Matumizi ya Magufuli, tuyajadili

Matumizi ya Magufuli, tuyajadili

Imagine unaingia ofisini kukutana na washauri wako na kitu cha kwanza wanafanya kukuonyesha wewe ni mjinga, kwamba maamuzi fulani uliyofanya ni ya kijinga na badala yake ungefanya hivi au vile. Unareact vipi??
Hiyo ndio sababu ni ngumu kuchukua au kufata ushauri wa watu dizaini ya The Boss They always want to make you feel stupid, sio aina ya kukupa afya kiakili kuwa around them hata wakiwa na mawazo sahihi!!

I am sure wapo watu around him wenye mawazo bora
awasikilize tu....

nilishangaa Marekani Rais ana washauri wa uchumi..halafu makamu wa Rais nae ana washauri wa uchumi'
na waziri wa uchumi nae ana washauri wa uchumi
kumbuka Rais na makamu sio watendaji wa moja kwa moja kwa masuala ya uchumi
lakini wana washauri....ili wasiweze kuibuka tu na mawazo yao yasiyopimwa kitaalamu...
 
Uzuri sasa hivi kila mtu anaimba wimbo wa Hapa Kazi Tu bila kufungua macho na kujadili nini kinatakiwa kufanyika.

Viongozi wetu wote hawajui Tanzania inataka nini?

Haha watu wanaimba hapa kazi tu ila hawasemi kazi zipi na hawajiulizi kazi hizo zina tija au mradi kazi tu?

Nimemsikia Magu akisema eti huko vijijini watu wanacheza pool table hawalimi akatoa agizo viongozi wasimamie watu walime kusiwe na njaa!!!

Kauli hii ilinistua mno na kujiuliza hivi huyu anajua hasa nini anachopaswa kufanya na nini ni kikwazo? Ni kweli vijijini wanacheza pool? Si huko vijijini watu wanalima vilimo visivyo na tija?

Watu wanafanya kazi ila hazina tija je serikali yake imejipangaje kuleta tija?

Watu wanapiga kazi tena sana ila tija hakuna!! Kama MTU analima eka 10 anapata junia 5 utamlaumu?

Ndio maana hawa watu wanakurupuka hovyo!!!
 
Haha watu wanaimba hapa kazi tu ila hawasemi kazi zipi na hawajiulizi kazi hizo zina tija au mradi kazi tu?

Nimemsikia Magu akisema eti huko vijijini watu wanacheza pool table hawalimi akatoa agizo viongozi wasimamie watu walime kusiwe na njaa!!!

Kauli hii ilinistua mno na kujiuliza hivi huyu anajua hasa nini anachopaswa kufanya na nini ni kikwazo? Ni kweli vijijini wanacheza pool? Si huko vijijini watu wanalima vilimo visivyo na tija?

Watu wanafanya kazi ila hazina tija je serikali yake imejipangaje kuleta tija?

Watu wanapiga kazi tena sana ila tija hakuna!! Kama MTU analima eka 10 anapata junia 5 utamlaumu?

Ndio maana hawa watu wanakurupuka hovyo!!!


Sasa utaona Paul Makonda akipiga marufuku pool mjini...
yote kum please ...
 
Vijembe vipo wapi? Ungekuwa na akili usingejibu utumbo ule....
Fact ni kuwa mapato yamepungua!
Kila mtu anakuja na sababu anazohisi zimepunguza mapato huwezi kupinga sababu ya mwenzio bila ya ku prove scientifically ile ya kwako unayoamini ni strong
 
Fact ni kuwa mapato yamepungua!
Kila mtu anakuja na sababu anazohisi zimepunguza mapato huwezi kupinga sababu ya mwenzio bila ya ku prove scientifically ile ya kwako unayoamini ni strong
Siku zote miezi ya 11,12, huwa ni mwisho Wa grace period za kodi kabla ya mwaka MPYA....

Watu hukimbizana sana kulipa malimbikizo ya kodi zao miezi hiyo ili kuanza mwaka MPYA na madeni mapya!!

