetu wote.
 
Mmomonyoko wa maadili na kiwango cha umasikini mtaani kuongezeka kwa kiwango cha kutisha huenda zikawa ndiyo sababu kuu za kushamiri kwa haya mauaji.
 
Usafiri wa boda boda umekuwa kipimbilio la vijana wengi kupata kipato.

Wengi wanaofeli shuleni na wale wanaohitimu na kukosa ajira hukimbilia kwenye shughuli hii ya kusafirisha watu na/au mizigo.

Usafiri wa boda boda una changamoto nyingi ambazo humpata mwendesha boda boda na abiria wake pia.

Mojawapo ya changamoto hizo ni mauaji holela na ya kikatili ya waendesha boda boda (mbali na ulemavu na vifo vitokanavyo na ajali). Katika sehemu mbalimbali ya nchi yetu kumekuwa na kesi nyingi za vijana waendesha boda kujeruhiwa au kuuawa na pikipiki zao kupotea.

Matukio mengi ya mauaji hufanyika nyakati za usiku kwenye vichochoro, misituni nk.

Simulizi nyingi ni za boda kupata abiria ambao huwaomba kupelekwa sehemu fulani ambapo mtego huwekwa wa kufanya uporaji wa chombo kwa kumjeruhi au kumtoa uhai mhusika.

Miili yao hutelekezwa ikiwa na majeraha ya kutisha ya vitu vyenye ncha kali, alama za kunyongwa au ikiwa imefungwa kwa kamba.

Kwenye matukio hayo ya uporaji waathirika wengi miongoni mwa waendesha boda boda ni wale ambao wana vyombo vipya, wanaoanza kazi hiyo kwa mara ya kwanza nk.

Mbali na mambo mengi yanayosababisha matukio haya kuna la waendesha boda boda kuchongeana wao kwa wao.

Ukilitafakari jambo hili utaona kwamba hata baadhi ya waendesha boda boda wenyewe kwa wenyewe hushiriki kuwapora, kuwajeruhi au kuua wenzao na kutoweka na vyombo vyao.

Unakuta kwenye vijiwe wenye vyombo vipya ndiyo waathirika wakubwa. Sasa utaujiuliza hao waporaji au wauaji wanajuaje kwamba kwenye kijiwe kuna pikipiki mpya na hivyo kuanza kumfuatilia au kumwinda mhusika?

Jamii sasa inashuhudia umwagaji wa damu na mauaji ya kikatili ya waendesha boda boda wasio na hatia na mwisho wake ni laana kwa jamii.

Matukio mengi ya mauaji ya waendesha boda boda hayafuatiliwi au kuchunguzwa kwa kina ili kubaini wahusika hivyo kukomesha kabisa matukio hayo.

Tusipochukua hatua tutaendelea kuwapoteza vijana wetu na kuijaza nchi yetu laana ya damu.

Tupendane, tulindane, tudumishe haki, tudumishe amani na usawa kwa watu wetu wote.
Inasikitisha sana.
 
Mojawapo ya changamoto hizo ni mauaji holela na ya kikatili ya waendesha boda boda (mbali na ulemavu na vifo vitokanavyo na ajali). Katika sehemu mbalimbali ya nchi yetu kumekuwa na kesi nyingi za vijana waendesha boda kujeruhiwa au kuuawa na pikipiki zao kupotea.
Siku ukiandika upumbavu wa bodaboda barabarani, kutia ndani umafia wao wa ku-mob watu wenye magari katika kuteteana hata pale wanapofanya makosa, niite nichangie thread.

Kwa sasa waache wafe ni nafuu ya sisi mdereva barabarani, wajinga sana hawa
 
Mmomonyoko mkubwa wa maadili na kiwango cha umasikini mtaani kuongezeka kwa kiwango cha kutisha huenda zikawa ndiyo sababu kuu za kushamiri kwa haya mauaji.
Ukiondoa utekaji wa vibaka kuwateka bodaboda kwa minajiri ya kuchukua mali ila nyuma yake kuna haya
1.wake za watu
2.boda
Wenye pikipiki mpya ndio wana siri pekee au ndio wanatembea na wake za watu tu
Nina ushuhuda wa matukio manane ya bodaboda kuuwawa na watatu kati yao walichinjwa kinyama sana
Uchunguzi wa matukio yote hayo, chanzo ilikuwa wake za watu
Na hapo kwenye wake za watu kuna mawili kutembea nao wao kama wao na kubeba wake za watu kuwapeleka kwa michepuko
Wenye pikipiki mpya ndio wana siri pekee au ndio wanatembea na wake za watu tu
 
Usafiri wa boda boda umekuwa kipimbilio la vijana wengi kupata kipato.

Wengi wanaofeli shuleni na wale wanaohitimu na kukosa ajira hukimbilia kwenye shughuli hii ya kusafirisha watu na/au mizigo.