Ndio maana kwa msiojua mlianza imba pambio za sifa kuwa wameboresha mno ukusanyaji na kuzuia mianya ya ukwepaji kodi...

Swami ni je why imerudi kule kule alikoachia JK? Au kontena zinaibiwa tena?

Ndo maana tulisema very soon waimbaji Wa hizi pambio watachoka watakapoona uhalisia!!!


Fact ni kuwa mapato yamepungua!
Kila mtu anakuja na sababu anazohisi zimepunguza mapato huwezi kupinga sababu ya mwenzio bila ya ku prove scientifically ile ya kwako unayoamini ni strong
 
Sasa utaona Paul Makonda akipiga marufuku pool mjini...
yote kum please ...
Haha na hivi kapewa sifa watamkomajeee....

Eti Makonda nae ni kiongozi mbele ya huyo anayejiona malaika Wa bongo hahahaha!!!
 
I am sure wapo watu around him wenye mawazo bora
awasikilize tu....

nilishangaa Marekani Rais ana washauri wa uchumi..halafu makamu wa Rais nae ana washauri wa uchumi'
na waziri wa uchumi nae ana washauri wa uchumi
kumbuka Rais na makamu sio watendaji wa moja kwa moja kwa masuala ya uchumi
lakini wana washauri....ili wasiweze kuibuka tu na mawazo yao yasiyopimwa kitaalamu...

Upo katika nchi ambayo mshauri wa uchumi mwenye elimu ya juu kabisa na Amefanya kazi katika taasisi za kimataifa lakini kitu cha kwanza anachofikiria ni personal gain, kifupi hata hiyo nafasi kwake anasema "Ameula"
Kuondoka mahali hapo u've to break all the rules first, muwe wavumilivu tu tunaelekea kwenye msitari!!
 
Miaka mitano inaweza kupita kama utani anakimbia kimbia na kufukuza watu then asifanye kitu alafu wabongo tulivyo mtu akifukuzwa kazi tunafurahi impact yake itakuja kuonekana baadae ya fukuza fukuza
Kama yule Wa Muhjmbili!!! Badala ya kumpa nyenzo na maarifa unatimua then anakuja mwingine inabidi aanze upya kuizoea kazi
 
jamaa ni kiongozi mzuri lakini kuna some elements anamiss,alafu ni very important...mfano hana vision nadhan hata yeye ukimuulza anaiona wapi nchi after 5years...sijui kama atakujibu.
 
kipi bora kwa sasa , kuimarisha huduma za afya katika kila wilaya au daraja la coco beach?.Ili kupunguza msongomano wa wagonjwa muhimbili ni kuimarisha hospitali za wilaya na mikoa wajawazito watapungua sana kwenda Muhimbili.Yaonekana Rais anajua matatizo ya Dar peke yake maana kila kitu dar sasa ni wakati wa kutembelea mikoani ili ayaone matatizo ya huko.
 
kipi bora kwa sasa , kuimarisha huduma za afya katika kila wilaya au daraja la coco beach?.Ili kupunguza msongomano wa wagonjwa muhimbili ni kuimarisha hospitali za wilaya na mikoa wajawazito watapungua sana kwenda Muhimbili.Yaonekana Rais anajua matatizo ya Dar peke yake maana kila kitu dar sasa ni wakati wa kutembelea mikoani ili ayaone matatizo ya huko.
subili kuitwa nyumbu
 
Kama yule Wa Muhjmbili!!! Badala ya kumpa nyenzo na maarifa unatimua then anakuja mwingine inabidi aanze upya kuizoea kazi

Nilicheka sana alivyorudi muhimbili na kukuta kila kitu kama alivyoacha.
 
Hakuna anaejua baada ya miaka mitano kutakuwa na bajeti hizi
usisahau sehemu ya pesa hizi ni misaada na hakuna gurantee misaada itakuwepo milele
kama kuna namna ya kumshauri tumshauri sasa na ndo tunachofanya

Magufuli hana budi kusikiliza na kufuata ushauri wa wataalam wanaolitakia mema Taifa letu kwasababu ameonesha nia ya kubadilisha maisha ya wananchi kwa muda mfupi iwezekanavyo!! Hayo ndio matakwa yake na matarajio ya wananchi wengi kuwa katika muda wa utawala wake kutakuwa na mabadiliko makubwa ya watu kutoka umasikini na kuwa na hali bora zaidi; kutoka kusumbuliwa na maradhi na kuwa na watu wenye afya nzuri; elimu yetu kwa ujumla wake kuwa ya kiwango cha juu.

Ukwell wa hali halisi ambayo hatuna budi kuifahamu na kuelewa ni kuwa mabadliko tunayotarajia kwa kawaida huja taratibu na huchukua muda. Mbadiliko katika nchi pia huhitaji watu kufanya kazi kwa bidii na ni lazima wawe wavumilivu.
 
Kumuelewa Magufuli Na Utawala Wake Kwa UJUMLA Unahitaji Kutulia Na Wala Usiwe Na Papara! Soon Mtamuelewa TU[/QUOT

we nae ni lile kundi la akina KIDUMU CHAMA CHA....... maana unajijaza matumain bila hata kureason
 
Ndio chaguo lenu hilo..Mimi yangu macho..Hapo kazi kwenu tu!!...
 
Daraja la kigamboni bilioni 200
daraja la furahisha mwanza bilioni 200 (nakaribisha masahisho)
daraja la coco beach-bilioni 200 zimetengwa
barabara ya dar-chalinze-zaidi ya trilioni 1.3(dollar milioni 500)
mabasi yaendayo kasi -zaidi ya bilioni 200
flyover ya ubungo bilioni 100

Iwapo serikali ingeamua kujenga treni za umeme
badala ya mabasi yaendayo kasi ingetumia dollar milion 430
kwa km 32...yaani karibu Dar yote ingekuwa unapanda treni dakika 10
uko popote pale hata kigamboni treni ingefika kupitia Mbagala..
hii ni link ya Ethiopia inaelezea gharama za treni hizo na tayari wenzetu wanatumia..
Ethiopia gets first sub-Saharan Africa metro - CNN.com

na kama hizo bilioni zingetumika kujenga vyuo vikuu
UDOM gharama zake ilikuwa kiasi cha bilioni 25....

Tanzania na hasa Dar es Salaam inahitaji yote uliyoandika, barabara, madaraja na treni za umeme. Baadhi ya miradi uliyotaja mfano, Daraja la Kigambano, mabasi yanaendayo kasi ingekuwepo na hela zingelipwa (zilishalipwa) regardless Mkazi wa Magogoni leo angekuwa Dovutwa, Lowassa, Hashim Rungwe or Mama Anna whatever! Hii ni kwa sababu uongozi uliopita ulishafanya committment na baadhi ya malipo yalishafanyika, hivyo kilichotakiwa na uongozi wa sasa ni kukamilisha malipo na/au kusimamia ili miradi ikamilike. Ingekuwa hasara (kwa mfano) kuanza kuelekeza hela kwa mradi mpya na kuacha ya zamani inaota majani!

Kwenye treni, nakubaliana na wewe kabisa kwamba Dar es Salaam inahitaji usafiri wa treni za umeme maana kwa kasi ya ongezeko la watu na shughuli za kiuchumi usafiri wa babaraba hautatosha. Hata hivyo, Tanzania ina kazi ya ziada kwenye hili la Treni za umeme kuliko ilivyo Ethiopia kwa sababu bado hatuna umeme wa kutosha. Na hili la umeme ndio tatizo kubwa sana hata kwa sekta binafsi (hususan viwanda). Kama nimemsikia Magufuli vizuri kwenye hotuba yake kwa wazee wa Dar es Salaam, serikali yake imetoa hela kukamilisha mradi wa kuzalisha umeme Kinyerezi II.

Mjadala mzuri!
 
ninachomuonea huruma ni pale anapowakela MSOGA na MTAMA..
Hakuna watu wazuri kwa Fitina na Visasi kama Hawa..

Mungu amuepushie mbali hasira zao..
 
Back
Top Bottom