Usafiri wa boda boda una changamoto nyingi ambazo humpata mwendesha boda boda na abiria wake pia.

Mojawapo ya changamoto hizo ni mauaji holela na ya kikatili ya waendesha boda boda (mbali na ulemavu na vifo vitokanavyo na ajali). Katika sehemu mbalimbali ya nchi yetu kumekuwa na kesi nyingi za vijana waendesha boda kujeruhiwa au kuuawa na pikipiki zao kupotea.

Matukio mengi ya mauaji hufanyika nyakati za usiku kwenye vichochoro, misituni nk.

Simulizi nyingi ni za boda kupata abiria ambao huwaomba kupelekwa sehemu fulani ambapo mtego huwekwa wa kufanya uporaji wa chombo kwa kumjeruhi au kumtoa uhai mhusika.

Miili yao hutelekezwa ikiwa na majeraha ya kutisha ya vitu vyenye ncha kali, alama za kunyongwa au ikiwa imefungwa kwa kamba.

Kwenye matukio hayo ya uporaji waathirika wengi miongoni mwa waendesha boda boda ni wale ambao wana vyombo vipya, wanaoanza kazi hiyo kwa mara ya kwanza nk.

Mbali na mambo mengi yanayosababisha matukio haya kuna la waendesha boda boda kuchongeana wao kwa wao.

Ukilitafakari jambo hili utaona kwamba hata baadhi ya waendesha boda boda wenyewe kwa wenyewe hushiriki kuwapora, kuwajeruhi au kuua wenzao na kutoweka na vyombo vyao.

Unakuta kwenye vijiwe wenye vyombo vipya ndiyo waathirika wakubwa. Sasa utaujiuliza hao waporaji au wauaji wanajuaje kwamba kwenye kijiwe kuna pikipiki mpya na hivyo kuanza kumfuatilia au kumwinda mhusika?

Jamii sasa inashuhudia umwagaji wa damu na mauaji ya kikatili ya waendesha boda boda wasio na hatia na mwisho wake ni laana kwa jamii.

Matukio mengi ya mauaji ya waendesha boda boda hayafuatiliwi au kuchunguzwa kwa kina ili kubaini wahusika hivyo kukomesha kabisa matukio hayo.

Tusipochukua hatua tutaendelea kuwapoteza vijana wetu na kuijaza nchi yetu laana ya damu.

Tupendane, tulindane, tudumishe haki, tudumishe amani na usawa kwa watu wetu wote.
Kazi ya Ofisa usafirishaji i.e. Boda boda yenyewe haina walakini ila watendaji waliomo kwenye Ofisi hiyo (waendeshaji)ndo wenye shida tena shida kubwa sana.
1. Baadhi ya maDereva wa Boda hufanya shughuli yao wakiwa tayari wametumia kilevi (Huchanganya Energy drinks na visungura.) wengine huvuta bangi kabla ya kuingia ofisini huku wengine wakivuta petroli au gundi..
2. Wengine hufanya kazi yao kibabe - hawajali sheria za barabarani na mwendo huwa ni kasi bila sababu ya maana.
3. Wanapopata changamoto katika utoaji wa huduma wanakuwa wajeuri e.g. Boda akimgonga mtu hata kwa bahati mbaya hukimbia badala ya kutoa msaada kwa majeruhi na wengine huondoa pikipiki eneo la ajali na kuipeleka mafichoni kusikojulikana chap-chap.
4. Wengi wao (nadhani ni wote) hutumia mob psycology kujitetea e.g. boda akikosana na dereva wa gari barabarani, boda wote walio jirani hujikusanya hapo na kuanza kutoa maneno, kelele za matusi, maswali , kupiga miluzi hovyo n.k. kiasi kwamba hali inakuwa sio hali na mara nyingi dereva wa gari hujiondokea kinyonge.
5. Wengi wa boda boda hawana msaada katika jambo lako hata kama analijua-ni wasiri sana. Wengine hutumika kuchora ramani za wizi esp. majumbani mwa watu ikiwa ni pamojka na kusafirisha wezi. Wengine huharibu ndoa au mahusiano ya watu Me na Ke.
Mwisho: Mambo ni mengi (Tuhuma) dhidi ya waendesha boda boda na wanavyo vikundi vyao na uongozi uliokamilika. Kwanini wasikae wakakubaliana utaratibu wa kutoa huduma? Kwanini dereva ukubali safari ya mbali usiku? Tamaa ya fedha au
Kwa nini kufitiniana(Husda) kwa boda wapya wanaoanza?
Naonaga Polisi huwaita kwenye semina fupi-fupi zinazohusu usalama lakini mahudhurio ni hafifu sana huku wengine huhudhuria dk. chache then kila mtu na hamsini zake. Tutafika kweli??
 
Back
Top Bottom